Ntemi Kazwile
JF-Expert Member
- May 14, 2010
- 2,182
- 307
Kufuatia kosa la uhujumu uchumi lililotokea Novemba 26, 2010 la Ndege ya Jeshi la Qatar kuingia nchini na kubeba shehena kubwa ya wanyama hi, ni wakati sasa wa mawaziri kujiuzuru kwa kuifedhehesha serikali yao na nchi inayowalipa mishahara.
Sidhani kuwa enzi za Mwl Nyerere kungetokea mgeni akawa na guts za kufanya hujuma iliyofanyika 26 November 2010! Sidhani kuwa hili lingewezekana enzi za akina Gen Musuguri!
- Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi - Twiga ni mnyama mkubwa ambaye huwezi kumsafilisha ukiwa umemficha na kwa kuwa watendaji walio chini ya waziri Nahodha walishindwa kutekeleza wajibu wao, waziri anayehusika na wizara hii ajiuzuru na asipojiudhuru afukuzwe kazi mara moja.
- Waziri wa Ulinzi na JKT - Ni hatari mno kama mtu anaweza kuingiza ndege bila kufuata utaratibu na bila kujua ni kitu gani ndege hiyo inachukua kutoka kwenye taifa hili na akaondoka bila hata kushitukiwa au kuzuiwa, achilia mbali ikiwa imebeba wanyama hai ambao wamechukuliwa bila vibali sitahiri... kama alishindwa kujiuzuru kwenye skendo ya mabomu itakuwa ajabu kama hii itashindwa kumuondoa!
- Waziri wa Mali Asili na Utalii - Kama wanyama wetu wanatoroshwa kwa madege je ni wangapi wanatoroshwa kwenye magari mipakani????
- IGP Mwema
- Mkuu wa majeshi ya ulinzi
- Mkuu wa Usalama wa Taifa (kama idara hii bado ipo)
- Wakuu wa polisi wa wilaya walimopitishwa wanyama hawa
- Mkuu wa polisi mkoa wa Arusha
- Mkuu wa Mkoa Arusha (yeye ndiye mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa taifa)
- Mkuu wa uwanja wa ndege wa KIA
Sidhani kuwa enzi za Mwl Nyerere kungetokea mgeni akawa na guts za kufanya hujuma iliyofanyika 26 November 2010! Sidhani kuwa hili lingewezekana enzi za akina Gen Musuguri!