Ngisibara
JF-Expert Member
- Jan 2, 2009
- 3,301
- 2,076
Kutokana na uzoefu tulioona katika uchaguzi wa 2005 na chaguzi ndogo zilizopita ni wazi kuwa CCM hushinda kwa uwizi, ujanjajanja wa mabox ya kura au kula njama na mawakala uchwala wenye njaa kali ambao hujifanya ni wakereketwa wa Chadema kumbe wao huomba uwakala ili tu wapate mshiko kutoka Chadema, hebu angalia kule Busanda mawakala walivyouza chama kwa kusaini ripoti mbili na kuishia porini, Hivyo wakereketwa wa Chadema mliopata bahati ya kuwa mawakala au kuwa na rafiki zenu wanaojua mbinu hizo hebu tujadili ni zipi? na ni jinsi gani tufanye kudhibiti upuuzi huu wa CCM, Mwaka huu kuna dalili nzuri kabisa kuwa majimbo mengi yataenda Chadema lakini mafisi haya yalivyo na njaa kali safari hii siamini kabisa kama tutapona na tayari tumejionea jinsi walivyokulana wao kwa wao kwenye kura za maoni bila chembe ya aibu, labda mie nianze kwa kusema kuwa kuanzia wakati huu Mawakala wawe screened uaminifu wao kwa chama halafu itakapofika wakati tusiokoteze okoteze mitaani kama dharula, tuwe nao tayari na tuwawezeshe katika kipindi chote cha kupiga kura na kuhesabu, na pia wawe wanacommunicate na viongozi mara kwa mara kujulisha nini kinaendelea na kama kuna tatizo basi wasaidiwe haraka kwani hili linawezekana kwa kutumia simu za kiganjani zipo nyingi siku hizi......nawasilisha tuchangie ndugu zangu wa Chadema tu na si vinginevyo