Jamani watanzania wenzangu mbona chama cha matusi aka chama cha majaji hakijawahi kumteua rais mstaafu Ally Hassan Mwinyi kushiriki kwenye kampeni za kumnadi mgombea wa CCM kwenye chaguzi ndogo kama mzee Mkapa,mwenye kujua sababu atujuze.
Mwinyi ni mtu mwenye heshima zake, anaheshimika sana TZ hii na hawezi kujivunjia heshima hasa katika kipindi hiki cha DOT.COM, we ukamtukane mwinyi kwenye hadhara ya watu ustaarabu kweli! mwacheni apumzike.
Sio kwamba Mkapa anapenda kushiriki katika kampeni. Ni kama kapewa adhabu na Kikwete siunajua ukiwa na makosa lazima unyenyekee ili usije ukaumbuliwa ndio haya yanayomsibu Mkapa. Mkapa ana issue ya ufisadi akiwa rais ivyo hawezi kukataa chochote kile ambacho ataambiwa na mwenyekiti wake. Anaogopa wasije wakaanza kumuulizia kiwira. Mwinyi alikuwa rais wa watanzania hivyo hawezi piga kampeni kwa chama kimoja wakati analipiwa gharama na watanzania wote bila kujali vyama.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.