Elections 2010 Mbona Barrack Obama anakubali kushindwa..?!

mi_mdau

JF-Expert Member
Oct 29, 2010
1,088
1,393
Ni bahati nzuri kuwa uchaguzi wetu hapa Tz umefanyika karibu kipindi sawa na ule wa nusu muhula (mid-term) wa marekani. Ni ukweli usiopingika kuwa umaarufu wa Barack Obama umeshuka na hivyo chama chake kupoteza viti vingi na nguvu ya utawala kwenye bunge nchini humo. Lakini Barack Obama hajakataa kushindwa kwa chama chake, ingawa imemuuma na ameona ni changamoto(He called the election a Democratic "shellacking" and lamented that "we lost track of the ways we connected with the folks who got us here in the first place." ) na kusema kuwa atatilia mkazo kukuza uchumi na ajira kipindi hiki kilichobaki. Aliendea kusema kuwa amethibitisha alichosikia toka kwa wapiga kura nchi nzima, watu wamefadhaishwa, (kama ni kiswahili sahihi)((Obama said Tuesday's results confirmed what he's heard from voters across the country: People are frustrated. He said the lesson of election was that he hasn't made enough progress in creating jobs). Jambo kuu hapa ni kuwa amekubali kushindwa kwa misingi ya kidemokrasia, ile iliyomuweka yeye madarakani kwa kishindo. Huu ni mfano mzuri toka kwa taifa lilioendelea ambalo tumekuwa tukienda kila siku kuomba misaada toka kwao. Swali ni Je, viongozi wetu wamefanya hili uchaguzi huu kutokana na matukio yanayotokana na matokeo ya kura yanayoendelea kutangazwa? Sidhani... Kwa nini hatuamini kuwa Rais anaweza asipendwe tena kama mwanzo? Kwa nini mawakala wa upinzani wanakuwa macho kulinda kura zao? Ni ishara kuwa waliopo madarakani hawataki kushindwa kwa haki! Kwa nini tusikubali kuwa wananchi walioelimika na wenye ufahamu wa ushindani wa demokrasia hawatukubali tena kama hapo awali? Tafakari, chukua hatua..
 
Ni bahati nzuri kuwa uchaguzi wetu hapa Tz umefanyika karibu kipindi sawa na ule wa nusu muhula (mid-term) wa marekani. Ni ukweli usiopingika kuwa umaarufu wa Barack Obama umeshuka na hivyo chama chake kupoteza viti vingi na nguvu ya utawala kwenye bunge nchini humo. Lakini Barack Obama hajakataa kushindwa kwa chama chake, ingawa imemuuma na ameona ni changamoto(He called the election a Democratic "shellacking" and lamented that "we lost track of the ways we connected with the folks who got us here in the first place." ) na kusema kuwa atatilia mkazo kukuza uchumi na ajira kipindi hiki kilichobaki. Aliendea kusema kuwa amethibitisha alichosikia toka kwa wapiga kura nchi nzima, watu wamefadhaishwa, (kama ni kiswahili sahihi)((Obama said Tuesday's results confirmed what he's heard from voters across the country: People are frustrated. He said the lesson of election was that he hasn't made enough progress in creating jobs). Jambo kuu hapa ni kuwa amekubali kushindwa kwa misingi ya kidemokrasia, ile iliyomuweka yeye madarakani kwa kishindo. Huu ni mfano mzuri toka kwa taifa lilioendelea ambalo tumekuwa tukienda kila siku kuomba misaada toka kwao. Swali ni Je, viongozi wetu wamefanya hili uchaguzi huu kutokana na matukio yanayotokana na matokeo ya kura yanayoendelea kutangazwa? Sidhani... Kwa nini hatuamini kuwa Rais anaweza asipendwe tena kama mwanzo? Kwa nini mawakala wa upinzani wanakuwa macho kulinda kura zao? Ni ishara kuwa waliopo madarakani hawataki kushindwa kwa haki! Kwa nini tusikubali kuwa wananchi walioelimika na wenye ufahamu wa ushindani wa demokrasia hawatukubali tena kama hapo awali? Tafakari, chukua hatua..

Mkuu, mimi siku zote huwa natamani Tanzania pia tuwe na chaguzi kama Amerika ambako wapigara wanaheshimika sana.

Tatizo hapa kwetu watu wanajua kuukwaa uongozi ni kuukwaa ulaji.

Leo Makongolo Mahanga ni Mbunge wa kufinyanga huko Segerea, na kwa maneno yake alitamka amewekeza "pesa nyingi sana" asingependa kuona "zinapotea".

Any way. I shut-up
 
Na kuchezea kura na matokeo yake inamaanisha kuchezea wananchi, na kuwaonyesha kuwa kura zao ni kama kuongeza chumvi baharini, kamwe hazitoleta tofauti
 
Huwezi kulinganisha uchaguzi kule Marekani na uhuni unaofanywa hapa kwetu! Kule Marekani mwaka 2000 wizi wa kura ulilikumba jimbo la Florida lililompa Bush ushindi mduchu ambao ulipingwa na Al Gore wa Democrat.

Kilichotokea? Kesi ikatinga mahakamani katika ngazi zote hadi Supreme Court ambapo iliamua kwa kura 5 kwa 4 kusitisha zoezi la kurudiwa kurudiwa kuhesabu kura na hivyo hatimaye kumpa ushindi Bush kwa kura 537 tu. Mchakato wa Mahakama ulichukuwa zaidi ya mwezi mmoja na nusu.

hapa kwetu kuna uhuni na ubabe.: Hakuna kupinga matokeo ya urais lakini unaweza kupinga matokeo ya Ubunge. Hapo kwanza ni ukiukwaji wa Katiba katika kutafuta haki -- na wanasheria waliangalie hili kwa namna ya kulipeleka mahakamani.

Pili hapa kuna haraka ya zima moto ya kumuapisha mshindi wa urais -- wakati wenzetu kwingine hakuna haraka hiyo -- na wao hufanya hivyo ili kutoa fursa kwa asiyeridhika kwenda mahakamani.

Katika chaguzi, huwezi kulinganisha uhuni wa hapa na ustaarabu wa nchi zingine.
 
ni lazima Obama ayaseme hayo, kwanzu tume ya uchaguzi si ya serikali na yeye hawezi kutia pua yake huko(tume), lakini hapa Tz utamsikia Jk akiiipongeza tume yake aliyoichagua(what a shame)m ulimwenguni kote computer ni chombo cha kurahisisha kazi lakini kwa NEC TZ the opposite is true, imani kwa wannchi imepotea ndo maana watu wanaweza kulala nje wakilinda kura ama kweli peoples pwr :hippie:
 
Huko kote ni kuheshimu mfumo mzima wa demokrasia. Kuanza kuchakachua kura na uwezo wa kufanya hivyo ni uthibitisho tosha kuwa viongozi waliopo madarakani ndio wanaotengeneza mfumo huo mbovu na kutuhadaa. Maana yangu ni kwamba kama kuna mtu anafikiria Tanzania kuna haki na demokrasia, au mfumo tulionao utatuletea maendeleo afikirie zaidi ya mara moja. Na wale wanaoshabikia mfumo wetu nawafananisha na mbu aliyefikiri anapigiwa makofi kumbe anawindwa
 
Nyerere - Baba wa Taifa
Mwinyi - Mzee Ruksa
Mkapa uwazi na ukweli
KIwete- Fisadi wa nchi na Fisadi wa kura... poor you sijui unajisikiaje unapotawala watu wanaojua wewe ni mwizi wa kutupaaa?? tulikupiga mawe.tukakuzomea, kwa sasa tutakushoot tu! miaka mitano na mganga wako yuko mbioni kuelekea ahera tutaona ......
usitembelee huku kwetu .................
tutakumaliza,
 
Huko kote ni kuheshimu mfumo mzima wa demokrasia. Kuanza kuchakachua kura na uwezo wa kufanya hivyo ni uthibitisho tosha kuwa viongozi waliopo madarakani ndio wanaotengeneza mfumo huo mbovu na kutuhadaa. Maana yangu ni kwamba kama kunaa mtu anafikiria Tanzania kuna haki na demokrasia, au mfumo tulionao utatuletea maendeleo afikirie zaidi ya mara moja. Na wale wanaoshabikia mfumo wetu nawafananisha na mbu aliyefikiri anapigiwa makofi kumbe anawindwa

nani alikuambia TZ kuna demokrasia, ni uongo wa CCm kusema kuna demokrasia utulivu na amani au TZ ni kisiwa cha amani, ukweli ni kwamba hata kwenye nchi 15 zenye demokrasia na utawal bora tz haipo, nafikiri una mfahamu Ibrahim MO, katika ranking ambazo kazitoa mwezi uliopita Tz haipo katika nchi 15 za afrika zenye demokrasia na utawala bora, kama unakumbuka Chisano alimbwaga mkapa kwa viongozi marais waadlifu kutoka afrika, leo tunadangannywa kuwa kuna demokrasia, in fact kuwa na demokrasia ni pamoja na kuwa na tume huru ya uchaguzi among other things:yield:
 
nani alikuambia TZ kuna demokrasia, ni uongo wa CCm kusema kuna demokrasia utulivu na amani au TZ ni kisiwa cha amani, ukweli ni kwamba hata kwenye nchi 15 zenye demokrasia na utawal bora tz haipo, nafikiri una mfahamu Ibrahim MO, katika ranking ambazo kazitoa mwezi uliopita Tz haipo katika nchi 15 za afrika zenye demokrasia na utawala bora, kama unakumbuka Chisano alimbwaga mkapa kwa viongozi marais waadlifu kutoka afrika, leo tunadangannywa kuwa kuna demokrasia, in fact kuwa na demokrasia ni pamoja na kuwa na tume huru ya uchaguzi among other things:yield:

Mkuu kama umenisoma hapo namaanisha Marekani ndiko kwenye demokrasia
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom