Matumizi ya neno ''Mheshimiwa'' kwa viongozi wenye nyadhifa

Lekanjobe Kubinika

JF-Expert Member
Dec 6, 2006
3,020
577
Lazima tutambue hapa kwamba CCM wanatumia strategy ile ya "Adui ya adui yangu ni rafiki yangu". Lakini ajabu kwamba spika amezidiwa mapema hivi, kiasi kwamba hata akiwapo kwenye kiti chake bado wabunge wanapafanya bungeni ni kijiwe cha taarab.

Wabunge kwa ujumla bunge la sasa wamejidhalilisha na kujipotezea heshima yao. Hata kule kuitwa mheshimiwa kwa sasa naiona kama wanajidhalilisha zaidi maana wamethibitisha kwamba hawastahili. bado kidogo tunawazidi majirani zetu Kenya tutaanza kutwangana bungeni kama hoja haitaeleweka kwa maneno ili kuonyesha msisitizo. I am so worried!

Tulishaambiwa sana tupingane lakini pasipo kupigana. Kuzomeana bungeni sikumbukikumewahi kutokea hapo nyuma. Wanaume kwa wanawake waisikika kuzomea na kutema maneno ya kejeli kwa sauti kubwa kiasi kwamba unaweza kujua anayeongea ni nani. Yaani hakukuwa tofauti na wavuta bhangi. Spika akakaa kimya maana hata akisema kitu alionekana sauti yake kuzamishwa na za wazomeaji. Ni aibu isiyo na ufafanuzi labda wanafiki tu wanaweza.

Ina mana wabunge wa sasa hawajui kwamba kuna aina nyingi za mtu kulalamikia kile anachoamini kuonewa na pasipo kupewa uhuru wa kusikilizwa? Kwani Tanzania tuko dunia ya wapi? Majuzi tu tuishaambiwa kwamba kutoka nje sio mojawapo ya makosa bungeni. Kwa hiyo wabunge wa sasa ina maana shule haipandi hata hawafundishiki?

Tuwakumbushe tu kwamba raha zao ni maumivu yetu tuliowatuma huko. Hatukuwatuma kule kujenga vigenge vya kihuni bali wapaze sauti juu ya mambo yanayotukera. Hivi sasa umeme ni shida achilia mbali gharama yake juu. Maisha ni hoi kwa kila mtanzania wa kawaida, hawaoni hayo?

CCM ina maana mko radhi kweli kuiongoza nchi ya watu hohehahe milele? Mnajidanganya, kama mnadhani natania subiri au ulizia dibaji ya Tu nisia na Egypt. Msifanye sherehe kwenye matanga ya mtu masikini, hata maiti zinaweza kuwageuka.

===========
August 2012:

Napendekeza Tanzania tuache kutumia neno "Mheshimiwa" kwa viongozi

Wakati wa utawala wa Mwinyi tulishuhudia kujikweza kwa viongozi wetu na kutaka waitwe "Waheshimiwa", wakibadili neno lililotumiwa kwa miaka mingi kwa viongozi na watanzania kwa ujumla wote kuitana "ndugu".

Ukweli ni kwamba wengi hatujagundua kwamba toka viongozi waanze kuitwa "waheshimiwa" walianza kujiona kama tabaka la aina iliyo juu mbali na mwananchi wa kawaida, wengi wao wakawa mafisadi na kusahau shida za wanachi wa kawaida waliowawakilisha.

Kumbuka neno "ndugu" lilitumika kwa kila mtanzania, hata katika katiba nadhani, tuna misemo kama "binadamu wote ni ndugu zangu na Afrika ni moja".

Tangu lianze kutumika, neno "mheshimiwa", lililopata baraka zote na viongozi wa CCM, lilimekuwa kama neno lilololeta laana kwa CCM na uongozi Tanzania.

Kwa msingi huu basi, napendekeza turudi tena kwenye matumizi ya neno "ndugu" badala ya "mheshimiwa". Na ukweli ni kwamba heshima inayohusiana na "uheshimiwa" ni jambo ambalo mtu analipata kwa matendo yake (you earn respect rather respect by default).

Na pia, japo tunawaita viongozi na wabunge "mheshimiwa" kuna wengi sana hawastahili kabisa kuitwa hivyo. Binafsi niko radhi sana kumwita kiongozi fisadi "ndugu" kuliko "mheshimiwa".
 
well said you have spoken my mind! watanzania wengi wameshawachoka hawa tumbo mbele ccm na nawapa rai kuwa Ben ALLI na MUBARAK walidhania wanapendwa kumbe wanachukiwa kuliko kawaida ni swala la muda tu hapa bongo litatokea.

