Jackbauer
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,038
- 2,199
hebu tujadili kwa kina bila hisia kali.
Ni ukweli usiopingika kuwa afya ni moja ya mambo muhimu katika maendeleo na ustawi wa mwanadamu.
Kusini mwa jangwa la sahara tumeshuhudia mamilioni ya watu wakikosa huduma ya daktari au afya ya msingi.
Zaidi ya nusu ya kina mama wajawazito hujifungua bila uangalizi wa mhudumu wa afya mwenye ujuzi juu ya maswala ya afya. Watoto wanaendelea kufa kutokana na magonjwa yanayozuilika mfano kifua kikuu,malaria,utapia mlo, magonjwa ya kuhara n.k
tukumbuke ni haki ya kila binadamu kupata huduma bora za afya popote pale alipo bila kujali dini,rangi,kabila au itikadi zake za kisiasa hata wale watekaji wanaofanyia shughuli zao kule msitu wa pande.
Bado kuna mamilioni ya watanzania huikosa haki hii kisa hakuna nesi, daktari au fundi sanifu wa maabara katika vituo vyetu vya afya au hakuna maji,umeme,usafiri,dawa na vifaa tiba.hili ni tatizo la msingi linalohitaji jibu la msingi na sio LIWALO NA LIWE.
Tatizo la watumishi wa afya kwa afrika ni kubwa sana ingawa afrika hubeba mzigo mkubwa sana wa magonjwa duniani.mbaya zaidi nchi za kiafrika (Tanzania ikiwa kati ya vinara watatu) hazijawekeza vya kutosha katika afya.
Tanzania inakadiriwa kuwa na uwiano wa daktari 1: watanzania 30000,kwa ujumla tuna upungufu wa zaidi ya wahudumu wa afya 80000 kwa mujibu wa shirika la afya duniani.uhaba huu unasababisha vifo sio utani!
Inakadiriwa kila ukitambea umbali wa kama kilometa 8 hapa Tanzania unaweza kukutana na kituo cha kutoa huduma za afya.km nane kwa mjini ni safari ya muda mfupi sana lakini kwa vijijini(huku ndipo 75% ya watanzania wanapoishi au kutakiwa kwenda) safari hii ni changamoto kubwa kwa mgonjwa na daktari wake. Mara nyingi utasikia mjamzito kajifungulia njiani au kakutana na tishio la wanyama wakali wa porini.pia unaweza kusikia daktari atekwa na majambazi yenye kutumia silaha za jadi alipokuwa anatoka kazini kuelekea nyumbani.
Safari ya kuitafuta huduma ya afya haishii hapo tu bali yaweza kuendelea pale utakapofika kwenye kituo cha afya na kukuta hakuna hata kipande cha panadol au rangi mbili, hakuna kanyula,hakuna maji ya kuongeza nguvu mwilini (IV fluids), hakuna sindano ya tetenasi au ya kuzuia kichaa cha mbwa, hakuna X ray machine, hakuna nyuzi, hakuna gauze, hakuna karatasi za rufaa yaani ni hakuna! Hakuna! Hakuna! sana sana utakachopata ni sura ya huruma ya muhudumu wa afya akikwambia POLE au uambiwe toa hela ya mafuta tujaze hili bajaji la wafadhili tukupeleke hospitali ya wilaya.
Umeshawahi kuona hospitali inakosa umeme,maji safi na salama, simu na mawasiliano mengine ambayo yamejaa kwenye maofisi pale posta? Njoo Tanzania ujionee. Ni kawaida kusikia kuwa tumehairisha operesheni kwa sababu hakuna umeme au maji ya kuoshea magauni.
Ni mara nyingi tu utamwona daktari akiinua simu yake ya mkononi kuongelea swala la mgonjwa au kuulizia ememe tanesko au kuulizia process za kununua dawa zimefikia wapi.
Si jambo la kushangaza kusikia wagonjwa wamelala watatu kwenye kitanda kimoja na wengine wanalala chini.
Ni ukweli usiopingika kuwa tuna tatizo kubwa la watumishi wa afya hapa Tanzania pamoja na kwamba kusomea udaktari ni ''bure''. Hivi ni kwa nini hatujiulizi kwa nini tuna wanafunzi wachahche wanaosoma sayansi au fani za tiba nchini?
Jibu liko wazi…..fani hii imesahaulika!!tuache siasa!!
Mfanyakazi wa afya anahitaji akili tulivu ili aweze kufanya kazi lukuki kama vile kufundisha wenzake na jamii,kuandaa tafiti za afya,kuhimiza mambo ya afya bora, kutibu n.k
Mtu huyu haitaji kufikiria juu ya watoto watasomaje,ngo'ombe wangu hana majani,nilipata ukimwi kwa kujichoma wakati wa operesheni nani atanitunza mimi na familia,nikitoka kazini nitafikaje nyumbani,hivi nitafia kwenye nyumba ya kupanga,????
Leo hii mtu huyu akidai haki yake mwampeleka mwituni mabwepande