Matumizi ya udi na faida zake

Makini Buz

Member
Jan 13, 2015
21
9
Wakuu habari.

Nimeona mara nyingi watu huchoma udi maduka majumbani mwao, najiuliza ni kwa sababu zipi, zina faida gani na kuna aina ngapi za udi maana harufu hutofautiana.

Asanteni.
 
yes kila ijumaa lazima nijifukize nasemea wa kujifukiza ule unanukiaaa na al-ud kidogo bas siku yangu huwa poa dini yangu inasema miongon mwa mambo matano ya kufanya siku ya ijumaa moja wapo ni hili ujipake manukato ila yasikere kuna aina nyingi za udi kuna huu niliosema na ule wa kijiti ule kwa kweli una matumizi mengi sana.

Kuna udi umekua diluted ni maji wamimina kiasi katika ndoo ukaogea kuna wa chenga chenga na wa magome ya mti inategemeana na harufu hizi ndo nijuazo mimi na hua nachoma huu udi wa kujifukiza napenda kunukia hii ni sababu niyonayo mm na sina nyingine hizo za vijiti zinahusiana na maombi flani mtu huchoma ikiambatana na nia labda mshana jr anajua zaidi
 
Huku uswazi magetoni UDI unachomwa masaa 24 siku 7 za wiki, sio mambo ya imani??hapana ni kupotezea harufu ya MAJANI.

Ukikatiza mitaa ya wahaya,mwanayamala,uwanja Wa fisi katika biashara zisizo na kodi zile pia wanapenda kichoma udi ili angalau ukiingia usisikie harufu ya bao la njemba iliyotoka kugegeda kabla yako wewe.
 
Wengi wametoa tafsiri zao kuhusu udi hasa #Madame ameelezea kwa ufasahau japo kidogo.
Udi upo wa aina nyingi na hutumika kwa matumizi mbalimbali. Kuna udi wa njiti ambayo ni ya kuchomana zipo aina tofauti na harufu tofauti, kuna udi wa kumimina kwenye maji kisha unayaogea nk.

Matumizi ya udi ni kama yafuatayo;
1. Hutumika kama manukato, hasa baadhi wa wanawake hutumia kufukizia nguo zao ziwe na harufu nzuri, pia wengine hufukiza mwilini.

2. Udi hutumika kufanya sala/dua au maombi kulingana a imani ya mtu. Unachoma udi na kuomba sala akati udi ukitoa moshi, pia hutumika kuita malaika wazuri au wabaya kwa lengo maalum. Mara nyingi hutumika majumbani au kwenye maduka. Pia kuna muda maalum ya kuchoma udi kwa ajili ya maombi isipokuwa ya manukato.
Kwa kuwa ulitaka kufahamu na si kutumia maelezo hayo yanakutosha.
 
Huku uswazi magetoni UDI unachomwa masaa 24 siku 7 za wiki,sio mambo ya imani??hapana ni kupotezea harufu ya majani,

Ukikatiza mitaa ya wahaya,mwanayamala,uwanja Wa fisi katika biashara zisizo na kodi zile pia wanapenda kichoma udi ili angalau ukiingia usisikie harufu ya bao la njemba iliyotoka kugegeda kabla yako wewe.
hahaha nicheke hivi iulishawahi fukiza udi?? inafanya kunakua na ile harufu nzur nzur ila uhakikishe umefunga madirisha na mapazia umeshusa kuzuia moshi kusambaa ikibidi limwagie maji kidogo ili moshi wake ukajikusanye pale pakikauka harufu yake sasa
 
Mti wa Chuma,
exactly....... ila niliwahi kuona kwa macho yangu hii ya kuchoma kuomba dua nilimsindikiza ndugu yangu kufanyiwa kisomo akaambiwa wakat anachoma udi asiombe udi aombe Mungu huku udi ukiendelea kutoa moshi wake na aushikilie mpaka kisomo kiishe asante kwa kujazia nyama mkuu
 
Huku uswazi magetoni UDI unachomwa masaa 24 siku 7 za wiki,sio mambo ya imani??hapana ni kupotezea harufu ya MAJANI

Ukikatiza mitaa ya wahaya,mwanayamala,uwanja Wa fisi katika biashara zisizo na kodi zile pia wanapenda kichoma udi ili angalau ukiingia usisikie harufu ya bao la njemba iliyotoka kugegeda kabla yako wewe.
Ha ha ha ha naona dalili ya JF ya zamani kuanz kurudi tena maana ilikuwa JF ya nondo
za nguvu na comment za kuondoa stress kabla ya virus vya siasa kuingia na matusi n.k
 
Huu ni mjadala mrefu sana na unahitaji mda kuujadili.
Kwa kweli uud au bakhoor ulianza miaka mingi sana iliyopita hata pharaoh walitumia na wakristo kwa waislam hata wayahudi wanatumia wote.

Sudan wanalima sana na wanatumia kwa mambo mengi sio tu kujifukiza na hata Egyptians wanatumia pia hata kwa kuondoa majini na pepo.

Ethiopians wanatumia kwa kazi maalumu zaidi mbali na kujifukiza kwa harufu nzuri.

Kiukweli napenda UUD kwa sababu inakufanya uwe relaxed zaidi and it keeps my mind allert
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom