Mazishi aina hii yanatisha

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
download+(14).jpg


Kuna njia mbalimbali za mazishi kadiri ya mila, desturi, tamaduni na mapokeo, hali kadhalika imani kama:
  • kuichoma moto miili ya watu,
  • kuivunja miguu ili shimo la kuzika liwe dogo,
  • kuitumbukiza shimoni na jaza udongo juu yake,
  • kuhifadhi mwili kwenye sanduku kisha kuutumbukisa shimoni,
  • kuchimba shimo na kutengeneza chumba ambacho hakifikiwi na udongo,
  • Kuitelekeza porini na kuhama makazi kama baadhi ya jamii za wachungaji, nk.

Wote hao na taratibu zao wanajali hadhi ya binadamu, na kwamba akishakata roho mwili ni udongo tu unaoweza kufanyiwa kwa namna ye yote ili kuufanya urudie udongo.


"Kumbuka binadamu u mavumbi na utarudia kuwa mavumbi."
 
jeneza kufukiwa na majari

Kwa sisi waislamu huwa hatuzikwi na jeneza wala sanduku, hapo mwili haujafunikwa na majani, kuna shimo jengine ndani ya hilo shimo kwa pembeni kabisa huitwa "MWANANDANI" kama hujawahi kusikia, mie ni mwanamke sijawahi kwenda makaburini, lakini tunasoma kwenye vitabu vya dini jinsi ya kuzika incase kama hakuna wanaume aula mwanamke kufanya hivo! kwa hiyo baada ya kuulaza mwili kwenye mwanandani , unafuata ubao! baada ya hapo ndio wengine wanaweka mchanga moja kwa moja na wengine ndio majani !

HATA HIVO SIJAONA CHOCHOTE KINACHOTISHA HAPO !, kuna maziko yanayotisha kuliko ya KUCHOMA MOTO? na baada ya hapo watu hukusanya majivu na kuhama hama nayo popote waendapo!

Wewe unanchekesha sana kajisemea FaizaFoxy! kinachokutisha hapo ni nini? au umeshaona maziko ya kiislamu basi unataka kuanza kutoa kashfa zako!
 
Mi nafikiri suala la majani ni uzingatiaji wa mila za makabila . Labda wenzetu wa mkoa wa Tanga hususan wasambaa wanaweza kutusaidia kuelewa mantiki ya kuweka majani kwani makabila mengine wanaweka vitu vingi kama mikeka, nguo, vyombo vya nyumbani, saa, redio n.k.
 
Hapa nafikiri Wachangiaji wengi hajaelewa desturi za mazishi ya kutumia "mwana ndani" kwenye kaburi, sehemu ambayo huchimbwa zaidi ya ile level ya kaburi saizi ya mwili wa mtu na baadae kufunikwa kwa ubao ili mchanga usimfikie yule maiti na baadae juu huwekwa majani kablaya kuanza kufukia kaburi.
Sio rahisi kuelewa kwa kuelezea kama hivi lakini kila siku tunazika na haikatazwi kwa mtu yeyote kuhudhuria na kuelewa zaidi.
 
kwani waislamu wanazika na sanduku? si wanatumia moja tu wafu wote mnabebwa na hilo halafu linarudishwa msikitini?
 
Hapa nafikiri Wachangiaji wengi hajaelewa desturi za mazishi ya kutumia "mwana ndani" kwenye kaburi, sehemu ambayo huchimbwa zaidi ya ile level ya kaburi saizi ya mwili wa mtu na baadae kufunikwa kwa ubao ili mchanga usimfikie yule maiti na baadae juu huwekwa majani kablaya kuanza kufukia kaburi.
Sio rahisi kuelewa kwa kuelezea kama hivi lakini kila siku tunazika na haikatazwi kwa mtu yeyote kuhudhuria na kuelewa zaidi.

Mapokeo na desturi ya kabila langu huzika kwa kuchimba shimo refu, halafu ubavuni mwa shimo huchimba chumba kidogo kadiri ya ukubwa wa maiti kisha kufunika kwa mbao na majani, udongo unapofukiwa haufikii maiti. Lakini hapa inavyoonyeshwa ni kama maiti imewekwa katikati ya shimo na juu yake kuweka majani kisha kufukia udongo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom