Maximo ajiuzulu kufundisha Stars

Mar 19, 2008
98
24
Maximo ajiuzulu kufundisha Stars

2008-04-01 09:27:45
By Mwandishi Wetu


Kocha Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mbrazil Marcio Maximo amejiuzulu kufundisha timu hiyo.

Watu walio karibu na Maximo waliitonya Nipashe jana kuwa kocha huyo amefikia uamuzi huo kufuatia shinikizo la wapenzi na wadau wa soka nchini kufuatia timu hiyo kuchapwa na timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, Jumamosi iliyopita.

Maximo inasemekana aliwasilisha barua yake kwa viongozi wa juu wa soka na nakala yake kupelekwa Ikulu.

Stars ililala 1-0 kwa Kenya, Jumamosi iliyopita, jijini Nairobi, Kenya katika mchezo wa kwanza wa mashindano mapya ya Kombe la Mataifa ya Afrika yanayohusisha wachezaji wanaocheza katika ligi za ndani.

Kufuatia kipigo hicho wadau na wapenzi wa soka walimlaumu Maximo kwa timu hiyo kufanya vibaya na kudai alikuwa hana uwezo wa kuinua kiwango cha timu hiyo.

Baadhi ya mashabiki wamefikia kukumbushia jinsi timu hiyo ilivyocharazwa na Senegal 4-0 na pia kuboronga kwa timu ya Tanzania Bara katika michuano ya soka ya Kombe la Chalenji iliyofanyika hapa nchini mwaka jana.

Maximo inadaiwa amekasirishwa na shutuma za wadau kwa madai watanzania walikuwa wanalazimisha matokeo mazuri ya haraka wakati bado angali anaisuka timu.

Maximo na msaidizi wake, Itamar Amorim wanatazamiwa kuondoka leo alfajiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATC) kurejea kwao Rio de Jeneiro, Brazil kuwahi kusherehekea Sikukuu ya Wajinga inayoadhimishwa duniani kote na kurejea baadae saa nne asubuhi ya leo wakati sikukuu hiyo itakapokuwa imemalizika.
 
Maximo ajiuzulu kufundisha Stars

2008-04-01 09:27:45
By Mwandishi Wetu


Kocha Mkuu wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Mbrazil Marcio Maximo amejiuzulu kufundisha timu hiyo.

Watu walio karibu na Maximo waliitonya Nipashe jana kuwa kocha huyo amefikia uamuzi huo kufuatia shinikizo la wapenzi na wadau wa soka nchini kufuatia timu hiyo kuchapwa na timu ya taifa ya Kenya, Harambee Stars, Jumamosi iliyopita.

Maximo inasemekana aliwasilisha barua yake kwa viongozi wa juu wa soka na nakala yake kupelekwa Ikulu.

Stars ililala 1-0 kwa Kenya, Jumamosi iliyopita, jijini Nairobi, Kenya katika mchezo wa kwanza wa mashindano mapya ya Kombe la Mataifa ya Afrika yanayohusisha wachezaji wanaocheza katika ligi za ndani.

Kufuatia kipigo hicho wadau na wapenzi wa soka walimlaumu Maximo kwa timu hiyo kufanya vibaya na kudai alikuwa hana uwezo wa kuinua kiwango cha timu hiyo.

Baadhi ya mashabiki wamefikia kukumbushia jinsi timu hiyo ilivyocharazwa na Senegal 4-0 na pia kuboronga kwa timu ya Tanzania Bara katika michuano ya soka ya Kombe la Chalenji iliyofanyika hapa nchini mwaka jana.

Maximo inadaiwa amekasirishwa na shutuma za wadau kwa madai watanzania walikuwa wanalazimisha matokeo mazuri ya haraka wakati bado angali anaisuka timu.

Maximo na msaidizi wake, Itamar Amorim wanatazamiwa kuondoka leo alfajiri kwa ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATC) kurejea kwao Rio de Jeneiro, Brazil kuwahi kusherehekea Sikukuu ya Wajinga inayoadhimishwa duniani kote na kurejea baadae saa nne asubuhi ya leo wakati sikukuu hiyo itakapokuwa imemalizika.

FOOLS' DAY!!!!! HAKUNA HILO
 
APRIL FOOLS DAY (01/04): “MASKINI WA AKILI” , please don’t fool us, we are adults !!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom