[h=2] [/h][h=2]Na,Jumbe Ismailly,Singida Apr,03,2012 Mahakama kuu[/h][h=2]Kesi ya kupinga matokeo ya Lissu yaibukika mambo mazito.[/h][h=2]Chiligati atajwa kuhusika kuandaa ushahidi,[/h][h=2]Mrema na mwanae watumika kusaidia CCM kumpinga Lissu,[/h][h=2]Mashahidi waingia tena mitini, jaji aamuru walalamikaji walipe gharama kwa uzembe[/h][h=2] [/h][h=2]KESI ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyompa ushindi wa ubunge wa jimbo la Singda mashariki (CHADEMA),Bwana Tundu Lissu jana na iliibua mambo mapya baada ya mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo kutoa waraka Mahakamani ulioandikwa na aliyekuwa Katibu wa Halmashauri kuu ya Taifa,Itikadi na Uenezi,Kapteni Mstaafu John Chiligati[/h][h=2]Kwa mujibu wa barua hiyo yenye kumbukumbu namba CCM/OND/559 VOL.II/10 ya machi,23,2011 iliyoandikwa na kusainiwa na John Chiligati iliomba kufahamu kama ni kweli TLP iliweka mawakala katika jimbo la uchaguzi la Singida mashariki,au kama mihuri iliyotumika ya TLP ilikuwa ni sahihi au ni ya kughushi[/h][h=2]Pamoja na barua hiyo kuna barua nyingine pia iliyotoa majibu kwa Chiligari ambayo iliwasilishwa Mahakamani hapo na Bwana Tundu Lissu iliyotoka kwa Hamadi R.Tao aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa TLP,yenye namba TLP/HQ/VOL.V/165 iliyokiri kuwa mawakala wa TLP hawakuteuliwa au kama waliteuliwa utaratibu haukufuta taratibu za chama.[/h][h=2]Hata hivyo barua ya TLP ilipingana vikali sana na barua ya Mwenyekiti wa TLP wilaya ya Singida iliyoindikwa kumjibu katibu wa TLP Taifa ya apr,12,2011juu ya mawakala hao kusimamaia katika uchaguzi mkuu bila malipo[/h][h=2]Hata hivyo mjadala wa mahakamani ulikuwa Mkubwa, baada ya Shahidi wa 19, Bw. John Madindilo, ambaye ni Mwenyekiti wa TLP Mkoa wa singida kukubaliana na hoja zote za Lissu, na kumtaja Mtoto wa mwenyekiti wa TLP Taifa,Bwana Augustino Mrema, Bwana Michael Mrema kuwa alitumwa singida kama afisa wa Chama kwenda kufuatilia suala hilo,hata hivyo alipopewa taarifa hiyo, hakuridhika nayo badala yake aliwaelekeza wale viongozi wa Singida, kuandika barua kwa Katibu Mkuu kadiri itakavyompendeza Mwenyekiti wa TLP, Augustino Mrema.[/h][h=2]Baadhi ya mahojiano yalikuwa kama ifuatavyo: Baina ya Tundu Lissu na SHAHIDI, JOHN MADINDILO[/h][h=2]T/L Ni kweli au si kweli kuwa ulikasimu madaraka kwa Mwenyekiti wa TLP wa wilaya ya Singida, kwa kuwa wewe ulikuwa Mgombea, na Mwenyekitji wa Wilaya ya singida, ulimwamini, kwa uwezo wake na uadilifu , na uzoefu wake?[/h][h=2]P/W:NDIYO NILIFANYA HIVYO LAKINI YEYE PIA YUPO MAKAO MAKUU YA MKOA HAPA MJINI.[/h][h=2]T/L Ni kweli au si kweli kuwa mliweka mawakala kulinda maslahi ya Chama,[/h][h=2]P/W NI kweli,[/h][h=2]T/L Ni sahihi au siyo sahihi, mnapokuwa na Mgombea urais, huwa mnaweka mawakala?[/h][h=2]P/W NI KWELI, pale ambapo mawakala wanakuwa tayari kujitolea.[/h][h=2]T/L Ni kweli au si kweli kuwa kwa mujibu wa barua ulizo nazo, kesi hii ipo kwa maslahi ya Chiligati na Mrema?[/h][h=2]P/W Ni kweli kwa mahusiano ya barua hizi walizoandikiana.[/h][h=2]T/L Kama nimekusikia vizuri uliiambia mahakama hii kuwa kuna Afisa wa Chama anakuja toka Mkao makuu, umpokee na umpe ushirikiano?[/h][h=2]P/W NI kweli.[/h][h=2]T/L Je huyo afisa wa chama alikuwa anaitwa nani?[/h][h=2]P/W: Siruhusiwi kumtaja[/h][h=2]JAJI: Kama umemtaja Augustino Mrema, Mwenyekiti wa TLP Taifa ni Afisa gani unashindwa kumtaja[/h][h=2]P/W: ni Mikaeli Mrema.[/h][h=2]T/L. Mikaeli Mrema ambaye ni mtoto wa Augustino Mrema?[/h][h=2]W/P.NDIYO[/h][h=2]T/L. Mikaeli Mrema alisema nini?[/h][h=2]P/w; alisema kuwa kulikuwa na mawakala hewa wa TLP waliwekwa Singida mashariki?[/h][h=2]T/L. Hukushangaa kupokea taarifa ya Malalamiko toka makao makuu wakati wewe Mwenyekiti wa Mkoa huna taarifa yeyote?[/h][h=2]P/W: NILISHANGAA SANA lakini nilipokea kwa kuwa inatoka kwa Mkubwa wangu wa Kazi.[/h][h=2]T/L: Nimeshtakiwa hapa, kwa mujibu wa barua mbalimbali ulizosoma, wanaitaka Mahakam itengue matokeo ya uchaguzi, kwa mujibu wa ufahamu wako, unasemahe juu ya hili?[/h][h=2]P/W: watakuwa wanakuonea.[/h][h=2]Kesi hiyo haikuendelea mchana, baada ya upande wa walalamikaji kushindwa kuleta Mashahidi mahakamani, kitendo kilichopelekea jaji kuwapiga faini ya kulipa nusu gharama ya siku katika kesi hiyo:[/h][h=2]Na mahojiano yalikuwa hivi:[/h][h=2]Wakili wa walalamikaji; Mheshimiwa jaji, naiomba Mahakama iahirishe kesi hii hadi kesho kwa kuwa shahidi wetu hajaja, na amefunga simu,[/h][h=2]JAJI: Ulichukua hatua kuleta shahidi mmoja tu?[/h][h=2]Wakili: huwa tunachelewa kutoka mahakamani, hivyo inakuwa vigumu kuwatafuta kwa siku inayofuata. Hata hivyo kazi ya kutafuta mashahidi sio yangu ni ya wateja wangu.[/h][h=2]TUNDU LISSU: Mheshimiwa jaji, uchelewashaji unaofanywa kwa makusudi unaniathiri mimi, kwanza kiuchumi kwa kuwa nakaa hotelini, pili ninashindwa kushiriki kazi za kibunge, na ninashindwa kuwatumikia wanachi wangu walionichagua. Siku nyingine ulinionya nisidai gharama, leo mheshimiwa jaji, naomba upande wa walalamikaji walipe gharama,[/h][h=2]Jaji: Mlalamikaji naomba usimame, unajua kuwa katika kesi hii mimi nalipwa na serikali, na hawa wanasheria watatu wa serikali, na katibu wangu?[/h][h=2]MLALAMIKAJI: NDIO,[/h][h=2]JAJI: mbona hampo serious . Kuna uzembe mkubwa unatokea na leo hii sitaki kukubali kirahisi uzembe huu. Kuna uzembe unafanywa na walalamikaji, na tayari nilionya hili tangu mwanzo. Mtumzembe hukumbushwa na leo naamuru mtalipa nusu gharama ya ahirisho la kesi leo kwa uzembe wenu ili mjitume na mjue wajibu wenu sio kutupotezea muda hapa.[/h][h=2] [/h][h=2]Kesi hiyo iliahirishwa mpaka kesho (LEO) saa 3 asubuhi[/h]