Jidu
JF-Expert Member
- Mar 9, 2011
- 1,232
- 754
Wife amekuwa akisumbuliwa na tatizo la kuumwa na miguu sehemu ya kukanyagia tokea ajifungue kwa Upasuaji zaidi ya mwaka sasa.miguu huwa inauma hasa wakati wa asubuhi ama akikaa muda mrefu bila kutembea.tumejaribu kumuona surgeon kwa kuangalia tatizo lake labda limetokana na upasuaji aliofanyiwa ,akasema anaupungufu wa calcium lakini tumeendelea na matibabu ya vidonge vyenye madini ya calcium na mchanganyiko wa madini mengine bila mafanikio sasa.naomba ushauri kwani kila kukicha ni malalamiko,wapi naweza kupata Mganga (Doctor) bingwa akani saidia hili tatizo likamuondoka na pia huwa inasababishwa na nini hasa?