payuka
JF-Expert Member
- Jun 17, 2010
- 829
- 127
Sina nia ya kuwaharibia hawa jamaa biashara, ila natoa angalizo kwa mtu ambaye bado hajaingia kwenye huu mkenge wa kununua mashine yao ....apige hesabu Nzuri.
Kwanza kabisa napongeza jitihada za Tanesco kujitahidi kuwasogezea wananchi vituo vingi zaidi vya mauzo la LUKU (TOKENS). Haya basi tuje kwa Max-Com Limited Company pale Millenium......Hawa jamaa wanatumia wafanyabiashara Katika Kuziuza hizi Mobile Vending Machine zao..Na utaratibu unakuwa kama ifuatavo:-
Kwanza kabisa napongeza jitihada za Tanesco kujitahidi kuwasogezea wananchi vituo vingi zaidi vya mauzo la LUKU (TOKENS). Haya basi tuje kwa Max-Com Limited Company pale Millenium......Hawa jamaa wanatumia wafanyabiashara Katika Kuziuza hizi Mobile Vending Machine zao..Na utaratibu unakuwa kama ifuatavo:-
- Bei ya Mashine ni laki tano (Tsh.500,000) ambapo inatakiwa ku-sign contract ya miaka miwili na ukiterminate contract yao @ any time before the expiry of contract unarudishiwa 50% ya deposit yako (Laki mbili na Nusu)
- Baada ya hapo Unaanza kuuza Luku Pamoja na Vocha..( Hapa ndo kichwa Kinauma)- Luku unapata asilimia 1.5 and Vocha Asilimia 4% .....sasa ukianzia kwenye luku Mfano: Ukiuza Luku ya Milioni Moja (1000,000) faida yako inakuwa ni Tshs. 15,000 .......(Swali ni je ...unatumia muda gani kuuza Kiasi hicho cha Luku ...wakati huo huo Competition ni kubwa mtaani i.e. Kila mtu ana hiyo mashine)
- Mbali na hapo kuna zile karatasi ambazo unatakiwa uzinunue kutoka kwao ...kwa ajili ya ku-print risit ....paper roll moja inauzwa Tsh.2000