Mbatia si mpinzani

Chilipamwao

JF-Expert Member
Nov 15, 2010
523
128
Katika mambo mbalimbali kuna ukweli wa aina mbili TRUTH na FACT. Kwa Mbatia Truth ni kwamba si mpinzani ila Fact ni mpinzani. Vyama tawala hasa nchi za ulimwengu wa tatu huweka vyama mamluki na kuweka viongozi kama mbatia kwa kazi maalum.

Mbatia alipishana na misimamo mingi ya Kafulila ambayo kila mtu ama aliyeisikia ama kuiona katika Televisheni atakubaliana nami kuwa ina-reflect mpinzani halisi.

Rai yangu ni kila anayetaka CCM iondoke madarakani 2015 ni muhimu tumwonyeshe Mbatia kuwa tunampuuza na tunamjua kuwa ni mamluki.
 
Mbatia is very intellectual! aliwateka akili wajumbe wakamfanya Kafulila miguu juu!
 
Ni mpinzani katika chama chake cha NCCR, na si mpinzani katika kutafuta demokrasia ya kweli nchini mwetu. Kumbukeni sakata lake huko Kawe ndo mtaujua ukweli. Pia ujue aliachiwa na nani madaraka katika NCCR, aliachiwa na mheshimiwa Lyatonga Mrema Augustino wa TLP kachero mkubwa wa CCM maana ni mwanachama hai. Kazi yake ndo hiyo na anaweka huku na huku kwa maslahi ya CCM ndo maana watawala wakakataa kambi rasmi ya upinzani mwaka jana wakati miaka mingine ilipokuwa CUF waliona hilo ni jema.

Kuikomboa Tanzania kutoka makuchani mwa mabeberu weusi wanaotumia mali zetu na rasilimali zetu kupitia migongo ya Kagoda na Meremeta, na kuwekeza katika migongo ya akina Manji na Rostam ni lazima vijana tuwe tayari kushiriki kikamilifu kuleta mabadiliko ya kweli kwa kutokukubali kuchakachuliwa.

Kwa hili la Kafulila na Mbatia, hapa ndo tunaona umuhimu wa wagombea wasiopita katika vyama ili wakimtimua katika chama asimame bila chama na atashinda. Nina hakika bunge letu litamkosa Kafulila na pia jimbo lake watamkosa maana kafichua uwekezaji na wizi mkubwa kule Uvinza na sasa mafisadi wamemtoa kwa staili ya katiba za vyama.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu bariki vyama vya kizalendo na Mungu onesha uasi wa wasioitakia mema nchi yetu ya Tanzania!
 
Ni mpinzani katika chama chake cha NCCR, na si mpinzani katika kutafuta demokrasia ya kweli nchini mwetu. Kumbukeni sakata lake huko Kawe ndo mtaujua ukweli. Pia ujue aliachiwa na nani madaraka katika NCCR, aliachiwa na mheshimiwa Lyatonga Mrema Augustino wa TLP kachero mkubwa wa CCM maana ni mwanachama hai. Kazi yake ndo hiyo na anaweka huku na huku kwa maslahi ya CCM ndo maana watawala wakakataa kambi rasmi ya upinzani mwaka jana wakati miaka mingine ilipokuwa CUF waliona hilo ni jema.

Kuikomboa Tanzania kutoka makuchani mwa mabeberu weusi wanaotumia mali zetu na rasilimali zetu kupitia migongo ya Kagoda na Meremeta, na kuwekeza katika migongo ya akina Manji na Rostam ni lazima vijana tuwe tayari kushiriki kikamilifu kuleta mabadiliko ya kweli kwa kutokukubali kuchakachuliwa.

Kwa hili la Kafulila na Mbatia, hapa ndo tunaona umuhimu wa wagombea wasiopita katika vyama ili wakimtimua katika chama asimame bila chama na atashinda. Nina hakika bunge letu litamkosa Kafulila na pia jimbo lake watamkosa maana kafichua uwekezaji na wizi mkubwa kule Uvinza na sasa mafisadi wamemtoa kwa staili ya katiba za vyama.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu bariki vyama vya kizalendo na Mungu onesha uasi wa wasioitakia mema nchi yetu ya Tanzania!

Na huo ndiyo uthibitisho kuwa hadi sasa chama cha upinzani kweli ni CDM tu.
 
Na huo ndiyo uthibitisho kuwa hadi sasa chama cha upinzani kweli ni CDM tu.

CHADEMA itakapochukua nchi 2015 sidhani kama kutakuwa na chama makini cha upinzani tena! maana CCM ndiyo itazikwa rasmi kipindi hicho!
 
Back
Top Bottom