Mbinu chafu za serikali kuficha ukweli juu ya Dr. Ulimboka

Whether it is a theory or not, your explication is somewhat bound to survive scrutiny. In fact, in such circumstances as the current Ulimboka incident, any kind of a well-presented hypothesis may easily be mistaken for a fact and is likely to strike the mind of a relatively credulous person. At any rate, I must acknowledge that your exposition--whether credible or not--is, without doubt, remarkably meticulously gathered and extremely superbly presented.

Komenti hii kiboko. Wapatie watu kwa kiswahili
 
Where did u get this secret story kama na wewe haumo?

Nafikiri jina lako linaeleza jinsi ulivyo, na mara nyingi mtu mwenye njaa huwa hamalizi kusoma taarifa yote, na akimaliza, basi kazi ya kufikiria huwa haipo kwake.

Soma mstari wa mwisho kabisa utapata jibu la swali lako.
 
Hizi ni Tuhuma nzito lakini itapendeza kama chanzo chake sio mambo ya siasa bali ukweli.

chanzo chako lazima kiwe karibu sana na waliohusika na kadhia hii ama serikalini au kutoka vyombo unavyovituhumu....yamkini wewe ni mmoja wao uliosaliti

Ukisoma habari hii vizuri, na kama unaelewa 'ufahamu' au 'comprehension' katika taaluma ya lugha ni kuwa mwandishi ameeleza wmishoni kuwa "si wote serikalini ambao wamefurahishwa na jambo hili (la kuficha ukweli juu ya Dr. Ulimboka)". Kutokana na kwamba si wote ambao wanaojua njama hizi wamefurahishwa nalo, ndio maana baadhi yao au mmoja wao, ameamua kuuambia umma ukweli.
 
Kwa wale wanaombeza mwanzilishi wa thread hii wakumbuke ya kwamba hapa Afrika mambo kama haya yamefanywa sana. Tanzania enzi za Mwalimu tulikuwa mstari wa mbele kuyakemea yalipotokea Uganda enzi za Idi Amin Dada. Ni jambo la kusikitisha sana kuyaona yanatokea nchini mwetu. Lakini kama ambavyo serikali zote za kidhalimu zilifikia ukingoni, viongozi wa serikali yetu ya 'kidhalimu' waelewe ya kwamba mwisho wao umekaribia. Tunakuombea Dr. Ulimboka mkono wa Mungu usimame juu yako na ukweli ujulikane.

Mungu Ibariki Tanzania!
 
Naona hili swala limefanywa kuwa la kisiasa zaidi. Serikali haiwezi kumteka na kumtesa Ulimboka adharani watu wakishuhudia mbaya zaidi mbele ya rafiki yake. Wanaodhani serikali inahusika watakuwa hawana ueleo wa idara za usalama zinavyofanya kazi. jamani serikali ikukutaka wala haikuteki mbele za watu na wala hawakutesi bali wanamaliza tu maramoja.

Huyu jamaa naona kaandika mawazo yake binafsi ili afurahishe genge tu kwa utashi wake wa kisiasa. Msione usalama wako kimya wanafuatilia wote wanaoipaka matope.
 
Ukwaju hajielewi kaa kimya, anadhani sisi ni watu wa mambo ya mwaka 47,
naomba hii habari isambazwe kwa wanafunzi wa primary na sekondari ili wao na vizazi vyao waichukie serikali hii ya kigaidi ya ccm.
Hivi hawa watu wanaabudu kweli, au wanazuzuliwa na ela, hawa ni wanyama kabisa, mambwa tu, nazidi kumshangaa askofu mmoja aloghafilika akadai ati jk ni chaguo la mungu, pole baba askofu sijui ulivutiwa na nini, nimeogopa sana
 
Naona hili swala limefanywa kuwa la kisiasa zaidi. Serikali haiwezi kumteka na kumtesa Ulimboka adharani watu wakishuhudia mbaya zaidi mbele ya rafiki yake. Wanaodhani serikali inahusika watakuwa hawana ueleo wa idara za usalama zinavyofanya kazi. jamani serikali ikukutaka wala haikuteki mbele za watu na wala hawakutesi bali wanamaliza tu maramoja.

Huyu jamaa naona kaandika mawazo yake binafsi ili afurahishe genge tu kwa utashi wake wa kisiasa. Msione usalama wako kimya wanafuatilia wote wanaoipaka matope.

Unavyosema ni sawa kabisa ila kwa serikali DHAIFU kama hii yawezekana
 
mzee wa njaa umesema kweli, mana wengine humu mnatujaza upepo tu!!!hizo information zote umezipata wapi au unataka kuleta mambo ya movies hapa!!toa point za kweli na zionekane za kweli na siyo utunzi kama hadithi!
 
Kamanda Kova nakuheshimu sana lakini kwa kuunda tume inayomshirikisha mtu anayehusika ni ukosefu wa uzalendo kwa nchi yenye serikali dhaifu kama hii
 
Kuna mbinu chafu zinapangwa katika kuficha ukweli wa kile kilichotokea kwa dr. Ulimboka. Mbinu hizi zinalenga kuficha maovu yaliyofanywa na serikali kwa dr ulimboka na hivyo kuisafisha serikali ili ionekane kuwa haihusiki na unyama huu.

