Elections 2010 Mbona idadi ya wapiga kura wa urais na ubunge ni tofauti kwa baadhi ya majimbo?

wihanzi

Member
Feb 10, 2009
62
3
Ndugu zangu nilikuwa napitia matoke ya urais katika website ya NEC nikaona kama vile data zinatofautiana na za ubunge nilizosoma kutoka vyombo tofauti vya habari kwa maana ya total casted votes. Bahati mbaya NEC hawajapost matokeo ya ubunge kupata uhakika lakini nimejaribu kuangalia kupitia mwananchi ambao wameonyesha matokeo ya jiji la Dar nikaona yako hivi
Nec Urais/ Gazeti Mwanchi ubunge
Ilala 39,406/ 34,498
Ukonga 53,457/ 46,891
Kigamboni 106,723/ 104,759

NB: Matokeo ya urais ni official lakini ya ubunge si official nimechukua kwenye website ya mwananchi kwenye habari isemayo CHADEMA yatikisa ngome ya CCM Dar. Kama kuna mdau anajua wapi nipate official votes za ubunge tafadhali anisaidie niweze cocompare.

Najua sababu pekee ya tofauti ingeweza kuwa kama kuna sehemu hawajapiga kura za ubunge lakini sikusikia hilo dar na isitoshe katika kila kituo tulikuwa tukipewa karatasi tau za kura

Naomba mnieleweshe.
 
Back
Top Bottom