Mawaziri Wasukuma

Hivi huwa najiuliza kwa nini mawaziri wasukuma wanakuwa waadilifu kwenye kazi zao wakitumikia serikali ipasavyo na kusahau majimbo yao?
Kwa nini hawatumii nafasi yao kuleta maendeleo majimboni? Utaona kama waziri Ngeleja yupo nishati na madini lakini miaka mitano ishapita kule kwao sengerema hata kusogeza umeme kidogo vijijini ameshindwa? kuna miji inakuwa sana kule mfano kutoka sengerema kuna nyehunge, nzela .katwe , kahunda kwa nini mawaziri wameshindwa kupeleka umeme kule wakati miji imepanuka imekuwa mikubwa kuliko hata sengerema mjini yenyewe?
Nilienda kikazi huko nilishangaa kama mbunge wao ni waziri wa nishati na madini. na ni hivyohivyo kwa hata aliyepita. hawaoni wenzao wa kilimanjaro umeme mpaka vijijini?
kwa kweli wana JF naomba kuwakilisha mada

Kweli kabisa ila mbona mawaziri wa kilimanjaro na kwingineko wameweza kufanya maendeleo huku wakiendelea kumtumia mwajiri wao. mtu akitoka vijijini moshi akaja mjini hashangai umeme wala bomba la maji ngoja atokee huko mamwanza na masengerema

Rafiki mimi ni msukuma lakini naomba kutofautiana na wewe kidogo. Mawaziri wasukuma sio wote ambao ni waadilifu. Mfano Chenge huyu ni mwizi na mtovu wa nidhamu wa hali ya juu na wote tunajua hilo. Maghufuli japo si kwa 100 % ana nafuu na kazi zake zinaonekana na huko kwao kawapelekea barabara nzuri sijui mengine. Ngeleja sioni uadilifu wake hata kidogo zaidi ya kuwepo pale wizarani kuendesha miradi ya bosi wake Rostam Azizi aliyempa Ubunge na huo uwaziri. Maige sina data zake kamili.

halafu kama mnachunguza vizuri sio Ngeleja tu anaharibu hata wenzake waliotangulia! kama Chenge alishiriki kuwapora Wasukuma wenzake ardhi yenye rasilimali ya madini kuwapa wawekezaji kwa mikataba isiyo na manufaa akiwa kama Mwanasheria Mkuu! Pia akiwa kama Waziri wa Miundo Mbinu Chenge huyo huyo alishiriki pia kuiuza TRL kwa kampuni ya kilaghai ya Rites zaidi ya hapo akagonga Wasukuma wenzake na gari sasa hatujui kama alitumwa maana alilipa laki mbili kama faini akaachiliwa! cha ajabu zaidi akashinda Ubunge kwa kishindo! Mbali ya hayo ukiacha ndg zetu Wasukuma hata wenzetu Nshomile hawako nyuma kuna wakina Karamagi pia walileta TICTs na mikataba ya kifisadi ya kusaini hotelini ughaibuni! Ukiachilia mbali ukweli usiofichika kuwa wako kwenye sehemu nyeti sasa katika serikali hii ya Kikwete yaani Ukatibu Mkuu na Ukurugenzi, utendaji wao na elimu zao ni tofauti yaani elimu inawekwa pembeni inabaki kulamba makalio ya mafisadi na kushibisha matumbo!

Angalia type ya Silver Rweyemamu, na Mkandara hapo UD! Pia watu kama mama Mongela amekuwa Mbunge miaka nenda miaka rudi hamna cha maana alichofanya huko Ukerewe na mavyeo yoote aliyopata kuwa nayo! Mpaka najiuliza hawa watu na kuelimika kote, tatizo ni nini haswa? hawana uchungu na nchi hii? walio wasafi toka mitaa hiyo ni Dr Magufuli na Prof. Tibaijuka (ambaye yeye bado tunampima) tu! Jamani mnatuaibisha! wenzetu wa Kilimanjaro hawana shida kama sisi, isitoshe hata wakiiba huwakumbuka wapiga kura wao (mf. Mramba, pia kumbukeni Msuya, Mama Malecela, Dr Mathayo anasaidia sasa huko Upareni)! pia kumbukeni Mzee wa Kiraracha naskia alipelekaga barabara kwao alipokuwa waziri wa mambo ya ndani ukiachia mbali kuishikisha adabu polisi! Mbali na hayo hata watu wa Mbeya wanatuacha mbaali sana! angalia wakina Prof. Mwakyusa na wenzie walivyopigania mpaka uwanja wa Songwe unajengwa! hospitali ya Mbeya pia imeboreshwa na mambo chungu nzima ya maendeleo! Sie wa lake Victoria tumelogwa!

kwa kweli ni kurogwa na mganga kafariki. nimeshangaa sana, anashindwa nini kutumia madaraka aliyonayo kuweka umeme hasa kwenye miji inayokua kwa kasi vile?


Mbona nasikia huko usukumani kuna bonge la jiji linaitwa Gamboshi, limeendelea kama New York! Mbunge wa Gamboshi ni nani? Anastahili kuigwa, lol :clap2::clap2:
 
Tatizo lipo kote kanda ya ziwa,mimi kwa maoni yangu nafikili tatizo liliwekwa tangu enzi ya marehemu baba wa taifa JKN.Mbali ya kuwa kiongozi kwa miaka 24 lakini angalia hali ya Musoma na Butiama.Viongozi wengi tu toka kanda hiyo wamekuwa kwenye mamlaka kwa muda mrefu lakini hakuna la maana.Ukiachilia mbali kuwa Kanda hiyo inachangia kwa kiwango kikubwa pato la Taifa.Pia huenda yawezekana ni sababu ukiangalia idadi kubwa ya hao viongozi waliowa Kilimanjaro, hivyo ilikuwa rahisi kwao kupeleka maendeleo ukweni.
 
Tatizo lipo kote kanda ya ziwa,mimi kwa maoni yangu nafikili tatizo liliwekwa tangu enzi ya marehemu baba wa taifa JKN.Mbali ya kuwa kiongozi kwa miaka 24 lakini angalia hali ya Musoma na Butiama.Viongozi wengi tu toka kanda hiyo wamekuwa kwenye mamlaka kwa muda mrefu lakini hakuna la maana.Ukiachilia mbali kuwa Kanda hiyo inachangia kwa kiwango kikubwa pato la Taifa.Pia huenda yawezekana ni sababu ukiangalia idadi kubwa ya hao viongozi waliowa Kilimanjaro, hivyo ilikuwa rahisi kwao kupeleka maendeleo ukweni.
acha kujitetea wa huko Kilimanjaro wako mind oriented towards maendeleo! si kwa vile wanawake zao ati waliolewa na watu wa lake Victoria! sanasana itakuwa baada ya kusoma watu wa huko wakataka wanawake wanaoendana nao! yaani waliosoma na modern pia! BTW huyo Nyerere mbona historia inasema alikuwa instrumental kurudisha nyuma maendeleo na sera zake za ujamaa!
 
Kwani waziri anateuliwa kwa maendeleo ya eneo lake la asili au kwa taifa zima. Kumlalamikia Ngeleja kuwa hajasambaza umeme Sengerema kwa kuwa ni waziri wa nishati, ni kumfanya anuke ukabila au ukanda.

Bahati mbaya natumia simu ya kiganjani. Ningekugongea thanks.
 
siyo wote, mfano dr pius mwandu alitatua tatizo la maji wilaya ya maswa na jama alikuwa na msimamo kweli..nasikia mradi huo ulikuwa ni wa dodoma akaubadilisha ukawa wa dodoma - maswa kwani kuna sehemu inaitwa dodoma wilaya ya maswa
 
sio Mawaziri bali Wasukuma wote ndio wanao irudisha hii nchi nyuma, Kwa wingi wao na rasirimali zilizopo kwao kama wasukuma wangeamka na kuwa kama Wachaga ama wahaya hii nchi ingekuwa mbali sana kimaendeleo, lakini kwa sasa angalau wanaonyesha kuamka
 
kama wasukuma wangekuwa wanakumbuka kwao usukumani kungekuwa mbali saaana hebu hesabu ni mawaziri wangapi wameshika nyadhifa toka uhuru wengine hata nyumba hawajajenga kwao. Mbali na uwaziri pia wasukuma wenye nyadhifa za juu ka ukurugenzi, ukuu wa idara ila nao bure kabisa
Pukudu, hii ni kweli kuhusu Wasukuma. Na mimi ni Msukuma kosa letu kubwa ni hatuna ukabila wala ubinafsi. Wasukuma wenye Nyadhifa kubwa serikani au kwenye mashirika na taasisi mbali mbali hawana upendeleo wa kujipendelea wao au kupendelea watu wa kabila lao.
Hii ni very fair. Fanya kajiutafiti ma bosi wa makabila fulani, kuanzia ofisini atajaza watu wa kabila lake na maendeleo kupeleka kwake. Huu ni ukabila na ubinafsi vitu ambavyo siyo hulka ya Wasukuma.

