Matumizi ya neno Nigger-nani alaumiwe?

Kana-Ka-Nsungu

JF-Expert Member
Oct 4, 2007
2,257
353
Kwa ambao mko majuu, naamini angalau mara moja ushawahi kuona jinsi watu weusi tunavyokuwa wakali wazungu wakituita 'nigger'. Kinachonishangaza ni jinsi ambavyo tunaweza kukubali matumizi ya neno hilo kama linatumika baina yetu sisi watu weusi. Utasikia weusi wakisalimiana- 'whats up nigger?' huku wakigongea na kucheka lakini tatizo linakua kama phrase hii itatokea kwenye kinywa cheupe! Huu si ubaguzi?
Na kwa upande mwingine pia, japokuwa neno hili linapigwa vita na kuonekana ni racism lakini sisi weusi wenyewe ndo tuna promote kwa kiasi kikubwa matumizi yake. Angalia movies za black, sikiliza mashairi ya rap songs za black americans, its nigger, nigger, nigger- from the begining to the end- na wazungu wanazisikiliza nyimbo hizi na kuzipenda.Sasa nani alaumiwe hapa?
 
Kwa kweli matumizi ya neno 'nigger' linanikera sana! Alafu kuna wabongo wanatumia tu ovyo bila kujua hata maana yake! Jamani it's derogative na inabidi sisi waafrika tuanze kupata self respect!
Mi naunga mkono jitihada za Bill Cosby na Oprah Winfrey waliosema kwamba African Americans waache kutumia maneno kama 'nigger' and 'bitch'! NI aibu.
Mi nadhani it's a sign of ignorance, self loathing and small or no self esteem! Mwanangu akitamka hilo neno nyumbani atakiona cha moto!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom