Matunda ya Lema yaanza kuonekana World Bank wahoji matumizi makubwa Arusha

EasyFit

JF-Expert Member
Jul 4, 2011
1,269
1,082
SAKATAla ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha katika Halmashauri ya Jiji la Arusha, limeingia katika hatua nyingine baada ya Benki ya Dunia nchini, kutaka maelezo ya kina vinginevyo itasitisha kuendelea kutoa misaada katika Jiji hilo baada ya kubaini fedha zaidi ya Sh milioni 100 kutumika kukarabati ofisi nne za Jiji hilo.

Vyanzo vya habari kutoka Halmashauri ya Jiji la Arusha vilisema kuwa fedha hizo ambazo katika mradi wa benki hiyo ujulikanao kwa jina la Tanzania Strategic Cities Programmes (TSCP) wa Jiji hilo, zimetumika kukarabati ofisi za Mkurugenzi, Biashara, Mchumi na Mhandisi.

Habari za uhakika zilieleza kuwa kutumika "hovyo hovyo" kwa mamilioni hayo ya fedha, hakukuridhisha uongozi wa Benki ya Dunia kwani ulieleza kuwa ni matumizi mabaya ya fedha hivyo walitaka maelezo ya kina kwa maandishi.

Uongozi huo wa benki ulimwandikia pia Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo juu yahali hiyo na uamuzi ambao ofisi hiyo inataka kuchukua, ndipo mkuu huyo alipoingilia kati nakuiahidi Benki ya Dunia kuwa itafuatilia na kama kuna ulaji, hatua kali zitachukuliwa.

Habari zilieleza kuwa baada ya ahadi hiyo, ndipo benki hiyo iliamua kuacha kwanza hatua yakehiyo mpaka watakapopata taarifa rasmi ya hatua za kuchukuliwa wahusika wa ubadhilifu wa fedha hizo.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Arusha, Estomih Chang'a alipoulizwa juu ya kiasi hicho kutumika kukarabati ofisi nne tu, alisema taratibu zote za kutangaza zabuni zilitumika hivyo kampuni iliyofanya kazi hiyo ilipewa kazi hiyo kwa uamuzi wa Bodi ya Ununuzi na Ugavi ya Jiji hilo.

Chang'a alisema kazi ya kukarabati ofisi ilitangazwa zabuni, ikafanyiwa tathmini, ikapita zabunina kuzingatiwa Sheria ya Manunuzi ya Umma kwa asilimia 100 na kama kuna lingine liko tofauti, aulizwe Mhandisi wa Jiji.

Alipobanwa ili atoe ufafanuzi iweje yeye kama kiongozi wa Jiji la Arusha na Mdhibiti Mkuu wa matumizi ya fedha, akubali kiasi hicho kikubwa cha fedha kutumika kukarabati ofisi mbili, alisisitiza aulizwe Mhandisi huyo kwa madai ndiye aliyefanya tathmini ya awali kabla ya utangazaji zabuni.

Mhandisi wa Jiji, Afwilile Lamsy alipoulizwa kwa njia ya simu, alisema na kupingana na Mkurugenzi wake kwa kueleza kuwa ofisi zilizofanyiwa ukarabati ni zaidi ya 10, hatua iliyoonekana kupingana na baadhi ya nyaraka zinazoonesha kuwa ukarabati huo ulifanywa kwaofisi nne tu.

Lamsy alisema akiwa ni mtendaji na msimamizi mkuu wa shughuli zote za ujenzi, anachojuani kuwa ofisi zilizofanyiwa ukarabati ni zaidi ya 10, lakini alishindwa kufafanua kama bajeti yake iliruhusu kampuni kutenda kwa zaidi ya Sh milioni 100 kukarabati ofisi hizo.

Mkuu wa Mkoa, Mulongo alipoulizwa kama anajua chochote juu ya utata wa matumizi ya fedhaza mradi huo, alikiri kuufahamu na kueleza kuwa kutumika kwa fedha hizo ni moja ya kazi za mradi huo.

