Mawaziri walio vuliwa uwaziri

kitero

JF-Expert Member
Feb 21, 2012
563
109
Katika vikao vilivyo pita vya Bunge,tuliona jinsi ripoti ya mkaguzi wa mahesabu wa serekalili ilivyo ibua uozo/ufujaji wa hela ulivyokuwa mkubwa,Vyama vya upinzani walipiga kelele mpaka mwisho, nikimnukuu Mh sugu/Josephu Mbilinyi alisema hiki ni kimbunga kama kisipo vunja nyumba ni lazima kitaezua japo paa,Tuliziona juhudi za upinzani kupinga ule ufisadi na tuliona juhudi za baadi ya wasio wapinzani wakitetea upandewao.Mwisho wa siku tuliona wakivuliwa uwaziri.Leo hii wale wale waliokuwa wakiwatetea wale mawaziri leo hii wanasema tunampongeza raisi kwakuwa msikivu kwa kuwavua uwaziri mawaziri wale kwa upande wao naona wanafanya unafiki kwao,maana kipindi wakiwa mawaziri waliwatetea baada ya kuvuliwa uwaziri wanasema raisi ni msikivu, na leo bungeni tunaona yale yale mbunge anasimama ana sema naunga bajeti mkono asilimia mia moja akianza kuchangia analalamika mwanzo mpaka mwisho naomba urekebishe hapa na pale na mwishoni ana sema naonga mkono hoja.Sasa mimi nashindwa kuelewa nikwamba hapa ni uchama au nini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom