Elections 2010 Mauaji yaliyofanywa na CCM na Kikwete Arusha, wamepata nini cha kujivunia?

"Wana JF, kinachonishangaza ni kuwa, sisikii mtu yeyote akimzungumzia Kikwete kuhusika na hili, na hii ni hatari sana katika kutafuta chanzo cha suala hili ambalo limeleta kilio kisicho na sababu kwa watanzania wapenda haki, pamoja na wapenda haki wote duniani. Rai yangu ni kuwa Kikwete awajibike kwa tukio hili maana ndiye mhusika wa jambo hili kimantiki, na kama IGP ndiye aliyehusika, basi amwajibishe haraka iwezekanavyo, vinginevyo awajibike mwenyewe! Asipofanya hivyo, umma utawawajibisha wote.' nimelazimikakuquote para hii kwa maana ya kutaka kukusaidia ewe mtanzania mwenzangu,
Mauaji arusha ni matokeo ya ukorofi wa viongozi wa cdm walipokataa kutii amri ya serikali, kataa kubali, nchi hii ina sheria na raisi na watawala ambao wanaangalia na kutulinda, ukitaka kuelewa kama una dini , utajua wazi ni wajibu wako kumtii raisi naserikali yake, hata dakika yamwisho amri ikitoka huna nguvu ya kupinga , slaa alivyo amrisha fujo kwa kutamka nanukuuu maana nilikuwepo "moja, mbili tatu twndeni tukawatoe mbowe na lema" alikuwa anamaanisha kitu gani ndugu yangu usijichoshe wala usituchoshe, na wala usilaumu raisi wako kwa miaka mitano ijayo na serikali yake,usiporidhika nae tafuta njia mbadala na iwe ya amani maana ya fujo utazibitiwa tu.
.
 
Walikuwa mamevalia kombati za kijeshi huku wakikimbia mchaka-mchaka na kuimba nyimbo za kivita, baadhi mikononi walishikilia mawe na virungu!

Inawezekana kabisa POLISI WALIPOONA KOMBATI NYINGI ZINAELEKEA KITUO CHA POLISI BAADA YA LILE TANGAZO LA MKUTANONI WAKAJUA VITA IMEKAMILIKA.

Inabidi kujiuliza je baada ya mtu kuvaa nguo za kijeshi nini kinafuata? (maana sare za kijeshi hazikamiliki mpaka na silaha ziwemo ndipo zinapendeza!) Je haiwezekani ule kuwa mpango wa kwanza kuteka kituo na kupata baadhi ya silaha na kuonesha kwamba nchi haitawaliki? (kuna mambo mengi yanahitaji majibu... hivi hakuna sare zingine kwa vyama ila hizo za kijeshi-jeshi? Mbona ni CCM, CDM na kile chama cha yule kamarade Dovutwa pekee ambavyo viongozi na wanachama wake wana sare za kijeshi? Hivi MNA AJENDA GANI NA WATANZANIA?

Mnaziogopa Kombati? Naam hili vazi lilibuniwa maksudi ili kuonyesha kuwa CDM ipo kwenye mapambano dhidi ya ufisadi na wizi wa rasilimali za nchi. Si mapambano ya kijeshi yanayotumia silaha, bali mapambano ya hoja na fikra sahihi za kuleta maendeleo tarajiwa ya Taifa. Ni ishara ya ukakamavu na ujasiri wa kusema na kutenda bila kujali vitisho vya mabeberu wa kiafrika kama ulivyojionea pale Arusha. I am dying why I wasn't in Arusha in that day. Ni ushupavu ambao ningeliuweka kwenye kitabu cha kumbukumbu ya maisha yangu kama maisha yangu yasingepotelea kwenye mikono ya hao mafedhuri!

Muziki ndo umeanza, hakuna kulala mpaka kitaeleweka tu, tunajua CCM wanaogopa maovu yao kuanikwa, ndo maana wanang'ang'ania madaraka kwa wizi, fitina na hata kuua. Tuko tayari kwa lolote ili tukiachie kizazi chetu urithi wa nchi nzuri na mahali pazuri pa kuishi.
 
Maneo ya Baba mkubwa wa marehemu Denis wakati wa mazishi ya mwanaye:
Alisema damu ya Denis itaendelea kudai 'ukweli, haki na amani'. Alisema damu ya Denis ikiachwa kupotea bure kesho itakuwa damu yako au yangu. Alisema atamwandikia barua Rais Kikwete ameueze Denis alifanya kosa gani na alihukumiwa na mahakama gani hukumu ya ya kupigwa risasi? Alisema kifo cha Denis kisifanye turudi nyuma katika kupigania 'ukweli, haki na amani'. source John Mnyika.

Inauma sana tusiache damu hii ipotee bure.

Hayo ni maneno mazito aliyoyatamka baba mwenye uchungu wa kupoteza mwanae kipenzi kwa upuuzi wa wajinga wachache. Nafikiri messege imewafikia walengwa na wala haitawaacha walale usingizi kuna siku watasema tu time will tell.
 
Back
Top Bottom