MB Zitto Kabwe na ripoti 2 za uchungu kwa sisi Watanzania!

Malafyale

JF-Expert Member
Aug 11, 2008
13,813
11,126
Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya UMMA(POAC) Mbunge Zitto Kabwe leo katupasha habari 2 za kusikitisha sana sis Watanzania;

Mosi;Tanzania lost USD 308m(Approx billion 450 in TZ shilling) as tax revenue from sale of Zain Africa assets in Tanzania to bhartel. Kasema wazi kuwa Source ni TRA

Pili;Waziri wa zamani wa Maliasili na Utalii Mama Mwangunga na baadae Waziri Maige bila kufuata sheria halali zilizopitishwa na bodi ya Wakurugenzi wa TANAPA wakaingiza sheria zao binafsi na kuikosesha Tanzania zaidi ya shilling bilion 19

Kwa nini Mawaziri wana nguvu ya kusamehe kodi ktk serikali ya Tanzania?Hizi ni pesa nyingi sana na wabunge wa upinzani wasiache ripoti hii ipite hivi hivi!Kutokusanywa kwa mapato mengi kama haya kunatufanya watz wote kwa ujumla bila kubagua itikadi zetu za kisiasa kukosa huduma muhimu za kimaendeleo na kijamii!

Kwa mtindo huu wa kila Waziri ktk serikali hii kuwa na nguvu ya kusamehe kodi;hadi kupata katiba mpya mwaka 2014 Tanzania itakuwa si imefilisika?Ndugu Watanzania je tusubiri hadi mwaka 2014 au kuna lolote tunaloweza kufanya kuzuia madudu haya?

Dondoo za Chanzo cha habari hii ni Page ya Zitto kabwe ktk Facebook na Gazeti la Citizen(25-03-2011)
 
Hizo taarifa tafadhari zifanyiwe kazi, nakuomba Mh. Mbowe (kwa sababu wewe ndiyo unaoongoza kambi inayotetea wananchi).Nakusihi, hakikisha kitu kinafanyika, yaani kurudisha pesa hizo.
 
Nasubiri kuona maoni ya wanaosema Zitto ni mtumwa wa CCM, angalau kwa hili.
 
ndiyo maana mara baada ya kuchaguliwa na tume kuwa raisi, kikwete alikimbilia kuzindua airtel....nilijua tu lazima ilikuwepo shida pale
 
nilijua tu kuwa Maige ni miongoni mwa mawaziri wezi na hilo linaonekana wazi kabisa..IQ yake kwenye kufanya mambo iko chini sana
 
Zitto bado kuaminika, inawezekana kundi mmoja ndani ya ccm wamempa nyaraka za kumuumbua CCM Mwingine - Maige. Zitto bado hajajibu hoja nyingi za MSINGI. Tuhuma za kubomoa chadema na kuhamia NCCR kwa maagizo ya Lowasa bado hajajibu. Hatumwani ngo. WACHA ATUMKEI NA CCM.
 
I never lost faith in Zitto kwa sababu najua despite everything Zitto anao uchungu na nchi yake!hongera kwa kazi nzuri na endelea kufichua maovu ya utawala unaojali maslahi binafsi!Mungu akulinde!
 
dah, tunalalamika ya dowans kulipwa bil 94 na huku kuna mwanya mkubwa kiasi hiki wa kutokulipa kodi. TRA is another trap that needs over the clock scrutiny.
 
Nasubiri kuona maoni ya wanaosema Zitto ni mtumwa wa CCM, angalau kwa hili.
Hata baadhi ya wanaCCM nao hawapendi yanayoendelea, tusihukumu teh whole CCM

Zitto... keep it up, hatukutoi vichwani kwani ukishanyea kambi unakuja na sabuni murua kudeki, good one!!
 
I never lost faith in Zitto kwa sababu najua despite everything Zitto anao uchungu na nchi yake!hongera kwa kazi nzuri na endelea kufichua maovu ya utawala unaojali maslahi binafsi!Mungu akulinde!
He is brilliant lakini je yaweza hii pia ikawa ni mtu kujipigia pande la kuongeza value?? au keshashiba?
 
