kinyoba
JF-Expert Member
- Jun 2, 2011
- 1,267
- 718
Habariza leo wadau? Huwa najiunga na tigo internet mara kwa mara kwenye simu yangu, sasa siku ambayo sina mpango nayo hasa ukizingatia na huu mgao kunasiku unakuta huna charge au unamambo mengine au huwa sijiungi nayo. Tatizo ni kuwa tigo wanakuunganisha na kukata sh 450 hatakama hujaomba. Customer care wanasema tuma neno DEACT na nimefanya hivyo asubuhi na kujibiwa kuwa nimejitoa kwenye kifurushi. Sasa nashangaa nimeunganishwa tena, SIJUI KAMA NA NYIE WADAU MMEONA HII KITU: huu ni wizi na usanii, lazima mteja awe na maamuzi na pesa zake katika akaunti yake, na hiyo custumer care ukipiga simu hadi upokelewe ni robo saa au zaidi.hata hii huduma ya kukopesha pesa ni usanii tu, iweje wao wao wakupangie kiasi cha kukopa? Eti kigezo ni wewe umekua mteja mzuri sana hivyo tutakukopa sh 800 au 1500; HUU PIA NI WIZI; wanapaswa kuweka options za kiasi gani mtu anataka kukopa kama wenzao voda. BINAFSI NAWAONA KAMA TIGO HAWAPO SMART.