Mawazo zaidi kuhusu maadili na nidhamu

Shayu

Platinum Member
May 24, 2011
608
1,653
Leo ningependa kuendelea kujadili jambo ambalo nimekuwa nikijadili kwa muda mrefu sana kuhusu maadili na nidhamu. Lakini leo nitajikita katika dhana yenyewe ya maadili na nidhamu na nitaongelea kidogo na mahusiano yake na kuendelea au kutokuendelea kwa taifa lolote.

Maadili ni kitu gani na nidhamu ni kitu gani na ni kwanini ni mambo muhimu sana ili taifa letu au taifa jingine lolote lile liendelee?

Neno maadili linatokana na neno '' Adili ''. Linahusiana sana na mwenendo wa binadamu. Adili maana yake kuenenda katika usahihi. Nidhamu na maadili vina mahusiano ya karibu sana. Huwezi kuwa muadilifu bila kuwa na nidhamu. Je nidhamu ni kitu gani?

Nidhamu ni uwezo wa akili kuongoza mawazo na matendo yake katika mkondo unaofaa ambao utakuwa na faida kwake na kwa jamii yake.

Kwa kawaida binadamu anawaza mamia ya mawazo kwa siku. Baadhi ya mawazo ni yenye faida na mazuri na baadhi ya mawazo ni mabaya. Kwa hakika ni mawazo yasiyofaa. Mawazo mabaya huzaa watu waovu na mawazo mema huzaa watu wema. Kwahiyo uwezo wa kujizuia na kuongoza mawazo yetu ndio kitu kinachoitwa nidhamu. Mtu asiyekuwa na uwezo huo ni mtu asiyekuwa na nidhamu.

Kwa mfano mwizi hawezi hatuwezi kumuita ni mtu mwenye nidhamu. Mtu anayetukana hatuwezi kumuita mtu mwenye nidhamu kwakuwa ameshindwa kuongoza mawazo yake katika mkondo unaofaa. Kwahiyo nidhamu ndiyo inayorekebisha tabia zetu. Nidhamu ni jeuri ya kushinda vishawishi na tamaa. Nidhamu hii humuongoza binadamu kuwa mtu mwema na mwenye faida kwa jamii na taifa.

Mahusiano yetu kama watu wa taifa hili yatajengwa kama tu tutakuwa na nidhamu na kudhibiti tabia zetu na mawazo yetu. Na kuelekeza tabia zetu na mawazo yetu katika mkondo unaofaa. Ili taifa hili liendelee nidhamu ni jambo la msingi sana. Hatuwezi kujenga taifa hili bila nidhamu na kiongozi yeyote asiyeongelea hili anawaongopea nchi hii haiwezi kutoka kwenye umaskini kama watu wake hawana nidhamu na maadili. Ni lazima tuangalie kwa ukaribu tabia za watu wetu.

Huo ni msingi wa kwanza wa taifa lolote lile imara na lenye akili. Hatutaweza kujenga familia imara au taifa imara pasipo nidhamu. Na mahusiano yetu kama watu wa taifa hili yatategemea sana nidhamu zetu. Hatutaweza kuheshimiana kama hatuna nidhamu. Hili jambo tunapaswa kulijenga kama taifa. Hatutaweza kufikia malengo yetu pasipo hili jambo kuzingatiwa.

Malengo yetu yeyote yale yawe ya muda mfupi au mrefu hatuta yafikia kama hatutajenga nidhamu, na elimu tunayotoa haitokuwa na faida kwa taifa hili. Kwahiyo ni lazima tujitolee kujenga taifa hili na tuwe na nidhamu. Nidhamu huleta dira. Naongea hili tena na tena sababu ni jambo muhimu. Ili watu wetu wawe na faida kwa taifa lao.

Kwahiyo tunatakiwa tubadili jinsi tunavyofikiri na tuongoze mawazo yetu katika mkondo unaofaa. Mawazo yeliyotawanyika hayawezi kuwa na faida. Kwahiyo ni lazima tuongoze mawazo yetu kwenye utaifa. Tukitambua kuwa tuna taifa ambalo kila mmoja wetu anapaswa kulijenga na kulipenda hatuna taifa jingine zaidi ya hili.

Tukiwa na nidhamu tutaweza kujenga mahusiano mazuri kati ya mtu na familia yake, mtu na majirani zake na mtaa wake na wilaya yake na taifa lake pia, Tujitoe ubinafsi tuuvae utaifa na tulpende taifa letu hiyo itakuwa hatua moja kubwa sana kwetu kuendelea.

Vyuo vyetu lazima vizalishe watu wenye nidhamu ya juu ambao wtakuwa chachu ya maendeleo yetu. Elimu yetu lazima iundwe ili kuwezesha taifa hili kusonga mbele. Kila mtu lazima atambue kuweka utaifa mbele ni heshima. Na umoja ni bora zaidi ya utengano na ubinafsi. Tunauwezo wa kujenga taifa zuri na kubwa. Tubadilishe tabia zetu sisi sote. Tubadilike na tutafute njia mpya ya kupita.

Lakini tuna bunge ambalo kazi yake ni kutunga sheria. Sheria hizi kazi yake ni ku shape behaviour za raia katika mkondo ambao tunadhani utakuwa na faida kwa taifa. Sheria hizi husaidia kujenga nidhamu za raia. Kama shule haikufanya kazi sawa sawa, kila sehemu ina kazi yake.

Bunge linapotunga sheria serikali inatakiwa ifanye enforcement. Kitu kimoja ambacho kinatufanya tushindwe kujenga raia wa namna hiyo ni kutokana na watu tunaowachagua kwenda bungeni na tunaowapa uongozi kuunda serikali. Haiwezekani serikali isiyokuwa na nidhamu ikajenga nidhamu kwa raia na utii wa sheria. Raia huvunja sheria wanapoona viongozi wakivunja sheria. Hapo ndipo tulipokwama. Sheria kama sheria ni nzuri kwa mustakabali wa taifa lolote lile kama ni zenye misingi ya haki.

Kwahiyo kushindwa kwa serikali kuondoa ufisadi ni matokeo ya kukosa nidhamu na uwajibikaji jambo hili madhara yake ni makubwa sana.

Jamii huparaganyisha na taifa kwa ujumla, na kufanya nchi kuwa ya makundi na magenge. Na ni chanzo cha kushindwa kwa utawala na utii wa sheria.

Raia wanapaswa kutii serikali yao lakini serikali inaposhindwa kusimamia sheria, raia wanakuwa sio watiifu kwa serikali yao. Na nchi inapokuwa na serikali isiyokuwa na nidhamu katika uendeshaji wake, inapokuwa na serikali ambayo haizuii rushwa na ufisadi sababu ya kutokuwa na nidhamu kwao hupelekea nchi kwenda shimoni.

kunapokosekana kushindwa kujizuia katika nchi na nidhamu, taifa haliwezi kuepuka vita vya wenyewe kwa wenyewe. Nidhamu ni kujizuia. Kwahiyo tunaposhindwa kutumia akili na kufuata matamanio yetu ya mali na kufanya mali ni kitu cha kwanza kuliko utu wetu na utaifa wetu, hatuta epuka na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Sasa tunaona viongozi wengi wanaenda kwenye siasa kwaajili ya manufaa binafsi. Kuna tokea misuguano mingi. Ukiangalia kwa ukaribu hayo yote ni kwasababu ya tamaa ya wengi miongoni mwao. Wamelirarua na kuligawa taifa.

Tunapochagua kiongozi wa namna yeyote yule kuingia madarakana raia watafanana na serikali ya namna hiyo. Serikali ikikosa nidhamu nchi inakosa nidhamu. Ikiwa serikali ya uongo uongo na ulaghai na raia watafuata mkondo. Kuharibika na kuoza kwa taifa lolote kunatoka na aina ya viongozi wanaoingia madarakani. Ni wao wanaotunga sheria na sera na kuzisimamia. Kiongozi mwenye nidhamu na adili atafanya taifa kuwa na nidhamu na adili. Kama mimi ni kiongozi mwenye hekima nitataka raia wangu wote wawe na hekima sitacheka na ujinga.

Ni ukweli tunauhitaji wa kubadilisha serikali na hivyo kubadilisha mwelekeo wa taifa letu. Hili jambo ni la msingi sana. Lakini ni lazima tutafute watu bora miongoni mwetu ili kufanya hayo mabadiliko. Ukweli ni kwamba tunauwezo wa kufanya taifa hili kuwa kubwa. Nguvu hiyo iko mikononi mwetu. Lakini kama tu tutabadili mwelekeo wa mawazo yetu na tabia zetu. Kama tutaheshimu taifa hili na kulipenda na kuwa tayari kulitumikia.


LET US HONOR THIS COUNTRY ABOVE ALL OTHER NATION. WE GOT VALUE.

WHAT I DESIRE IS THE CHANGE NOT OF THE GOVERNMENT BUT CHANGE OF THE HEARTS TO THOSE PEOPLE WHO ARE IN GOVERNMENT AND TO ALL CITIZENS OF THIS COUNTRY. LAZIMA TUJE PAMOJA TUUNDE TAIFA MOJA. NA MUNGU ATAKUWA UPANDE WETU. MUNGU HAPENDI MGAWANYIKO. TAIFA MOJA CHINI YA MUNGU MMOJA.

Kama nembo yetu ya taifa inavyoonyesha mwanamke na mwanaume wakifanya kazi pamoja kujenga taifa hili. We must work together. ili taifa hili lisonge mbele bila ubinafsi najua tunaweza kama tukiamua. Hii nguvu iko ndani yetu kama tutajitoa kwa nguvu zetu zote na akili zetu zote. Najua una uwezo wa kulinyanyua taifa hili.


'' Taifa halijengwi kwa kuwa na maghorofa mengi au magari mengi. Taifa hujengwa katika mioyo na akili za watu na hubomolewa katika akili na mioyo ya watu. Hili pia ni sawa katika familia kuna familia zina mali lakini ndani hapakaliki. Ni wakati sasa wa kujenga taifa letu. Tutakapoanza kujenga taifa hili kwenye mioyo na akili za watu hakuna kurudi nyuma. Na uhakika tutashinda. Familia zitakuja pamoja na taifa litakuja pamoja. Hatutakuwa na furaha ya mtu mmoja au familia moja bali ya taifa zima. Tutapunguza kutokuwepo usawa katika nchi hii na maskini watafurahia. Siku ya ukombozi wa taifa hili itakuja haiko mbali. Ni katika ukweli na haki.''
 
