Mazingira ya JK yalivyoathiri Utendaji Kazi wake wa Urais

Bora tu ungekuwa muwazi zaidi ukasema kuwa kuzaliwa kwake na kulelewa katika uislam ndilo tataizo badala ya kuzunguka.
Wanaosema nchi imemshinda wao hasa walitaka nchi iweje? Labda watoe mfano wa nchi yoyote ya kiafrika ambayo ina kiongozi shupavu amabe ameivusha nchi yake kutoka ktk dimbwi la umaskini? Hakuna.Nchi zote za jirani zina matatizo

Napenda kuheshimu maoni yako lakini utakuwa hukunitendea haki kusema kuwa dhamira yangu ilikuwa 'kosa kulelewa katika uislam'. Natambua kabisa kuwa mataifa yetu ya kiafrika ni maskini LAKINI Tanzania ni maskini kupindukia (we are below poverty line). Nchi kama Botswana na Namibia zipo mbali sana kutoka kwetu kimaendeleo, na Mwananchi mmoja wa Botswana alipohojiwa juu ya nini sababu ya mafanikio yao alisema hivi, 'There are people who think Botswana development is because of diamonds but if that is the reason, they need to understand that the same diamonds have been the cause of war and subsequently a source of poverty. If there is a reason behind Botswana achievement then it is not natural resources but we have been lucky, since independence we are have been blessed to have good and visionary leadership'.

Pamoja na kwamba nchi zote za kiafrika ni maskini lakini karibu nchi zote, pamoja na zile ambazo sehemu kubwa ya maeneo yao ni majangwa, zimekuwa na maendeleo makubwa zaidi ya kiuchumi kuliko Tanzania yenye rasiliamali nyingi za asili.

Tusikimbilie kwenye ukabila, udini, n.k. Daima tuyaangalie mambo katika uhalisia wake, tukiweza kufanya hivyo tutakuwa katika nafasi ya kuona kama malezi ya watoto wetu yanawajenga kuelekea tunakotaka tufike au hapana, kwa sababu tusingependa na wao waje waishi kwa shida na mateso kama tulivyo sisi. Mimi naamini kuwa malezi yetu yana mchango mkubwa kutufanya hivi tulivyo, kama ni watu wazuri au wabaya. Hatua ya kwanza ya maendeleo ni kuyatambua mapungufu yako na kuweka dhamira ya kubadilika. Kama kuna makuzi katika jamii ya Pwani yanayozorotesha maendeleo ya watu wake, ni lazima tuyakubali ili tuweke nia ya kubadilika.

Amani na ustawi wa Taifa hili utategemea sana maendeleo na ustawi wa watu wake wote wala siyo kundi fulani. Tukisema kuwa watu wa Pwani huzipa uzito mkubwa sherehe (wenyewe huita shughuli) kuliko kazi siyo dharau au dhihaka bali tunaitaja hiyo kama kasoro katika ustawi wa watu wake, na hapa tunaangalia jamii kubwa ya Pwani ambayo ipo vijijini na wala siyo kundi dogo la wasomi wa Pwani ambao wameachana na tabia hizo.

Bwana Kalamazoo, mimi naheshimu sana imani za watu, siyo uislam tu bali zote. Na utambue pia kuwa kwa vile jamii kubwa ya wakazi wa Pwani ni waisam, viongozi wa dini ya kiislam wana nafasi kubwa sana ya kubadilisha makuzi ya watu wa Pwani. Kupenda sherehe kuliko kufanya kazi sidhani kama ni hitaji la dini yeyote. Kufanya kazi kwa bidii, sidhani kama kuna dini yeyote inayozuia hilo. Kuongea sana kuliko kutenda, siamini kama ni hitaji la dini yeyote. Tusipende kukimbila kwenye dini, hata kwa yale mapungufu yetu ya kila siku, ili ionekane kuwa kutotimiza wajibu wetu kama raia na kama wazazi ni hitaji la dini, na hivyo anayetamka kuwa tabia hiyo siyo njema anaishambulia dini fulani.
 
Kwa maana hiyo wachagga hawafai kuwa Rais kwani ni watu ambao wana hulka ya kutafuta pesa hata kwa njia ya wizi ili mradi awe tajiri

Sioni uchambuzi katika hoja yako! Sijui umepata wapi takwimu zilizokuwezesha kufikia uamuzi huu kuhusu wachagga. Jambo usilolijua pengine ni kwamba watendaji wengi katika nafasi za Makatibu wakuu na mashirika yanayofanya vizuri katika taifa hili zimekaliwa na Wachagga. Sijui kama ni kwa bahati au ni kwa makusudi. Makampuni ya uzalishaji, huduma na habari yanayofanya vizuri yanamilikiwa au kuongozwa na wachagga. Hii mila kwamba aliyefanikiwa ni lazima awe ameiba ni potofu. Wapo wafanyabiashara wengi tunaowafahamu walivyoanza maisha kwa shida, wakijinyima na mwishowe wamefanikiwa, ipo mifano mingi. Lakini wengi wao ni wachagga, na sio wenzi.

Ukiacha Mramba ambaye anaonekana kuwa pande la fisadi, kwa nini tusingeweza kujumuisha kwamba Wasukuma mathalani ni Wezi wakubwa, kwa kuangalia waliohusika na kashfa kubwa za kifisadi katika taifa hilli- lakini ni sahihi kweli, yaani tumwone Chenge, Peter, Rostam(nasikia ni msukuma) nk kwamba hawa ni wasukuma!

Haka ni kale katabia kwa kuwaonea geri wachagga wanaojituma, waliotapakaa mipaka yote ya nchi kwa njia ya ndoa, biashara na kazi. Mimi nilidhani hawa wana utaifa na wanapaswa kupewa nafasi ya uongozi.
ku
 
Napenda kuheshimu maoni yako lakini utakuwa hukunitendea haki kusema kuwa dhamira yangu ilikuwa 'kosa kulelewa katika uislam'. Natambua kabisa kuwa mataifa yetu ya kiafrika ni maskini LAKINI Tanzania ni maskini kupindukia (we are below poverty line). Nchi kama Botswana na Namibia zipo mbali sana kutoka kwetu kimaendeleo, na Mwananchi mmoja wa Botswana alipohojiwa juu ya nini sababu ya mafanikio yao alisema hivi, 'There are people who think Botswana development is because of diamonds but if that is the reason, they need to understand that the same diamonds have been the cause of war and subsequently a source of poverty. If there is a reason behind Botswana achievement then it is not natural resources but we have been lucky, since independence we are have been blessed to have good and visionary leadership'.

Pamoja na kwamba nchi zote za kiafrika ni maskini lakini karibu nchi zote, pamoja na zile ambazo sehemu kubwa ya maeneo yao ni majangwa, zimekuwa na maendeleo makubwa zaidi ya kiuchumi kuliko Tanzania yenye rasiliamali nyingi za asili.

Tusikimbilie kwenye ukabila, udini, n.k. Daima tuyaangalie mambo katika uhalisia wake, tukiweza kufanya hivyo tutakuwa katika nafasi ya kuona kama malezi ya watoto wetu yanawajenga kuelekea tunakotaka tufike au hapana, kwa sababu tusingependa na wao waje waishi kwa shida na mateso kama tulivyo sisi. Mimi naamini kuwa malezi yetu yana mchango mkubwa kutufanya hivi tulivyo, kama ni watu wazuri au wabaya. Hatua ya kwanza ya maendeleo ni kuyatambua mapungufu yako na kuweka dhamira ya kubadilika. Kama kuna makuzi katika jamii ya Pwani yanayozorotesha maendeleo ya watu wake, ni lazima tuyakubali ili tuweke nia ya kubadilika.

Amani na ustawi wa Taifa hili utategemea sana maendeleo na ustawi wa watu wake wote wala siyo kundi fulani. Tukisema kuwa watu wa Pwani huzipa uzito mkubwa sherehe (wenyewe huita shughuli) kuliko kazi siyo dharau au dhihaka bali tunaitaja hiyo kama kasoro katika ustawi wa watu wake, na hapa tunaangalia jamii kubwa ya Pwani ambayo ipo vijijini na wala siyo kundi dogo la wasomi wa Pwani ambao wameachana na tabia hizo.

Bwana Kalamazoo, mimi naheshimu sana imani za watu, siyo uislam tu bali zote. Na utambue pia kuwa kwa vile jamii kubwa ya wakazi wa Pwani ni waisam, viongozi wa dini ya kiislam wana nafasi kubwa sana ya kubadilisha makuzi ya watu wa Pwani. Kupenda sherehe kuliko kufanya kazi sidhani kama ni hitaji la dini yeyote. Kufanya kazi kwa bidii, sidhani kama kuna dini yeyote inayozuia hilo. Kuongea sana kuliko kutenda, siamini kama ni hitaji la dini yeyote. Tusipende kukimbila kwenye dini, hata kwa yale mapungufu yetu ya kila siku, ili ionekane kuwa kutotimiza wajibu wetu kama raia na kama wazazi ni hitaji la dini, na hivyo anayetamka kuwa tabia hiyo siyo njema anaishambulia dini fulani.

Tatizo lako porojo nyingi halafu unakosa muelekeo, tuambie JK kama Rais na kutoka pwani kumeathiri nini kwa vigezo sahihi ya uongozi?

Vigezo ntakutajia achana na vipi anakuudhi anapotaja taarab blah blah hata sisi wengine tunakasirika kina mura na mangi wanavyongea ok!

Vigezo vya Uchumi ni barabara ngapi zimejengwa? pesa kiasi gani inakusanywa? utegemezi umepungua kiasi gani? (comperative statistics siyo blah blah zako za hapa JF ok?

Vigezo vya Kijamii ni Shule ngapi zimejengwa? Hospitali ngapi zimejengwa? walimu wamelipwa mafao yao? etc

Vigezo vya kisiasa ni issue za Good governance, nimesema jinsi alivyo ruhusu CAG kuwahoji miungu watu katika halmashauri etc...

Hivyo ni vitu vya kuongea siyo huyu mswahili/mtu wa pwani/ mtu kalelewa na kanisa so what?

Sasa inakuonyesha tu kwamba una element za kibaguzi backward thinking

Watu wa pwani wasingefanya kazi si wangekuwa omba omba kwa watu dodoma? streotype?
 
Napenda kuheshimu maoni yako lakini utakuwa hukunitendea haki kusema kuwa dhamira yangu ilikuwa 'kosa kulelewa katika uislam'. Natambua kabisa kuwa mataifa yetu ya kiafrika ni maskini LAKINI Tanzania ni maskini kupindukia (we are below poverty line). Nchi kama Botswana na Namibia zipo mbali sana kutoka kwetu kimaendeleo, na Mwananchi mmoja wa Botswana alipohojiwa juu ya nini sababu ya mafanikio yao alisema hivi, 'There are people who think Botswana development is because of diamonds but if that is the reason, they need to understand that the same diamonds have been the cause of war and subsequently a source of poverty. If there is a reason behind Botswana achievement then it is not natural resources but we have been lucky, since independence we are have been blessed to have good and visionary leadership'.

Pamoja na kwamba nchi zote za kiafrika ni maskini lakini karibu nchi zote, pamoja na zile ambazo sehemu kubwa ya maeneo yao ni majangwa, zimekuwa na maendeleo makubwa zaidi ya kiuchumi kuliko Tanzania yenye rasiliamali nyingi za asili.

Tusikimbilie kwenye ukabila, udini, n.k. Daima tuyaangalie mambo katika uhalisia wake, tukiweza kufanya hivyo tutakuwa katika nafasi ya kuona kama malezi ya watoto wetu yanawajenga kuelekea tunakotaka tufike au hapana, kwa sababu tusingependa na wao waje waishi kwa shida na mateso kama tulivyo sisi. Mimi naamini kuwa malezi yetu yana mchango mkubwa kutufanya hivi tulivyo, kama ni watu wazuri au wabaya. Hatua ya kwanza ya maendeleo ni kuyatambua mapungufu yako na kuweka dhamira ya kubadilika. Kama kuna makuzi katika jamii ya Pwani yanayozorotesha maendeleo ya watu wake, ni lazima tuyakubali ili tuweke nia ya kubadilika.

Amani na ustawi wa Taifa hili utategemea sana maendeleo na ustawi wa watu wake wote wala siyo kundi fulani. Tukisema kuwa watu wa Pwani huzipa uzito mkubwa sherehe (wenyewe huita shughuli) kuliko kazi siyo dharau au dhihaka bali tunaitaja hiyo kama kasoro katika ustawi wa watu wake, na hapa tunaangalia jamii kubwa ya Pwani ambayo ipo vijijini na wala siyo kundi dogo la wasomi wa Pwani ambao wameachana na tabia hizo.

Bwana Kalamazoo, mimi naheshimu sana imani za watu, siyo uislam tu bali zote. Na utambue pia kuwa kwa vile jamii kubwa ya wakazi wa Pwani ni waisam, viongozi wa dini ya kiislam wana nafasi kubwa sana ya kubadilisha makuzi ya watu wa Pwani. Kupenda sherehe kuliko kufanya kazi sidhani kama ni hitaji la dini yeyote. Kufanya kazi kwa bidii, sidhani kama kuna dini yeyote inayozuia hilo. Kuongea sana kuliko kutenda, siamini kama ni hitaji la dini yeyote. Tusipende kukimbila kwenye dini, hata kwa yale mapungufu yetu ya kila siku, ili ionekane kuwa kutotimiza wajibu wetu kama raia na kama wazazi ni hitaji la dini, na hivyo anayetamka kuwa tabia hiyo siyo njema anaishambulia dini fulani.

Jaribu kutulia ktk hoja zako. Mwanzo ulianza na watu wa pwani na sasa umerukia Botswana lakin hukueleza kua wale watu wa Botswala ni watu wa bara au pwani, relevance? Jaribu kua makini ktk kujenga hoja, ninachokiona sasa ni kua unapoteza muelekeo.

Anyway kanuni za uongozi bora zinaeleweka na hazina uhusiano na ubara au upwani. Tunachohitaji ni kila raia kua serious na sio rais peke yake kwa sababu rais muajiri wake ni raia. Raia wakiwa serious wanachokitaka kinakua na huo ndio uhalisia. Naomba urekebishe msemo wako wa kujadili uongozi bora kwa kigezo cha upwani na bara kwa kua ni wa kimakosa.

Kwanini unakataa watu wasistarehe sasa nini faida ya kufanya kazi kwa bidii. Unafanya kazi kwa bidii ukimaliza unastarehe otherwise utakua huna maisha hapa duniani hasa kwa wale ndugu zetu ambao hawana dini. Starehe ni moja ya vitu muhimu ktk maisha ya binadamu, hata hao viongozi unaowasifu wote wanatembea na magari kama hawapendi starehe wangetembea kwa mguu tu au wangepanda punda.
 
Aloleta thread hii nae angetuambia ni mtu wa wapi ili tutathmini uelewa wake kwani analidanganya Taifa Hadharani eti JK anaendeleza ombaomba WB statistics shows Budget yetu ina depend Donors by 28 % while Mkapa aliacha 48% je kitu gan kinamfanya asitambue kupungua kwa Uombaomba ni Chuki au tatizo la Eneo alilotoka? anajaribu kumhusisha Mkapa na Malezi ya Ndanda, atueleze Contribution ya malezi hayo kwenye Wizi wa Rasilimali za Taifa kama Nyumba za Serikali, Migodi ya kiwira, kuanzisha biashara Ikulu,Meremeta, Epa, n.k ,By now anapaswa kutambua kuwa JK AMEINGIA KWENYE hISTORIA YA KUWABURUZA vigogo wengi zaidi Mahakamani, mawaziri 2, makatibu na watumishi wengine wakubwa na mabalozi anaebisha atoe data za kupinga hili, akina Mahalu, mgonja, mramba,liyumba, patel tumewashuhudia cortin, kama Nyerere alifia Record hii mtu ajitokeze alete ushahidi,Demokrasia imeshehena zaidi kuliko kipindi chochote anaebisha aje na ushahidi, kabla ya kumuona mzee Mwinyi kuwa ni mzembe atu alete ushahidi wa hali ya uchumi 1985 wakati anaingia tufanye tathmini na wakati anaondoka tuone kama alivurunda au ni kitchen words,
Mmesahau kuwa Ubishi wa Nyrere wa kupinga :Mawzo ya Hayati Kambona kwenye Azimio la Arusha, Edwin Mtei kwenye sera za kiuchumi, Mzee Christopher Kasanga Tumbo kwenye Operation vijiji ndo matokeo ya haya tunayoyaona,

Tafadhali usifiche ajenda yako ya siri kwenye kichaka cha umaeneo, tushafyeka kichaka hicho weka ajenda yako hadharani bila woga,

Unapotoa hoja, toa hoja. Huna sababu ya kufikiria kuwa kuna ajenda ya siri. Umetoa takwimu zako, ni vizuri sana, hiyo ndiyo inayoeleza uzito wa argument yako. Naomba usome vizuri hoja yangu ili uweze kuelewa nilichokusudia kusema. Katika hoja yangu, kikubwa nlichokielezea ni jinsi makuzi ya mtu yanavyomwathiri mhusika katika maisha yake ya kila siku. Nilipomwelezea Mwalimu Nyerere na Mkapa, nimeelezea uwezo wa kusimamia mambo wanayoyaamini bila ya kujali kama ni mazuri au mabaya. Huwezi kupata shida kujua kama Nyerere au Mkapa walikuwa wanataka nini bila ya kujali kama kitu hicho ni kibaya au kizuri. Angalia uwezo na dhamira ya kusimamia waliyokuwa wanataka.

Kikwete kama walivyo watu wengi wa Pwani, ni vigumu sana kujua anataka nini (si moto si baridi), mtu asiyetaka kuwa na maadui. Hatujui kama yupo na sisi raia wema au yupo na mafisadi maana kote kote yupo. Akija kwetu anatuambia kuwa hana suluhu na mafisadi, TAKUKURU amewapa mamlaka yote, wawashughulikie LAKINI anaenda Kilimanjaro anasema, 'Mramba ni jembe la zamani, makali yale yale'; anaenda Monduli anasema, 'Sijawahi kuona kiongozi mzuri kama Lowasa'. Tabia ya ukigeugeu. Mwalimu alikuwa akisema kiongozi huyu hafai, atalisimamia hilo analoliamini mpaka mwisho.

JK kuwapeleka watuhumiwa wa EPA haikuwa matakwa yake bali lilikuwa ni sharti alilopewa na nchi wahisani kuwa wasingesaidia budget mpaka waone hatua zinachukuliwa dhidi ya mafisadi, na ndipo mashtaka dhaifu yalipoandaliwa dhidi yao. Nayo hiyo ni ile ile tabia yake ya kutaka kuonekana anachukia ufisadi ingawa siyo dhamira yake kuondoa na kuwachukulia hatua mafisadi. Najua angekuwa Mkapa, kwa vile hao mafisadi walitenda yote kwa blessing zake, angesema kuwa, 'siwezi kuwapeleka', na sisi wote tungejua kuwa Mkapa na mafisadi lao moja. Kikwete, watu wengi hawajui yupo kwa mafisadi au kwa Watanzania walio wengi.

Mambo mengine tutakuwa tunaenda nje ya mada lakini takwimu umezichukua na kuzibandika bila ya kuelewa tafsiri yake. Kwa ufupi tu ni kuwa pamoja na madudu yote aliyofanya Mkapa katika kipindi chake cha pili lakini alifanya kazi kubwa sana kwenye uchumi. Aliingia kwenye madaraka uchumi ukiwa umeparanganyika kabisa kiasi cha hata mataifa wahisani kusimamisha misaada yote, hazina ikiwa haina kitu zaidi ya madeni makubwa ya kupindukia. Inflation ikiwa 30%, ujenzi wa miradi mipya ikiwa pamoja na barabara vikiwa vimesimama. Aliishusha inflation mpaka 4% ambayo JK mwakajana aliwahi kuifikisha mpaka 17%. Taratibu Mkapa alianza kuujenga uchumi na kuweka misingi imara ya uchumi. Aliingia ikulu hazina ikiwa haina kitu, akaondoka akiwa ameacha U$5 billion.

Kipindi cha Mwinyi, wahisani wakiwa wamechoshwa na siasa za kijamaa za Mwalimu Nyerere, wakitaka kuonesha uzuri wa uchumi wa kireberali, walitoa misaada mingi kwa Tanzania kuliko kipindi chochote cha uhai wa Tanzania. Wastani wa misaada kipindi hicho ulifia U$800 kwa kila familia. Lakini pesa hiyo yote ilipotea, na Mzee Mwinyi aliondoka huku hazina haina chochote zaidi ya madeni makubwa. Kipindi hicho hakuna miradi mikubwa yoyote iliyowahi kujengwa. Kipindi cha Mwinyi hakuna barabara mpya iliyojegwa, hakuna hospitali kubwa iliyojengwa, hakuna vyuo vikubwa vilivyojengwa, pesa yote iliishia kujenga nyumba za watu binafsi huko Mikocheni na Mbesi beach.

Mwalimu Nyerere aliongoza katika kipindi kirefu, alifanya vizuri sana kipindi cha Mwanzo. Hakuna Rais yeyote aliyeanzisha miradi mingi mikubwa zaidi ya Mwalimu Nyerere. Barabara ndefu za rami (baadaye alishindwa kuzitunza), shule, vyuo, hospitali, taasisi za utafiti, na hata viwanda ambavyo vilikuja kuuzwa baadaye kama vya sigara, bia, nyama, nguo, vifaa vya kilimo, n.k. ni miradi mikubwa ya Mwalimu.

JK ameingia katika utawala kukiwa tayari kuna misingi mizuri ya uchumi, na kama angekuwa makini Tanzania ingepaa. Tatizo lake kubwa ni kuwa haeleweki anasimamia nini, anataka afanikiwe katika kuleta maendeleo bila kusimamia mapato ya serikali. Mapato yameongezeka sana lakini uwekezaji katika miradi ya maendeleo umeendelea kutegemea wahisani. Kiongozi yeyote makini ni lazima ajitambulishe mambo makubwa ya msingi anayoyasimamia, na watu wajue kuwa wewe kiongozi unataka nini. Hata unapokuwa Manager, secretary wako, na watu unawaongoza ni lazima wajue kuwa, nikitaka kumfurahisha manager wangu ni lazima nifanye hiki na kile, na nikifanya jambo fulani Manager wangu kamwe hawezi kunisamehe. Hiyo JK hana, sababu ni nini, ni suala lake binafsi ndivyo alivyo au ni makuzi yake?
 
Jaribu kutulia ktk hoja zako. Mwanzo ulianza na watu wa pwani na sasa umerukia Botswana lakin hukueleza kua wale watu wa Botswala ni watu wa bara au pwani, relevance? Jaribu kua makini ktk kujenga hoja, ninachokiona sasa ni kua unapoteza muelekeo.

Anyway kanuni za uongozi bora zinaeleweka na hazina uhusiano na ubara au upwani. Tunachohitaji ni kila raia kua serious na sio rais peke yake kwa sababu rais muajiri wake ni raia. Raia wakiwa serious wanachokitaka kinakua na huo ndio uhalisia. Naomba urekebishe msemo wako wa kujadili uongozi bora kwa kigezo cha upwani na bara kwa kua ni wa kimakosa.

Kwanini unakataa watu wasistarehe sasa nini faida ya kufanya kazi kwa bidii. Unafanya kazi kwa bidii ukimaliza unastarehe otherwise utakua huna maisha hapa duniani hasa kwa wale ndugu zetu ambao hawana dini. Starehe ni moja ya vitu muhimu ktk maisha ya binadamu, hata hao viongozi unaowasifu wote wanatembea na magari kama hawapendi starehe wangetembea kwa mguu tu au wangepanda punda.

Nashukuru kwa maoni yako. Nimeitaja Botswana kwa vile tu niliyekuwa nikimjibu alikuwa ameeleza kuwa nchi zote za Afrika ni maskini, na hivyo kuonesha kuwa tatizo ni uafrika wetu wala siyo makuzi yetu.
 
Nashukuru kwa maoni yako. Nimeitaja Botswana kwa vile tu niliyekuwa nikimjibu alikuwa ameeleza kuwa nchi zote za Afrika ni maskini, na hivyo kuonesha kuwa tatizo ni uafrika wetu wala siyo makuzi yetu.

Kwahiyo hoja ya ubara na pwani unaitupilia mbali?
 
Ushauri: Kuanzia sasa watu wa pwani marufuku kupewa uraisi, iandikwe hivyo kwenye katiba yetu mpya au mwasemaje wandugu zangu wa chadema?
Maana iko clear kwamba matatizo yote ya nchi hii chanzo ni mwinyi, kikwete.
Nyerere is a saint, he never sinned, or did anything wrong!!
Na tena.. Ahh nlisahau kwa sababu waislamu wote wana mambo ya upwani nao pia wasiwe maraisi wa nchi hii. Iwekwe pia kwenye katiba. Mwasemaje?
 
Tatizo lako ni udini tu!!
unapotoa hoja, toa hoja. Huna sababu ya kufikiria kuwa kuna ajenda ya siri. Umetoa takwimu zako, ni vizuri sana, hiyo ndiyo inayoeleza uzito wa argument yako. Naomba usome vizuri hoja yangu ili uweze kuelewa nilichokusudia kusema. Katika hoja yangu, kikubwa nlichokielezea ni jinsi makuzi ya mtu yanavyomwathiri mhusika katika maisha yake ya kila siku. Nilipomwelezea mwalimu nyerere na mkapa, nimeelezea uwezo wa kusimamia mambo wanayoyaamini bila ya kujali kama ni mazuri au mabaya. Huwezi kupata shida kujua kama nyerere au mkapa walikuwa wanataka nini bila ya kujali kama kitu hicho ni kibaya au kizuri. Angalia uwezo na dhamira ya kusimamia waliyokuwa wanataka.

Kikwete kama walivyo watu wengi wa pwani, ni vigumu sana kujua anataka nini (si moto si baridi), mtu asiyetaka kuwa na maadui. Hatujui kama yupo na sisi raia wema au yupo na mafisadi maana kote kote yupo. Akija kwetu anatuambia kuwa hana suluhu na mafisadi, takukuru amewapa mamlaka yote, wawashughulikie lakini anaenda kilimanjaro anasema, 'mramba ni jembe la zamani, makali yale yale'; anaenda monduli anasema, 'sijawahi kuona kiongozi mzuri kama lowasa'. Tabia ya ukigeugeu. Mwalimu alikuwa akisema kiongozi huyu hafai, atalisimamia hilo analoliamini mpaka mwisho.

Jk kuwapeleka watuhumiwa wa epa haikuwa matakwa yake bali lilikuwa ni sharti alilopewa na nchi wahisani kuwa wasingesaidia budget mpaka waone hatua zinachukuliwa dhidi ya mafisadi, na ndipo mashtaka dhaifu yalipoandaliwa dhidi yao. Nayo hiyo ni ile ile tabia yake ya kutaka kuonekana anachukia ufisadi ingawa siyo dhamira yake kuondoa na kuwachukulia hatua mafisadi. Najua angekuwa mkapa, kwa vile hao mafisadi walitenda yote kwa blessing zake, angesema kuwa, 'siwezi kuwapeleka', na sisi wote tungejua kuwa mkapa na mafisadi lao moja. Kikwete, watu wengi hawajui yupo kwa mafisadi au kwa watanzania walio wengi.

Mambo mengine tutakuwa tunaenda nje ya mada lakini takwimu umezichukua na kuzibandika bila ya kuelewa tafsiri yake. Kwa ufupi tu ni kuwa pamoja na madudu yote aliyofanya mkapa katika kipindi chake cha pili lakini alifanya kazi kubwa sana kwenye uchumi. Aliingia kwenye madaraka uchumi ukiwa umeparanganyika kabisa kiasi cha hata mataifa wahisani kusimamisha misaada yote, hazina ikiwa haina kitu zaidi ya madeni makubwa ya kupindukia. Inflation ikiwa 30%, ujenzi wa miradi mipya ikiwa pamoja na barabara vikiwa vimesimama. Aliishusha inflation mpaka 4% ambayo jk mwakajana aliwahi kuifikisha mpaka 17%. Taratibu mkapa alianza kuujenga uchumi na kuweka misingi imara ya uchumi. Aliingia ikulu hazina ikiwa haina kitu, akaondoka akiwa ameacha u$5 billion.

Kipindi cha mwinyi, wahisani wakiwa wamechoshwa na siasa za kijamaa za mwalimu nyerere, wakitaka kuonesha uzuri wa uchumi wa kireberali, walitoa misaada mingi kwa tanzania kuliko kipindi chochote cha uhai wa tanzania. Wastani wa misaada kipindi hicho ulifia u$800 kwa kila familia. Lakini pesa hiyo yote ilipotea, na mzee mwinyi aliondoka huku hazina haina chochote zaidi ya madeni makubwa. Kipindi hicho hakuna miradi mikubwa yoyote iliyowahi kujengwa. Kipindi cha mwinyi hakuna barabara mpya iliyojegwa, hakuna hospitali kubwa iliyojengwa, hakuna vyuo vikubwa vilivyojengwa, pesa yote iliishia kujenga nyumba za watu binafsi huko mikocheni na mbesi beach.

Mwalimu nyerere aliongoza katika kipindi kirefu, alifanya vizuri sana kipindi cha mwanzo. Hakuna rais yeyote aliyeanzisha miradi mingi mikubwa zaidi ya mwalimu nyerere. Barabara ndefu za rami (baadaye alishindwa kuzitunza), shule, vyuo, hospitali, taasisi za utafiti, na hata viwanda ambavyo vilikuja kuuzwa baadaye kama vya sigara, bia, nyama, nguo, vifaa vya kilimo, n.k. Ni miradi mikubwa ya mwalimu.

Jk ameingia katika utawala kukiwa tayari kuna misingi mizuri ya uchumi, na kama angekuwa makini tanzania ingepaa. Tatizo lake kubwa ni kuwa haeleweki anasimamia nini, anataka afanikiwe katika kuleta maendeleo bila kusimamia mapato ya serikali. Mapato yameongezeka sana lakini uwekezaji katika miradi ya maendeleo umeendelea kutegemea wahisani. Kiongozi yeyote makini ni lazima ajitambulishe mambo makubwa ya msingi anayoyasimamia, na watu wajue kuwa wewe kiongozi unataka nini. Hata unapokuwa manager, secretary wako, na watu unawaongoza ni lazima wajue kuwa, nikitaka kumfurahisha manager wangu ni lazima nifanye hiki na kile, na nikifanya jambo fulani manager wangu kamwe hawezi kunisamehe. Hiyo jk hana, sababu ni nini, ni suala lake binafsi ndivyo alivyo au ni makuzi yake?
 
REFER HII PARAGRAPH:
Mwalimu Nyerere aliongoza katika kipindi kirefu, alifanya vizuri sana kipindi cha Mwanzo. Hakuna Rais yeyote aliyeanzisha miradi mingi mikubwa zaidi ya Mwalimu Nyerere. Barabara ndefu za rami (baadaye alishindwa kuzitunza), shule, vyuo, hospitali, taasisi za utafiti, na hata viwanda ambavyo vilikuja kuuzwa baadaye kama vya sigara, bia, nyama, nguo, vifaa vya kilimo, n.k. ni miradi mikubwa ya Mwalimu.

VIWANDA VILISHAKUFA!!


Unapotoa hoja, toa hoja. Huna sababu ya kufikiria kuwa kuna ajenda ya siri. Umetoa takwimu zako, ni vizuri sana, hiyo ndiyo inayoeleza uzito wa argument yako. Naomba usome vizuri hoja yangu ili uweze kuelewa nilichokusudia kusema. Katika hoja yangu, kikubwa nlichokielezea ni jinsi makuzi ya mtu yanavyomwathiri mhusika katika maisha yake ya kila siku. Nilipomwelezea Mwalimu Nyerere na Mkapa, nimeelezea uwezo wa kusimamia mambo wanayoyaamini bila ya kujali kama ni mazuri au mabaya. Huwezi kupata shida kujua kama Nyerere au Mkapa walikuwa wanataka nini bila ya kujali kama kitu hicho ni kibaya au kizuri. Angalia uwezo na dhamira ya kusimamia waliyokuwa wanataka.

Kikwete kama walivyo watu wengi wa Pwani, ni vigumu sana kujua anataka nini (si moto si baridi), mtu asiyetaka kuwa na maadui. Hatujui kama yupo na sisi raia wema au yupo na mafisadi maana kote kote yupo. Akija kwetu anatuambia kuwa hana suluhu na mafisadi, TAKUKURU amewapa mamlaka yote, wawashughulikie LAKINI anaenda Kilimanjaro anasema, 'Mramba ni jembe la zamani, makali yale yale'; anaenda Monduli anasema, 'Sijawahi kuona kiongozi mzuri kama Lowasa'. Tabia ya ukigeugeu. Mwalimu alikuwa akisema kiongozi huyu hafai, atalisimamia hilo analoliamini mpaka mwisho.

JK kuwapeleka watuhumiwa wa EPA haikuwa matakwa yake bali lilikuwa ni sharti alilopewa na nchi wahisani kuwa wasingesaidia budget mpaka waone hatua zinachukuliwa dhidi ya mafisadi, na ndipo mashtaka dhaifu yalipoandaliwa dhidi yao. Nayo hiyo ni ile ile tabia yake ya kutaka kuonekana anachukia ufisadi ingawa siyo dhamira yake kuondoa na kuwachukulia hatua mafisadi. Najua angekuwa Mkapa, kwa vile hao mafisadi walitenda yote kwa blessing zake, angesema kuwa, 'siwezi kuwapeleka', na sisi wote tungejua kuwa Mkapa na mafisadi lao moja. Kikwete, watu wengi hawajui yupo kwa mafisadi au kwa Watanzania walio wengi.

Mambo mengine tutakuwa tunaenda nje ya mada lakini takwimu umezichukua na kuzibandika bila ya kuelewa tafsiri yake. Kwa ufupi tu ni kuwa pamoja na madudu yote aliyofanya Mkapa katika kipindi chake cha pili lakini alifanya kazi kubwa sana kwenye uchumi. Aliingia kwenye madaraka uchumi ukiwa umeparanganyika kabisa kiasi cha hata mataifa wahisani kusimamisha misaada yote, hazina ikiwa haina kitu zaidi ya madeni makubwa ya kupindukia. Inflation ikiwa 30%, ujenzi wa miradi mipya ikiwa pamoja na barabara vikiwa vimesimama. Aliishusha inflation mpaka 4% ambayo JK mwakajana aliwahi kuifikisha mpaka 17%. Taratibu Mkapa alianza kuujenga uchumi na kuweka misingi imara ya uchumi. Aliingia ikulu hazina ikiwa haina kitu, akaondoka akiwa ameacha U$5 billion.

Kipindi cha Mwinyi, wahisani wakiwa wamechoshwa na siasa za kijamaa za Mwalimu Nyerere, wakitaka kuonesha uzuri wa uchumi wa kireberali, walitoa misaada mingi kwa Tanzania kuliko kipindi chochote cha uhai wa Tanzania. Wastani wa misaada kipindi hicho ulifia U$800 kwa kila familia. Lakini pesa hiyo yote ilipotea, na Mzee Mwinyi aliondoka huku hazina haina chochote zaidi ya madeni makubwa. Kipindi hicho hakuna miradi mikubwa yoyote iliyowahi kujengwa. Kipindi cha Mwinyi hakuna barabara mpya iliyojegwa, hakuna hospitali kubwa iliyojengwa, hakuna vyuo vikubwa vilivyojengwa, pesa yote iliishia kujenga nyumba za watu binafsi huko Mikocheni na Mbesi beach.

Mwalimu Nyerere aliongoza katika kipindi kirefu, alifanya vizuri sana kipindi cha Mwanzo. Hakuna Rais yeyote aliyeanzisha miradi mingi mikubwa zaidi ya Mwalimu Nyerere. Barabara ndefu za rami (baadaye alishindwa kuzitunza), shule, vyuo, hospitali, taasisi za utafiti, na hata viwanda ambavyo vilikuja kuuzwa baadaye kama vya sigara, bia, nyama, nguo, vifaa vya kilimo, n.k. ni miradi mikubwa ya Mwalimu.

JK ameingia katika utawala kukiwa tayari kuna misingi mizuri ya uchumi, na kama angekuwa makini Tanzania ingepaa. Tatizo lake kubwa ni kuwa haeleweki anasimamia nini, anataka afanikiwe katika kuleta maendeleo bila kusimamia mapato ya serikali. Mapato yameongezeka sana lakini uwekezaji katika miradi ya maendeleo umeendelea kutegemea wahisani. Kiongozi yeyote makini ni lazima ajitambulishe mambo makubwa ya msingi anayoyasimamia, na watu wajue kuwa wewe kiongozi unataka nini. Hata unapokuwa Manager, secretary wako, na watu unawaongoza ni lazima wajue kuwa, nikitaka kumfurahisha manager wangu ni lazima nifanye hiki na kile, na nikifanya jambo fulani Manager wangu kamwe hawezi kunisamehe. Hiyo JK hana, sababu ni nini, ni suala lake binafsi ndivyo alivyo au ni makuzi yake?
 
Wataalam wa Saikoljia watanisaidia pia, lakini ni ukweli kuwa miaka ya mwanzo ya malezi yako, 3 mpaka 15, humtengeneza binadamu, na ndiyo ina uwezekano mkubwa wa kuelezea binadamu atakuwa wa namna gani atakapokuwa mtu mzima. Mtoto huangalia mazingira yake, watu wanaongeaje, wanafanya nini, wanaishi vipi, n.k. Mtoto anayesikia kila siku watu wakitukanana, akiona watu asubuhi wakinywa pombe na kucheza ngoma, akiona watu wanaombaomba, au akiona wazazi wake saa 12 asubuhi wanakwenda mashambani, n.k, uwezekano mkubwa ndivyo mtoto huyo atakavyokuwa siku atakapokuwa mtu mzima, hata kama si kwa 100%.

Wengine wanaweza kufikiria kuwa nazungumzia kishabiki lakini siyo nia yangu. Waangalieni marais wetu, kuanzia Mwl. Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Mkapa na Jakaya Kikwete. Pamoja na kwamba walisoma, wameishi maeneo mbalimbali, wamesafiri nchi mbalimbali lakini kuna nafasi fulani utaona mazingira waliyokulia yakionekana katika maisha na utendaji wao wa kazi.

Mwalimu alitoka Musoma, watu wengi wa Musoma huwa ni straight forward - kisu huitwa kisu, na panga huitwa panga. Mwalimu hakuwa na shida ya kueleza au kutamka anachotaka, iwe ni kizuri au kibaya. Sikiliza hotuba zake, ni zile zenye kuweka wazi msimamo wake bila kuzunguka au kuwa katika nafasi isiyoeleweka. Sikumbuki kusikia akitoa mfano wa chakula, ngoma, n.k. Kwa makabila mengi ya bara, chakula siyo jambo linalopewa umuhimu sana, wao alimradi tumbo limejaa, kumuwezesha kufanya kazi.

Akaja Mzee wetu Mwinyi, huyu ni mswahili wa Unguja. Ukisikiliza hotuba zake mara nyingi usingekosa kumsikia mifano yake ya ubwabwa, pilau, biriani, visu vya kukatia mboga, nyanya, n.k. Kwa watu wa Pwani chakula kina heshima kubwa sana, mtu mzima kabisa anaweza kupewa rushwa ya pilau, na rushwa hiyo ikafanya kazi. Mwinyi hotuba zake nyingi alikuwa akitumia mifano ya chakula hata kwenye masuala makubwa kabisa ya kitaifa. Maneno yalikuwa mengi sana lakini matendo yalikuwa kidogo, na watu wengi kipindi chake walifanya kama walivyotaka - ruksa kwa kila kitu. Wapo waliomsema sana na kumdhihaki kwa maneno ya kejeli za kila namna, haikumpa shida sana hiyo. Watu wa Pwani ni watu wenye maneno mengi sana, na kwao maneno yanayotamkwa huwa hayana uzito wowote, awe anatukanwa au kufanyiwa kejeli kwao huwa ni sehemu ya maisha. Ndiyo maana kipindi cha Mwinyi watu waliona kuwa demokrasia ya kusema ilikuwa imeongezeka sana, wasingeweza kuthubutu kutamka maneno hayo hayo akiwepo Mwalimu Nyerere. Kwa watu wa bara kila neno hupimwa na kutafsiriwa, na hata katika maisha ya kawaida watu wanaweza wasielewane maisha yao yote kutokana na maneno fulani ya kejeli yaliyozungumzwa na mmoja dhidi ya mwenzie.

Akaja Benjamin Mkapa, huyu japo sina uhakika na mazingira ya familia yake lakini ninachojua ni kuwa alisoma na kukulia mazingira ya Wamisionari wa Ndanda, ambao pia maisha yao hayana tofauti na watu wa bara, hawataki mtu awe ombaomba, wanasisitiza sana kuzingatia muda na kufanya kazi kwa bidii, na hupenda zaidi matendo kuliko maneno (ndiyo falsafa ya Biblia). Mkapa kila mara alisema anachukia sana kuomba. Mkapa alipokuwa Rais, ukimlinganisha na mtangulizi wake, alikuwa ni mtu ambaye alitaka kifanyike kitu anachotaka yeye kufanyika, haijalishi kama ni kizuri au kibaya alimradi kama yeye anaamini kuwa ni kizuri. Hotuba na matendo yake vilionesha wazi kuwa hakujali kama watu watampenda au kumchukia, bali yeye alijali anachotaka yeye kifanyike. Nakumbuka kuna wakati alitamka kuwa, 'Serikali itafanya kazi na wanaouchukia umaskini, wanaopenda umaskini itawaacha waendelee nao', hii ni kauli ya mtu asiyebembeleza.

Hatimaye amekuja JK, Mkwere aliyekulia mazingira ya Pwani yenye tabia za uswahili. Makabila mengi ya Pwana, watu wake ni wenye maneno mengi sana, na aghalabu maneno hayo, mengi huwa ni utani na uwongo, na huwa hakuna uzito wowote katika yale yanayotamkwa. Watu wa Pwani unaweza kumtukana hata matuzi ya nguoni lakini wala isimsumbue sana, mwishowe kama una chochote, ukampa, yote huyasahau kabisa, na wewe huwa ni rafiki yake mkubwa. Hata humu kwenye JF, hata bila ya kuambiwa, unaweza ukajua yupi ni mtu wa Pwani na yupi ni mtu bara. Wanaendeshwa na msemo wa, 'Mkono mtupu haulambwi'. Tabia hiyo ni tofauti sana na makabila ya bara ambapo ukimkejeli mtu hata kama ni maskini, unaweza hata kumpa msaada akaukataa - akaona aheri aishi kwa shida kuliko kudharaulika. Hiyo ndiyo maana ya maskini jeuri.

Watu wa Pwani hupenda sana starehe hata kama hana kipato. Wanathamini sana sherehe, ngoma, kazi za kuongea kuliko zile za kutumia misuli. Huamini kuwa wao ni maskini, na hivyo wao wanastahili kusaidiwa, hawawezi kubadili hali hiyo. Ukimtazama Rais wetu, anapenda sana kuomba (aliwahi pia kutamka kuwa sisi ni maskini na huko nje kuna pesa nyingi, tunachotakiwa ni kueleza ili watuelewe; huwa anaenda nje kuhemea, n.k), anapenda sana kuongea (matendo hakuna), hasumbuliwi na maneno wala kejeli wanazozitoa wananchi wengi dhidi yake, anapenda sana michezo (yeye mwenyewe alisema anapenda sana mpira na dansi), na kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa bunge safari hii ameelezea kuwa ameridhishwa sana na maendele ya sanaa (muziki, tamthilia, na akawataja wanamuziki wa taarabu kama mfano wa mafanikio).

Ninachojiuliza, utendaji usioridhisha wa Rais wetu ni upungufu wake binafsi au matokeo ya mazingira aliyokulia? Na ikiwa ndiyo hivyo, kuna umuhimu wowote wa kuangalia mazingira ya mtu aliyokulia kabla ya kumchagua kuwa kiongozi mkuu wa nchi? Na je, ikifanyika hivyo itakuwa ni ubaguzi wa kikabila au kimaeneo? Kama tunataka viongozi wazuri na watakaofanya mambo ya kusaidia nchi yetu, tunafanya nini katika kuwaandalia mazingira watoto wetu yasiyo hasi kwa maendeleo ili waje kuwa viongozi wazuri na raia wenye mchango mkubwa kwa Taifa letu?


ni uhuru wako kusema chochote.mi ni mtu wa bara lakin nakataa kabisa na uchambuzi wako.hali halisi inaonesha kuwa maendeleo yalianzia pwani,hata sasa linganisha dsm na mkoa wowote wa bara hadi ukizungumza tz unamaanisha dsm ambao ni mkoa wa pwani,mchango mkubwa wa maendeleo haya ya pwani ni watu wake hasa wenyeji.kama isingekuwa ni siasa ya nyerere ya kuwabeba wabara na kuwanyanyapaa wapwani baada ya uhuru kamwe haya usingeyaongea.umaskin wa nchi yetu hautokani na mwinyi wala jk,mchango mkubwa wa umaskin unaanzia kwa nyerere.kwanza siasa ya ujamaa,pili rasilimali zetu nyingi zilitumika ktk ukombozi wa mataifa yaliyokuwa bado makoloni.tatu viwanda unavyosema vingi havikuanzishwa na nyerere bali alivitaifisha na ndio maana vikamshinda kuviendesha,tano vita vya kagera ambavyo havikuwa vya lazima.sita madini hayakchimbwa wakati wake ispokuwa almasi mwadui na makaburu nasi hatukunufaika nayo.nyerere nchi ilimshinda akaamua kuachia ngazi.mwinyi alichukua nchi iliyofilisika kabisaa,nchi haikuwa na pesa na watu hawakuwa na kitu hata bidhaa muhim sana kama sembe,sukari,sabuni,mafuta ya aina zote.pengine sifa moja ya kuomba ndio ilimsaidia mwinyi kutoka ktk nchi muflisi hadi watu wakawa na pesa,nyerere aliacha barabara zote za dar ni mashimo matupu ziliboreshwa kipindi cha mwinyi.eg ali h mwinyi rd,kawawa rd,morogoro rd nk.ni mengi ya kuandika ngoja niishie hapa ila nilichogundua kwako ni udini tu ndio maana uakmtaja mkapa na biblia ukimaanisha biblia ndio iliyomshepu na kumpa tabia aliyonayo,umejificha kwenye upwani tu lakin ulimaanisha uislam
 
Wataalam wa Saikoljia watanisaidia pia, lakini ni ukweli kuwa miaka ya mwanzo ya malezi yako, 3 mpaka 15, humtengeneza binadamu, na ndiyo ina uwezekano mkubwa wa kuelezea binadamu atakuwa wa namna gani atakapokuwa mtu mzima. Mtoto huangalia mazingira yake, watu wanaongeaje, wanafanya nini, wanaishi vipi, n.k. Mtoto anayesikia kila siku watu wakitukanana, akiona watu asubuhi wakinywa pombe na kucheza ngoma, akiona watu wanaombaomba, au akiona wazazi wake saa 12 asubuhi wanakwenda mashambani, n.k, uwezekano mkubwa ndivyo mtoto huyo atakavyokuwa siku atakapokuwa mtu mzima, hata kama si kwa 100%.

Wengine wanaweza kufikiria kuwa nazungumzia kishabiki lakini siyo nia yangu. Waangalieni marais wetu, kuanzia Mwl. Nyerere, Ali Hassan Mwinyi, Mkapa na Jakaya Kikwete. Pamoja na kwamba walisoma, wameishi maeneo mbalimbali, wamesafiri nchi mbalimbali lakini kuna nafasi fulani utaona mazingira waliyokulia yakionekana katika maisha na utendaji wao wa kazi.

Mwalimu alitoka Musoma, watu wengi wa Musoma huwa ni straight forward - kisu huitwa kisu, na panga huitwa panga. Mwalimu hakuwa na shida ya kueleza au kutamka anachotaka, iwe ni kizuri au kibaya. Sikiliza hotuba zake, ni zile zenye kuweka wazi msimamo wake bila kuzunguka au kuwa katika nafasi isiyoeleweka. Sikumbuki kusikia akitoa mfano wa chakula, ngoma, n.k. Kwa makabila mengi ya bara, chakula siyo jambo linalopewa umuhimu sana, wao alimradi tumbo limejaa, kumuwezesha kufanya kazi.

Akaja Mzee wetu Mwinyi, huyu ni mswahili wa Unguja. Ukisikiliza hotuba zake mara nyingi usingekosa kumsikia mifano yake ya ubwabwa, pilau, biriani, visu vya kukatia mboga, nyanya, n.k. Kwa watu wa Pwani chakula kina heshima kubwa sana, mtu mzima kabisa anaweza kupewa rushwa ya pilau, na rushwa hiyo ikafanya kazi. Mwinyi hotuba zake nyingi alikuwa akitumia mifano ya chakula hata kwenye masuala makubwa kabisa ya kitaifa. Maneno yalikuwa mengi sana lakini matendo yalikuwa kidogo, na watu wengi kipindi chake walifanya kama walivyotaka - ruksa kwa kila kitu. Wapo waliomsema sana na kumdhihaki kwa maneno ya kejeli za kila namna, haikumpa shida sana hiyo. Watu wa Pwani ni watu wenye maneno mengi sana, na kwao maneno yanayotamkwa huwa hayana uzito wowote, awe anatukanwa au kufanyiwa kejeli kwao huwa ni sehemu ya maisha. Ndiyo maana kipindi cha Mwinyi watu waliona kuwa demokrasia ya kusema ilikuwa imeongezeka sana, wasingeweza kuthubutu kutamka maneno hayo hayo akiwepo Mwalimu Nyerere. Kwa watu wa bara kila neno hupimwa na kutafsiriwa, na hata katika maisha ya kawaida watu wanaweza wasielewane maisha yao yote kutokana na maneno fulani ya kejeli yaliyozungumzwa na mmoja dhidi ya mwenzie.

Akaja Benjamin Mkapa, huyu japo sina uhakika na mazingira ya familia yake lakini ninachojua ni kuwa alisoma na kukulia mazingira ya Wamisionari wa Ndanda, ambao pia maisha yao hayana tofauti na watu wa bara, hawataki mtu awe ombaomba, wanasisitiza sana kuzingatia muda na kufanya kazi kwa bidii, na hupenda zaidi matendo kuliko maneno (ndiyo falsafa ya Biblia). Mkapa kila mara alisema anachukia sana kuomba. Mkapa alipokuwa Rais, ukimlinganisha na mtangulizi wake, alikuwa ni mtu ambaye alitaka kifanyike kitu anachotaka yeye kufanyika, haijalishi kama ni kizuri au kibaya alimradi kama yeye anaamini kuwa ni kizuri. Hotuba na matendo yake vilionesha wazi kuwa hakujali kama watu watampenda au kumchukia, bali yeye alijali anachotaka yeye kifanyike. Nakumbuka kuna wakati alitamka kuwa, 'Serikali itafanya kazi na wanaouchukia umaskini, wanaopenda umaskini itawaacha waendelee nao', hii ni kauli ya mtu asiyebembeleza.

Hatimaye amekuja JK, Mkwere aliyekulia mazingira ya Pwani yenye tabia za uswahili. Makabila mengi ya Pwana, watu wake ni wenye maneno mengi sana, na aghalabu maneno hayo, mengi huwa ni utani na uwongo, na huwa hakuna uzito wowote katika yale yanayotamkwa. Watu wa Pwani unaweza kumtukana hata matuzi ya nguoni lakini wala isimsumbue sana, mwishowe kama una chochote, ukampa, yote huyasahau kabisa, na wewe huwa ni rafiki yake mkubwa. Hata humu kwenye JF, hata bila ya kuambiwa, unaweza ukajua yupi ni mtu wa Pwani na yupi ni mtu bara. Wanaendeshwa na msemo wa, 'Mkono mtupu haulambwi'. Tabia hiyo ni tofauti sana na makabila ya bara ambapo ukimkejeli mtu hata kama ni maskini, unaweza hata kumpa msaada akaukataa - akaona aheri aishi kwa shida kuliko kudharaulika. Hiyo ndiyo maana ya maskini jeuri.

Watu wa Pwani hupenda sana starehe hata kama hana kipato. Wanathamini sana sherehe, ngoma, kazi za kuongea kuliko zile za kutumia misuli. Huamini kuwa wao ni maskini, na hivyo wao wanastahili kusaidiwa, hawawezi kubadili hali hiyo. Ukimtazama Rais wetu, anapenda sana kuomba (aliwahi pia kutamka kuwa sisi ni maskini na huko nje kuna pesa nyingi, tunachotakiwa ni kueleza ili watuelewe; huwa anaenda nje kuhemea, n.k), anapenda sana kuongea (matendo hakuna), hasumbuliwi na maneno wala kejeli wanazozitoa wananchi wengi dhidi yake, anapenda sana michezo (yeye mwenyewe alisema anapenda sana mpira na dansi), na kwenye hotuba yake ya ufunguzi wa bunge safari hii ameelezea kuwa ameridhishwa sana na maendele ya sanaa (muziki, tamthilia, na akawataja wanamuziki wa taarabu kama mfano wa mafanikio).

Ninachojiuliza, utendaji usioridhisha wa Rais wetu ni upungufu wake binafsi au matokeo ya mazingira aliyokulia? Na ikiwa ndiyo hivyo, kuna umuhimu wowote wa kuangalia mazingira ya mtu aliyokulia kabla ya kumchagua kuwa kiongozi mkuu wa nchi? Na je, ikifanyika hivyo itakuwa ni ubaguzi wa kikabila au kimaeneo? Kama tunataka viongozi wazuri na watakaofanya mambo ya kusaidia nchi yetu, tunafanya nini katika kuwaandalia mazingira watoto wetu yasiyo hasi kwa maendeleo ili waje kuwa viongozi wazuri na raia wenye mchango mkubwa kwa Taifa letu?

...kama kuna jambo la kujifunza kutokana na mienendo na utendaji wa marais tuliopata kuwa nao basi jambo hilo ni kutokukubali kuwa na rais muislamu au aliekulia pwani!!
 
Jaribu kutulia ktk hoja zako. Mwanzo ulianza na watu wa pwani na sasa umerukia Botswana lakin hukueleza kua wale watu wa Botswala ni watu wa bara au pwani, relevance? Jaribu kua makini ktk kujenga hoja, ninachokiona sasa ni kua unapoteza muelekeo.

Anyway kanuni za uongozi bora zinaeleweka na hazina uhusiano na ubara au upwani. Tunachohitaji ni kila raia kua serious na sio rais peke yake kwa sababu rais muajiri wake ni raia. Raia wakiwa serious wanachokitaka kinakua na huo ndio uhalisia. Naomba urekebishe msemo wako wa kujadili uongozi bora kwa kigezo cha upwani na bara kwa kua ni wa kimakosa.

Kwanini unakataa watu wasistarehe sasa nini faida ya kufanya kazi kwa bidii. Unafanya kazi kwa bidii ukimaliza unastarehe otherwise utakua huna maisha hapa duniani hasa kwa wale ndugu zetu ambao hawana dini. Starehe ni moja ya vitu muhimu ktk maisha ya binadamu, hata hao viongozi unaowasifu wote wanatembea na magari kama hawapendi starehe wangetembea kwa mguu tu au wangepanda punda.

Huyu jamaa nimeshindwa kumuelewa unazungumzia watu wa pwani na starehe??? Wewe angalia Mabaa, Grosari na Pabu hapa Dar utakuta mijitu haina week end wala nini Jumatatu saa 10 imeshafurika baa kwenda kunywa..fanya tafiti na uje na data hapa kama asilimia kubwa ya wanaojaza sehemu hizi za starehe ni watu kutoka wapi?
 
Facts hizi hapa:

1. Vision:

Watu wa pwani wanavision kuliko wa bara, wao ndio wa kwanza kuona kuna umuhimi na wakaanza harakati za kugombea uhuru, wakati huo sisi huku bara tumejisahau.

2. Creative;

Wanaleta mabadiliko hali inapokuwa mbaya, wakati Mwinyi anachukua nchi iliyo kuwa hali mbaya kiuchumi chini ya Nyerere, Mwinyi aliweza kuijenga nchi kwa kutumia mbinu nyingine na kuweka misingi inayo fuatwa na viongozi waliopita na watakao kuja.

Kiswahili, watu wa pwani ni waanzilishi wa lugha hii, wakati sisi huku bara tulishindwa


3. Honest;

Wapawani ni watu wasio na tamaa ni waaminifu wanajali utu, na ndio mpaka leo hii mafisadi wanao haribu nchi hii ni wabara.

4. Deplmatics;

Viongozi wapwani walionyesha umahiri na ukaribu wao na wananchi, kila mtanzania leo anahisi ni part ya tanzania, ukilinganisha wakati wa viongozi wa bara ambao waliongoza nchi kwa kutumia ki-network chake, nakumbuka wakati wa mwinyi alianzisha system ya kukutana na wananchi kila wiki

Diaspora pia wanaelewa ni wakati wa viongozi wa pwani uhusiano wao na mabalozi au na nchi umekuwa wa karibu zaidi, mfano; mabalozi wa kibara wameshindwa kuunda uhusiano mzuri na wananchi waishio ugenini

5.n.k nisiwachoshe
 
Back
Top Bottom