I never lost faith in Zitto kwa sababu najua despite everything Zitto anao uchungu na nchi yake!hongera kwa kazi nzuri na endelea kufichua maovu ya utawala unaojali maslahi binafsi!Mungu akulinde!
Hakuna kitu,haka ni kapepo kadogo kanako jigeuza huku na kule,huyu mtu anafanya haya kwa maslahi,inawezekana ameishiwa anaamua kuanzisha hoja ili wamuonge kwa kumpoza,zito kuwa macho janja yako tunaijua lakini pia anajaribu kukwepa hoja NSSF mkishaisahau ataachana navyo kwani hizi hoja halishawahi kuzisema sana tuwe tunakumbuka wajameni.
 
He is brilliant lakini je yaweza hii pia ikawa ni mtu kujipigia pande la kuongeza value?? au keshashiba?

MTM sidhani kama hii ni kujipigia pande ama kuongeza value,naona kama kuna nia ya dhati hapo kupigania haki na maendeleo ya taifa.tusubiri tuone mwisho wake.i think the old Zitto is coming back!!au we unaonaje?
 
Nasubiri kuona maoni ya wanaosema Zitto ni mtumwa wa CCM, angalau kwa hili.
We acha janja yako tunajua wewe ni Zitto mwenyewe umejipa id za kutosha hapa JF,unajua tunakusoma nyendo zako kuwa makini.
Tangu ulipoanza kuisema Airtel mbona hujatoa hoja Bungeni!tunajua walikuonga.swala la TaNaPa kwani wewe si ndiye ulikuwa mwenyekiti wa mashirika hukuliona,au unafikiri walipokuwa wanakuonga mamilioni na kukatiwa ticketi za ndege kwenda Ujerumani eti shule hatukujua.umeongwa mamilioni mangapi kupindisha taarifa!tunakujua bwana wadanganye wengine.hoja ni za msingi lakini hauna uchungu na nchi yako you are after money and leadership ndiyo maana JK anakutumia kama dampo. walikuonga ngapi ukanyamaza ume
 
Hakuna kitu,haka ni kapepo kadogo kanako jigeuza huku na kule,huyu mtu anafanya haya kwa maslahi,inawezekana ameishiwa anaamua kuanzisha hoja ili wamuonge kwa kumpoza,zito kuwa macho janja yako tunaijua lakini pia anajaribu kukwepa hoja NSSF mkishaisahau ataachana navyo kwani hizi hoja halishawahi kuzisema sana tuwe tunakumbuka wajameni.

Kagemro mimi naamini anafanya haya kwa maslahi ya taifa na si binafsi.tatizo tulishajenga imani ya "Zitto anatumiwa na CCM" na hatutaki kubadili fikra hizo kwa lolote lile hata Zitto angefanya nini.labda alitumiwa mimi sijui lakini cha msingi ni kumuunga mkono pale anapotetea maslahi ya taifa,je angekaa kimya na mambo haya yakafichuka si ndio tungebeba mabango na kusema nae alipata share katika ufisadi huo na ndio maana akanyamaza?so atleast be positive for once!
 
Kwa Hili nampongeza Zitto, ila msimamo wangu unabaki pale pale Zitto si mtu wa kuaminika, nimemfuatilia sana katika kazi zake za siasa, sijawahi kumwamini au hata kukaribia kumwamini, ila akiweza kutuzihirishia kwamba anania safi na taifa hili na wala si tamaa ya mali, sifa na uongozi naweza kumwamini, lakini kwa sasa Chadema chunga sana Zitto, namini hata sina haja ya kuwaeleza Chadema juu yake nafikiri wanamfahamu zaidi yangu.
 
Kagemro mimi naamini anafanya haya kwa maslahi ya taifa na si binafsi.tatizo tulishajenga imani ya "Zitto anatumiwa na CCM" na hatutaki kubadili fikra hizo kwa lolote lile hata Zitto angefanya nini.labda alitumiwa mimi sijui lakini cha msingi ni kumuunga mkono pale anapotetea maslahi ya taifa,je angekaa kimya na mambo haya yakafichuka si ndio tungebeba mabango na kusema nae alipata share katika ufisadi huo na ndio maana akanyamaza?so atleast be positive for once!
Sina hukika kama unamjua Zitto ni mtu wa namna gani,ninaamini nachokisema,nakubaliana na wewe pia kuwa mtu akifanya vema tumuunge mkono,zitto najua unafatilia mjadala hakikisha hoja hizi unazifanyia kazi vinginevyo zitakugeuka mwenyewe.
 
Back
Top Bottom