Mbinguni kuzuri bwana..

TheChoji

JF-Expert Member
Apr 14, 2009
4,966
15,268
"...unaambiwa mbinguni ni noma. Kwanza kule si kama huku, hali ya hewa ya kule ni ka ubaridi fulani yani kuna ka upepo mwanana muda wote. Mazingira ya kule ndio kabisaaa... kila mahali ni ukoka, miti ya kivuli na miashoki kila kona. Barabara za kule ni kama sakafu maana hazina makorongo wala nini na hakuna bamsi. Kule dabo rodi zao za ukweli.. Ma flai ova ya kule, we acha mchezo, hakuna foleni wala nini mwendo mdundo spidi mia ishirini. Ma skai skrepa gorofa mia sita na ushee.. unafanya masihara?
Kule huwezi kukuta vigari mikweche kama huku.. ni ma latesti modo, unaambiwa ma posh kayene, ma doji kaliba, ma bima eksi siksi, ma vogi, ee? ma eskaledi, ma jiiemsii ya ukweli, ma vii dabliyuu tuaregi.. e bwana e. Watu mnagawiwa bure unachagua tu unalotaka.
...Mbinguni kuna ma supamaketi si ya kitoto.. ma shopingi moli ya kule aibuu! kila kitu mazagazaga yote unapata frii.. ma butik ya hatari pamba za kufa mtu unajichagulia tu. Kule unaruhusiwa kuvaa vyovyote.. ukiamua kupiga kadeti, jinzi kali, tisheti na bodi taiti nini.. suti za madizaina kibao tu..pensi za ukweli, shati kalikali zipo tele.. Ma hea saluni, ma baba shopu ya hatari mtu unagonga ma wevu, ma loo kati, ..
Kule huwezi kuta mtu anatumia simu ya kichina.. mwendo ni ma blakiberi, ma soni eriksoni, ma samsang galaksi, ma aifoni foo, ma nokia eni naini, ma lumia, ma hechi tii sii, yaani eti umkute mtu ana li deski topu? waapi... kule sanasana ni vi epo mini laputopu na vi ai padi ndio vimetawala. Mwendo wa tachi skrini kwa sana yani.. wayalesi netiweki kila mahali, hai spidi intaneti unadaunlodi tu ma muvi, ma siriz na ma em pii thirii bureeee... Ukizingatia hadi diski zinaanzia ma terabaiti ya kutosha.. flashi diski kule ndogo kabisa ni jibii mia nane!
Kule ma sosho netiweki ni kibao yani watu ni fulu kukomyuniketi kwa ma video komferensi.. Tivii za kule ni flati skrini nchi stini na kuendelea.. kitu thrii dii. Unazani kule kuna sijui kebo, sijui ving'amuzi? vya nini? kule antena za ndani tu unashika chaneli zaidi ya buku mbilli.. Unacheki tu mamechi na mavipindi ya ukweli.. ma big braza, ma toku shoo, ma zis wiki ini pasipektivu, ma laivu kavareji, we acha kabisa..
Viwanja vya kule sasa ni balaa.. Klabu si za kitoto vitu fulu saundi prufu, ngoma mpya mpya tu ndio huwa zinapigwa.. ma swimingi puli yani watu wanajiachia kinoma.. Ma muvi thieta, ma koti ya basketi kila mtaa, ma softi drinks, ma aisi krimu, ma chokoleti... ma vinywaji ya kumwaga ukitaka ma waini, ma shampein, ma vodka, sijui ma tikila, yamejaa halafu yote ni ma nan alikoholik yani.. sio viroba kama huku... Ma babakyu ya ukweli ukitaka ma poku, ma bifu, ma chikeni, ma soseji.. duh"
Mi lazma nifanye mpango nizame
 
Mbinguni ya kwa shetani hiyo na wala si ya Mungu Muumba wa mbingu na nchi na bahari.
 
...unaambiwa madakitari wa kule hawagomi wala nini.. kwanza hospitali za kule mavifaa ya kumwaga hadi ma dispensari ya kule yana ma eksi ree, ma ultra saundi, ma sii tii skani kama uchafu.. Mshahara wa dakitari kule ni kitu kama em kumi hapo hujahesabu ma hauzingi alawansi, ma transpoti alawansi, ee? ma pa diiemu, ma ovataimu, ma weiva kibaaaao!
 
Dah kazi ipo

Ushaona eh? kule ma jei efu memba hawa haidi aidii zao, kule ni ma rili nemu yanatumika. Ma modz wa kule hawapigagi watu bani wala nini, yani fulu raha mwanawane.. mambo ya ma friidomu ovu eksipresheni...
 
Kweli kabisa, nakubaliana..........

 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom