Waridi
JF-Expert Member
- Mar 30, 2008
- 1,025
- 172
Mbatia awapasha wanasiasa
Imeandikwa na Waandishi Wetu;
Tarehe: 18th October 2009
MWENYEKITI wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia, amewalaumu wanasiasa kwa kudai kuwa wanafanya suala la mgawo wa umeme kuwa la kisiasa wakati ni la kitaalamu.
Mbatia amedai kuwa, wanasiasa ni chanzo cha mgawo unaondelea nchini hivi sasa kwa kuwa hawathamini mawazo ya watalaamu.
Kwa mujibu wa mwanasiasa huyo, vitendo vya wanasiasa hao vinaathiri sana uchumi wa nchi, na kwamba,wajasiriamali wengi wanapata hasara. Amesema, wanasiasa hao badala ya kutafuta suluhisho la kudumu la tatizo la umeme, wanalumbana.
Mbatia amesema watanzania wanahitaji umeme na si malumbano, na kama kuna waliokosea kuingia mikataba wachukuliwe hatua, na umeme upatikane.
Amesema jijini Dar es Salaam, kuwa, mgawo unaoendelea sasa umedhihirisha kwamba wanasiasa hawaheshimu mawazo ya wataalamu. Ameonyesha kusikitika kuona watanzania wanaumia, uchumi unadidimia lakini fikra za wanasiasa zipo kwenye migogoro.
Kwa mujibu wa mtaalamu huyo wa masuala ya umeme na maji, wataalamu wa nishati hiyo hawana kazi kwa sababu wanawaangalia wanasiasa wanalumbana kuhusu suala hilo.
Tuwaachie wataalam watupe suluhisho la umeme hili suala si la kisiasa, amesema Mbatia na kuhoji iweje nchi iwe na hazina kubwa ya gesi lakini bado kuna tatizo la umeme.
Amesema, Uholanzi ina gesi kidogo lakini inaitumia vizuri kupata nishati ya uhakika.
Mbatia amesema, sambamba na tatizo la umeme kufanywa la kisiasa, ubinafsi wa baadhi ya wanasiasa pia umechangia kuwepo kwa mgawo wa nishati hiyo.
Mwanasiasa huyo amesema, ni dhana potofu kuamini kwamba, mitambo ya kampuni ya Dowans ni suluhisho pekee la tatizo la umeme nchini.
Shirika la umeme Tanzania (Tanesco) juzi lilitangaza kwamba, makali ya mgawo wa umeme yataongezeka kwa kuwa, kiasi cha cha nishati hiyo kinachoingia kwenye gridi ya taifa kinazidi kupungua.
Kwa mujibu wa Meneja Mawasiliano Tanesco, Badra Masoud, wakati mgawo unaanza kulikuwa na upungufu wa megawati 65 katika gridi ya taifa, baadaye kukawa na upungufu wa megawati 90, lakini hadi juzi kulikuwa na upungufu wa megawati 150 kwa kuwa uzalishaji katika mitambo ya Kihansi, Kidatu, na Pangani unazidi kupungua.
Hivi katribuni, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kabwe Zitto, alisema, kama mitambo ya Dowans ikifanya kazi, tatizo la umeme nchini litakwisha. Zitto aliishauri Serikali iitaifishe mitambo hiyo, Serikali imekataa.
Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema, Serikali ikifanya hivyo itakiuka Katiba ya nchi .
Imeandikwa na Waandishi Wetu;
Tarehe: 18th October 2009
MWENYEKITI wa Chama cha NCCR Mageuzi, James Mbatia, amewalaumu wanasiasa kwa kudai kuwa wanafanya suala la mgawo wa umeme kuwa la kisiasa wakati ni la kitaalamu.
Mbatia amedai kuwa, wanasiasa ni chanzo cha mgawo unaondelea nchini hivi sasa kwa kuwa hawathamini mawazo ya watalaamu.
Kwa mujibu wa mwanasiasa huyo, vitendo vya wanasiasa hao vinaathiri sana uchumi wa nchi, na kwamba,wajasiriamali wengi wanapata hasara. Amesema, wanasiasa hao badala ya kutafuta suluhisho la kudumu la tatizo la umeme, wanalumbana.
Mbatia amesema watanzania wanahitaji umeme na si malumbano, na kama kuna waliokosea kuingia mikataba wachukuliwe hatua, na umeme upatikane.
Amesema jijini Dar es Salaam, kuwa, mgawo unaoendelea sasa umedhihirisha kwamba wanasiasa hawaheshimu mawazo ya wataalamu. Ameonyesha kusikitika kuona watanzania wanaumia, uchumi unadidimia lakini fikra za wanasiasa zipo kwenye migogoro.
Kwa mujibu wa mtaalamu huyo wa masuala ya umeme na maji, wataalamu wa nishati hiyo hawana kazi kwa sababu wanawaangalia wanasiasa wanalumbana kuhusu suala hilo.
Tuwaachie wataalam watupe suluhisho la umeme hili suala si la kisiasa, amesema Mbatia na kuhoji iweje nchi iwe na hazina kubwa ya gesi lakini bado kuna tatizo la umeme.
Amesema, Uholanzi ina gesi kidogo lakini inaitumia vizuri kupata nishati ya uhakika.
Mbatia amesema, sambamba na tatizo la umeme kufanywa la kisiasa, ubinafsi wa baadhi ya wanasiasa pia umechangia kuwepo kwa mgawo wa nishati hiyo.
Mwanasiasa huyo amesema, ni dhana potofu kuamini kwamba, mitambo ya kampuni ya Dowans ni suluhisho pekee la tatizo la umeme nchini.
Shirika la umeme Tanzania (Tanesco) juzi lilitangaza kwamba, makali ya mgawo wa umeme yataongezeka kwa kuwa, kiasi cha cha nishati hiyo kinachoingia kwenye gridi ya taifa kinazidi kupungua.
Kwa mujibu wa Meneja Mawasiliano Tanesco, Badra Masoud, wakati mgawo unaanza kulikuwa na upungufu wa megawati 65 katika gridi ya taifa, baadaye kukawa na upungufu wa megawati 90, lakini hadi juzi kulikuwa na upungufu wa megawati 150 kwa kuwa uzalishaji katika mitambo ya Kihansi, Kidatu, na Pangani unazidi kupungua.
Hivi katribuni, Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kabwe Zitto, alisema, kama mitambo ya Dowans ikifanya kazi, tatizo la umeme nchini litakwisha. Zitto aliishauri Serikali iitaifishe mitambo hiyo, Serikali imekataa.
Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, alisema, Serikali ikifanya hivyo itakiuka Katiba ya nchi .
Jumla Maoni (2)
Maoni
Maoni
Mimi ninaunga mkono kauli ya Mheshimiwa James Mbatia kuhusu wanasiasa kuacha kuingilia masuala ya kitaalamu wakati wao si wataalamu, ukichukulia mfano wa mitambo ya Dowans,serikali ilikuwa na nia nzuri ya kuinunua kwa manufaa ya umma na wataalamu wa kimataifa wakaipitisha na kuikubali kama ni mizuri na inafaa kununuliwa,lakini wanasiasa wetu wakaleta mizozo na makelele makubwa kupinga kununuliwa kwa mitambo hiyo hadi kuifanya Serikali yetu kusita kuinunua na sasa tunaona matokeo yake,nchi nzima IPO GIZANI !!!!
HONGERA MBATIA KWA KULIONA HILO.
WASIPO DHIBITIWA,KUNA SIKU WANASIASA WETU HAWA WATAKWENDA MUHIMBILI NA KUWAELEKEZA MADAKTARI NAMNA YA KUWAFANYIA OPARESHENI WAGONJWA KWA KISINGIZIO CHA KUPAMBANA NA UFISADI!!!
SASA HIVI WAO WANAFAIDI NA MAJENERETA YAO,SISI WANYONGE TUNATESEKA GIZANI.