Mazishi ya waliouwawa na polisi tarime- serikali yakataa marehemu wasiagwe uwanjani na uma

samora10

JF-Expert Member
Jul 21, 2010
7,594
4,798
wana JF habari toka tarime zinasema serikali imekataa kuruhusu wale marehemu waliouwawa na polisi kuagwa uwanjani kabla ya kwenda kuzikwa...


source; tundu lissu
Tundu Lissu
(7 minutes ago)

Niko Tarime tangu jana jioni. Na jana mchana Jeshi la Polisi likiongozwa na Kamishna wa Polisi Chagonja walikubalina na ndugu wa marehemu pamoja na uongozi wa CHADEMA ukiongozwa na Wakili Mabere Marando kwamba marehemu wataagwa katika uwanja wa Saba Saba kesho kuanzia saa 2 asubuhi kabla ya kupelekwa katika vijiji vyao kwa ajili ya mazishi. Tumekuwa katika maandalizi ya mazishi hayo tangu jana jioni. Hata hivyo, jioni hii tumeletewa barua ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Tarime kututaarifu kwamba haturuhusiwi tena kuwaaga marehemu wetu kama ilivyokubaliwa jana. Nimewasiliana na uongozi wa juu wa CHADEMA i.e. Mwenyekiti Mbowe na Dr. Slaa juu ya jambo hili na wao wakazungumza na IGP Mwema. Inaelekea, according to Mwenyekiti quoting IGP Mwema kwamba amri ya utukataza kuwaaga marehemu imetoka juu zaidi na nje ya Jeshi la Polisi. This could only mean Ikulu au Ofisi ya Waziri Mkuu Pinda. Msimamo wetu ni kwamba polisi waliowaua Watanzania hawa hawawezi kutufundisha namna ya kuomboleza au kuwalilia hao waliowaua! Inaelekea wanachotaka kufanya na kuzuia Arusha kujirudia: mara baada ya mauaji ya Arusha tulifanya mazishi ya umma kwenye viwanja vya NMC ambayo yalihudhuriwa na zaidi ya watu laki moja na ambayo yalikuwa ya amani entirely. Kama mnavyojua, mjadala ulioibuka baada ya mazishi hayo ya amani ulihoji kama polisi walikuwa na sababu yoyote ya kuua waandamanaji waliokuwa wanaandamana kwa amani. Kuna hoja imejengwa kwa muda mrefu sana kwamba watu wa Tarime ni wakorofi na wapenda fujo. Hoja hiyo imetumika kuhalalisha mauaji ya wananchi wa Tarime: waliouawa wiki iliyopita wanafikisha idadi ya wananchi wa Nyamongo waliouawa kwenye Mgodi wa North Mara kufikia 28 tangu tarehe 20 Julai 2005 walioua watu watatu wa kwanza. Hadi sasa hakuna mtu yeyote ambaye amewahi kukamatwa au kushtakiwa au kuwajibishwa kwa namna yoyote ile kutokana na kuhusika na vifo hivi. Wote waliouawa wameuawa mchana kweupe mbele ya mashahidi. Utaratibu wetu wa kisheria unataka kifo chochote chenye utata kichunguzwe katika Mahakama ya Korona (Coroner's Court) ili kuthibitisha kama kina lawama au la! Hakujawahi kuwa na mahakama ya aina hiyo katika mauaji yote 28. Umefikia wakati wa kumaliza tatizo hili la mauaji ya wananchi wetu. Kama ni kweli ni wavamizi au majambazi kama alivyodai Waziri Kagasheki ni wajibu wa Mahakama ya Korona kuamua hilo sio mkuu wa wauaji! Kama majambazi hawa wanastahili adhabu ya kifo au la ni kwa mahakama za nchi yetu kuamua na sio police executioners! Sisi hatutakubali kuliachia hili liishe hivi hivi. Watu 28 ni wengi sana kufa bila maelezo ya kuridhisha. Tuko hospitali ya Tarime usiku huu na hatutaondoka hapa mpaka tuwazike wafu wetu kwa tunayoifahamu sisi na sio tunayotakiwa kufundishwa na Jeshi la Polisi la Tanzania! Kama waliua hadharani kwa nini hawataki tuomboleze hadharani? Tunaomba Watanzania mtusaidie kwenye jambo hili
 
Nguvu ya uma itumike nashauri mana risasi za polisi haziwezi kuuwa watu wote watakaokwenda kwenye mazishi
 
kikwete kaogopa ba itaonyesha ni jinsi gani itakavyo idhalilisha serikali na mbunge wake
 
Nionavyo mimi, kama kuna mtu wa CCM humu jamvini basi awashauri hao wanaoitwa 'watu wa juu' ili wasiingilie kabisa huu msiba wa Tarime pamoja na taratibu zote za maziko. Walau kwa sasa wangejiweka kando maana tactics kama hizi za kuzuia sehemu ya kuwaaga marehemu is the 'ULTIMATE' humiliation kwa watu wa Tarime.

Wakubwa hawa wanaonekana wanashindana na CHADEMA as chadema -a political party. Wasichokijua au wasichotaka kujua ni kwamba CHADEMA is now beyond a politcal party. Ni nyenzo ya watanzania waliopigika kimaisha kudai UTU wao na kupata haki sawa ikiwa ni pamoja na kufaidi rasilimali zilizomo nchini. Ni kupitia Chadema watanzania for the first time in the history of this country wanasema bila kumumunya maneno taabu na mateso wanayopata kutokana utawala mbovu. Ni kupitia Chadema umma unaeleza aina ya utawala wanaotaka na ndio tuko kwenye mchakato wa kupata katiba mpya. Ni kupitia Chedema watanzania, wake kwa waume, vijana kwa wazee wanainuka na kusema - YES WE CAN build the type of Tanzania that we want. Tuanchie hapo.

Kwa nchi yeyote inayofuata utawala wa sheria mtuhumiwa yeyote is innocent until proven guilty by the courty of law. Kama kuna wananchi waliovamia mgodi huko North Mara, police walitakiwa wawakamate na kuwapeleka mbele ya vyombo vya sheria. basi. Kuuwa kwa risasi mtuhumiwa asiyekuwa na silaha ni kosa - it is murder!

Uniulie mtoto na bado unipangie namna ya kuombeleza? hiii sio sahihi. Halafu huku watu wanajidai kuna utawala wa sheria unaoheshimu haki za binadamu? Nijuavyo mimi haki ya mtu haipotei, inaweza kufunikwa funikwa lakini ipo siku haki hiyo itapitakana. Na hakuna mzazi anayependa kumzika mwanawe lakini kesho wazazi wenzetu Tarime watazika watoto wao.

Wakubwa hawa wana nguvu, tena sana na hata hiyo kesho wanaweza kabisa kuzuia uwanja usitumiwe na wazazi hawa kuwaaga watoto wao kwenye safari yao ya mwisho. Ila wajue, pamoja na nguvu zao hawana uwezo wa kumzuia mungu kutoa haki kwa viumbe wake. Na uzuri ni kwamba kila mtu ana equal access kwa mungu.
 
Jamani hii ni private side ya maisha, serikali haina haki ya kuingilia watu wazikweje kama wanaogopa kutokea kwa vurugu inawabidi waimarishe ulinzi lakini sio kuzuia.
 
Jamani uongozi wa juu utakapoyalazimisha maji kupanda mlima itakuwia gharama kubwa sana kwa nini usiyaache maji yatelemke yenyewe na wala hutatumia nguvu yoyote. Cha msingi imarisheni ulinzi tu hilo ndio la msingi.
 
hii hali ni hatari, polisi washaona wamefika na wanachoamua ndo wanachofanya, hatutoweza kamwe kukubali vitendo kama hivi viendelee kutokea katika ardhi ya tanzania, uvunjifu wa amani unafanywa na jeshi lapolisi ambao ndo wana dhamana ya kusimamia amani, mhesjhimiwa Mwema kama upo kwenye hii forum lazima uwajibike katika hili kwani watu wetu hawezi kuwa wanapoteza maisha, nguvu kazi ya nchi inpotea nawewe upo. mambo ya kukandamizwa yamepitwa na wakati na sasa tunajua haki zetu, nabado hamjalitambua hilo mnazidi kuchokonoa wananchi na ubabe wenu usiokuwa wa msingi. Tarime ni mfano wa mauaji mliyoyafanya na mizimu ya hao marehem itawatafuna,
 
Mambo ya dhuluma kwa wananchi nilikuwa nayasikia South Africa,Zimbwabwe,katika utoto wangu nilishiriki katika nyimbo za Kaburu kamata kamata,haini smith ,mchokozi Banda,sikutegemea katika maisha yangu haya mambo nitayaona katika nchi yangu nzuri ya Tanzania nilikozaliwa na ambako nitazikwa,kweli ni kichefuchefu,Askari wanapora maiti wanaenda kutupa barabarani,mbona tumeona Raisi Kikwete akiahirisha mkutano Namibia kuja kumzika Jini Lake,Sheikh Yahaya,hivi katika nchi hii kuna ambao wanavibali vya kuzikwa kama binadamu na wengine kutendwa kama wanyama,Polisi anayang'anya maiti kwenda kutupa barabarani mambo gani hayo mbona yanatisha
Uko wapi utawala wa sheria
Yuko wapi KIKWETE aliyesema maauaji hayatatokea tena mbele ya uso wake
Kweli tunaserikali
wanataka wananchi tuamua tutakayo ,sawa bwana bado kitambo kidogo amini usiamini nchi hii itarudi kwenye enzi zake
 
Hapa hakuna utawala kabisa hata kidogo, sembuse huo utawala wa kisheria utauona wapi?

hiyo amri iliyotoka juu ni wapi? Ina mana huyu rais wetu hata hao washauri wake ni wakwere au?

yani haoni kwamba kuzuia umma kuaga hao maiti anataka kuanzisha vurugu nyingine?
Hili halihitaji hata elimu ya darasa la saba kuelewa

na huyu MBAYUWAYU..........

mbona yeye hachanganyi akili zake na za kuambiwa na wenzie, au anatudanganya tu sisi tuchanganye, au hao MBAYUWAYU waliokuwa karibu nae wana akili kama zake...so
MBAYUWAYU+MBAYUWAYU=MAGAMBA?
f......k all
 
Hii sasa ni hatari!!

Politik inapoingia hadi kwenye misiba sijui mwisho wake!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom