mi_mdau
JF-Expert Member
- Oct 29, 2010
- 1,088
- 1,393
Ni bahati nzuri kuwa uchaguzi wetu hapa Tz umefanyika karibu kipindi sawa na ule wa nusu muhula (mid-term) wa marekani. Ni ukweli usiopingika kuwa umaarufu wa Barack Obama umeshuka na hivyo chama chake kupoteza viti vingi na nguvu ya utawala kwenye bunge nchini humo. Lakini Barack Obama hajakataa kushindwa kwa chama chake, ingawa imemuuma na ameona ni changamoto(He called the election a Democratic "shellacking" and lamented that "we lost track of the ways we connected with the folks who got us here in the first place." ) na kusema kuwa atatilia mkazo kukuza uchumi na ajira kipindi hiki kilichobaki. Aliendea kusema kuwa amethibitisha alichosikia toka kwa wapiga kura nchi nzima, watu wamefadhaishwa, (kama ni kiswahili sahihi)((Obama said Tuesday's results confirmed what he's heard from voters across the country: People are frustrated. He said the lesson of election was that he hasn't made enough progress in creating jobs). Jambo kuu hapa ni kuwa amekubali kushindwa kwa misingi ya kidemokrasia, ile iliyomuweka yeye madarakani kwa kishindo. Huu ni mfano mzuri toka kwa taifa lilioendelea ambalo tumekuwa tukienda kila siku kuomba misaada toka kwao. Swali ni Je, viongozi wetu wamefanya hili uchaguzi huu kutokana na matukio yanayotokana na matokeo ya kura yanayoendelea kutangazwa? Sidhani... Kwa nini hatuamini kuwa Rais anaweza asipendwe tena kama mwanzo? Kwa nini mawakala wa upinzani wanakuwa macho kulinda kura zao? Ni ishara kuwa waliopo madarakani hawataki kushindwa kwa haki! Kwa nini tusikubali kuwa wananchi walioelimika na wenye ufahamu wa ushindani wa demokrasia hawatukubali tena kama hapo awali? Tafakari, chukua hatua..