Mawaziri wenye PhD Feki hawa hapa!

Asante mdondoaji.

Hukumu nzuri kwa hawa WADHARAULIKA (maana si waheshimiwa tena) itapatikana hukohuko majimboni kwao, kama wananchi wao wataendelea kuwachagua basi kazi ipo na hata hapa JF tukipiga kelele haitakuwa na msaada tena.

Pia tusitegemee kama JK atafanya lolote la maana kwa sababu hili suala analifahamu vizuri tena kabla yetu wote hapa.
Amani.
 
hiki ndio nilikuwa nataka kuwapa watu kwenye hoja mchanganyiko lakini nilikuwa naandaa data vizuri ila poa kwani tayari kipo hapa na walioumbuka mmeshawajua...kama vipi yangu kwenye hoja mchanganyiko muipotezee...
 
Hizo taarifa umezitoa kwenye gazeti, kuna wataalam walifanya utafiti wao wakaja na data so kama unalo hilo gaziti basi paste hapa watu wengine wasome kuliko kusema eti umesikia wakati iliandikwa front page,usiwe mchoyo weka kipande cha gazeti hapa!
 
Kanda2,
MKANDARA
IKITOKEA UNAUMWA MOYO NA NCHIMBI AKAJA NA CHETI FEKI CHA UDAKTARI AKATAKA AKUFANYIE OPARESHENI UTAKUBALI?

AKIJA KAMALA NA LESENI YA URUBANI AMBAYO NI FEKI AKASEMA ANATAKA KUPAKIA ABIRIA UTAKUBALI? KUWA NI KIONGOZI NI ACCOUNTABILITY TUMOENA BUNGE LA UINGEREZA WABUNGE WAKIJIUZULU KWA KUTUMIA POUNDS TANO-SAWA NA ELFU KUMI ZA TANZANIA.NAGU ANATUWAKILISHA MIKUTANO MINGAPI YA BIASHARA KAMA WAZIRI MWENYE PHD? KINA KOMBA WAMEKOSA UWAZIRI KWA VILE ELIMU YAO INAONEKANA NDOGO. HAWA WENYE PHD FEKI HAKUNA HATA MMOJA ASIYE WAZIRI.WAMEDANGANYA WAFUKUZWE KAMA NI JAMAA ZAO SORRY.WEWE UKO CANADA UNASHINDWA KUJUA NINI MAANA YA KUWAJIBIKA

Mkuu wangu Nchimbi hawezi kuwa daktari wa kufanya Operation ikiwa hakusoma na hana cheti cha kufanya kazi hiyo.. Sii kila daktari anafanya upasuaji hata kidogo wala rubani wa ndege ya abiria hawezi kuajiriwa pasipo kupitishwa na pia mwanachama wa marubani.. ila waziri anaweza kuwa waziri pasipo cheti wala digrii ya taaluma fulani (specific), hivyo digrii ya chuo fulani kinachotambulika sio kigezo cha uwaziri pamoja na kwamba binafsi ningependa iwe hivyo.

Tatizo langu ni kwa wale waliosoma shule za Open University kuwa nao wamegushi vyeti, hivi mlitaka waweseme kitu gani?..kusoma wamesoma kweli lakini sii vyuo vinavyotambulika kwa hiyo kosa ni lazima liwe tofauti. Mkuu hata mahakamani upande wa mashtaka wakikosea ku register shtaka, hakimu huwa hana sababu ya kubadilisha hukumu yake hata kama itaonekana kuna makosa yamefanyika, itakuwa hana budi ila kuwachia mshtakiwa.

Hilo la Nchimbi, lilitakiwa toka mwanzo mtu huyu asiajiriwe, kutokana na kutoridhishwa na hizo degree zake lakini mnapomshuku kitu ambacho mlikifahamu toka mwanzo machizi ni sisi wenyewe.
Kusoma sii kuhitimu..na ndilo kosa kubwa tunalofanya. Mkuu wangu sote tumeenda shule na wengine tumetoka watupuuuu, pamoja na kwamba nilikuwa mtu wa mwisho toka shule ya msingi. Lakini maadam nilifanya mtihani wa mwisho kwa elimu yangu yamadrasa kwa nini nisiandike nilisoma hadi darasa la saba?. Hata kama niliruka au kurushwa madarasa kulingana na taratibu ilikuwa jukumu lenu kufahamu kwa nini nimechukua muda mfupi hivyo kabla sijaajiriwa. Sasa nini sababu ya kuwa na interview ikiwa leo cheti ndicho kinatoa ajira badala ya elimu kuwa ni uwezo wa mtu huyo ktk kuimudu nafasi anayogombea.

Hivyo kipimo cha elimu ya mtu ni lazima kiambatane na maswali yanayohusu kazi husika, ikiwa wewe kabuntas utatoka kapa, kama kweli Nchimbi hakusoma ama hana elimu anayodai yapo maswali madogo sana yangemwengua toka ktk wagombea, wala asingethubutu kujitangaza. licha ya yote haya aliyemchagua ni JK, yeye anajua zaidi sifa alozitaka toka kwa kiongozi ngazi ya Nchimbi.. pengine jamaa mchawi mzuri wa tungule, wee unaweza kucheza uchi usiku wa manane makaburini!
Mkuu wangu ikiwa leo tunaweza kuwaengua wagombea Ukatibu kata kwa vigezo vya ajabu ajabu unategemea nini huko juu. Wa kulaumiwa ni Mkulu pamoja na washauri wake kina Lowassa na Rostam kwani hao ndio walikuwa waajiri.
 
a. Wakibainika na mojawapo ya makosa ya ufeki wa elimu wachuliwe hatua mara moja pasi kusita. Si kila kitu tukimbilie kumlaumu rais, ebu tuwe objective tuache sheria ichukuwe mkondo wake kuangalia nani kafanya kosa na nani alishiriki kwa kuelewa ufeki huo na akaukumbatia,maana athari za kukumbatia makosa haya ni makubwa katika Taifa.

Mkuu Kibunango,

Nakubaliana na hoja zako lakini la kusema Rais asilaumiwe nitatofautiana na wewe kidogo. Mimi nafikiri Rais kabla ya kuteua watu lazima awe na habari kamili juu ya watu hao si kwa utendaji wao wa siku za nyuma tu bali hata elimu yao na kila kitu. Je tuseme UWT hawafanyi kazi yao sawasawa na kupeleka taarifa sahihi kwa Rais kuhusu watu anaotarajia kuwateua? Hata hivyo Rais hawezi kukwepa lawama hapa kwani UWT wako chini ya ofisi yake!!!! Nina imani alijua kwamba hawa watu wana vyeti feki lakini kwa kuwa uwanamtandao ndio kilikuwa kigezo, aliamua kufumba macho.

Tiba
 
Gelange & Tiba

Heshima kwenu. Naheshimu mawazo yenu ya kutokubaliana nami.
Hakika maelezo yangu ya mwishoni sikusema tusimlaumu au tusije kumlaumu rais katika uteuzi wake wa watu waliojipa elimu au viwango vya elimu wasizo nazo. Nilichoonya ni hatua ya " kukimbilia = rush into..... " lawama kabla ya uchunguzi unaostahili kuhusu nani aliyehusika kukumbatia kosa. Tafadhali someni tena nilichosema kama ifuatavyo:

"Si kila kitu tukimbilie kumlaumu rais, ebu tuwe objective tuache sheria ichukuwe mkondo wake kuangalia nani kafanya kosa na nani alishiriki kwa kuelewa ufeki huo na akaukumbatia,maana athari za kukumbatia makosa haya ni makubwa katika Taifa".

Narudia tena kwa maneno mengine.

"YEYOTE ATAKAYEBAINIKA KUSHIRIKI KUELEWA UFEKI/UDANGANYIFU HUO NA AKAUKUMBATIA NAYE YUKO HATIANI"
 
"Si kila kitu tukimbilie kumlaumu rais, ebu tuwe objective tuache sheria ichukuwe mkondo wake kuangalia nani kafanya kosa na nani alishiriki kwa kuelewa ufeki huo na akaukumbatia,maana athari za kukumbatia makosa haya ni makubwa katika Taifa".

Kibs, Rais hawezi kukwepa lawama kwa sababu ana access ya information za kila aina za wale anaowateua au anaotaka kuwateua. Vetting System yetu ina mushkeli.
 
hao mafisadi wa elimu mbona wanafahamika siku nyingi na wameshasemwa sana lakini hakuna hatua iliyochukuliwa. Kuna mwingine moses warioba alifoji phd, akapewa hadi uprofesa na ukuu wa chuo mzumbe kwa cheti cha kughushi, na amekula bata kwa kwenda mbele hadi amestaafu, kudadadeki! Nchi hii bwana! Kama kuna maprofesa wa kughushi katika vyuo vikuu, unategemea nini katika sehemu nyingine?

Nafikiri hii nchi inahitaji jitu kama benito mussolini au adolf hitler.


mi nadhani tu import katiba ya china
 
Sirikali vipi hawa mafisadi wa Elimu mbona hamchukui hatua au mnaonea watoto wa wakulima walioshindwa kusoma kutokana na ukata wakaamua kujiongeza na vyeti feki? HAWA MAFISADI MBONA KIMYA?

Miaka 7 mmekula Ganzi kama hamuoni.
 
Dr. Chegeni bana

" Mtu akikuuliza mimi ni mume wa mama yako utamwambiaje?"

Kumbe majibu ya mwendokasi yalikuepo toka zamani
 
Zama hizi hadhi ya elimu imeshuka, siku hizi imekukuwa kama fashion kusikia mtu ana phd au masters, lkn cha ajabu uwezo na ufanisi ktk Kazi hakuna,.
Sasa tusibweteke kuzingatia sana phd holders au master tumpime mtu kwa uwezo wake wa kudiliver. Vinginevyo wasomi fake wataliangiza taifa letu.
 
Wakati spika akihesabu Ph.D za CCM ndani ya Bunge, akumbuke nasi tuna kumbukumbu na historia ya elimu ya wanasiasa.
 
Back
Top Bottom