CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimemshutumu Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, kuwa ni miongoni mwa wanasiasa wanaowahadaa wananchi kutojiunga na Chadema kwa sababu ya dini zao.
Akituhubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Tunduru jana, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema kwa muda mrefu viongozi wa CCM wakiwatumia viongozi wa dini na baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakitoa shutuma kuwa chama hicho kina udini na ukabila na kueleza kuwa madai hayo hayana ukweli wowote.
"Mheshimiwa Lipumba namuheshimu sana, lakini amekuwa akiwahadaa wananchi kwa kuwataka wasijiunge na CHADEMA kwa kuwa ni chama cha udini na ukabila". Tanzania hakuna chama kama hicho alisema.
"CHADEMA kina watu wa dini na makabila tofauti. Kuna watu wanaotoka Arusha, Mbeya, Iringa na hata Zanzibar, sasa huo udini wanaosema unatokea wapi?" alihoji Mbowe ambaye pia ni mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.
Katika mkutano huo, Mbowe alionyesha barua aliyoeleza kuwa imesambazwa na maofisa wa usalama wa taifa kwa masheikh wa Ruvuma na mkoani Mbeya ikiwataka Waislamu kutohudhuria mikutano ya CHADEMA kwa madai ya udini na ukabila.
"Watu wa Usalama wa Taifa wamesambaza barua kwa masheikh wa Ruvuma na Mbeya inayoeleza kuwa waumini wa dini hiyo wasihudhurie mikutano ya CHADEMA kwa kuwa ni chama cha Kikristo na kina Ukabila," alisema Mbowe huku akionyesha barua hiyo kwa umati wa wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Source: Tanzania Daima
Akituhubia katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Tunduru jana, Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe, alisema kwa muda mrefu viongozi wa CCM wakiwatumia viongozi wa dini na baadhi ya wanasiasa wamekuwa wakitoa shutuma kuwa chama hicho kina udini na ukabila na kueleza kuwa madai hayo hayana ukweli wowote.
"Mheshimiwa Lipumba namuheshimu sana, lakini amekuwa akiwahadaa wananchi kwa kuwataka wasijiunge na CHADEMA kwa kuwa ni chama cha udini na ukabila". Tanzania hakuna chama kama hicho alisema.
"CHADEMA kina watu wa dini na makabila tofauti. Kuna watu wanaotoka Arusha, Mbeya, Iringa na hata Zanzibar, sasa huo udini wanaosema unatokea wapi?" alihoji Mbowe ambaye pia ni mbunge wa Hai na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni.
Katika mkutano huo, Mbowe alionyesha barua aliyoeleza kuwa imesambazwa na maofisa wa usalama wa taifa kwa masheikh wa Ruvuma na mkoani Mbeya ikiwataka Waislamu kutohudhuria mikutano ya CHADEMA kwa madai ya udini na ukabila.
"Watu wa Usalama wa Taifa wamesambaza barua kwa masheikh wa Ruvuma na Mbeya inayoeleza kuwa waumini wa dini hiyo wasihudhurie mikutano ya CHADEMA kwa kuwa ni chama cha Kikristo na kina Ukabila," alisema Mbowe huku akionyesha barua hiyo kwa umati wa wananchi waliohudhuria mkutano huo.
Source: Tanzania Daima