Mtu aliyekuwa anajitambulsha kwa dr. Ulimboka na kuwa na mawasilinao nae kwa mda mrefu akitumia jina la Abduel (si jina lake halisi na wengine humuita abedi) alikabidhiwa kazi ya kumfatilia dr ulimboka siku mbili baada ya waziri mkuu pinda kwenda kuonana na madaktari pale Muhimbili. Kitu cha kwanza alichofanya ni kujiweka karibu na ulimboka katika kuzungumzia matatizo yao lakini pia huyu jamaa alikuwa link kati ya ulimboka na serikali. Katika kipindi chote hicho mwanausalama huyu likuwa akimfatilia ulimboka ili kumjua kwa undani zaidi.

Baada ya kuona msimamo wa dr ulimboka juu ya swala hili la madaktari hautetereki na habadiri msimamo wake maana walishataka kumpatia pesa ili anyamaze ; ndipo sasa maandalizi ya kumnyamazisha kwa kutumia formula ya ’’ maiti haisemi’’ yalianza. Lengo lilikuwa ni kumuua kabisa na hiyo juzi walidhani wamemuua.wazo la kumnyamazisha jumla ulimboka halikutoka kwa huyo mwana usalama bali nae alipokea maelezo toka juu kwa watawala. Mpango wa kutekwa ulimboka ulipangwa na kitengo anachofanyia kazi mwana usalama huyo na kutekelezwa na maafisa wapolisi waliokabidhiwa jukumu hilo.

MBINU CHAFU
Baada ya kufanikiwa kumteka na kumpiga vibaya dr ulimboka na hatimae kumtupa huko msitu wa pande huku wakidhani tayari adhma imetimia ya kumtoa uhai sasa serikali dhaifu imepanga mipango michafu ili kujisafisha ili isionekane kuwa imehusika na unyama huu.


1. Abduel amesafirishwa na kuondolewa nchini Tanzania usiku wa tarehe 27 kwa kupita Nairobi na baadae ataelekea kwenye ubalozi wa afrika ya kusini atakapopangiwa majukumu mengine. Hii yote ni katika kuficha ukweli . hao maafisa wa polisi watano waliomteka ulimboka wapo nchini na mmoja amewekwa kwenye tume ya kuchunguza utekwaji nyara wake iliyoundwa na kova nahii imefanywa makusudi kwa malengo flani; wanne waliobaki wamesambazwa kwenda mikoan na hawapo dar.


2. Kamanda wa polisi kova ameelekezwa KUHAKIKISHA anailinda serikali katika jambo hili na afanye awezalo kuonyesha umma wawatanzia kuwa serikali haihusiki na jambo hili.katika kuficha na kuilinda serikali kova, mwema na maafisa wa wajuu wa usalama wa taifa walishauliana ili kuilinda serikali na kadhia hii mahabusu 5 wenye makosa ya ujambazi wanahitajika kutoka katika magereza yaliyopo mwanza, songea, tabora, tanga na kigoma waletwe dar ili hao waweze kuonyeshwa kwenye vyombo ya habari kuwa ni majambazi yaliyomteka ulimboka na kumpiga. wakishapatikana wataonyeshwa kwenye vyombo vya habari na umma wa watanzania utaambiwa kuwa wale ndio walifanya unyama huo wako chini ya ulinzi na kuwa maohojiano yanaelendelea na uchunguzi ukikamilika watapelekwa mahakamani na hapo ndipo utakuwa mwisho wa mchezo.
3. mbinu nyingine ni kuwa mahabusu hao wasafirishwe hadi pwani na wauwawe wote na taarifa itoke kuwa ndio waliomteka dr ulimboka na wamekamatwa wakiwa mkoa wa pwani katika msako mkali wa jeshi la polisi. Na katika kujibizana risasi polis ilifanikiwa kuwaua majambazi hayo. Na hapo ndo itakuwa mwisho wa swala hili na serikali itakuwa imenawa mikono na kujisafisha

Kwa sasa kinachofanyika ni kuwasiliana na magereza husika ili kila gereza litoe mtu mmoja (mahabusu) atakayesafirishwa hadi dar/pwani na wataunganishwa kisha kuonyeshwa kwenye vyombo vya habari wakiwa hai au maiti ili kuuaminisha umma kuwa wao ndio walimvamia dr.ulimboka
Upelelezi na uchunguzi unaofanyika sasa ni changa la macho kwa watanznai na hiyo tume aliyoiunda kova nayo ni changa la macho ,na kama ulimboka alifanikiwa kuwaona vizuri na kuzishika sura zao ,mmoja wao yupo katika kamati hiyo. hakuna uchunguzi wowote utakaofanyika wenye tija kwa taifa juu ya kilichotokea.Kamanda Kova anasimamia operation hii na ameambiwa HAKIKISHA serikali inasafishika.

