Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,316
- 33,125
MSAMIATI
Kinywaji cha viungo:
Hiki ni kinywaji chochote ambacho kimetengenezwa kwa kuwekwa
viungo. Kinywaji hiki kinaweza kuwa cha moto au cha baridi. Kinywaji
cha baridi kinapotengenezwa, yatumike maji yaliyochemshwa.
Chai:
Hiki ni kinywaji ambacho hutengenezwa kwa kutumia maji ya moto na
majani ya chai. Wakati mwingine sukari na maziwa huongezwa.
Mara nyingine watu wanapotengeneza vinywaji vya viungo huviita
"chai" hata kama havina majani ya chai. Ukweli ni kwamba chai ni yale
majani ya chai. Katika kijitabu hiki vinywaji vya viungo havikuitwa chai.
BAADHI YA VIUNGO, MATUMIZI NA FAIDA
ZAKE
Kitunguu saumu (Garlic)
Kitunguu saumu ni kiungo ambacho kimekuwa maarufu kwa matumizi
mbalimbali. Vipo vitunguu saumu vya rangi nyeupe ambavyo mara
nyingi huwa na tumba kubwa ambazo ni chache. Vingine ni vile vyenye
rangi ya zambarau au pinki ambavyo huwa na tumba ndogo
na nyingi. Vitunguu hivi vina ubora sawa.
Kitunguu saumu hufaa katika matatizo mengi
kama kusaidia kuzuia maambukizi yatokanayo
katika utumbo, mapafu na sehemu za ukeni.
Vilevile husaidia katika uyeyushwaji wa chakula,
kuzuia kuharisha na pia hupunguza fangasi za kinywani,
maambukizi katika koo na hata mkanda wa jeshi.
Kitunguu saumu kinaweza kutumika katika mapishi ya chakula, chai au
kinywaji chochote cha baridi au cha moto. Mtu anapotumia vitunguu
saumu atumie kwa kiasi. Inashauriwa kutumia vitumba visivyozidi sita
kwa siku hasa kama vitatumika vibichi .
Tangawizi (Ginger)
Tangawizi ni kiungo ambacho kinatokana na mizizi ya mmea wa
tangawizi. Kiungo hiki huweza kutumika kikiwa kibichi au kikiwa
kimekaushwa na kutengenezwa unga. Ta n g a w i z i
inaweza kutumika katika vinywaji vilivyochemshwa.
Pia huweza kuongezwa kwenye vinywaji vingine au
kwenye chakula.
Tangawizi husaidia kuongeza hamu ya kula,
kupunguza kichefuchefu, kutapika, kuharisha,
maumivu ya tumbo na gesi tumboni. Pia husaidia
uyeyushwaji wa chakula tumboni. Vilevile husaidia wakati wa
matatizo ya mafua au flu.
Iliki (Cardamom)
Iliki ni mbegu zinazotokana na mmea wa iliki ambazo
hutumika kama kiungo. Mbegu hizi huweza kusagwa
au kutwangwa na kuongezwa kwenye chakula au
katika vinywaji.
Iliki ni nzuri katika kusaidia kupunguza maumivu,
kichefuchefu au kutapika. Pia husaidia uyeyushwaji
wa chakula na huongeza hamu ya kula.
Mdalasini (Cinnamon)
Mdalasini ni kiungo kinachotokana na magome ya
mmea wa mdalasini. Kiungo hiki huweza kusagwa
au kutumika bila kusagwa. Vilevile mdalasini
h u weza kuongezwa kwe n ye chakula au katika
vinywaji vilivyochemshwa au baridi.
Mdalasini huweza kusaidia kupunguza matatizo kama mafua au flu,
vidonda vya kinywani na hata fangasi za ngozi. Vilevile kiungo hiki
huongeza hamu ya kula, pia husaidia kupunguza baadhi ya matatizo
katika mfumo wa chakula kama kichefuchefu, kutapika au kuharisha.
Kinywaji kilichochemshwa chenye mchanganyiko wa mdalasini na
tangawizi kinaweza kutuliza kikohozi.
Giligilani (Coriander)
Giligilani ni aina ya kiungo ambacho
majani na mbegu zake huwez a
kutumika kama kiungo katika mapishi
ya vyakula mbalimbali kama nyama,
supu au mchuzi.
Kiungo hiki husaidia kuongeza hamu ya kula na
kupunguza gesi tumboni. Pia husaidia kuzuia maambukizi
ya bakteria na fangasi.
Kotimiri (Parsley)
Kotimiri ni aina ya mmea ambao majani yake na mbegu
zake huweza kutumika kama kiungo katika vyakula.
Majani ya kotimiri husaidia kupunguza msokoto wa
tumbo ambao mara nyingi hausababishi kuharisha.
Vilevile kiungo hiki huchochea vimeng' e n yo
tumboni na hivyo kuongeza hali ya kuhisi njaa.
Mbegu za kotimiri huweza kusaidia kuondoa maji ya
ziada katika mwili. Kiungo hiki huweza kuongezwa
katika chakula wakati wa kupika au wakati wa kula.
Karafuu (Cloves)
Karafuu hutokana na mmea wa mkarafuu. Kiungo
hiki huweza kutumika peke yake au kwa
kuchanganya na viungo vingine. Kiungo hiki
husaidia kuleta hamu ya kula na kubore sha
uyeyushwaji wa chakula tumboni. Vilevile karafuu husaidia kupunguza
kichefuchefu, kutapika na kuharisha.
Ni nzuri ikitumiwa katika supu, mchuzi, juisi ya matunda yenye
uvuguvugu au vinywaji vingine vilivyochemshwa.
Kinywaji cha viungo:
Hiki ni kinywaji chochote ambacho kimetengenezwa kwa kuwekwa
viungo. Kinywaji hiki kinaweza kuwa cha moto au cha baridi. Kinywaji
cha baridi kinapotengenezwa, yatumike maji yaliyochemshwa.
Chai:
Hiki ni kinywaji ambacho hutengenezwa kwa kutumia maji ya moto na
majani ya chai. Wakati mwingine sukari na maziwa huongezwa.
Mara nyingine watu wanapotengeneza vinywaji vya viungo huviita
"chai" hata kama havina majani ya chai. Ukweli ni kwamba chai ni yale
majani ya chai. Katika kijitabu hiki vinywaji vya viungo havikuitwa chai.
BAADHI YA VIUNGO, MATUMIZI NA FAIDA
ZAKE
Kitunguu saumu (Garlic)
Kitunguu saumu ni kiungo ambacho kimekuwa maarufu kwa matumizi
mbalimbali. Vipo vitunguu saumu vya rangi nyeupe ambavyo mara
nyingi huwa na tumba kubwa ambazo ni chache. Vingine ni vile vyenye
rangi ya zambarau au pinki ambavyo huwa na tumba ndogo
na nyingi. Vitunguu hivi vina ubora sawa.
Kitunguu saumu hufaa katika matatizo mengi
kama kusaidia kuzuia maambukizi yatokanayo
katika utumbo, mapafu na sehemu za ukeni.
Vilevile husaidia katika uyeyushwaji wa chakula,
kuzuia kuharisha na pia hupunguza fangasi za kinywani,
maambukizi katika koo na hata mkanda wa jeshi.
Kitunguu saumu kinaweza kutumika katika mapishi ya chakula, chai au
kinywaji chochote cha baridi au cha moto. Mtu anapotumia vitunguu
saumu atumie kwa kiasi. Inashauriwa kutumia vitumba visivyozidi sita
kwa siku hasa kama vitatumika vibichi .
Tangawizi (Ginger)
Tangawizi ni kiungo ambacho kinatokana na mizizi ya mmea wa
tangawizi. Kiungo hiki huweza kutumika kikiwa kibichi au kikiwa
kimekaushwa na kutengenezwa unga. Ta n g a w i z i
inaweza kutumika katika vinywaji vilivyochemshwa.
Pia huweza kuongezwa kwenye vinywaji vingine au
kwenye chakula.
Tangawizi husaidia kuongeza hamu ya kula,
kupunguza kichefuchefu, kutapika, kuharisha,
maumivu ya tumbo na gesi tumboni. Pia husaidia
uyeyushwaji wa chakula tumboni. Vilevile husaidia wakati wa
matatizo ya mafua au flu.
Iliki (Cardamom)
Iliki ni mbegu zinazotokana na mmea wa iliki ambazo
hutumika kama kiungo. Mbegu hizi huweza kusagwa
au kutwangwa na kuongezwa kwenye chakula au
katika vinywaji.
Iliki ni nzuri katika kusaidia kupunguza maumivu,
kichefuchefu au kutapika. Pia husaidia uyeyushwaji
wa chakula na huongeza hamu ya kula.
Mdalasini (Cinnamon)
Mdalasini ni kiungo kinachotokana na magome ya
mmea wa mdalasini. Kiungo hiki huweza kusagwa
au kutumika bila kusagwa. Vilevile mdalasini
h u weza kuongezwa kwe n ye chakula au katika
vinywaji vilivyochemshwa au baridi.
Mdalasini huweza kusaidia kupunguza matatizo kama mafua au flu,
vidonda vya kinywani na hata fangasi za ngozi. Vilevile kiungo hiki
huongeza hamu ya kula, pia husaidia kupunguza baadhi ya matatizo
katika mfumo wa chakula kama kichefuchefu, kutapika au kuharisha.
Kinywaji kilichochemshwa chenye mchanganyiko wa mdalasini na
tangawizi kinaweza kutuliza kikohozi.
Giligilani (Coriander)
Giligilani ni aina ya kiungo ambacho
majani na mbegu zake huwez a
kutumika kama kiungo katika mapishi
ya vyakula mbalimbali kama nyama,
supu au mchuzi.
Kiungo hiki husaidia kuongeza hamu ya kula na
kupunguza gesi tumboni. Pia husaidia kuzuia maambukizi
ya bakteria na fangasi.
Kotimiri (Parsley)
Kotimiri ni aina ya mmea ambao majani yake na mbegu
zake huweza kutumika kama kiungo katika vyakula.
Majani ya kotimiri husaidia kupunguza msokoto wa
tumbo ambao mara nyingi hausababishi kuharisha.
Vilevile kiungo hiki huchochea vimeng' e n yo
tumboni na hivyo kuongeza hali ya kuhisi njaa.
Mbegu za kotimiri huweza kusaidia kuondoa maji ya
ziada katika mwili. Kiungo hiki huweza kuongezwa
katika chakula wakati wa kupika au wakati wa kula.
Karafuu (Cloves)
Karafuu hutokana na mmea wa mkarafuu. Kiungo
hiki huweza kutumika peke yake au kwa
kuchanganya na viungo vingine. Kiungo hiki
husaidia kuleta hamu ya kula na kubore sha
uyeyushwaji wa chakula tumboni. Vilevile karafuu husaidia kupunguza
kichefuchefu, kutapika na kuharisha.
Ni nzuri ikitumiwa katika supu, mchuzi, juisi ya matunda yenye
uvuguvugu au vinywaji vingine vilivyochemshwa.