Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,955
- 22,135
KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu leo inakutana na Waziri wa Miundombinu, Profesa Shukuru Kawambwa, kupata taarifa za utendaji wa kampuni za Reli (TRL) na Ndege (ATCL).
Kulingana na ratiba ya Kamati hiyo ambayo tangu ianze vikao chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango-Malecela, kikao na Waziri kitafanyika kabla ya majumuisho ya miswada na kukamilisha maoni ya Kamati.
Kikao hicho kinafanyika Dar es Salaam ukiwa ni mfululizo wa vikao vya kamati za kudumu za Bunge, huku kukiwa na mkanganyiko kutokana na kauli mbili tofauti zilizotolewa wiki iliyopita juu ya uvunjaji wa mkataba kati ya Serikali na Kampuni ya Rites inayoendesha TRL.
Wiki iliyopita, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Omari Chambo, aliiambia Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC) kwamba mkataba huo utavunjwa mwezi ujao, baadaye Waziri Kawambwa akakaririwa na baadhi ya vyombo vya habari, akisema mchakato unaendelea na haijafahamika ni lini utavunjwa.
Uendeshaji wa TRL inayotoa huduma katika Reli ya Kati, umegubikwa na migogoro ya mara kwa mara kati ya menejimenti na wafanyakazi.
Alipokuwa akitoa taarifa kwa PAC, Chambo aliweka bayana kwamba migogoro inayoikabili kampuni hiyo inatokana na uongozi mbovu wa Rites ya India, yenye hisa 51 TRL.
Vilevile utendaji wa kampuni hiyo umekuwa ukinyooshewa vidole na watu mbalimbali hususan watumiaji wa reli hiyo, kutokana na kushindwa kuboresha huduma. Mambo hayo yanatarajiwa kuhojiwa na wabunge ikiwamo hatma ya mkataba.
Kuhusu ATCL, Kamati ya PAC iliambiwa kwamba wanaendelea kutafuta mbia atakayeiendesha.
Kulingana na ratiba ya Kamati hiyo ambayo tangu ianze vikao chini ya uenyekiti wa Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango-Malecela, kikao na Waziri kitafanyika kabla ya majumuisho ya miswada na kukamilisha maoni ya Kamati.
Kikao hicho kinafanyika Dar es Salaam ukiwa ni mfululizo wa vikao vya kamati za kudumu za Bunge, huku kukiwa na mkanganyiko kutokana na kauli mbili tofauti zilizotolewa wiki iliyopita juu ya uvunjaji wa mkataba kati ya Serikali na Kampuni ya Rites inayoendesha TRL.
Wiki iliyopita, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Omari Chambo, aliiambia Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC) kwamba mkataba huo utavunjwa mwezi ujao, baadaye Waziri Kawambwa akakaririwa na baadhi ya vyombo vya habari, akisema mchakato unaendelea na haijafahamika ni lini utavunjwa.
Uendeshaji wa TRL inayotoa huduma katika Reli ya Kati, umegubikwa na migogoro ya mara kwa mara kati ya menejimenti na wafanyakazi.
Alipokuwa akitoa taarifa kwa PAC, Chambo aliweka bayana kwamba migogoro inayoikabili kampuni hiyo inatokana na uongozi mbovu wa Rites ya India, yenye hisa 51 TRL.
Vilevile utendaji wa kampuni hiyo umekuwa ukinyooshewa vidole na watu mbalimbali hususan watumiaji wa reli hiyo, kutokana na kushindwa kuboresha huduma. Mambo hayo yanatarajiwa kuhojiwa na wabunge ikiwamo hatma ya mkataba.
Kuhusu ATCL, Kamati ya PAC iliambiwa kwamba wanaendelea kutafuta mbia atakayeiendesha.