Mazingira yote yanayoihusisha serikali kwa watu wake kufanya ushenzi kuna jitihada kubwa inafanyika ili kufuta dhana hiyo. Si maraya kwanza kwa serikali kuua watu inaowaona ni mwiba kwake. Wapo wengi na wengi wamezikwa kwenye msitu huo wa pande, kuna msitu uko kibaha(kama uamzi wa kuwaua mahabusu utakubaliwa basi watauliwa kwenye msitu huo) na wengine hutupwa baharini .
Kusamilika kwa ulimboka ni kuwa Mungu ana mpango nae na serikali inafanya kila linalowezekana kujinasua. si wote serikalini wamefurahishwa na kilichotokea wengine wamechukia tena sana

Well done! endelea kutuhabarisha. Mwisho wa uovu aibu. Hata wanaoifagilia serikali kwa kusema uongo wanakesi ya kuibu, kama ambavyo serikali hiyohiyo ilivyo na kesi ya kujibu kwa kufuga mafisadi na kuumiza wanyonge kwa kuwachonganisha. Kinachofanyika sasa hivi ni kuwachonganisha madaktari na wanainci, lakini wananchi wenye hekima wanaelewa kinachoendelea, wale walionyimwa hekima na kwa bahati mbaya ni wengi, wako usingizini. Waache walale, wengine ni wafu wanaotembea.
Siri nje! alal-lubadil itamfuata hata chini ya bahari. Hawezi kukimbia mkono huo! Pole kwa mkewe na watoto, kazi yake ya kipumbavu akiyoichagua itamfanya mkimbizi. Mungu ana makusudi yake, tusubiri tuone. Hata Misri ilianza hivi hivi, jiandaeni kufungasha vibaraka wa sindbad na beast
 
Ahsante sana kwa taarifa de'levis kwa moyo wako wa uzalendo Mungu atakusimamia ,Ili mradi waandishi nao ni wana JF watumie hii taarifa kuwaumbua serikali wawapigie simu wawaulize huo mpango wao wa kuuendelea kuua wananchi wasio na hatia

De`levis tunashukuru kwa taarifa nzuri sana , nashangaa kwanini watanzania na wapenda haki wanasubiri nini kuiondoa hii serikali hata kwa nguvu kuepusha laana inayokwenda kulikumba Taifa maana tutaumia wote tukisubiri hadi Mungu aingilie kati
 
Ni vigumu kutoiamini post hii, kwa jinsi mfumo wa maisha nchini mwetu kwa sasa usivyo onyesha uwepo wa nia ya serikali kuboresha huduma kwa wananchi... Hii ndo 'liwalo na liwe'
 
Ninasikia Mkuu leo amewa summon Baraza la usalama wa Taifa, anataka maelezo ya kina kwanini mpango wa kumuua Dr. Ulimboka uli fail?

Hata wakitumia hiyo mbinu ya kuleta majambazi kutoka magereza sura ya Abeid Ofisa usalama wa IKULU inafahamika kwa madaktari wengi walioko kwenye timu ya majadiliano including Dr. Deo. Huyo Askari aliyewekwa na Kova kwenye tume tunamjua kwa jina na sura Hemedi Msangi.

Ninakwambia kwa hili serikali imekula kwao. The last option walionayo serikali wataanza kuwauwa wote waliotumwa na kushindwa kuafanikisha operation hiyo akina Abeid, Hemedi Msangi na askari hao wengine wanne. Serikali imekuwa ya kigaidi.

Ninasema huu ni mwanzo wa mwisho. haiwezekani kuendesha nchi kwa damu za watu hata kidogo. Watanzania hao wawapigie kura ili wangie madarakani, watanzania haohao wauwawe kwa ajili ya wakuu wa nchi kuingia kwenye mikataba ya kuzimu, watanzania haohao wadhulumiwe ardhi, maliasili zao kwa ulafi wa waliowaingiza madarakani, watanzania haohao waishi maisha ya dhiki yasiyo na matumaini kwa ajili ya waroho wachache, watanzania haohao wafe njaa kutokana na hali mbaya ya maisha iliyosababishwa na waliowapigia kura, watanzania hao hao wanapodai haki zao haki zao wauwawe!! hiki ni kizazi cha nyoka!!!!! They must go, they are no longer human beings but devils.
 
Naona hili swala limefanywa kuwa la kisiasa zaidi. Serikali haiwezi kumteka na kumtesa Ulimboka adharani watu wakishuhudia mbaya zaidi mbele ya rafiki yake. Wanaodhani serikali inahusika watakuwa hawana ueleo wa idara za usalama zinavyofanya kazi. jamani serikali ikukutaka wala haikuteki mbele za watu na wala hawakutesi bali wanamaliza tu maramoja.

Huyu jamaa naona kaandika mawazo yake binafsi ili afurahishe genge tu kwa utashi wake wa kisiasa. Msione usalama wako kimya wanafuatilia wote wanaoipaka matope.
kama jf imewapaka matope! basi wananchi wataongezea masizi! kwa kifupi kama na we ni mmoja wapo, kawaambie TUMECHOKA, NA HATUWAOGOPI TENA! Mmoja tu alianzishe tutaingia kama nyuki! WE ARE TIRED!
 
Back
Top Bottom