Nimesoma hoja nyingi amabazo zinadai waislamu tumekandamizwa tangu Tanganyika ipate uhuru. Lakini katika malalamiko hayo sijaona mahali tunailalamikia CCM kwa kutukandamiza kwa zaidi ya miaka 50 bali tunamtuhumu nyerere na wakatoliki. Nyerere amekuwa kiongozi kati ya 1961 na 1984 wastani wa miaka 24 na baada ya 1984 mpaka leo 2011 wamekuwa madarakani viongozi wengine wa CCM takribani maiaka 26 sasa, kama Nyerere alitukandamiza je hawa wengine waliopo kwa miaka 26 wametufanyia nini?. Ndugu zangu waislamu kiini cha matatizo yetu ni CCM kwa ujumla wake bila kujali kiongozi mmoja mmoja na wala sio wakatoliki ambao ni sehemu tu ya raia . Tangu tupate uhuru maeneo ambayo waislamu tupo wengi tumekuwa na wabunge waislamu kupitia CCM je wametufanyia nini? Tangu tupate uhuru tumekuwa na mawaziri waisla japo wachache je wamefanya nini katika majimbo yao?. Ndugu zangu waislamu CCM inatudanganya itatusaidai kutatuma matatizo tuliyonayo ya kiuchumi na kielimu wakati ukiangalia taifa lianagamia kwa umaskini hatuna viwanda, wawekezaji wezi, shule mbovu za kata hata waalimu hazina, hospitali shida, maji shida, ufumuko wa bei n.k je haya matatizo tuliyonayo CCM watayatatua kwa njia ipi wakati tuona wazi inchi inateketea. Kama waislamu tunataka mafanikio lazima tupambane na CCM ambayo ndio kiini cha matatizo na kuwaweka madarakani watu wanyeuwezo wa kutujengea uchumi imara wa taifa letu ambao unaweza kutatua matatizo yanayotukabili sisi waislamu pamoja na watanzania wengine kwa ujumla wao.
Wenu: Muislamu mwenye uchungu wa maendeleo.
Wenu: Muislamu mwenye uchungu wa maendeleo.