Ila alienda mbali zaidi na kueleza kwamba tatizo ni kiasi hicho cha fedha na ndio maana Tume imeundwa kuchunguza.

"Kukarabati ofisi ni moja ya package (sehemu) ya mradi huo, lakini kuna tatizo katika utoaji wazabuni kwa kampuni kwa fedha hizo nyingi na ndio maana Tume ya Bodi ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) inachunguza kubaini ukweli," alisema Mkuu wa Mkoa.

::HabariLeo::
 
Una-aleji na Lema wewe.....?

sina allergy na LEma and he know it, tatizo ninachopenda ni kuwa realistic na facts tunazoweka ili kuondoa any kind of hey-way thinking kwani Arusha ni zaidi ya jimbo kwa nchi yetu, it is a strategic political centre by any standard na mara nyingi ni vyema kuwa na all cards right ili mambo yakae vizuri

efforts zote za matumizi, mapitio ya matumizi na hata any interventions hupitia mfumo fulani na ndio maana nikahoji kama ni mtu mmoja as we try to portray,,,,

vipi wewe unayo allergy na mtu anayetaka kujua zaidi hata pale usipotaka ahoji??
 
tuna uhakika ni influence ya lema pekee?
Uwepo wa Lema unaweza kuwa factor mojawapo ya madudu kuanza kuanikwa wazi, Arusha kuna mauchafu mengi sana ndio maana wanafanya juu chini waendelee kuhodhi baraza la madiwani ili kuficha aibu kama hii isitokee. Big up Lema na Madiwani hasa wa CDM.
 
Nawapongeza WB kwa kufuatilia lakini ninawasiwasi na maelezo ya mkuu wa mkoa. Hivi hizi tume ndio zimekuwa organs za kuchunguza utendaji wa serikali. Hakuna watu wenye wajibu huo hadi kuendelea kupukutisha hela zetu "za dhamani" kwa kuunda vitume kwenye kila jambo! Something must be done!
 
SAKATAla ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha katika Halmashauri ya Jiji la Arusha, limeingia katika hatua nyingine baada ya Benki ya Dunia nchini, kutaka maelezo ya kina vinginevyo itasitisha kuendelea kutoa misaada katika Jiji hilo baada ya kubaini fedha zaidi ya Sh milioni 100 kutumika kukarabati ofisi nne za Jiji hilo.

Vyanzo vya habari kutoka Halmashauri ya Jiji la Arusha vilisema kuwa fedha hizo ambazo katika mradi wa benki hiyo ujulikanao kwa jina la Tanzania Strategic Cities Programmes (TSCP) wa Jiji hilo, zimetumika kukarabati ofisi za Mkurugenzi, Biashara, Mchumi na Mhandisi.

Habari za uhakika zilieleza kuwa kutumika “hovyo hovyo” kwa mamilioni hayo ya fedha, hakukuridhisha uongozi wa Benki ya Dunia kwani ulieleza kuwa ni matumizi mabaya ya fedha hivyo walitaka maelezo ya kina kwa maandishi.

Uongozi huo wa benki ulimwandikia pia Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo juu yahali hiyo na uamuzi ambao ofisi hiyo inataka kuchukua, ndipo mkuu huyo alipoingilia kati nakuiahidi Benki ya Dunia kuwa itafuatilia na kama kuna ulaji, hatua kali zitachukuliwa.

Habari zilieleza kuwa baada ya ahadi hiyo, ndipo benki hiyo iliamua kuacha kwanza hatua yakehiyo mpaka watakapopata taarifa rasmi ya hatua za kuchukuliwa wahusika wa ubadhilifu wa fedha hizo.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Arusha, Estomih Chang’a alipoulizwa juu ya kiasi hicho kutumika kukarabati ofisi nne tu, alisema taratibu zote za kutangaza zabuni zilitumika hivyo kampuni iliyofanya kazi hiyo ilipewa kazi hiyo kwa uamuzi wa Bodi ya Ununuzi na Ugavi ya Jiji hilo.

