Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Usiku wa leo na mchana wa kesho ni siku ambayo CCM inapitisha na itapitisha unyama wa aina yake wa kutumia hila zao walizozitayarisha kwa ajili ya kupora uchaguzi.
Hivyo wananchi wale wote ambao wapo karibu na maeneo ya vituo wawe macho na hali yeyote ngeni itakayojitokeza katika vituo hivyo ,kwani Zanzibar hivi sasa wamegundua mbinu mbalimbali na wamezizima ,yaani WaZanzibar hapa niandikapo onyo hili wapo macho na wanalinda vituo vyote na mpaka pale ambapo masanduku yamefikia basi wanalinda na kurekodi nyendo zote na wapo tayari kwa kumhoji yeyite yule anaeingia au kutoka katika vituo hivyo.
Kwa upande wa Tanganyika ambako imegundulika ni rahisi walinzi kurubunika inatakiwa wawepo zaidi ya walinzi au raia wakawaida wajumuishwe katika ulinzi huo baada ya kuwaachia watu wawili au watatu kukiwakilisha Chama ,watu wachache ni rahisi kurubunia ,inasemekana laki moja au chini ya hapo inaweza kutumika kumrubuni mlinzi wa upinzani na kuwacha CCM wafanye watakavyo kwani hata Kikwete amegusia kwa mbali na kusikika akisema ni taabu kuiba lakini na mawakala nao(wenu)wasikubali kuambiwa nenda ukapate soda huku akitiliwa laki mbili mkononi eti akapate chai na baridi kumbe huwa anaondolewa kijanja ili watu wamalize kazi kwa mwendo na kasi ya ajabu.
Ulinzi wa vituo ulitakiwa uwanze mara moja baada ya karatasi za kupigia kura kuwasili. MpoooH ,basi msije kuachwa kwenye milango mkilinda mchana kumbe kazi imefanywa usiku huu ,leo asilale mtu na ukimaliza kusoma hapa pigia simu kila kiongozi wako unaemjua umjulishe mambo na utekaji unafanyika usiku huu.:israel:
Hivyo wananchi wale wote ambao wapo karibu na maeneo ya vituo wawe macho na hali yeyote ngeni itakayojitokeza katika vituo hivyo ,kwani Zanzibar hivi sasa wamegundua mbinu mbalimbali na wamezizima ,yaani WaZanzibar hapa niandikapo onyo hili wapo macho na wanalinda vituo vyote na mpaka pale ambapo masanduku yamefikia basi wanalinda na kurekodi nyendo zote na wapo tayari kwa kumhoji yeyite yule anaeingia au kutoka katika vituo hivyo.
Kwa upande wa Tanganyika ambako imegundulika ni rahisi walinzi kurubunika inatakiwa wawepo zaidi ya walinzi au raia wakawaida wajumuishwe katika ulinzi huo baada ya kuwaachia watu wawili au watatu kukiwakilisha Chama ,watu wachache ni rahisi kurubunia ,inasemekana laki moja au chini ya hapo inaweza kutumika kumrubuni mlinzi wa upinzani na kuwacha CCM wafanye watakavyo kwani hata Kikwete amegusia kwa mbali na kusikika akisema ni taabu kuiba lakini na mawakala nao(wenu)wasikubali kuambiwa nenda ukapate soda huku akitiliwa laki mbili mkononi eti akapate chai na baridi kumbe huwa anaondolewa kijanja ili watu wamalize kazi kwa mwendo na kasi ya ajabu.
Ulinzi wa vituo ulitakiwa uwanze mara moja baada ya karatasi za kupigia kura kuwasili. MpoooH ,basi msije kuachwa kwenye milango mkilinda mchana kumbe kazi imefanywa usiku huu ,leo asilale mtu na ukimaliza kusoma hapa pigia simu kila kiongozi wako unaemjua umjulishe mambo na utekaji unafanyika usiku huu.:israel: