Gavana
JF-Expert Member
- Jul 19, 2008
- 33,233
- 8,779
Mauaji ya Kisiasa Zanzibar
==========================
Mwandishi wetu aliyewahoji waadhiriwa katika mauaji ya kisiasa Zanzibar, anakuletea ripoti yenye majonzi na huzuni tele.
Tunaanzia nyumbani kwa mjane Bi Mwajuma Omari. Ukiingia tu kwenye nyumba yao ya chumba kimoja na sebule utaona picha kubwa ukutani ambayo wanadai ilikuwa ya Bwana Omari ambaye aliuawa kinyama na askari wa CCM.
Akisimulia kuhusu kisa hicho, Bi Mwajuma alisema." Ilikuwa kama saa saba usiku, na tayari tulikuwa tumeshalala kwani kulingana na hofu iliyokuwa imetanda Zanzibar kila mtu aliwahi kujifungia ndani hasa kwa kuogopa askari waliokuwa wametanda kila mahali. Pamoja na kukosa usingizi siku hiyo, tuliamshwa na kishindo kikubwa mlangoni pamoja na sauti za ukali zilizotutaka tufungue mlango."
"Binti zetu watatu walikuwa sebuleni na walikuja haraka kugonga mlango wa chumbani kwetu. Mume wangu alifungua mlango haraka na kutoka kuelekea sebuleni wakati binti zetu waliingia haraka chumbani kwa hofu ya wale waliokuwa wakigonga nje."
"Nilimsikia mume wangu akiwauliza walikuwa wakitaka nini usiku huo, lakini walisisitiza tufungue au waanze kumimina risasi ndani ya nyumba." "Baada ya mlango kufunguliwa, waliingia watu zaidi ya kumi na kumwamuru mume wangu akae chini."Walianza kupekua kila mahali na kubeba kila walichokiona kinawafaa, kuanzia vito vya dhahabu pamoja na pesa kidogo tulizokuwa nazo. Katika kipindi chote hicho binti zetu walikuwa wameingia uvunguni mwa kitanda chetu."
Tulipowaliza walikuwa wakitafuta nini, walijibu kuwa wanawatafuta waliohusika na maandamano, na mume wangu alikuwa mmoja wao. Jitiada za mume wangu kujaribu kuwaeleza kuwa yeye hakuusika na maandamano hazikuweza kufua dafu." "Walipomaliza kupekua mmoja wao aliwaona binti zangu uvunguni na kuwaamuru watoke na waandamane nao. Nilijaribu kuwaomba wawaache binti zangu ,lakini
walisisitiza kwamba lazima waende nao. Mume wangu alionekana kuchukizwa na kitendo cha mmoja wa askari hao kumpapasa mmoja wa binti zetu mbele yetu. Aliwaambia kuwa haiwezekani kuwanyanyasa kijinsia binti zake mbele yake. Aliwaambia heri wamuue kuliko wafanye hayo mbele yake. Alimshika askari aliyekuwa anamvua nguo binti yetu na kuanza kungangana naye. Katika harakati hizo askari alifyatua risasi mbili na mume wangu alianguka chini, huku akivuja damu nyingi sana."
"Haraka haraka waliwatoa binti zangu nje na kuniacha mimi na mume wangu ndani. Hawakwenda mbali, kwani niliwasikia wakisemezana hapo nje. baada ya muda
kidogo niliwasikia binti zangu wakilia kwa sauti na wakiniita mama mama. Sikuweza kutoka kwani nilikuwa nikijaribu kumsaidia mume wangu ambaye kwa wakati wote
huo alikuwa anavuja damu nyingi sana lakini alikuwa hajafa. Nilitumia mashuka kujaribu kuzuia damu lakini wapi. Alikuwa anavuja damu kama maji ya bomba."
Nayakumbuka maneno ya mume wangu kabla hajapoteza fahamu. alisema: " Wako wapi wanangu?" Nikamwambia wale askari wameenda nao. Akasema CCM waliiba kura na sasa wamewaiba binti zangu. hata kama nitakufa leo lakini uchungu ninaousikia waambie waislamu wote duniani ili walipize kisasi hata kama ni baada ya miaka mia moja. Waambie binti zangu kama watarudi wakiwa hai kwamba ninawapenda kama baba yao, na nimejitahidi kuwazuia askari wa CCM wasiwadhuru na yaliyonipata waliyaona. Mungu ambaye hapokei rushwa atamhukumu Mkapa na serikali yake ya mabavu ambayo inawatendea wananchi wasio na hatia madhambi ya jinsi hii."
Alipomaliza maneno hayo, alipoteza fahamu na hakupata tena fahamu mpaka tulipomzika.
"Binti zangu walirudi karibu kunapambazuka, na waliyonielezea ni aibu hata kuyasema hapa. Sasa hivi ninavyozungumza binti zangu wawili wamepimwa na kukutwa na virusi vya ukimwi. Sijui kama wanaweza kuwasamehe askari waliowabaka kwa zamu, na mbaya zaidi sijui kama wanaweza kuisamehe serikali ya CCM inayoongozwa na Mkapa." Alimaliza mama huyo aliyekuwa anatoa machozi wakati wote wa mahojiano.