Chang’a alisema kazi ya kukarabati ofisi ilitangazwa zabuni, ikafanyiwa tathmini, ikapita zabunina kuzingatiwa Sheria ya Manunuzi ya Umma kwa asilimia 100 na kama kuna lingine liko tofauti, aulizwe Mhandisi wa Jiji.

Alipobanwa ili atoe ufafanuzi iweje yeye kama kiongozi wa Jiji la Arusha na Mdhibiti Mkuu wa matumizi ya fedha, akubali kiasi hicho kikubwa cha fedha kutumika kukarabati ofisi mbili, alisisitiza aulizwe Mhandisi huyo kwa madai ndiye aliyefanya tathmini ya awali kabla ya utangazaji zabuni.

Mhandisi wa Jiji, Afwilile Lamsy alipoulizwa kwa njia ya simu, alisema na kupingana na Mkurugenzi wake kwa kueleza kuwa ofisi zilizofanyiwa ukarabati ni zaidi ya 10, hatua iliyoonekana kupingana na baadhi ya nyaraka zinazoonesha kuwa ukarabati huo ulifanywa kwaofisi nne tu.

Lamsy alisema akiwa ni mtendaji na msimamizi mkuu wa shughuli zote za ujenzi, anachojuani kuwa ofisi zilizofanyiwa ukarabati ni zaidi ya 10, lakini alishindwa kufafanua kama bajeti yake iliruhusu kampuni kutenda kwa zaidi ya Sh milioni 100 kukarabati ofisi hizo.

Mkuu wa Mkoa, Mulongo alipoulizwa kama anajua chochote juu ya utata wa matumizi ya fedhaza mradi huo, alikiri kuufahamu na kueleza kuwa kutumika kwa fedha hizo ni moja ya kazi za mradi huo.

Ila alienda mbali zaidi na kueleza kwamba tatizo ni kiasi hicho cha fedha na ndio maana Tume imeundwa kuchunguza.

“Kukarabati ofisi ni moja ya package (sehemu) ya mradi huo, lakini kuna tatizo katika utoaji wazabuni kwa kampuni kwa fedha hizo nyingi na ndio maana Tume ya Bodi ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) inachunguza kubaini ukweli,” alisema Mkuu wa Mkoa.

::HabariLeo::
Mhs Lema komaa nao hao, kuna miradi mingi tuu hewa ndio maana wanangangania Umeya kuficha maovu yao!!!!!!! Kuna maovu ya sasa pia maovu ya nyuma, yote hayo inahitaji yafichuliwe tuu!!!!!!!! Zama na TANAPA kwenye fedha nyingi na matumizi ya ajabu ajabu, tujue hiyo budget ya TANAPA pamoja na mbuga zetu, mapato, matumizi na zinamnufaisha vipi Mtanzania na mwana Arusha kwenye mbuga hizo???????????

 
sina allergy na LEma and he know it, tatizo ninachopenda ni kuwa realistic na facts tunazoweka ili kuondoa any kind of hey-way thinking kwani Arusha ni zaidi ya jimbo kwa nchi yetu, it is a strategic political centre by any standard na mara nyingi ni vyema kuwa na all cards right ili mambo yakae vizuri

efforts zote za matumizi, mapitio ya matumizi na hata any interventions hupitia mfumo fulani na ndio maana nikahoji kama ni mtu mmoja as we try to portray,,,,

vipi wewe unayo allergy na mtu anayetaka kujua zaidi hata pale usipotaka ahoji??
Unafikiri ni kwa nini wanangangania Umeya wa mji wa Arusha, si kwamba wanazo siri nyingi hawataki zifichuke?????????
Lema ni catalyst wenye uchungu na nchi hii wanapata pa kusemea!!!!!!!!!!

 
Kuna mchezo unataka kufanywa, mkurugenzi anasema wametumia mil. 100 kukarabati ofisi 4 wakati mhandisi anaema 10, nafikiri walikuwa anataka kuomba pesa zingine kwa ofisi 6 wanazoficha.
 
