chuwaalbert
JF-Expert Member
- Sep 17, 2010
- 3,598
- 2,115
Ndugu wana jamvi, nimesoma Hotuba aliyoitoa Mwalimu Nyerere, wakati huo akiwa Rais, kwenye mkesha wa kuamkia 1.1.1970. Nawashirikisha sehemu yeke, maana hotuba yenyewe iko kwenye kijitabu chenye kurasa nyingi.
Hatuwezi kungoja mpaka watoto wetu wamalize shule ndipo tupate maendeleo ya uchumi na maisha. Ni wajibu wa wale watu wazima wa nchi hii kuanza kazi hii ya maendeleo.
Elimu ni kitu ambacho sisi wote tunapaswa kuendelea nacho toka siku ya kuzaliwa mpaka siku ya kuiacha dunia. Taifa ambalo watu wake hawajifunzi wala hawaotumii elimu yao, litabaki nyuma kwa kuwa maskini daima. Taifa hilo uhuru wake siku zote utakuwa katika hatari ya kumezwa na mataifa yenye elimu zaidi na nguvu zaidi, na watu wake daima watakuwa katika hatari ya kunyonywa na kukandamizwa na watu wengine.
Elimu haiishi ukimaliza ulichosoma darasani. Tuna mambo mengi zaidi ya kujifunza juu ya kazi zetu na juu ya mambo ambayo tulipokuwa shule hatukupata nafasi ya kujifunza. Najua kuwa kuna wasomi wenzangu ambao sasa hawasomi kabisa. Nia yao ya kwenda shule ilikuwa kutafuta hati ambayo wangeweza kutumia kama hirizi kupata kazi. Baada ya kuipata hati hiyo kweli iliwapa kazi na sasa imetundikwa ukutani mahali ambapo kila mtu anaweza kuiona. Lakini kusoma sasa hawasomi kabisa. Hili ni kosa kubwa ambalo limetokana na mawazo ya kikoloni.
Nchi nyingine zinatumia maarifa mapya ya kuzalisha mali na zinajitegemeza kwa faida yao wenyewe. Tusipoazimia kujielimisha tutaachwa nyuma. Uhuru wetu utategemea tu huruma za watu wengine na mataifa mengine, siyo uwezo wetu sisi wenyewe. Na uhuru wa kutegemea watu wengine si uhuru, ni kilemba cha ukoka.
Source; Elimu haina Mwisho. Risala ya Rais kwa Taifa katika Mkesha wa Mwaka 1970.
Hatuwezi kungoja mpaka watoto wetu wamalize shule ndipo tupate maendeleo ya uchumi na maisha. Ni wajibu wa wale watu wazima wa nchi hii kuanza kazi hii ya maendeleo.
Elimu ni kitu ambacho sisi wote tunapaswa kuendelea nacho toka siku ya kuzaliwa mpaka siku ya kuiacha dunia. Taifa ambalo watu wake hawajifunzi wala hawaotumii elimu yao, litabaki nyuma kwa kuwa maskini daima. Taifa hilo uhuru wake siku zote utakuwa katika hatari ya kumezwa na mataifa yenye elimu zaidi na nguvu zaidi, na watu wake daima watakuwa katika hatari ya kunyonywa na kukandamizwa na watu wengine.
Elimu haiishi ukimaliza ulichosoma darasani. Tuna mambo mengi zaidi ya kujifunza juu ya kazi zetu na juu ya mambo ambayo tulipokuwa shule hatukupata nafasi ya kujifunza. Najua kuwa kuna wasomi wenzangu ambao sasa hawasomi kabisa. Nia yao ya kwenda shule ilikuwa kutafuta hati ambayo wangeweza kutumia kama hirizi kupata kazi. Baada ya kuipata hati hiyo kweli iliwapa kazi na sasa imetundikwa ukutani mahali ambapo kila mtu anaweza kuiona. Lakini kusoma sasa hawasomi kabisa. Hili ni kosa kubwa ambalo limetokana na mawazo ya kikoloni.
Nchi nyingine zinatumia maarifa mapya ya kuzalisha mali na zinajitegemeza kwa faida yao wenyewe. Tusipoazimia kujielimisha tutaachwa nyuma. Uhuru wetu utategemea tu huruma za watu wengine na mataifa mengine, siyo uwezo wetu sisi wenyewe. Na uhuru wa kutegemea watu wengine si uhuru, ni kilemba cha ukoka.
Source; Elimu haina Mwisho. Risala ya Rais kwa Taifa katika Mkesha wa Mwaka 1970.