Kwa vile haya ni mapungufu kwa Kabila la Wasukuma sio vibaya tukayabainisha na mema machache ya Wasukuma.Kwanza ndilo kabila linaloongoza kwa watu wenye roho nzuri. Ndilo kabila lenye wanaume wanaaongoza kwa kupenda, hatuna wivu, husuda wala kijicho. Tuko very open na very co-oparative tuki work well in team spirit.

Udhaifu wetu ni ma spender wazuri, extra vagant tukipenda good time kupindukia, kinywaji kwa sana na zile starehe za yatokanayo.

Angalizo:There are always exceptional to the general rule, hivyo sio lazima Wasukuma wote ndio wako hivyo.

Msukuma Pasco.
 
Samaki mmoja akioza unamtoa yule aliyeoza na kumtupa na kuacha wengine ambao ni wazima
 
Sidhani kama ni haki kwa kigogo kutumia wadhfa wake ku-polarise mtawanyiko wa huduma za kijamii au miradi ya maendeleo na kuipeleka kwao. This only happens in an anarchy or semi-anarchy societies like our bongoland.

Pathetic.
 
Hivi huwa najiuliza kwa nini mawaziri wasukuma wanakuwa waadilifu kwenye kazi zao wakitumikia serikali ipasavyo na kusahau majimbo yao?
Kwa nini hawatumii nafasi yao kuleta maendeleo majimboni? Utaona kama waziri Ngeleja yupo nishati na madini lakini miaka mitano ishapita kule kwao sengerema hata kusogeza umeme kidogo vijijini ameshindwa? kuna miji inakuwa sana kule mfano kutoka sengerema kuna nyehunge, nzela .katwe , kahunda kwa nini mawaziri wameshindwa kupeleka umeme kule wakati miji imepanuka imekuwa mikubwa kuliko hata sengerema mjini yenyewe?
Nilienda kikazi huko nilishangaa kama mbunge wao ni waziri wa nishati na madini. na ni hivyohivyo kwa hata aliyepita. hawaoni wenzao wa kilimanjaro umeme mpaka vijijini?
kwa kweli wana JF naomba kuwakilisha mada
ngeleja nae mwdilifu... kwa watanzania au mafisadi? LOL

ukabila, ukabila, ukabila.... my foot!!!!
 
Sidhani kama ni haki kwa kigogo kutumia wadhfa wake ku-polarise mtawanyiko wa huduma za kijamii au miradi ya maendeleo na kuipeleka kwao. This only happens in an anarchy or semi-anarchy societies like our bongoland.

Pathetic.

Tena wanafanya kama vile katiba inawaruhusu
 
sio Mawaziri bali Wasukuma wote ndio wanao irudisha hii nchi nyuma, Kwa wingi wao na rasirimali zilizopo kwao kama wasukuma wangeamka na kuwa kama Wachaga ama wahaya hii nchi ingekuwa mbali sana kimaendeleo, lakini kwa sasa angalau wanaonyesha kuamka
Kituko kweli huu ni udhaifu ila udhaifu huu ndio salama ya umoja na utaifa wetu. Tukianza hizi siasa za ukanda na ukabila, amini nakuambia ni Wasukuma watatawala Tanzania milele. Kwa idadi yetu pekee 6 Million plus!, ukijumlisha utajiri wa kanda ya ziwa, si tungeyameza na kuyafunika makabila mengine yote kuanzia Ikulu mpaka mawizarani na kila Idara kila shirika mpaka kila mtaa na kama tukidumisha mila ya wake wengi, wengine hata kupata mke wa kuoa ingekuwa issue!.
 
Hivi huwa najiuliza kwa nini mawaziri wasukuma wanakuwa waadilifu kwenye kazi zao wakitumikia serikali ipasavyo na kusahau majimbo yao?
Kwa nini hawatumii nafasi yao kuleta maendeleo majimboni? Utaona kama waziri Ngeleja yupo nishati na madini lakini miaka mitano ishapita kule kwao sengerema hata kusogeza umeme kidogo vijijini ameshindwa? kuna miji inakuwa sana kule mfano kutoka sengerema kuna nyehunge, nzela .katwe , kahunda kwa nini mawaziri wameshindwa kupeleka umeme kule wakati miji imepanuka imekuwa mikubwa kuliko hata sengerema mjini yenyewe?
Nilienda kikazi huko nilishangaa kama mbunge wao ni waziri wa nishati na madini. na ni hivyohivyo kwa hata aliyepita. hawaoni wenzao wa kilimanjaro umeme mpaka vijijini?
kwa kweli wana JF naomba kuwakilisha mada

hebu wataje hao mawaziri wasukuma waadilifu
 
Mimi nafikiri tatizo ni utashi na mapenzi ya mbunge binafsi kwa wananchi wake. Hao mliowataja ni watu ambao wanaangalia yao binafsi na familia zao ili wawe wafalme katikati ya umaskini uliokithiri wa wananchi wao, halafu wakati wa uchaguzi wanaishia kuwapa fulana na kapelo. Mimi nafikiri suala la maendeleo ya jimboni ni juhudi na dhamira binafsi ya mbunge husika maana tunafahamu majimbo yaliyokuwa hoi kuliko hayo ya usukumani na sasa hivi kwa juhudi za mbunge wao wana ahueni ya hali ya juu. Kufanikisha hilo unahitaji mbunge anayeumwa na umaskini na shida za watu wake. na hiyo maana yake ni kukubali kujinyima hata kile cha kwako kufanikisha hilo, jambo ambalo hawa jamaa hawawezi!
 
Suala siyo kabila. Suala ni mtu binafsi. Huwezi kumlinganisha Dr. Magufuli na Ndg. Ngeleja kwa vipimo vyovyote! Thread haijatulia hii!
 
Hivi huwa najiuliza kwa nini mawaziri wasukuma wanakuwa waadilifu kwenye kazi zao wakitumikia serikali ipasavyo na kusahau majimbo yao?
Kwa nini hawatumii nafasi yao kuleta maendeleo majimboni? Utaona kama waziri Ngeleja yupo nishati na madini lakini miaka mitano ishapita kule kwao sengerema hata kusogeza umeme kidogo vijijini ameshindwa? kuna miji inakuwa sana kule mfano kutoka sengerema kuna nyehunge, nzela .katwe , kahunda kwa nini mawaziri wameshindwa kupeleka umeme kule wakati miji imepanuka imekuwa mikubwa kuliko hata sengerema mjini yenyewe?
Nilienda kikazi huko nilishangaa kama mbunge wao ni waziri wa nishati na madini. na ni hivyohivyo kwa hata aliyepita. hawaoni wenzao wa kilimanjaro umeme mpaka vijijini?
kwa kweli wana JF naomba kuwakilisha mada

Mkuu, naunga mkono hoja yako kwamba ili maendeleo yapatikane nchi nzima kwa usawa basi wabunge wote wawe mawaziri ili wapate fursa ya kupeleka rasilimali za taifa kwenye majimbo yao. Reshuffle ifanyike kila baada ya muda fulani ili kuhakikisha kwamba mbunge husika anashika wizara zote kabla ya kumaliza kipindi chake. Ili jimbo lake lipate huduma zote, yaani maji, barabara, afya, elimu, kilimo, etc.

Hivi kwa nini mikoa ya kusini bado ni maskini zaidi ya mikoa ya kaskazini wakati Mkapa alikuwa rais kwa miaka kumi? Hivi Umeme wa kilimanjaro uliletwa na wabunge mawaziri au zao la kahawa na makanisa? Hivi mashule kilimanjaro yamejengwa na serikali au wamisionari, makanisa, na kipato cha kahawa? Orodha ndefu kidogo, endeleza.

Kwa hiyo, waziri fulani akiingia kwenye wizara akakuta aliyemtangulia alitumia kila kitu kuendeleza jimbo lake na huyu mpya akakosa rasilimali za kupeleka jimboni kwake, basi wananchi wa jimbo lilokosa rasilimali waanzishe chuki na mapigano na wananchi waliopata! Wafipa wafunge safari wakazipige na wasambaa. Njiani wapishane na wapogoro wanakwenda kuzipiga na wanyaturu. Hivyo hivyo nchi nzima.

Naam, kila waziri aendeleze kwao?
 
Back
Top Bottom