Mbeya nako! Mibalaa mipya kila kukicha

Kana-Ka-Nsungu

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
2,257
353
Ajali zote mbaya na zilizochukua maisha ya watu wengi mwaka huu zimetokea Mbeya.Lakini wakazi wa Mkoa huo nao kila kukicha wanaamka na balaa jipya, imani za ushirikina na watu kutaka utajiri bila kufanya kazi zinawafanya waendelee kutoana roho.

Juzi tena nimefanikiwa kukutana na mdau mmoja wa Mbeya ambaye pamoja na kunikumbushia enzi zile za watu kuchunwa ngozi na wenye vipara kukatwa vichwa pia amenipa mpya mbili ambazo zimeniacha kinywa wazi.

Inayotamba sasa hivi inaitwa "NONDO"- watu wenye imani za kishirikina, katika harakati zao za kusaka utajiri, wanatumia vipande vya nondo kuua binadamu wenzao then kipande cha nondo kilichotumika kinapelekwa kwa 'mtaalamu', kinachoendelea huko wanajua wenyewe.

Kali nyingine ni watu kuuwawa na kutolewa mioyo. Kuna imani kuwa yupo samaki mmoja mkubwa sana ambaye anaishi chini kabisa ya bahari, inasemekana samaki huyu ana madini ya thamani sana tumboni mwake, hupenda mioyo ya watu kwa chakula, ndo maana basi watu wanaitumia mioyo hiyo kama chambo cha kumuwinda samaki huyo.

Chanzo changu cha habari kilinijulisha pia kwamba waganga wengi wa kienyeji wanaowachuuza watu kufanya ukatili huu sio wa mkoani hapo bali wako kwenye nchi jirani za Malawi, Zambia na Kongo.

Je una ufahamu zaidi juu ya habari hizi? Umewahi kusikia lolote kuhusu haya?
 
balaa hili, du walah.
nilikuwa nina mpango wa kwenda mbeya ila nahairisha mpaka nipate wigi la kufunika upara wangu
 
KanaKansungu,
Naona hapo kuna habari/hoja mbili au tatu tofauti, zikitenganishwa miye naona itakuwa rahisi kuziongelea kwa kina zaidi. Kuna za ushirikina na ajali, lakini pia kuna hiyo ambayo inataja Mbeya kama pahala pa hayo yote..

Kwa vile umeuliza maswali hapo chini kuhusiana na mawili , miye natoa jibu kuwa - sijawahi kusikia hayo ya bahari, ila kutokana na imani zetu na mazingira yetu, kuwepo kwa mambo hayo mawili ya ushirikina na ajali hakupingiki, kwani jamii tunayoishi yote yamo.


SteveD.
 
KanaKansungu,
Naona hapo kuna habari/hoja mbili au tatu tofauti, zikitenganishwa miye naona itakuwa rahisi kuziongelea kwa kina zaidi. Kuna za ushirikina na ajali, lakini pia kuna hiyo ambayo inataja Mbeya kama pahala pa hayo yote..

Watu wengi sana wamepoteza maisha yao kwa ajali za barabarani (au sijui niseme na anga?) na nilitarajia kwa sababu hii wangekua wanaonea huruma kidogo na kuacha kutoana roho kwa sababu za kijinga.
 
Back
Top Bottom