1. Nidhamu ni mtindo wa fikara mantiki katika binadamu ambao humwongoza mtu kutenda kwa kufuata mfumo sahihi wa kufikiri kadri ya urazini wake. Mfumo huu humwongoza mtu kufikia hitimisho la kukubali uamuzi wa fikra mantiki zake na kutenda au kuishi kwa kufuata kama ilivyomwelekeza. Maadili ni zao la matendo ya mtu ambayo hufanywa chini ya msukumo na mwongozo wa kuishi maelekezo yaamuliwayo na fikara mantiki zake mwenyewe ili kuitimiza nidhamu. Kama ulivyoyaeleza maadili katika makala hizi, hufasiriwa, maadili, tofauti tofauti na watu kulingana na jamii zao kama muono wao. Ni kwamba, maadili huhusisha jumla ya matendo yake mtu ( kutokana na hayo matendo tunaweza kushuhudia yale mabaya na mema). Huu ni mtazamo mpya wa kuyaangali maadili kidunia kuwa, wapo wanaoyaona matendo fulani kuwa adilifu(mema) na matendo fulani si adilifu(maovu). Na wapo ambao huyaona matendo haya au yale kwao si adilifu na yale ni adilifu kulingana na mwono wao wa kimazingira na kijamii. Hoja yako juu ya maadili ya taifa haitakuwa ya mashiko kwa mtazomo huu mpya, hasa pale unapohusisha maadili kuwa kitu cha kitaifa. Kwanini nasema hivyo? Ni kwa sababu mimi mwenyewe nilishalifikiria hilo kuwa kwa siku nyingi tumekuwa tukilia na suala la maadili ya taifa lakini, nikagundua kuwa ugumu wa kulitimiza hilo upo pale sisi tunaposhindwa kujua kuwa taifa hili lina watu mbalimbali ambao kila sekunde hufikiri na wana mitazamo tofauti tofauti kulingana na uelekeo wa maisha yao katika jamii zao wenyewe. Na hivyo, mkondo huu huwaleta kama jamii fulani kuwa na aina fulani ya mkondo wao wa maadili na kuishi (matendo yao). Na kwao hapo ndipo wajengapo hoja msingi na madhubuti ya nidhamu ya maisha yao. Hivyo, sioni katika tamko lako, nguvu yoyote ambayo inaweza kulibadili taifa kutufanya kuwa na maadili au mkondo sawa wa kuishi kwani bado sisi wenyewe kama taifa lenye jamii tofauti hatujaweka wazi au kubainisha mkondo wetu wa maisha ambao utaweka bayana ni mambo yapi kama taifa tukiyaishi kwa pamoja yatakuwa ndio maadili ya taifa.

2. Ni kwa namna au njia ipi hayo mabadiliko uliyoyapendekeza yanaweza kufikiwa. Matahalani, kama mimi ninaona kudhulumu, kuiba, kulaghai, kutapeli, kunanipa manufaa na nikifanya hivyo ninakidhi haja ya maisha yangu naondokana na dhiki; ni kivipi utanishawishi nibadlilike? Ubaya wa hayo matendo uko wapi? Nitaujuaje mimi kuwa ninayofanya si matendo mema kwa sababu yananipatia kile nachokitaka?

3.
Sheria ni matokeo ya msukumo wa ndani wa fikara matiki za mtu au watu, ambao (msukumo) husukuma nguvu ya pamoja ya kuweka matamko(sheria) kama nguzo za kulinda matendo yetu (kusimamia maadili) hasa mazuri. Lakini sisi kama taifa hatuna mfumo wetu thabiti uliokubaliwa na jamii zote kuwa hayo ndio maadili bainishwa ya taifa letu ili utuongoze pia kuweka sheria zitakazotuongoza. Hivyo, hizo sheria zinazotungwa na bunge hazitakuwa / hazina maana yoyote ile bali ni kufanya tu kama bunge pasi kujua ukiini wa kazi hiyo ili kutimiza majukumu yake ya kutunga sheria bila kuangali msingi wa sheria hizo ni upi. Na yule amabeye huwekewa sheria hizo huwa ameelimika juu ya dhana ya umaadili ili hizo sheria zimsaidie kulinda hayo maadili pindi aghafirikapo.
Kumbe shule zetu kutokuweka mfumo wa kulinda na kujenga tabia zetu si kosa lao kwani shule hizo hizo ni zao letu sisi ambao hatuna dira ya nini tunapaswa kuwa (yapi ni yetu madili). Na hivyo, nidhamu haitokuwepo kamwe unayoisema au itakuwepo ile usioisema wewe kwa mantiki ya kuwa kila mtu anayo maadili yake yanayomwongoza kwenye maisha kulingana na mfumo wa fikara mantiki za jamii yake. Na nidhamu kwao ipo kwa mujibu wao na haipo kwa muji Huyu mtu hawezi kulaumiwa kutoka na na mfumo wake wa maisha unaofuata au kuongozwa na mkondo wa maono ya jamii yake.

4. Kama mtoto amezaliwa akawakuta baba, mama, kaka, na dada, wote ni walafi, na wapaofanya hivyo wanashiba; hakika, naye huyo mtoto atafuata mkondo ule ule na ndio utakao mlea, kwani mazingira jamii na watu ndio humlea mtu na kumjenga kwa kiasi kikubwa kuwa kama alivyo kitabia kwani huiga kile anachoona aliowakuta wanafanya. Kwahiyo, mtoto huyo katika akili yake hilo jambo (ulafi) litakuwa ni jambo la kibinadamu, la kawaida na linalotakiwa kufanywa na watu na ni jema. Itakuwa ni mshangao mkubwa ati, mtoto huyo kaenda shule kabadilika wakati hata huko huko shuleni kuna watoto ambao nao wana tabai ya ulafi waliourithi kutoka katika familia zao. Mtoto huyu ata katika ushirika wowote ule atakaoomba ridhaa ya kuuongoza kama kiongozi ama mdogo au mkubwa bado watu wale ni walafi na yeye wanamjua ni mtu mwenye tabia zinazoendana…..ataendelea kuwa mlafi hivyo hiyo ata akipewa ikulu kwa kuwa ulafi huo umemkuza toka utotoni na umewakuza jamii yake iliyomweka madarakani na umekuwa ukimtimizia mahitaji yake ya kushiba. Kwa maana hiyo, yule kiongozi mvunja sheria, mkosa nidhamu, ni zao la jamii (watu waliompa madaraka) yake amabayo nayo hiyo jamii ni vunjifu ya sheria, isiyo na nidhamu pia. Serikali inapokuwa mbovu, ni matokeo ya jamii hiyo hiyo mbovu. Viongozi wavunja sheria ni wale wale ambao walikuwa wakifanya hivyo kabla hawajawa viongozi na waliowachagua nao walikuwa wakiwaunga mkono. Kushindwa kuondoa au kukemea ufisadi katika serikali ni kiashirio kuwa taifa zima kuwa na elementi za ufisadi kwa watu wake kwa maana ya kuwa ufisadi ndio maisha ya taifa zima. Kiongozi mwenye hekima, busaram adili ndani yake huwekwa madarakani na wananchi wenye tabia hizo. Kinyume chaki itakuwa sahihi. Raia hawaifanani wala kuifauata serikali yao, bali serikali yao huwafanana na kuwafuata watu wake, kwa mantiki ya kuwa wao(raia) ndio walioiweka serikali madarakani kwa makubaliano ya mkataba wao wa kuweka pamoja sehemu ya nguvu yao na uhuru wao kukubaliana kama wamoja kulinda haki zao. Na serikali ni simamizi ya mkataba huo. Mwono huo wa kulipenda na kulijenga taifa chini ya mhimili wa maadili ya taifa hautokuwepo kwa umaneno tu; bali, kwa matendo ambayo msingi wake ni watu kujua asili ya kiini cha utaifa wao na kujua kwa kina uhimara na ubora wa wao kuwa wazalendo; na hili, haliji tu kwa kuwalaumu wasiofanya hivyo, bali kwa kuwafanya wajue hivyo tangu wanapozaliwa. Je, mfumo huu katika nchi hii upo?
 
1. Nidhamu ni mtindo wa fikara mantiki katika binadamu ambao humwongoza mtu kutenda kwa kufuata mfumo sahihi wa kufikiri kadri ya urazini wake. Mfumo huu humwongoza mtu kufikia hitimisho la kukubali uamuzi wa fikra mantiki zake na kutenda au kuishi kwa kufuata kama ilivyomwelekeza. Maadili ni zao la matendo ya mtu ambayo hufanywa chini ya msukumo na mwongozo wa kuishi maelekezo yaamuliwayo na fikara mantiki zake mwenyewe ili kuitimiza nidhamu. Kama ulivyoyaeleza maadili katika makala hizi, hufasiriwa, maadili, tofauti tofauti na watu kulingana na jamii zao kama muono wao. Ni kwamba, maadili huhusisha jumla ya matendo yake mtu ( kutokana na hayo matendo tunaweza kushuhudia yale mabaya na mema). Huu ni mtazamo mpya wa kuyaangali maadili kidunia kuwa, wapo wanaoyaona matendo fulani kuwa adilifu(mema) na matendo fulani si adilifu(maovu). Na wapo ambao huyaona matendo haya au yale kwao si adilifu na yale ni adilifu kulingana na mwono wao wa kimazingira na kijamii. Hoja yako juu ya maadili ya taifa haitakuwa ya mashiko kwa mtazomo huu mpya, hasa pale unapohusisha maadili kuwa kitu cha kitaifa. Kwanini nasema hivyo? Ni kwa sababu mimi mwenyewe nilishalifikiria hilo kuwa kwa siku nyingi tumekuwa tukilia na suala la maadili ya taifa lakini, nikagundua kuwa ugumu wa kulitimiza hilo upo pale sisi tunaposhindwa kujua kuwa taifa hili lina watu mbalimbali ambao kila sekunde hufikiri na wana mitazamo tofauti tofauti kulingana na uelekeo wa maisha yao katika jamii zao wenyewe. Na hivyo, mkondo huu huwaleta kama jamii fulani kuwa na aina fulani ya mkondo wao wa maadili na kuishi (matendo yao). Na kwao hapo ndipo wajengapo hoja msingi na madhubuti ya nidhamu ya maisha yao. Hivyo, sioni katika tamko lako, nguvu yoyote ambayo inaweza kulibadili taifa kutufanya kuwa na maadili au mkondo sawa wa kuishi kwani bado sisi wenyewe kama taifa lenye jamii tofauti hatujaweka wazi au kubainisha mkondo wetu wa maisha ambao utaweka bayana ni mambo yapi kama taifa tukiyaishi kwa pamoja yatakuwa ndio maadili ya taifa.

2. Ni kwa namna au njia ipi hayo mabadiliko uliyoyapendekeza yanaweza kufikiwa. Matahalani, kama mimi ninaona kudhulumu, kuiba, kulaghai, kutapeli, kunanipa manufaa na nikifanya hivyo ninakidhi haja ya maisha yangu naondokana na dhiki; ni kivipi utanishawishi nibadlilike? Ubaya wa hayo matendo uko wapi? Nitaujuaje mimi kuwa ninayofanya si matendo mema kwa sababu yananipatia kile nachokitaka?

3.
Sheria ni matokeo ya msukumo wa ndani wa fikara matiki za mtu au watu, ambao (msukumo) husukuma nguvu ya pamoja ya kuweka matamko(sheria) kama nguzo za kulinda matendo yetu (kusimamia maadili) hasa mazuri. Lakini sisi kama taifa hatuna mfumo wetu thabiti uliokubaliwa na jamii zote kuwa hayo ndio maadili bainishwa ya taifa letu ili utuongoze pia kuweka sheria zitakazotuongoza. Hivyo, hizo sheria zinazotungwa na bunge hazitakuwa / hazina maana yoyote ile bali ni kufanya tu kama bunge pasi kujua ukiini wa kazi hiyo ili kutimiza majukumu yake ya kutunga sheria bila kuangali msingi wa sheria hizo ni upi. Na yule amabeye huwekewa sheria hizo huwa ameelimika juu ya dhana ya umaadili ili hizo sheria zimsaidie kulinda hayo maadili pindi aghafirikapo.
Kumbe shule zetu kutokuweka mfumo wa kulinda na kujenga tabia zetu si kosa lao kwani shule hizo hizo ni zao letu sisi ambao hatuna dira ya nini tunapaswa kuwa (yapi ni yetu madili). Na hivyo, nidhamu haitokuwepo kamwe unayoisema au itakuwepo ile usioisema wewe kwa mantiki ya kuwa kila mtu anayo maadili yake yanayomwongoza kwenye maisha kulingana na mfumo wa fikara mantiki za jamii yake. Na nidhamu kwao ipo kwa mujibu wao na haipo kwa muji Huyu mtu hawezi kulaumiwa kutoka na na mfumo wake wa maisha unaofuata au kuongozwa na mkondo wa maono ya jamii yake.

4. Kama mtoto amezaliwa akawakuta baba, mama, kaka, na dada, wote ni walafi, na wapaofanya hivyo wanashiba; hakika, naye huyo mtoto atafuata mkondo ule ule na ndio utakao mlea, kwani mazingira jamii na watu ndio humlea mtu na kumjenga kwa kiasi kikubwa kuwa kama alivyo kitabia kwani huiga kile anachoona aliowakuta wanafanya. Kwahiyo, mtoto huyo katika akili yake hilo jambo (ulafi) litakuwa ni jambo la kibinadamu, la kawaida na linalotakiwa kufanywa na watu na ni jema. Itakuwa ni mshangao mkubwa ati, mtoto huyo kaenda shule kabadilika wakati hata huko huko shuleni kuna watoto ambao nao wana tabai ya ulafi waliourithi kutoka katika familia zao. Mtoto huyu ata katika ushirika wowote ule atakaoomba ridhaa ya kuuongoza kama kiongozi ama mdogo au mkubwa bado watu wale ni walafi na yeye wanamjua ni mtu mwenye tabia zinazoendana…..ataendelea kuwa mlafi hivyo hiyo ata akipewa ikulu kwa kuwa ulafi huo umemkuza toka utotoni na umewakuza jamii yake iliyomweka madarakani na umekuwa ukimtimizia mahitaji yake ya kushiba. Kwa maana hiyo, yule kiongozi mvunja sheria, mkosa nidhamu, ni zao la jamii (watu waliompa madaraka) yake amabayo nayo hiyo jamii ni vunjifu ya sheria, isiyo na nidhamu pia. Serikali inapokuwa mbovu, ni matokeo ya jamii hiyo hiyo mbovu. Viongozi wavunja sheria ni wale wale ambao walikuwa wakifanya hivyo kabla hawajawa viongozi na waliowachagua nao walikuwa wakiwaunga mkono. Kushindwa kuondoa au kukemea ufisadi katika serikali ni kiashirio kuwa taifa zima kuwa na elementi za ufisadi kwa watu wake kwa maana ya kuwa ufisadi ndio maisha ya taifa zima. Kiongozi mwenye hekima, busaram adili ndani yake huwekwa madarakani na wananchi wenye tabia hizo. Kinyume chaki itakuwa sahihi. Raia hawaifanani wala kuifauata serikali yao, bali serikali yao huwafanana na kuwafuata watu wake, kwa mantiki ya kuwa wao(raia) ndio walioiweka serikali madarakani kwa makubaliano ya mkataba wao wa kuweka pamoja sehemu ya nguvu yao na uhuru wao kukubaliana kama wamoja kulinda haki zao. Na serikali ni simamizi ya mkataba huo. Mwono huo wa kulipenda na kulijenga taifa chini ya mhimili wa maadili ya taifa hautokuwepo kwa umaneno tu; bali, kwa matendo ambayo msingi wake ni watu kujua asili ya kiini cha utaifa wao na kujua kwa kina uhimara na ubora wa wao kuwa wazalendo; na hili, haliji tu kwa kuwalaumu wasiofanya hivyo, bali kwa kuwafanya wajue hivyo tangu wanapozaliwa. Je, mfumo huu katika nchi hii upo?


Tunaangalia tabia ambazo zenye faida na zisizo faida kutokana na matunda yanayotokana na tabia hizo. Binadamu ameumbwa na fikra anajua jambo gani baya na jambo gani zuri hili sio suala la maadili ya jamii fulani !! Ni universal principal. Na matokeo ya kuwa na maadili mabovu au mema yanaonekana ndani ya jamii husika. Tunaangalia matunda yanayopatikana kutokana na matendo hayo iwe matokeo ya karibu au yale yanayokuja baada ya muda mrefu. Ni kweli hatutaweza kutoka hapa tulipo kama taifa bila ya vitu hivyo nilivyovitaja kuzingatiwa. Ni ngumu sana. Na ningependa kama tunajadilianda tuangalie sana kwamba mjadala tutakaofanya usiwe tu kubishana bali kutafuta ukweli ambao utasaidia taifa letu. Yawe majadiliano chanya yenye nia ya kusaidia taifa letu na watu wengi zaidi kupata uelewa.
 
usifikiri kuwa kila anayekuonesha ufa katika hoja yako ana lengo la kukupinga. soma vizuri hoja zangu utagundua kuwa najaribu kuzichambua njia zako ulizoziainisha kama kweli ni msingi imara wa kupata kile unachokitaka. huwezi kuongelea kuwa mataendo haya yakifanywa ni mazuri na haya ni mabaya wakati huo huo matendo hayo mabaya kwa wengine ni mazuri na mazuri kwa mengine ni mabaya. huwezi kunielezea kuwa suala la ubaya na uzuri kwenye maadili ni universal principle wakati jamii zenyewe watu hao hao wanaofikiri wanapinga kwa kuwa na msimamo mmoja kwa sababu hakuna kiunganishi cha kutufanya wote tuufikie ule wezo wa tendo moja kuwa zuri au baya kwa wakati mmoja. zitazame hoja zangu zimejengeka katika misingi ipi ndio uzikosoe. Mf. kutoa mimba ni kuua, lakini ni kwanini kuna baadhi ya jamii/ mataifa wanaruhusu tendo hilo? kimsingi mawazo yako ni kimaneno tu si kimatendo, japo yapo sahihi,
 
usifikiri kuwa kila anayekuonesha ufa katika hoja yako ana lengo la kukupinga. soma vizuri hoja zangu utagundua kuwa najaribu kuzichambua njia zako ulizoziainisha kama kweli ni msingi imara wa kupata kile unachokitaka. huwezi kuongelea kuwa mataendo haya yakifanywa ni mazuri na haya ni mabaya wakati huo huo matendo hayo mabaya kwa wengine ni mazuri na mazuri kwa mengine ni mabaya. huwezi kunielezea kuwa suala la ubaya na uzuri kwenye maadili ni universal principle wakati jamii zenyewe watu hao hao wanaofikiri wanapinga kwa kuwa na msimamo mmoja kwa sababu hakuna kiunganishi cha kutufanya wote tuufikie ule wezo wa tendo moja kuwa zuri au baya kwa wakati mmoja. zitazame hoja zangu zimejengeka katika misingi ipi ndio uzikosoe. Mf. kutoa mimba ni kuua, lakini ni kwanini kuna baadhi ya jamii/ mataifa wanaruhusu tendo hilo? kimsingi mawazo yako ni kimaneno tu si kimatendo, japo yapo sahihi,[/QUOTE

Kwahiyo wizi na ufisadi ni matendo mema? unasimamia misingi ipi ya kifalsafa? Hakuna mataifa yanayoanza kwa kuwa na maadili na kuporomoka maaba ya maadili kuharibika? Tafuta vitabu soma kwanini himaya ya warumi iliporomoka.
 
katika subjectivism point of view, morality depends on the views of person or certain social conducts not universally. ndio maana objectivism and subjectivism bado havijafikia mwafaka. ufisadi na wizi ni mabaya kwa wale ambao unawaathiri ila sio kwa wale wanaonufaika nao
 
Leo ningependa kuendelea kujadili jambo ambalo nimekuwa nikijadili kwa muda mrefu sana kuhusu maadili na nidhamu. Lakini leo nitajikita katika dhana yenyewe ya maadili na nidhamu na nitaongelea kidogo na mahusiano yake na kuendelea au kutokuendelea kwa taifa lolote.

Maadili ni kitu gani na nidhamu ni kitu gani na ni kwanini ni mambo muhimu sana ili taifa letu au taifa jingine lolote lile liendelee?

Neno maadili linatokana na neno '' Adili ''. Linahusiana sana na mwenendo wa binadamu. Adili maana yake kuenenda katika usahihi. Nidhamu na maadili vina mahusiano ya karibu sana. Huwezi kuwa muadilifu bila kuwa na nidhamu. Je nidhamu ni kitu gani?

Nidhamu ni uwezo wa akili kuongoza mawazo na matendo yake katika mkondo unaofaa ambao utakuwa na faida kwake na kwa jamii yake.

Kwa kawaida binadamu anawaza mamia ya mawazo kwa siku. Baadhi ya mawazo ni yenye faida na mazuri na baadhi ya mawazo ni mabaya. Kwa hakika ni mawazo yasiyofaa. Mawazo mabaya huzaa watu waovu na mawazo mema huzaa watu wema. Kwahiyo uwezo wa kujizuia na kuongoza mawazo yetu ndio kitu kinachoitwa nidhamu. Mtu asiyekuwa na uwezo huo ni mtu asiyekuwa na nidhamu.

Kwa mfano mwizi hawezi hatuwezi kumuita ni mtu mwenye nidhamu. Mtu anayetukana hatuwezi kumuita mtu mwenye nidhamu kwakuwa ameshindwa kuongoza mawazo yake katika mkondo unaofaa. Kwahiyo nidhamu ndiyo inayorekebisha tabia zetu. Nidhamu ni jeuri ya kushinda vishawishi na tamaa. Nidhamu hii humuongoza binadamu kuwa mtu mwema na mwenye faida kwa jamii na taifa.

Mahusiano yetu kama watu wa taifa hili yatajengwa kama tu tutakuwa na nidhamu na kudhibiti tabia zetu na mawazo yetu. Na kuelekeza tabia zetu na mawazo yetu katika mkondo unaofaa. Ili taifa hili liendelee nidhamu ni jambo la msingi sana. Hatuwezi kujenga taifa hili bila nidhamu na kiongozi yeyote asiyeongelea hili anawaongopea nchi hii haiwezi kutoka kwenye umaskini kama watu wake hawana nidhamu na maadili. Ni lazima tuangalie kwa ukaribu tabia za watu wetu.

Huo ni msingi wa kwanza wa taifa lolote lile imara na lenye akili. Hatutaweza kujenga familia imara au taifa imara pasipo nidhamu. Na mahusiano yetu kama watu wa taifa hili yatategemea sana nidhamu zetu. Hatutaweza kuheshimiana kama hatuna nidhamu. Hili jambo tunapaswa kulijenga kama taifa. Hatutaweza kufikia malengo yetu pasipo hili jambo kuzingatiwa.

Malengo yetu yeyote yale yawe ya muda mfupi au mrefu hatuta yafikia kama hatutajenga nidhamu, na elimu tunayotoa haitokuwa na faida kwa taifa hili. Kwahiyo ni lazima tujitolee kujenga taifa hili na tuwe na nidhamu. Nidhamu huleta dira. Naongea hili tena na tena sababu ni jambo muhimu. Ili watu wetu wawe na faida kwa taifa lao.

Kwahiyo tunatakiwa tubadili jinsi tunavyofikiri na tuongoze mawazo yetu katika mkondo unaofaa. Mawazo yeliyotawanyika hayawezi kuwa na faida. Kwahiyo ni lazima tuongoze mawazo yetu kwenye utaifa. Tukitambua kuwa tuna taifa ambalo kila mmoja wetu anapaswa kulijenga na kulipenda hatuna taifa jingine zaidi ya hili.

Tukiwa na nidhamu tutaweza kujenga mahusiano mazuri kati ya mtu na familia yake, mtu na majirani zake na mtaa wake na wilaya yake na taifa lake pia, Tujitoe ubinafsi tuuvae utaifa na tulpende taifa letu hiyo itakuwa hatua moja kubwa sana kwetu kuendelea.

Vyuo vyetu lazima vizalishe watu wenye nidhamu ya juu ambao wtakuwa chachu ya maendeleo yetu. Elimu yetu lazima iundwe ili kuwezesha taifa hili kusonga mbele. Kila mtu lazima atambue kuweka utaifa mbele ni heshima. Na umoja ni bora zaidi ya utengano na ubinafsi. Tunauwezo wa kujenga taifa zuri na kubwa. Tubadilishe tabia zetu sisi sote. Tubadilike na tutafute njia mpya ya kupita.

Lakini tuna bunge ambalo kazi yake ni kutunga sheria. Sheria hizi kazi yake ni ku shape behaviour za raia katika mkondo ambao tunadhani utakuwa na faida kwa taifa. Sheria hizi husaidia kujenga nidhamu za raia. Kama shule haikufanya kazi sawa sawa, kila sehemu ina kazi yake.

Bunge linapotunga sheria serikali inatakiwa ifanye enforcement. Kitu kimoja ambacho kinatufanya tushindwe kujenga raia wa namna hiyo ni kutokana na watu tunaowachagua kwenda bungeni na tunaowapa uongozi kuunda serikali. Haiwezekani serikali isiyokuwa na nidhamu ikajenga nidhamu kwa raia na utii wa sheria. Raia huvunja sheria wanapoona viongozi wakivunja sheria. Hapo ndipo tulipokwama. Sheria kama sheria ni nzuri kwa mustakabali wa taifa lolote lile kama ni zenye misingi ya haki.

Kwahiyo kushindwa kwa serikali kuondoa ufisadi ni matokeo ya kukosa nidhamu na uwajibikaji jambo hili madhara yake ni makubwa sana.

Jamii huparaganyisha na taifa kwa ujumla, na kufanya nchi kuwa ya makundi na magenge. Na ni chanzo cha kushindwa kwa utawala na utii wa sheria.

Raia wanapaswa kutii serikali yao lakini serikali inaposhindwa kusimamia sheria, raia wanakuwa sio watiifu kwa serikali yao. Na nchi inapokuwa na serikali isiyokuwa na nidhamu katika uendeshaji wake, inapokuwa na serikali ambayo haizuii rushwa na ufisadi sababu ya kutokuwa na nidhamu kwao hupelekea nchi kwenda shimoni.

kunapokosekana kushindwa kujizuia katika nchi na nidhamu, taifa haliwezi kuepuka vita vya wenyewe kwa wenyewe. Nidhamu ni kujizuia. Kwahiyo tunaposhindwa kutumia akili na kufuata matamanio yetu ya mali na kufanya mali ni kitu cha kwanza kuliko utu wetu na utaifa wetu, hatuta epuka na vita vya wenyewe kwa wenyewe. Sasa tunaona viongozi wengi wanaenda kwenye siasa kwaajili ya manufaa binafsi. Kuna tokea misuguano mingi. Ukiangalia kwa ukaribu hayo yote ni kwasababu ya tamaa ya wengi miongoni mwao. Wamelirarua na kuligawa taifa.

Tunapochagua kiongozi wa namna yeyote yule kuingia madarakana raia watafanana na serikali ya namna hiyo. Serikali ikikosa nidhamu nchi inakosa nidhamu. Ikiwa serikali ya uongo uongo na ulaghai na raia watafuata mkondo. Kuharibika na kuoza kwa taifa lolote kunatoka na aina ya viongozi wanaoingia madarakani. Ni wao wanaotunga sheria na sera na kuzisimamia. Kiongozi mwenye nidhamu na adili atafanya taifa kuwa na nidhamu na adili. Kama mimi ni kiongozi mwenye hekima nitataka raia wangu wote wawe na hekima sitacheka na ujinga.

Ni ukweli tunauhitaji wa kubadilisha serikali na hivyo kubadilisha mwelekeo wa taifa letu. Hili jambo ni la msingi sana. Lakini ni lazima tutafute watu bora miongoni mwetu ili kufanya hayo mabadiliko. Ukweli ni kwamba tunauwezo wa kufanya taifa hili kuwa kubwa. Nguvu hiyo iko mikononi mwetu. Lakini kama tu tutabadili mwelekeo wa mawazo yetu na tabia zetu. Kama tutaheshimu taifa hili na kulipenda na kuwa tayari kulitumikia.


LET US HONOR THIS COUNTRY ABOVE ALL OTHER NATION. WE GOT VALUE.

WHAT I DESIRE IS THE CHANGE NOT OF THE GOVERNMENT BUT CHANGE OF THE HEARTS TO THOSE PEOPLE WHO ARE IN GOVERNMENT AND TO ALL CITIZENS OF THIS COUNTRY. LAZIMA TUJE PAMOJA TUUNDE TAIFA MOJA. NA MUNGU ATAKUWA UPANDE WETU. MUNGU HAPENDI MGAWANYIKO. TAIFA MOJA CHINI YA MUNGU MMOJA.

Kama nembo yetu ya taifa inavyoonyesha mwanamke na mwanaume wakifanya kazi pamoja kujenga taifa hili. We must work together. ili taifa hili lisonge mbele bila ubinafsi najua tunaweza kama tukiamua. Hii nguvu iko ndani yetu kama tutajitoa kwa nguvu zetu zote na akili zetu zote. Najua una uwezo wa kulinyanyua taifa hili.


'' Taifa halijengwi kwa kuwa na maghorofa mengi au magari mengi. Taifa hujengwa katika mioyo na akili za watu na hubomolewa katika akili na mioyo ya watu. Hili pia ni sawa katika familia kuna familia zina mali lakini ndani hapakaliki. Ni wakati sasa wa kujenga taifa letu. Tutakapoanza kujenga taifa hili kwenye mioyo na akili za watu hakuna kurudi nyuma. Na uhakika tutashinda. Familia zitakuja pamoja na taifa litakuja pamoja. Hatutakuwa na furaha ya mtu mmoja au familia moja bali ya taifa zima. Tutapunguza kutokuwepo usawa katika nchi hii na maskini watafurahia. Siku ya ukombozi wa taifa hili itakuja haiko mbali. Ni katika ukweli na haki.''

I have read your post and here is what I could say about maadili and nidhamu. To me they are networks of social contracts which represent three important groups of attributes at every level of society (Family, religion, tribe, Nation).

The first group of attributes is the group of rules which defines what members of the society should follow and honor. For example, at family level, the very basic unit of the society, parents will teach their children the value of not stealing from their neighbor. At faith level, the person will be told that stealing is a sin. At the nationality level, stealing is a crime.

The second group defines the expectations and the levels of efforts for each individual member of society. The child who steals a toy from another child will be treated differently from a grown up man who steal the same item: the same crime different expectations.

The third group includes penalties and consequences imposed on offenders: members of the society who fail to follow and honor the rules. For example in Tanzania, when somebody loses his family member, it’s customary to visit and help him. If you don’t, people will not force you to do so, but they will not show up when you lose yours. It isn’t a written rule, but it’s ingrained in our psyche. If society can punish people who don’t attend funerals, in theory, it should be able to punish those who steal public funds.

At every level of society a typical Tanzanian approaches maadili with different degree of intensity. For example, at family level, we are very good. The same could be said when it comes to tribe and religion affiliations. However, the degree of intensity starts to drop when it comes to running government businesses. For example, majority of Tanzanians don’t steal from their neighbors, but they don’t feel guilt if they steal government properties or resources.
 
Hoja yako ni nzuri sana na lengo lako lina mantiki sahihi na mimi ninakubaliana na hoja yako mhimiri. Ila ninakwenda kinyume kidogo na mbinu unayoipendekeza kuweza kulifikia lengo hilo. Kwa maelezo yako mengi yamejikita katika kulaumu na kusema kauli kama inpaswa, lazima….nk . Kauli kama hizi ni bora kwa wale unaowaambia kama wanatambua kile unachowasisitizia ila walikuwa wameteleza ila sio kwa watanzania.

Labda nizifafanue hoja zangu ili unielewe nachokimaanisha. Maadili, kwa neno la kingereza (morality) lina maana ya matendo yote yanayomhusu binadamu. Miendendo na taratibu zote zinazomhusu binadamu. Unapoongelea maadili unazungumzia kaida zote katika maisha ya binadamu anayeishi katika jumuiya fulani ya watu. Matendo hayo yote huwa yamegawanyika katika makundi mawili, yaani matendo mema na maovu.
Lakini umaadili au elimu maadili (ethics) ni taaluma ambayo hutoa misingi au kanuni ambazo ndizo hutumika kuyafasiri matendo yanayotendeka kama ama ni mema au maovu. Na hapo ndipo tunapobaini kuwa kitendo kile ama ni chema au kiovu. Bila misingi hiyo itolewayo na elimu maadili hakika hatuwezi kulitambua tendo lolote kama ni jema au baya hata kama ni jema na baya kwa lenyewe au zuri kwa lenyewe.

Lakini pia, katika taaluma hii ya umaadili, ipo mitazamo mbalimbali ya kuyatazama matendo au kuyafasiri matendo ya binadamu kama ni maovu au mema. Mtazamo wa kwanza ni ule unaopendekeza kuwa maadili ni dhana moja na sawa kwa kila mtu na kwa watu wote (moral objectivism). Mtazamo huu hupendekeza ya kuwa, ubaya au uzuri/wema wa tendo umo katika tendo lenyewe na binadamu wote hulitazama sawa kuwa ni baya au jema na ni kwa watu wote ulimwenguni. [Moral absolutism – state that, all human acts are evil or good to all people universally – everywhere and to any person] kwamba, kwa mfano kuua ni tendo baya kwa kila mtu kwani tendo lenyewe ni baya na kila mtu hakuna nayependa kufanyiwa hivyo. Wafuasi wa mtazamo huu ni wengi wakiwemo wanafalsafa wa zamani wa maadili.

Mtazamo wa pili ni ule unaoyaangalia maadili au kuyafasiri kuwa matendo ya binadamu ni mabaya au mazuri kulingana na mtu au jamii yake mwenyewe ambapo kupitia jamii hiyo wanayo misingi na vigezo vyao vya kimaadili. Na hivyo, huwezi kuwa utamaduni wa watu fulani ni mzuri na wa watu fulani ni mbaya, kwani kila watu wanao utamaduni wao ambao ni mzuri kwa wao japo unaweza pia kwa wengine ukawa mzuri au mbaya pia. Hawa hudai kuwa hakuna kanuni maalumu na za kijumla kwa watu wote na mahala pote zenye kutumika kufasiria matendo fulani kuwa haya ni mema na haya ni maovu bali jamii yenyewe ndio kipimo cha ubaya na uzuri wa utamaduni wao. Hii ni (moral subjectivism approach). Wao hukanusha uwepo wa kanuni jumuishi zinzotambuliwa na wanadamu wote kuhusu maadili. Kwa hiyo kwao, huyaangalia maadili kwa mtazamo wa mtu, watu au jamii fulani. Baadhi ya wafuasi wa mitazamo hiyo ni wanaelimu jamii (sociologists).

Mtazamo wa tatu ni ule unaodai kuwa sio kila sehemu maadili au kanuni za maadili hufuatwa, mtazamo huu huitwa (amorality au amoral approach). Mtzamo huu hufuatwa zaidi na wanaelimu biashara au uchumi. Katika biashara, hudai kuwa biashara haina cha maadili au haifuati/kufungamana na kanuni za kijamii au za ulimwengu kuhusu maadili ya kawaida, bali biashara ina maadili yake ambayo ndio taratibu na msingi wa biashara. Na misingi hiy au kanuni hizo ni kukuza uchumi au kuongeza faida katika biashara kwa njia yoyote ile. Kwa maana hiyo, wafanya biashara na wanaelimu biashara hujali faida inayopatikana kwa biashara na kukuza uchumi na wala sio maadili. Hapo ndipo matendo kama ulaghai, wizi, uongo, kuuza bidhaa feki huhusika pia, lengo ni kuongeza faida kiuchumi. Kwa mfano, kampuni inaweza kuzalisha bidhaa ambayo inawezakuwa na madhara kwa watumiaji wake na ikagundulika kuwa kampuni ilishazalisha bidhaa hizo, lakini wakisitisha kuzipeleka sokoni, kampuni itapata hasara kubwa…na hivyo, inaamuliwa kuzipeleka bidhaa hizo sokoni haijalishi watu wataathirika au la. Ilmradi faida ipatikane…..katika msingi huo wafanya biashara hudai kuwa kitendo hicho ni kufanya biashara bila kuhusika na kanuni za kimaadili. na katika ulimwengu huu wengi hukimbilia kwenye biashara, hakika watakuwa na mtazamo huo.

Mtazamo mwingine wa kimaadili ni ule unaoitwa “utilitalianism approach of morality” ambao hudai kuwa tendo ni jema au baya kulingana na mtazamo wa walio wengi kuona kuwa kile kilicho na manufaa kwa wengi na maafa kwa wengi, hivyo wao huamua kuwa tendo hilo ni jema au ovu. Kumbe jamii ikiona hili suala sio zuri kwao basi linakuwa baya au ovu, ikiona zuri basi linakuwa zuri.

Mtazamo mwingine ni ule unaofuatwa na wale wanaodai kuwa hakuna tendo baya au zuri kwa lenyewe isipokuwa kila tendo ni zuri bali huja kuwa baya pale ambapo mtu humuumiza, na huja kuwa zuri pale linapokuwa na manufaa kwake. Kumbe, kwa mtazamo huu mtu akiiba au kufisadi lakini akanufaika kama yeye hakika hawezi kuacha matendo hayo na huwezi kumwambia kuwa hayo matendo ni maovu. Kwake ni mazuri, yaani yamemnufaisha.

Kwa maelezo haya mafupi kuhusu maadili, naomba niseme kuwa, mitazamo ya “moral subjectivism, utilitarianism, amorality, na ule unaosema tendo ni baya au zuri pale linaponufaisha au kuumiza” ndio mitazamo ambayo hufuatwa na watu wengi katika ulimwengu wa sasa, zikiwemo nchi tajiri ulimwenguni. Nchi hizi hufuata mitazamo hiyo na ndio maana wao hufanya kila njia iwe bora au mbaya kuzinyonya nchi masikini, kwao, matendo ya nchi masikini ndio mabaya, ila kwa wao yao ndiyo mazuri, ndio maana tunao uvamizi na vita kwa nchi zetu ilmradi wao wapate kile wanachotaka kutoka kwetu ili wakuwe kiuchumi.

Sanjali na hilo, viongozi wengi, katika jamii zetu na nchi kwa ujumla, ni wafanya niashara ambao hufuata mtazamo wa ‘amorality’, ambao kwao pesa na utajiri ndio kila kitu na hivyo wao wako tayari kufanya kila kitu ikiwa hata ni kuua, kuiba, kuhonga kupata uongozi, kufisadi mali za umma n.k ilmradi wapate kile wanachokitaka. Hawa watu hatuwezi kuwalaumu bali msingi ni kuwarudisha katika njia kwa kuwaelimisha japo ni jambo gumu sana, maan samaki mkunje angali mbichi. Vilevile katika suala la uongozi kuna falsafa ya siasa(uongozi) ambayo iliasisi wan a mwanafalsafa wa kiitaliano Nicollo Maciavelli, ambayo inaitwa “principle of double effects” ambayo aliijengea hoja madhubuti ya kuyakana maadili na kuzalisha falsafa ya utawala anayoieleza katika andiko la ‘the perice’, yaani utawala wa mwanamfale. Huyu yeye anakanusha kufuata misingi ya kimaadili katika kupata uongozia, bali kiongozi aanweza kuwa mlaghai, mwizi, meongo yaani (pretender) ilimradi aendane na kukamata miatazamo ya jamii anayotaka kuiongoza, na apate madaraka. Yeye, anasema kuwa kiongozi atumie njia au mbinu zozote zile hadi afanikishe kupata huo uongozi, ziwe mbinu mbaya au nzuri. Alafu baada ya hapo kiongozi atumia mbinu zozote zile kulinda nafasi hiyo. Kwanini, anasema hivyo, kwa muono wake alisema hivyo, kulingana machafuko ya maadili kwa ufalme wa Roma ambao ulienea hadi kwa makasisi wa makanisa hadi kiongozi mkuu, papa. Kwahyo, Machieavelli akahitimisha kuwa binadamu ni wabaya kwa wenyewe kwahiyo hahitaji mtu kuwahurumia na kuonesha upendo kwao, na ukifanya hivyo, wanakumaliza. Ndio maana akakanusha kiongozi kufuata maadili. Viongozi wengi wetu wan chi hii hasa walioenda shule wameiga falsafa hiyo kwa kulaghai wananchi na kufanya uovu huo unaouona lengo wanufaike wao na kulinda kwa njia yoyote ile uongozi huo. Hawna elimu ya maadilia na hawayajui maadili.

Nilitoa mfano mzuri kuhusu viongozi wetu wasiofuata sheria, kuwa kama jamii au kabila lina mwono wake wa kimaisha na matendo yake – ambapo, kuna matendo fulani wao ni mema, na ni mabaya na kwa jamii nyingine sio mazuri au mabaya. Mtu aliyezaliwa kwa familia yenye uchu wa vitu vya kiulimwengu, ukosefu wa fadhila kwa wengine, wezi, watusi, walaghai n.k, hakika na yeye atakuwe katika maisha hayo hadi anakuwa mtu mzima. Tabia hizo zitaendelea kwa kuwa katika makuzi yake tabia hizo amezizoea. Mfano, kama baba ni tajiri lakini ni mlaghai, na mdhulumaji watu madeni yao, na kufanya hivyo kuna mfanya awe na mali hizo, anasomesha watoto katika shule za matajiri, ana mali kibao….mwishowe huyu mwanae, atakuwa akiwa na mawazo ya kuwa ulaghai ni mzuri na ni njia ya kuendelea, hakika huyu akiwa kiongozi fulani hawezi kujua kuwa yale ni matendo maovu bali ataendelea na tabia hizo zilizomkuza ndio utasikia, kaiba pesa za umma, fisadi, hatojali watu wanapopata hadha za kimaisha. Huyo anapochaguliwa huwezi kumlaumu. Wengi wa viongozi wetu wameumbwa kwa maisha na mazingira kama hayo, ndio maana unasikia kashfa kama ESCROW, IPTL,RICHMOND, DOWANS MELEMETA,BOT, WAUZAJI WA MADAWA YA KULEVYA, MAJANGILI n.k. alafu baada ya kashfa hizo wanajiuzulu na wanatembea makanisani na majukwaani wanaanza kujitamba na kutoa misaada na wanaonekana mashujaa kwao, hatimaye wanaomba kuwa viongozi tena alafu mnawarudisha madarakani tena, alafu ati utegemee hao hao utawaambia wabadilike wafuate maadili, au wajali pesa na mali za umma, wakuelewe. Wakifanya hivyo, huo utakuwa ni muujiza.

Kwa maoni yangu ni kuwa hatuwezi kulalama kuwa nchi haina maadili, nidhamu na watu wakajua na kuwa na tunu hizo, la hasha! Unahitajika msasa wa uhakika. Nchi nzima watu wake wamo katika dimbwi la kutokujua maadili ni nini, na mmomonyoko wake, kwa kuwa kila mtu anao mtazamo wake wa kimaadili uliomkuza. Ndio maana hata bunge letu wabunge wake hutunga sheria si chini ya msingi wa maadili ya taifa, bali kwa kuwa wao hujua kuwa kazi kuu ya bunge ni kutunga shria, pasi kujua sheria hizo zitatumika na kusimamiwa ipi na kwa misingi ipi. Bila kujua mantiki sahihi ya sheria hizo ni ipi itakayoiongoza nchi yetu katika kilele cha mafanikio. Hawawezi kutunga sheria zenye manufaa ya kitaifa kwa sababu, taifa kama taifa hatuna misingi yetu ya pamoja tulioibaini kama sisi na kuamua kuwa ni maadili ya taifa popote pale nchini. Ndio maana kila mbunge akiamka akawaza na wala sio kufikiri anakuja na hoja binafsi kwa ajili ya kutunga sheria anayodhani yeye ni sahihi kwake kumbe pengine in audhaifu ndani mwake na haikidhi haja kwa watanzania wote.

Mathalani, nilishawahi kujiuliza kuhusu sheria kusimamia haki au kutoa haki kwa wale walionyang’anywa hali hizo. Na hudai kuwa hakimu au wanasheria wao hufasiri sheria ili kutenda haki kwa watu, ila mimi hujiuliza swali moja kuwa haki hubainishwa na sheria au sheria hulinda na kusimamia haki? Vilevile, mwanasheria au hakimu yeye ndiye mtoa haki au yeye ni chanzo cha kuitambua na kumwonesha mdai haki yake? Kama sheria ni msumemo, inakuwaje mtuhumiwa nakuwa amefanya kosa kweli, ila mshitaki ameshinwa kudhibitisha, na mtuhumiwa anashinda kesi na tunasema haki imetendeka? Je, kushindwa kuwa na ushahidi wa kutosha au kushindwa kujieleza kwa mshitaki kunaondoa kosa liliotendwa? Wakati huo huo kuna watu wanashindwa kwa sababu mbalimbali kuthibitisha madai yao juu ya kesi lakini wametendewa visivyo, ila hukumu inatoka kuwa watuhumiwa wameshinda? Hizo ndizo sheria zetu zinazotungwa na watu ambao wametoka katika jamii zetu. Hakimu, kwa mfano, anaweza akaifasiri vibaya sheria na kutoa hukumu isiyo, mhusika akakata rufaa na kwenda mahakama za juu, na kweli ikabainika kuwa hakutendewa haki na hukumu ya mwanzo. Lakini hakimu aliyekiuka au kushindwa kuifasiri sheria vizuri ama kwa maksudi au bila kudhamiria hachukuliwi hatua yoyote ya kumwadhibu kwa kosa lile. Sheria inamlinda hakimu kuwa inategemea uwezo wa a hakimu wa kuifasiri sheria….alafu kwa sheria hiyo usema sheria ni msumeno. Hiyo ndio nchi yetu na watu wake. Sheria kimsingi ipo kulinda maadili na bila maadili hakuna sheria, lakini sheria zetu hazina misingi madhubuti ya kulinda maadili yetu bali ni matamko tu kwa sababu na sisi huwa tunashuhudia wenzetu wengine wakitoa matamko hayo.

Kwa maoni yangu yenye kukubaliana na hoja yako, ni kwamba, nchi nzima imeoza, imekiuka maadili kama taifa ambayo angalau mwl Nyerere alikuwa ameanza kuiweka kwa mwono mmoja uliotokana na falsafa ya ujamaa, ambapo kumbe Nyerere ni mwanafalsafa mfalme aliyependekezwa na Plato, mwenye uwezo wa kuiongoza jamii kwa misingi ya haki na kuona ni kipi kinatakiwa. Ili nchi yetu irudi katika maadili ya kitaifa yaliyojengwa chini ya msimamo na mtazamo mmoja kama taifa, tunahitaji kufikiri upya na sio kuwaza kujua kuwa nchi yetu itakuwaje inavyotakiwa iwe. Na hili suala, linawahitaji watu waliobarikiwa kimaono hasa wanafalsafa na wenye uwezo wa kufikiri na kuufikia ukweli thabiti. Naamini wapo mmoja wapo ni wewe, na mimi ambao tunachangia mada kama hizi hapa. Tunapaswa kuendeleza elimu hii kwa watanzania wenzetu, kwa njia yoyote ile ila watu waweze kufunguka macho.

Kwa kuwa watanzania ni mchanganyiko na ni jamii tofautitofauti, hatuwezi kuegemea mtazamo wa kuwa kila mtu anafikiri ana akili hivyo anajua jema na baya. La hasha! Sio wote wanaojua hivyo, kumbe kama hawajui, inatupasa kuzunguka nchi nzima upya, kusoma na kuzichunguza jamii zetu na tabia zake ili tubaini ni matendo yapi kwao ni mabaya au mazuri kwa mitazamo na utamaduni wao, alafu tuunganishe, ufanano na utofauti huo kwa ujumla tuyaweke pamoja yale amabayo ni mema kwa kila upande, na kupitia elimu na taasisi na vyombo vya kiserikali – serikali kuu, bunge na mahakama, wajadili chini ya uongozi wa wataalamu waliochagulia kama wanafalsafa, na wasomi wenye ung’amuzi wa ajabu juu ya maadili ambao tayari watakuwa wameisoma mitazamo yote ya maadili na kuunganisha na kuja na matazamo mmoja ambao utayafasiri maadili kwa mwono mzuri wa kitanzania na kuitwa kuwa haya ndio maadili kwa mujibu wa mtazania. Na tutoe elimu ya kina kuhusu dhana ya kuyaangalia maadili kwa mwono mmoja kuwa maadili au matendo ya binadamu ni mazuri na mabaya kwa yenyewe (moral universal principle – moral objectivism/absolutism). Hayo ndiyo yatakayotufasiri na hata mtu akikosea atajua dhahiri kuwa kakiuka maadili ya kitanzani, na ama ataelimishwa au kuadhibiwa kwa misingi ya maadili ya kitanzania na hapo ndipo tutakuwa sahihi kusema nchi yetu ina maadili kwa kuwa sisi kama taifa tayari tulishakuabaini na yapo hadi katika vitabu na adidu rejea za taifa. Hata vyombo vya kutunga sera na sheria vitatunga sera/ sheria hizo chini ya misingi hiyo ya umaadili wa taifa letu na si kama wanavyofikiri wao.

Tukishakuyagundua hayo, ni jukumu pia hayo mambo kuingizwa katika mitaala ya elimu yetu, na kuanzisha somo la maadili kwa ngazi zote na somo hilo liwe la lazima na msingi kwa wanafunzi wetu wote na lihimizwe. Pili hilo liende sambamba na tafakuri kuu juu ya falsafa na mwono wa misingi ya kitaifa ambayo ndio hiyo itatuongoza katika kupanga kila jambo kwa maadili ya taifa letu, na hivyo kuwakuza vijana wetu katika misingi hiyo amabayo ndiyo hiyo itakuwa inawafasiri watanzania mahara popote. Kwa kipindi kirefu, elimu hii ya umaadili kwa watu wetu ikitolewa mwishowe watu watautambua mwelekeo wao na kulijua taifa lao na kuwa tayari kuipigania kwani wanao utambulisho wao wa taifa. Huwezi kusema maadili ya taifa bila taifa lenyewe kuwa na maadili hayo ambayo watu wake wamebaini wao.

Hili jambo aliliona mwl Nyerere ndio maana aliamua kuunda falsafa ya ujamaa na kujitegemea ambayo kila kitu kilichokuwa kikiibuliwa kiliaksi misingi ya ujamaa, na maadili yakiwemo. Lakini, baadaye uhuni uliliingilia taifa hili na kupoteza utambulisho wetu ambapo waliofanya hivyo, ndio hao hao wanaokiuka miongozo hiyo na kuliharibu taifa kulifanya lisiwe na mwelekeo.
YANGU NI HAYO
 
Philosophy:

I think when it comes to maadili, the country or the society in general has a set of maadili. So to me having maadili isn't an issue. The issue is how to enforce them. Even when the country followed the ujamaa policies, the enforcement of maadili was an issue. So instead of perpetuating length discussions that don't bring any tangible results, can the country learn from its past mistakes or from other countries?

Countries in Northern Europe, North America, Australia or Japan have good tax systems which fund all public activities. In this countries, there's a direct relationship between the tax individuals pay and the services they receive in return. I might be wrong, but taxation has enforced ethical behaviors because people question the actions of their leaders.

On other hand, where you start moving southward where tax systems are weaker, the ethical issues are rampant. Even in Southern Europe, countries such as Greece and Italy are struggling. My question is can we equate the tax system in Tanzania with the country's ethical issues, in particular at highest level of leadership?

If a police office doesn't think that your tax pays his salary, why should he respect you or his job? If the president thinks that his efforts to procure foreign aid build schools for your children, hospitals and pay for your salaries, why should he respect the law?
 
Philosophy:

I think when it comes to maadili, the country or the society in general has a set of maadili. So to me having maadili isn't an issue. The issue is how to enforce them. Even when the country followed the ujamaa policies, the enforcement of maadili was an issue. So instead of perpetuating length discussions that don't bring any tangible results, can the country learn from its past mistakes or from other countries?

Countries in Northern Europe, North America, Australia or Japan have good tax systems which fund all public activities. In this countries, there's a direct relationship between the tax individuals pay and the services they receive in return. I might be wrong, but taxation has enforced ethical behaviors because people question the actions of their leaders.

On other hand, where you start moving southward where tax systems are weaker, the ethical issues are rampant. Even in Southern Europe, countries such as Greece and Italy are struggling. My question is can we equate the tax system in Tanzania with the country's ethical issues, in particular at highest level of leadership?

If a police office doesn't think that your tax pays his salary, why should he respect you or his job? If the president thinks that his efforts to procure foreign aid build schools for your children, hospitals and pay for your salaries, why should he respect the law?[/QUOTE

Uko sahihi. Lakini kwenye hoja yangu sikuzungumzia maadili peke yake bali pia nidhamu. Unapozungumza suala la kodi mwananchi anayolipa na matokeo ya kodi hiyo kwa maendeleo ya nchi na ya watu nadhani unaongelea kwa kiasi fulani nidhamu na uwajibikaji. Nidhamu ya kutimiza majukumu ambayo mtu amepewa katika utumishi wa umma. Kwahiyo hivi vitu viwili vinaendana kama nilivyoongea. Hatutaweza kuendelea kama taifa kama hatuna nidhamu ya fedha na matumizi yake lakini pia bila nidhamu hiyo hatutaweza kufikia malengo yetu katika nyanja mbali mbali.
 
nadhani kuwa kwa kutokumuelewa mtu hoja yake kwa sababu ama ya ulefu wa maelezo au kutokutaka kufungua macho kuelewa kile knachomaanishwa haimaanishi kuwa ni mjadala usiona na msingi bali kutokuwa na umsingi kuko ndani ya yule asiyewezakung'amua kile kinachomaanishwa.

katika hoja yetu msingi ya maadili na nidhamu ya taifa.....naomba nieleze kuwa, nidhamu ni kipengele kisichoweza kuepa katika maadili. matendo yote ya kinidhamu ni matokeo ya maadili ya watu fulani au mtu mwenyewe. mimi nachokimaanisha ni kuwa hauwezi kulaumu watu kutokuwa na maadili wakati taifa halina mfumo au mwongozo fulani ambao kama wao taifa wameufuata ili uwaongoze kama maadili yao. nchi zote zenye kuwa na maadili, na nidhamu ya mambo yao kama kodi na matumizi ya kodi hizo, hawafanyi hivyo kutoka kusikokuwepo; bali, hufanya hivyo kwa kuegemea misingi ya umaadili wa taifa ambao wao wanaufuata. kusimamia maadili na kuyafuata na kutekeleza sheria, ni matokeo ya watu hao kuwa na utambuzi juu ya kile walichokubaliana kama taifa ili kusimamia misingi ya taifa lao iliyotokana na maadili ya taifa chini ya mfumo fulani wa ama falsafa yao(imani), au mfumo fulani wa maisha walioufuata.

mathalani marekani ambao wao waliufuata mfumo wa ubepari, tayari kwa msingi huo wamejenga utambuzi wao na misingi ya utaifa wao ambao ulikuwa ni matokeo fulani ya maadili waliyojiwekea ili yawaongoze kuwatambulisha kama wao. kipaumbele chao kikubwa ni kuwa taifa kubwa na lenye kuongoza kwa uchumi duniani. hivyo, maadili yao yamejengeka katika kulinda kipaumbele hicho, na sheria zote na nidhamu yao imejikita kulinda mfumo huo na si vinginevyo. maadili na mfumo fulani wa maisha huwezi kuvichenganisha na ukasema una maadili.
 
Uko sahihi. Lakini kwenye hoja yangu sikuzungumzia maadili peke yake bali pia nidhamu. Unapozungumza suala la kodi mwananchi anayolipa na matokeo ya kodi hiyo kwa maendeleo ya nchi na ya watu nadhani unaongelea kwa kiasi fulani nidhamu na uwajibikaji. Nidhamu ya kutimiza majukumu ambayo mtu amepewa katika utumishi wa umma. Kwahiyo hivi vitu viwili vinaendana kama nilivyoongea. Hatutaweza kuendelea kama taifa kama hatuna nidhamu ya fedha na matumizi yake lakini pia bila nidhamu hiyo hatutaweza kufikia malengo yetu katika nyanja mbali mbali.

Shayu:

Yes in my post I used maadili and nidhamu interchangeably. My question to you now is what should be done to reverse the trend. It seems to me we know the problem and at various points committees have been selected to investigate the matter and proposal solutions. However, it doesn’t seem that there are any commitments to get rid of the problem or to reduce it to an acceptable level.

When I was growing up, my parents didn’t raise me to be somebody who isn’t committed to excellence. The same could be said about any Tanzanian child, even the most hated Fisadi on the land. However, due to various reasons, my work environments changed me. Take for example my first job (it was a government job). The monthly salary I received in this job didn’t last for more than two weeks and without taking a second thought I found myself accepting bribes and committing corruption just to survive. In essence, I was irresponsible and unethical public servant. This story can be repeated by many public servants.

The question is if I had been still working, what would you have done to change me and other in similar situation? To state it differently, what practical solution would you offer?

I know for both of you, the entire discourse is a philosophical one. However, in real life, one has to be pragmatic in order to bring out practical solutions which change society.
 
nadhani kuwa kwa kutokumuelewa mtu hoja yake kwa sababu ama ya ulefu wa maelezo au kutokutaka kufungua macho kuelewa kile knachomaanishwa haimaanishi kuwa ni mjadala usiona na msingi bali kutokuwa na umsingi kuko ndani ya yule asiyewezakung'amua kile kinachomaanishwa.

katika hoja yetu msingi ya maadili na nidhamu ya taifa.....naomba nieleze kuwa, nidhamu ni kipengele kisichoweza kuepa katika maadili. matendo yote ya kinidhamu ni matokeo ya maadili ya watu fulani au mtu mwenyewe. mimi nachokimaanisha ni kuwa hauwezi kulaumu watu kutokuwa na maadili wakati taifa halina mfumo au mwongozo fulani ambao kama wao taifa wameufuata ili uwaongoze kama maadili yao. nchi zote zenye kuwa na maadili, na nidhamu ya mambo yao kama kodi na matumizi ya kodi hizo, hawafanyi hivyo kutoka kusikokuwepo; bali, hufanya hivyo kwa kuegemea misingi ya umaadili wa taifa ambao wao wanaufuata. kusimamia maadili na kuyafuata na kutekeleza sheria, ni matokeo ya watu hao kuwa na utambuzi juu ya kile walichokubaliana kama taifa ili kusimamia misingi ya taifa lao iliyotokana na maadili ya taifa chini ya mfumo fulani wa ama falsafa yao(imani), au mfumo fulani wa maisha walioufuata.

mathalani marekani ambao wao waliufuata mfumo wa ubepari, tayari kwa msingi huo wamejenga utambuzi wao na misingi ya utaifa wao ambao ulikuwa ni matokeo fulani ya maadili waliyojiwekea ili yawaongoze kuwatambulisha kama wao. kipaumbele chao kikubwa ni kuwa taifa kubwa na lenye kuongoza kwa uchumi duniani. hivyo, maadili yao yamejengeka katika kulinda kipaumbele hicho, na sheria zote na nidhamu yao imejikita kulinda mfumo huo na si vinginevyo. maadili na mfumo fulani wa maisha huwezi kuvichenganisha na ukasema una maadili.

Philosophy:


Life evolves and there are a lot of unknown variables that come into play in life without our knowledge and we have to adapt and in some cases abandon the conventional wisdom. The capitalism that is practiced in the United States today isn’t the same that was practiced 100 years ago.


If the form of modern capitalism had existed during the days of Karl Marx, probably he wouldn’t have written Das Kapital. If Julius Nyerere and other socialists had known beforehand that socialism wouldn’t triumph by 1990, probably they would have tried other means of social reforms. What I am trying to say is maadili and nidhamu didn’t fall from outer space or cast in stones. They evolve and define cumulative human experience.


The founding fathers of the USA didn’t envision the creation of a super power. As a matter of fact some of them opposed the use of USA power outside the country. So whatever feature of American capitalism you observe today is a work of later generations.

What I am trying to say is the current generation of Tanzanians has the responsibility to define its own destiny which includes maadili and nidhamu as well. The work of Nyerere can inspire us; nonetheless, we can’t emulate it in its entirety or the way he thought it should be because we live in different generations.
 
Maadili na nidhamu ni silaa kubwa towards our success,sometimes we can even be favoured in some of the areas not because we are the best ila ni kwa maadili na nidhamu uliyonayo

Mtoto huzaliwa akiwa kama an empty box,therefore the society & the environment which is responsible of this kid determine alot on how the kid will be,kwa kuona tuyafanyayo,kusikia tuyaongeayo e.t.c

Let us be the best role models to the young ones by doing what is right kwa sababu u never know kwa mabaya au mazuri tuyafanyayo kuna ambao wanaiga
 
Nice thread, but I think , it could have garnered a lot of inputs if it was shared in the intelligence forum.
 
Shayu:

Yes in my post I used maadili and nidhamu interchangeably. My question to you now is what should be done to reverse the trend. It seems to me we know the problem and at various points committees have been selected to investigate the matter and proposal solutions. However, it doesn't seem that there are any commitments to get rid of the problem or to reduce it to an acceptable level.

When I was growing up, my parents didn't raise me to be somebody who isn't committed to excellence. The same could be said about any Tanzanian child, even the most hated Fisadi on the land. However, due to various reasons, my work environments changed me. Take for example my first job (it was a government job). The monthly salary I received in this job didn't last for more than two weeks and without taking a second thought I found myself accepting bribes and committing corruption just to survive. In essence, I was irresponsible and unethical public servant. This story can be repeated by many public servants.

The question is if I had been still working, what would you have done to change me and other in similar situation? To state it differently, what practical solution would you offer?

I know for both of you, the entire discourse is a philosophical one. However, in real life, one has to be pragmatic in order to bring out practical solutions which change society.


Swali la kujiuliza ni kweli serikali haina pesa ya kuwalipa wafanyakazi wake vizuri ili wasiingie kwenye majaribu? swali la pili je watu wetu wako committed kutaka kuona taifa letu likiendelea ? Nakubaliana na wewe kabisa wafanyakazi wa umma wanahitajika kupewa mishahara itakayo kidhi mahitaji yao lakini pia kwa upande wao wana majukumu kwa taifa hili je wanawajibika ipasavyo? Nadhani kama tukiweka taifa hili mbele na kufanya kazi pamoja kwaajili ya matokeo ya pamoja kwa maenndeleo ya nchi yetu mambo mengi tutayamaliza. Lakini sisi ambao tuko kwenye utumishi wa umma lazima tujue hatuwezi kuwa matajiri kwenye utumishi wa umma. Serikali itengeneze mazingira ambayo mtumishi wa umma ataishi maisha ambayo siyo ya umaskini. Serikali iboreshe elimu na huduma ya afya iwe bora na iboreshe mifuko ya hifadhi za jamii ili mfanyakazi wa umma aishi bila hofu na kulitumikia taifa lake kwa moyo wake wote. Tuende mbele turudi nyuma lazima wawepo watumishi wa umma watu watakaofanya taifa hili lisonge mbele. Sisemi kama watumishi wa umma peke yake ndio watakaofanya taifa hili liendelee bali wao ndio wanaotumikia muundo. Wengine ambao hawako katika serikali ni wazalishaji mali na baadhi watoa humuma binafsi. Kama tukifanya mfumo huu kuwa na muingiliano mzuri kwa faida ya pamoja taifa hili litasonga mbele. Tutakapojua hatufanyi kazi kwaajili yetu binafsi bali pia kwa taifa letu kwanini tusiendelee? Tujuulize how much energy we use for development of this country both intellectual and physical? Tuna behave kama vile tayari tumeendelea. Sheria iko hivi unapata kulingana na juhudi zako. so if we change our mind kutoka katika ubinafsi kuja kwenye utaifa ni hatua moja kubwa ya maendeleo. Naamini kabisa tunaweza kuongeza uchumi wa taifa hili na wafanya kazi wa taifa hili wakalipwa vizuri.