Nawapongeza WB kwa kufuatilia lakini ninawasiwasi na maelezo ya mkuu wa mkoa. Hivi hizi tume ndio zimekuwa organs za kuchunguza utendaji wa serikali. Hakuna watu wenye wajibu huo hadi kuendelea kupukutisha hela zetu "za dhamani" kwa kuunda vitume kwenye kila jambo! Something must be done!

Hizo tume ni ishara tu kwamba serikali ina very weak internal control na inahitaji msaada wa tume, unfortunately tume nyingi huandaliwa na walewale wanaotakiwa kuchunguzwa
 
Unafikiri ni kwa nini wanangangania Umeya wa mji wa Arusha, si kwamba wanazo siri nyingi hawataki zifichuke?????????
Lema ni catalyst wenye uchungu na nchi hii wanapata pa kusemea!!!!!!!!!!

Thanks alot mtumishi, uweiweka vyema.... tatizo hapa ni namna tunavyoripoti kishabiki kiasi cha kufanya as if one person is working alone

At least umenielewesha kwamba Lema ni catalyst wa hayo mapambano which means he is not alone, na nasema hivi kwasbabu kazi ya makamanda wengine walio arusha ni kubwa sana na katu tusiizamishe chini ya blanket/carpet moja.... pia kuna watendaji ndani arusha ingawa ni wa serikali lakini nao wamchoshwa na unyang'au na sasa wanasaidia kuibua madudu

one...
 
Mhs Lema komaa nao hao, kuna miradi mingi tuu hewa ndio maana wanangangania Umeya kuficha maovu yao!!!!!!! Kuna maovu ya sasa pia maovu ya nyuma, yote hayo inahitaji yafichuliwe tuu!!!!!!!! Zama na TANAPA kwenye fedha nyingi na matumizi ya ajabu ajabu, tujue hiyo budget ya TANAPA pamoja na mbuga zetu, mapato, matumizi na zinamnufaisha vipi Mtanzania na mwana Arusha kwenye mbuga hizo???????????

Duh! Hao TANAPA wameanza kula ela zamani mkuu, yakifichuliwa yote mtashangazwa na itakuwa vigumu kuamini, yani i mean kiwango cha pesa...
 
hapa Lemma ameingiaje mbona story nzima hamna panapo mtaja Lemma au Lemma alienda WB kuwaambia fedha hazifanyi kazi ili wazuie msaada huo mbeleni
 
Sasa hapa Lema anaingiaje? ..... Mbona mnakuwa na ushabiki wa kipuuzi?

Ila tungejua mkandarasi ni nani, maana yule meya naye ni mkandarasi.

Pia nao WB waache upumbavu, 100m kwa ofisi nne ni sawa na 25m kwa ofisi moja hivi 25m inatosha hata stationeries ukizingatia hela zetu za madafu?
 
Sasa hapa Lema anaingiaje? ..... Mbona mnakuwa na ushabiki wa kipuuzi?

Ila tungejua mkandarasi ni nani, maana yule meya naye ni mkandarasi.

Pia nao WB waache upumbavu, 100m kwa ofisi nne ni sawa na 25m kwa ofisi moja hivi 25m inatosha hata stationeries ukizingatia hela zetu za madafu?
Usiwaite wapumbavu WB wanafuatilia pesa zao, Lema anaingia hapa kama diwani na mbunge wa jimbo la Arusha mjini.
 
hapa Lemma ameingiaje mbona story nzima hamna panapo mtaja Lemma au Lemma alienda WB kuwaambia fedha hazifanyi kazi ili wazuie msaada huo mbeleni
Hujui Lema ni mmoja wa madiwani na mbunge wa jimbo la Arusha mjini.
 
Tulikionya CCM juu ya matumizi mabaya ya kodi zetu pamoja na hela za wahisani na wala hawakutaka kusikiliza kitu. Mwakani ni kilio kitupu!!
 
Back
Top Bottom