white wizard
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 8,307
- 13,269
Wakulima poleni sana, jitihada zenu zinakwamishwa na mfumo wa kifisadi uliopo nchini na hawana nia nzuri na nyie. Haiwezekani mtu anajipinda kulima kwa muda mrefu anakwenda kununua anapewa mbolea iliyochanganywa na majivu, matokeo yake haambulii chochote! jamani mwogopeni Mungu, kuna mbolea tani elfu moja imekamatwa leo katika ghala moja huko wilayani Mbozi na mkurugenzi wa kitengo cha ukaguzi wa ubora wa mbolea, na wanachofanya eti ni kumnyang'anya leseni! tu kweli hii ni adhabu tosha? wakiwa jukwaani ohoo kilimo kwanza kwa staili hii! nchi hii tumelogwa na nani jamani? waziri Malima anasema hayupo ofisinI hawezi kulizungumzia kwani hana uhakika nalo!
source.TBC taifa.
source.TBC taifa.