Kama watu wakifanya kazi kwa bidii katika uzalishaji kwa mfano; na serikali ikikusanya kodi na kubana matumizi yake yasiyo ya lazima wafanya kazi watalipwa vizuri. Kwahiyo ni lazima tujenge uzalendo kwa watu wetu ili wapende kulipa kodi. Kodi ambayo itatumika kwa ulinzi na usalama wa mali na wa watu wa taifa hili wote kwa ujumla na kwa huduma za jamii. Kwahiyo hili ni suala la committment kwa upande wa serikali. Kujitolea kutaka taifa hili liendelee na maisha ya watu yaboreke. Naamini serikali ina uwezo wa kulipa watu wake vizuri kama watakuwa na nidhamu katika ukusanyaji wa kodi na matumizi yake. Hapo ndipo kuna matatizo. Sidhani kama tutapungukiwa kama tutafanya yaliyo sahihi na kama tutafanya kazi kwa bidii. We must have free minds.
 
Philosophy:


Life evolves and there are a lot of unknown variables that come into play in life without our knowledge and we have to adapt and in some cases abandon the conventional wisdom. The capitalism that is practiced in the United States today isn't the same that was practiced 100 years ago.


If the form of modern capitalism had existed during the days of Karl Marx, probably he wouldn't have written Das Kapital. If Julius Nyerere and other socialists had known beforehand that socialism wouldn't triumph by 1990, probably they would have tried other means of social reforms. What I am trying to say is maadili and nidhamu didn't fall from outer space or cast in stones. They evolve and define cumulative human experience.


The founding fathers of the USA didn't envision the creation of a super power. As a matter of fact some of them opposed the use of USA power outside the country. So whatever feature of American capitalism you observe today is a work of later generations.

What I am trying to say is the current generation of Tanzanians has the responsibility to define its own destiny which includes maadili and nidhamu as well. The work of Nyerere can inspire us; nonetheless, we can't emulate it in its entirety or the way he thought it should be because we live in different generations.
........"
What I am trying to say is the current generation of Tanzanians has the responsibility to define its own destiny which includes maadili and nidhamu as well. The work of Nyerere can inspire us; nonetheless, we can't emulate it in its entirety or the way he thought it should be because we live in different generations. "]


I think your conclusion follow into the logic of my conclusion though it's contradictory in itself, and I can not see any new idea instead of contradiction in your conclusion. That, when we talk about national morality/technicalities, we have already placed ourselves as a nation in which we view as one in every aspect of life. Therefore, the morality ​​is the result of an integrated national idea in general about their system of life. So morality ​​comes from the citizens themselves who exist with common consensus approaches to follow as a community. in the sense that every action done as a nation must be in the form of national moral guide aimed at making the nation to be as it is for its uniqueness. That's why I offered an example of capitalism in the United States, or socialism in the past Tanzania. That, in Tanzania, for example, its people under the leadership of a great insights felt their nation will be built under socialism where the system itself would lead one interpretation and direction of their moral mode ​​together and build on the discipline among such people. US, they were led or guided by the perspective that's capitalism that explores their values ​​and discipline as well.
 
Swali la kujiuliza ni kweli serikali haina pesa ya kuwalipa wafanyakazi wake vizuri ili wasiingie kwenye majaribu? swali la pili je watu wetu wako committed kutaka kuona taifa letu likiendelea ? Nakubaliana na wewe kabisa wafanyakazi wa umma wanahitajika kupewa mishahara itakayo kidhi mahitaji yao lakini pia kwa upande wao wana majukumu kwa taifa hili je wanawajibika ipasavyo? Nadhani kama tukiweka taifa hili mbele na kufanya kazi pamoja kwaajili ya matokeo ya pamoja kwa maenndeleo ya nchi yetu mambo mengi tutayamaliza. Lakini sisi ambao tuko kwenye utumishi wa umma lazima tujue hatuwezi kuwa matajiri kwenye utumishi wa umma. Serikali itengeneze mazingira ambayo mtumishi wa umma ataishi maisha ambayo siyo ya umaskini. Serikali iboreshe elimu na huduma ya afya iwe bora na iboreshe mifuko ya hifadhi za jamii ili mfanyakazi wa umma aishi bila hofu na kulitumikia taifa lake kwa moyo wake wote. Tuende mbele turudi nyuma lazima wawepo watumishi wa umma watu watakaofanya taifa hili lisonge mbele. Sisemi kama watumishi wa umma peke yake ndio watakaofanya taifa hili liendelee bali wao ndio wanaotumikia muundo. Wengine ambao hawako katika serikali ni wazalishaji mali na baadhi watoa humuma binafsi. Kama tukifanya mfumo huu kuwa na muingiliano mzuri kwa faida ya pamoja taifa hili litasonga mbele. Tutakapojua hatufanyi kazi kwaajili yetu binafsi bali pia kwa taifa letu kwanini tusiendelee? Tujuulize how much energy we use for development of this country both intellectual and physical? Tuna behave kama vile tayari tumeendelea. Sheria iko hivi unapata kulingana na juhudi zako. so if we change our mind kutoka katika ubinafsi kuja kwenye utaifa ni hatua moja kubwa ya maendeleo. Naamini kabisa tunaweza kuongeza uchumi wa taifa hili na wafanya kazi wa taifa hili wakalipwa vizuri.

Kama watu wakifanya kazi kwa bidii katika uzalishaji kwa mfano; na serikali ikikusanya kodi na kubana matumizi yake yasiyo ya lazima wafanya kazi watalipwa vizuri. Kwahiyo ni lazima tujenge uzalendo kwa watu wetu ili wapende kulipa kodi. Kodi ambayo itatumika kwa ulinzi na usalama wa mali na wa watu wa taifa hili wote kwa ujumla na kwa huduma za jamii. Kwahiyo hili ni suala la committment kwa upande wa serikali. Kujitolea kutaka taifa hili liendelee na maisha ya watu yaboreke. Naamini serikali ina uwezo wa kulipa watu wake vizuri kama watakuwa na nidhamu katika ukusanyaji wa kodi na matumizi yake. Hapo ndipo kuna matatizo. Sidhani kama tutapungukiwa kama tutafanya yaliyo sahihi na kama tutafanya kazi kwa bidii. We must have free minds.

Shayu:

Your post bring out some moral questions. Is it ok for the society to achieve social and economic progress at the expense of its public workforce? Is it ok for the government to devalue it currency or quality of life so it could employee many workers? For example if the government has X amounts of financial resources and wants to employee well qualified individuals as primary school teachers, the financial resources will only maintain few positions. However, if it wants to employees many with the same amounts of financial resources, it will be forced to use the pool of unqulified teachers.

Furthermore, in the name of development, is it ok for the society to live beyond its means? In your post you said the government doesn't have money. So why do we demand social services which we can't afford and which erode moral values of those who are employed in those services?

Any country or society goes through bad time and it's ok to underpay the workforce for a short period of time. However, when underpay persists for generations, then it a crisis which can erodes the moral values of society and I think Tanzania is a typical example.
 
I think your conclusion follow into the logic of my conclusion though it’s contradictory in itself, and I can not see any new idea instead of contradiction in your conclusion. That, when we talk about national morality/technicalities, we have already placed ourselves as a nation in which we view as one in every aspect of life. Therefore, the morality ​​is the result of an integrated national idea in general about their system of life. So morality ​​comes from the citizens themselves who exist with common consensus approaches to follow as a community. in the sense that every action done as a nation must be in the form of national moral guide aimed at making the nation to be as it is for its uniqueness. That's why I offered an example of capitalism in the United States, or socialism in the past Tanzania. That, in Tanzania, for example, its people under the leadership of a great insights felt their nation will be built under socialism where the system itself would lead one interpretation and direction of their moral mode ​​together and build on the discipline among such people. US, they were led or guided by the perspective that's capitalism that explores their values ​​and discipline as well.

Philosophy:

You have interject an imaginary contradiction in my conclusion when there's none. If you have read my post in its entirety, you would have understood I was talking about unknown variables which shape ourselves, our maadili and nidhamu. And my conclusion reflects just that.

Now with regard to common consensus, contrary to your assertion, the national consensus didn't come from people. The country has always been a TOP-DOWN one. People at the to have always decided your fate and the closest to the national consensus was the process to write the new constitution. Please educate me if I am wrong.
 
Shayu:Your post bring out some moral questions. Is it ok for the society to achieve social and economic progress at the expense of its public workforce? Is it ok for the government to devalue it currency or quality of life so it could employee many workers? For example if the government has X amounts of financial resources and wants to employee well qualified individuals as primary school teachers, the financial resources will only maintain few positions. However, if it wants to employees many with the same amounts of financial resources, it will be forced to use the pool of unqulified teachers.Furthermore, in the name of development, is it ok for the society to live beyond its means? In your post you said the government doesn't have money. So why do we demand social services which we can't afford and which erode moral values of those who are employed in those services?Any country or society goes through bad time and it's ok to underpay the workforce for a short period of time. However, when underpay persists for generations, then it a crisis which can erodes the moral values of society and I think Tanzania is a typical example.
Mimi nafikiri serikali inawajibika kutoa elimu ambayo itakayowafanya watu wetu wajitegemee na wasiwe tegemezi kwa serikali. Kama elimu yetu ikiwa bora ambayo itawafanya watu wetu wawe wenye kuweza kujitegemea kimawazo na kubuni mbinu mbali mbali za kuzalishaji mali na kujiongezea kipato tutapunguza tatizo la ajira. Kwahiyo elimu ya kujitegemea lilikuwa wazo zuri sana. Nadhani serikali inawajibika kuajiri watu wachache sana lakini wote wanaobaki wanawajibika kujiajiri na kutengeneza maisha yao wenyewe. Baada ya kuwapa elimu inawapasa kujitegemea. Kama elimu yetu haitowapa uwezo huo kwa kuwafanya waweze kusimama peke yao itakuwa tatizo. Hili sio suala la kuajiri watu wengi tu bali watu watakaokuwa na skills na uwezo wa kutumikia vizuri zaidi katika serikali. Watu wenye maadili, nidhamu na uwezo wa kuwa watumishi wa umma. Kwa mfano jambo rahisi sana la kupunguza ajira ni kwenye kilimo ni watu wangapi wanashiriki katika kilimo na tuna ardhi ya kutosha? nadhani hii pia inahitaji nia ya dhati ya watu kutoka katika umaskini.Katika post yangu nilisema sio kweli serikali haina pesa inaweza kuwalipa vizuri wafanyakazi wa serikali kama ikibana matumizi yasiyo ya lazima na kukusanya kodi ipasavyo. Ikiwemo jamii yenyewe kuzingatia uzazi wa mpango kwakuwa kama hatutazingatia uzazi wa mpango huduma za jamii hazitotosheleza daima au pengine kuwa bora.Kwahiyo suala la kujiuliza hapa ni tufanye nini ili kuengeneza elimu itakayo wafanya watu wetu wawe na uwezo wa kuzazlisha na kujitegemea? Nadhani tukiwapa skills za kazi hasa kazi za uzalishaji tutakuwa tumepunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la ajira. Tutakuwa na uwezo wa ku regulate uchumi wetu vyema kama watu wetu wakizalisha vya kutosha.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom