Ibrah
JF-Expert Member
- Mar 22, 2007
- 2,729
- 528
Mwaka 2005, Mgombea wa CCM Jakaya Kikwete alituchota sana na kauli mbiu ya Maisha Bora kwa Kila Mtanzania hadi tukampa kura za ushindi wa kishindo. KIlichofuatia baada ya hapo ni kwa Watanzania wengi kukata tamaa ya hayo maisha bora kiasi cha kuwauliza Viongozi wetu mbona maisha bora hatuyaoni? Tukapewa majibu mepesi kweli kweli atri Maisha bora hayaji hivi hivi bila kufanya kazi kwa bidii! Wafanyakazi wamejitahidi kudai hata kwa kutumia nguvu za TUCTA lakini wapi.
Umefika mwaka 2010, ile kauli mbiu ya Miasha Bora kwa Kila Mtanzania hatuisikii tena, hata yale mabango ya kumnadi Kikwete mwaka huu hayana ile kauli mbiu ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania; sijui wamesahau kuiweka au wanaogopa kuulizwa kwenye mikutano yao ya kampeni, wanajua wao wenyewe. Ajabu ni kuwa hata kwenye mikutano yao ya Kampeni Wananchi hawawaulizi au kuwakumbusha juu ya kauli mbiu ya Maisha Bora. Si ajabu ndo maana CCM wamekacha midahalo.
Kwa wale wanaohudhuria mikutano ya CCM ya KAmpeni muwakumbushe na kuwauliza ile Kauli mbiu ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania imeishia wapi?
Umefika mwaka 2010, ile kauli mbiu ya Miasha Bora kwa Kila Mtanzania hatuisikii tena, hata yale mabango ya kumnadi Kikwete mwaka huu hayana ile kauli mbiu ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania; sijui wamesahau kuiweka au wanaogopa kuulizwa kwenye mikutano yao ya kampeni, wanajua wao wenyewe. Ajabu ni kuwa hata kwenye mikutano yao ya Kampeni Wananchi hawawaulizi au kuwakumbusha juu ya kauli mbiu ya Maisha Bora. Si ajabu ndo maana CCM wamekacha midahalo.
Kwa wale wanaohudhuria mikutano ya CCM ya KAmpeni muwakumbushe na kuwauliza ile Kauli mbiu ya Maisha Bora kwa kila Mtanzania imeishia wapi?