Ni kweli usemayo lakini mimi nimekutana na watu ambo hawana hili tatizo la kikabila au mazoea ya kilugha lakini wanaiga hili tatizo ili waendane na kundi au mkusanyiko walipo.Mkuu hii inatokana na kabila ya watu jamani, hili tatizo ni la kitaifa hasa kikanda ya ziwa huwa tuna shida sana kule kwetu kila kitu huwa ni r rrrrrrr na wenzetu wao ni llllllll na pengine hhhhhhhh kwenye A so nikukubali kuwa ni tatizo na kuanza kulipunguza. Babu yangu alisoma wakati wa mkoloni na alinambia kulikuwa na kipindi (subject) cha kutamka maneno inavyopaswa. siku hizi hakuna!
Kweli wakuu, hili jambo linanikera kulikoni. Bora hata ukutane na mtu hajui kutamka, utaelewa. Ila ikija takita kusoma hua nachanganyikiwa, naanza kujiuliza mwandishi alimaanisha nini. Utakuta mtu kaandika "polini", mngine kaandika "piripiri". Kha!Wanakoseaga tu kwenye Ngeli, na sio kwenye majina. Umewahi kuwasikia wakiita Lostam?
Hii inaonyesha ni jinsi gani kiwango cha elimu kimeshuka. Hata kama mtu atakuwa hawezi kutamka herufi fulani kwa sababu ya athari ya lugha yake ya kwanza, inabidi aweze kuandika vizuri. Nadhani jambo hili halikuzingatiwa mashuleni, na sasa jambo hili la kuchanganya herufi, hasa katika uandishi, limekuwa jambo la kawaida.