Wanabodi,
Natumaini hamjambo na kila mmoja anaendelea na ujenzi wa Taifa letu la Tanzania. Leo hapa Mwanza kuna jambo limenishangaza sana. Nimekutana na Gari la polisi likisindikiza gari la idara ya Elimu. Nilipofuatilia zaidi nikajulishwa lilikuwa limebeba mitihani ya darasa la saba kutoka Mwanza airport. mitihani imetoka Dar es salaam.
Na katika hiyo mitihani kulikuwa na mitihani ya kanda mbalimbali ikiwemo tabora, mara, bukoba na mikoa mingine.
Ninachopenda tujadili hapa ni kujua kama bado ni muhimu kusafirisha mitihani kwenye hard copy.
Bila Jazba kwa wale wasiopenda uongozi wa baraza la mitihani, je sio wakati muafaka wa technologia kutumika kusafirisha hata flush disk, au kuprint kwenye wilaya husika? gharama za usafiri nilizoziona hapa ni kubwa sana. Pia wasindikizaji zaidi ya kumi pamoja na polisi. Je huu mfumo wa hard copy hauongezi risk ya mtihani kuvuja?
Au ndio mfumo wa kuhakikisha perdiem zinaliwa kipindi hichi?
Kwa mawazo yangu wakati umefika wa kuhakikisha technologia inatusaidia kupunguza gharama na kuepusha mitihani kuvuja. Naomba Dada Dr ndalichako apokee hii changamoto.
Naomba kuwakilisha kwa majadiliano.
Natumaini hamjambo na kila mmoja anaendelea na ujenzi wa Taifa letu la Tanzania. Leo hapa Mwanza kuna jambo limenishangaza sana. Nimekutana na Gari la polisi likisindikiza gari la idara ya Elimu. Nilipofuatilia zaidi nikajulishwa lilikuwa limebeba mitihani ya darasa la saba kutoka Mwanza airport. mitihani imetoka Dar es salaam.
Na katika hiyo mitihani kulikuwa na mitihani ya kanda mbalimbali ikiwemo tabora, mara, bukoba na mikoa mingine.
Ninachopenda tujadili hapa ni kujua kama bado ni muhimu kusafirisha mitihani kwenye hard copy.
Bila Jazba kwa wale wasiopenda uongozi wa baraza la mitihani, je sio wakati muafaka wa technologia kutumika kusafirisha hata flush disk, au kuprint kwenye wilaya husika? gharama za usafiri nilizoziona hapa ni kubwa sana. Pia wasindikizaji zaidi ya kumi pamoja na polisi. Je huu mfumo wa hard copy hauongezi risk ya mtihani kuvuja?
Au ndio mfumo wa kuhakikisha perdiem zinaliwa kipindi hichi?
Kwa mawazo yangu wakati umefika wa kuhakikisha technologia inatusaidia kupunguza gharama na kuepusha mitihani kuvuja. Naomba Dada Dr ndalichako apokee hii changamoto.
Naomba kuwakilisha kwa majadiliano.