funzadume
JF-Expert Member
- Jan 28, 2010
- 13,559
- 21,040
Kwa wale wenzangu na mie wanandoa kuna ile hali kipindi cha uchumba na kipindi cha ndoa kabla ya kupata watoto na kuwa na wafanyakazi ndani ya nyumba kuna zile za kukumbatiana au kupigana mabusu, kulaliana kwenye makochi mkiangalia TV na vimbwanga vingine vya kimahaba vinavyofanyika nje ya chumba mfano sebuleni, jikoni na sehemu nyingine.
Je mkipata watoto inabidi vitu vile mviache na kuvifanya chumbani tu ambako kwa kawaida hamshindi huko muda mrefu au viendelee tu mbele ya watoto?
Je mkipata watoto inabidi vitu vile mviache na kuvifanya chumbani tu ambako kwa kawaida hamshindi huko muda mrefu au viendelee tu mbele ya watoto?