-----
Mwandishi wa habari BBC
==========================
Mwandishi wetu aliyewahoji waadhiriwa katika mauaji ya kisiasa Zanzibar, anakuletea ripoti yenye majonzi na huzuni tele.
Tunaanzia nyumbani kwa mjane Bi Mwajuma Omari. Ukiingia tu kwenye nyumba yao ya chumba kimoja na sebule utaona picha kubwa ukutani ambayo wanadai ilikuwa ya Bwana Omari ambaye aliuawa kinyama na askari wa CCM.
Akisimulia kuhusu kisa hicho, Bi Mwajuma alisema." Ilikuwa kama saa saba usiku, na tayari tulikuwa tumeshalala kwani kulingana na hofu iliyokuwa imetanda Zanzibar kila mtu aliwahi kujifungia ndani hasa kwa kuogopa askari waliokuwa wametanda kila mahali. Pamoja na kukosa usingizi siku hiyo, tuliamshwa na kishindo kikubwa mlangoni pamoja na sauti za ukali zilizotutaka tufungue mlango."
"Binti zetu watatu walikuwa sebuleni na walikuja haraka kugonga mlango wa chumbani kwetu. Mume wangu alifungua mlango haraka na kutoka kuelekea sebuleni wakati binti zetu waliingia haraka chumbani kwa hofu ya wale waliokuwa wakigonga nje."
"Nilimsikia mume wangu akiwauliza walikuwa wakitaka nini usiku huo, lakini walisisitiza tufungue au waanze kumimina risasi ndani ya nyumba." "Baada ya mlango kufunguliwa, waliingia watu zaidi ya kumi na kumwamuru mume wangu akae chini."Walianza kupekua kila mahali na kubeba kila walichokiona kinawafaa, kuanzia vito vya dhahabu pamoja na pesa kidogo tulizokuwa nazo. Katika kipindi chote hicho binti zetu walikuwa wameingia uvunguni mwa kitanda chetu."
Tulipowaliza walikuwa wakitafuta nini, walijibu kuwa wanawatafuta waliohusika na maandamano, na mume wangu alikuwa mmoja wao. Jitiada za mume wangu kujaribu kuwaeleza kuwa yeye hakuusika na maandamano hazikuweza kufua dafu." "Walipomaliza kupekua mmoja wao aliwaona binti zangu uvunguni na kuwaamuru watoke na waandamane nao. Nilijaribu kuwaomba wawaache binti zangu ,lakini
walisisitiza kwamba lazima waende nao. Mume wangu alionekana kuchukizwa na kitendo cha mmoja wa askari hao kumpapasa mmoja wa binti zetu mbele yetu. Aliwaambia kuwa haiwezekani kuwanyanyasa kijinsia binti zake mbele yake. Aliwaambia heri wamuue kuliko wafanye hayo mbele yake. Alimshika askari aliyekuwa anamvua nguo binti yetu na kuanza kungangana naye. Katika harakati hizo askari alifyatua risasi mbili na mume wangu alianguka chini, huku akivuja damu nyingi sana."
"Haraka haraka waliwatoa binti zangu nje na kuniacha mimi na mume wangu ndani. Hawakwenda mbali, kwani niliwasikia wakisemezana hapo nje. baada ya muda
kidogo niliwasikia binti zangu wakilia kwa sauti na wakiniita mama mama. Sikuweza kutoka kwani nilikuwa nikijaribu kumsaidia mume wangu ambaye kwa wakati wote
huo alikuwa anavuja damu nyingi sana lakini alikuwa hajafa. Nilitumia mashuka kujaribu kuzuia damu lakini wapi. Alikuwa anavuja damu kama maji ya bomba."
Nayakumbuka maneno ya mume wangu kabla hajapoteza fahamu. alisema: " Wako wapi wanangu?" Nikamwambia wale askari wameenda nao. Akasema CCM waliiba kura na sasa wamewaiba binti zangu. hata kama nitakufa leo lakini uchungu ninaousikia waambie waislamu wote duniani ili walipize kisasi hata kama ni baada ya miaka mia moja. Waambie binti zangu kama watarudi wakiwa hai kwamba ninawapenda kama baba yao, na nimejitahidi kuwazuia askari wa CCM wasiwadhuru na yaliyonipata waliyaona. Mungu ambaye hapokei rushwa atamhukumu Mkapa na serikali yake ya mabavu ambayo inawatendea wananchi wasio na hatia madhambi ya jinsi hii."
Alipomaliza maneno hayo, alipoteza fahamu na hakupata tena fahamu mpaka tulipomzika.
"Binti zangu walirudi karibu kunapambazuka, na waliyonielezea ni aibu hata kuyasema hapa. Sasa hivi ninavyozungumza binti zangu wawili wamepimwa na kukutwa na virusi vya ukimwi. Sijui kama wanaweza kuwasamehe askari waliowabaka kwa zamu, na mbaya zaidi sijui kama wanaweza kuisamehe serikali ya CCM inayoongozwa na Mkapa." Alimaliza mama huyo aliyekuwa anatoa machozi wakati wote wa mahojiano.
-----
Mwandishi wa habari BBC