Anayedai mbunge wake kabaki bungeni (yaan hao CCM)kutetea maslahi yao atueleze ni hoja gani huyo mbunge aliitoa kwa manufaa yataifa kama sio kuzuia hoja za kukomesha ufisadi
 
Lekanjobe Kubinika, Wabunge wetu siku ukiwaondolea neno Mhe. wataathirika kisaikojia , maana wao wanaamini hivyo na hilo Jumba la dodoma ni jumba Tukufu ambalo nadhani rais wa JMT ndiye source huo utukufu --
 
Last edited by a moderator:
yaani ....................SHAME SHAME SHAME on them - niliwasikia kwenye Radio BBC wakizomea.................sikuelewa .........nilidhani radio imeharibika ...........kumbe eti ni WABUNGE WA CCM - wanakaa kuzomea zomea tu - ngoja na wao wakipita tutawazomea .......si ndiocho wanacho-onyesha mfano?????????????? WABUNGE WAZOMEE - WANAFUNZI WAZOMEEE - MTAANI WAZOMEEE - WATOTO WADOGO WAZOMEE ..................... they have degraded themselves to 0 .........mimi siwaiti tena WAHESHIMIWA ... they dont deserve it.
 
Hali iliyojitokeza pale bungeni majuzi inaonyesha wazi kuwa spika ameshindwa kazi. Hayo ndo madhara ya vikao vya siri vya wabunge wa CCM na huo ni mkakati waliojiwekea wa kuhakikisha wanadhoofisha upinzani bungeni kwani kwa nguvu aliyonayo sipika angeweza kudhibiti fujo zilizokuwa zinatokea bungeni za kuzomeazomea, haiwezekani watu wazima tena waheshimiwa wanaonyesha utovu wa nidhamu bungeni halafu spika anakenua meno tu,utamuachiaje mtu aongee wakati hujamruhusu kufanya hivyo? je wangekuwa ni wabunge toka upinzani waliofanya hivyo si wangesimamishwa kuhudhuria vikao vya bunge?

Japokuwa kuwazuia nako ni kukiuka haki ya wananchi kuwakilishwa bungeni ila wengetakiwa wawe wanakatwa posho pamoja na adhabu zingine zinazostahili.Hapa maana yake ni kwamba spika aliruhusu fujo bungeni ili hoja za wapinzani zisisikike au kuwafanya wakasirike hatimaye washindwe kuwakilisha hoja kifasaha.

Na badala yake wabunge wa chadema wanaonekana wao ndio wamekomaa kisheria kwani walikuwa na haki ya kimsingi na kikatiba kutoka nje ya kikao kuonyesha kupinga kwao kutokusikilizwa hoja zao ,wa CCM wakaonekana ndo watoto kwa kuzomeazomea na hii inaonyesha picha halisi ya wanayoyafanya katika familia zao,kwa mfano wake zao au watoto wao au majirani zao na pia ndugu zao wakikosea au wakipishana kwa mawazo wao huanza kuwazomea badala ya kukaa nao kitako na kutoa hoja zao,inaonekana haya ndiyo waliyojifunza katika semina elekezi kule ubungo plaza na hali hii anayoiruhusu spika siku moja atakuja kushindwa kubeba msalaba wake kwani inaashiria kuwa 'waheshimiwa' iko siku moja watatwangana makofi kisa tu ukosefu wa staha, maadili, uwajibikaji na kutokutambua haki za wenzio kwa kuona kuwa wao pekee ndo wana haki pekee ya kuongea au kusikilizwa katika nchi hii.

Nami nadiriki kusema kuwa hii ni tabia ya matumizi mabaya ya madaraka waliyopewa kwani ndio kila siku wanaopinga mabadiliko katika nchi yetu yenye utulivu bila amani,bado wanaota katika zama zile za watawala,hawajui kuwa siku hizi nchi zinazoendelea zinaongozwa na viongozi na sio watawala kama wao wanavyotaka.

I N A K E R A SAAAAAAAAAANA
 
Kama kuna makosa tunayofanya raia wa kawaida ni hili la kuwaabudu wanasiasa na kuwaita waheshimiwa. Nakukumbusha ewe mwananchi kwamba hawa jamaa wanadharau ya hali ya juu.

Wanapotafuta vyeo vyao e.g ubunge huwa wanapiga magoti na kukubembeleza uwapigie kura. Wakishapata tu wanaanza kujiweka juu na kuwaona wananchi si lolote si chochote.

Ndg mwananchi kwa kuwapa heshima ambayo wewe ndio unasitahili kuwa nayo huoni kwamba unajidhalilisha na hivyo wewe ni MDHARAULIWA?
 
Wakati wananchi wakiendelea kuwaita wabunge "waheshimiwa"baadhi yao wameendelea kuhoji ni kwa nini wanaiitwa waheshimiwa ukizingatia kwamba wanawakilisha wananchi,hivi hilo neno linaashiria hofu au heshima?mbona wakati wa kampeni wanajishusha sana,hata rais huwa anatumia neno mbunge anayegombea kupitia chama fulani,lakini baada ya kupiga kura hali ya kuitwa waheshimiwa hujirudia,kwanini?
 
Wakati wananchi wakiendelea kuwaita wabunge "waheshimiwa"baadhi yao wameendelea kuhoji ni kwa nini wanaiitwa waheshimiwa ukizingatia kwamba wanawakilisha wananchi,hivi hilo neno linaashiria hofu au heshima?mbona wakati wa kampeni wanajishusha sana,hata rais huwa anatumia neno mbunge anayegombea kupitia chama fulani,lakini baada ya kupiga kura hali ya kuitwa waheshimiwa hujirudia,kwanini?

Provide some facts please. Baadhi yao ni akina nani? Wataje, tuwajue...... Nashauri utafute kwanza maana neno MHESHIMIWA kabla hujaja na VIASHIRIA ulivyokuja navyo. Maana ukija hivyo nami naweza sema QUEENTAR inaashiria $$$$$$$$ au "Mwalimu" Nyerere ..... Mwalimu inaashiria $$$$$$$, au "Dkt". Queentar, DkT inaashiria $$$$$$$$$.

BTW, you should know hizi titles zinategemea na mambo mengi... professional/ discipline, ofisi, wadhifa etc................. Kama swali hilo linajadilika na hivyo unanonymously watanzania twaweza likataa ifanyike.......
 
Kwa sababu tulikoiga habari ya Bunge kama tunavyolijua leo, huko Westminster, wabunge huitwa "Honourable". Sie tumetafsiri tu.

Lakini hili linazaa swali. Watu wengine ambao si wabunge hawastahili heshima? Kama wanastahili kwa nini wasiitwe waheshimiwa?
 
Msaada: Naomba kuelimishwa kupitia Jukwaa Hili la Great thinkers kwamba KIMANTIKI kwa nini Wabunge waitwe Waheshimiwa.

Me mwenyewe siijui maana hasa ni nini,Ila nnaona Kama vile bado tunauendeleza ukoloni.
 
Ngoja tuwasubirie wengine....akina Boflo, Rejao, Maxence na mwanakijiji n.k.
 
Nilishawahi ku-differ na mbunge mmoja R S T kwa kusahau kutanguliza neno Mheshimiwa. Sioni haja ya mbunge kuitwa Mheshimiwa kama atakaa kwenye mjengo na kuchapa usingizi bila kuwakilisha shida zangu pale mjengoni.
 
Kwa sababu tumewapa heshima ya kwenda kutuwakilisha bungeni.....hii ni heshima kubwa,wasipoithamini...nasi tunawadharau kupitia sanduku la kura na kuwa sio waheshimiwa tena. That's all.
 
Kwa sababu tumewapa heshima ya kwenda kutuwakilisha bungeni.....hii ni heshima kubwa,wasipoithamini...nasi tunawadharau kupitia sanduku la kura na kuwa sio waheshimiwa tena. That's all.
 
Mheshimiwa ni neno ambalo maana yake kwa kiingereza ni "Honorable". Matumizi ya neno mheshimiwa au Honorable linatokana na kuweo kwa matabaka baina ya raia: yaani kuna wale wa kuheshimiwa na wale wa kutoheshimiwa.

Zamani sana tulipokuwa katika harakati za kufuta matabaka miongoni mwetu tulikuwa tumeondoa neno "Mheshimiwa" katika katika msamiati wetu, tukawa tunatumia taito ya "Ndugu" ambayo ilikuwa ni tafsiri ya neno comrade iliyorithiwa kutoka China na Korea. Neno "Mheshimiwa" lilirudi tena katika jamii yetu mwaka 1987 ambapo wabunge walipitiisha azimio kuwa wawe wanaitwa waheshimiwa.

Matumizi ya neno mheshimiwa katika jamii yetu ilikuwa si jambo jema kwa vile jamii yetu ilikuwa haijaelimika vya kutosha kujua haki zao kama raia. Kwa sasa bado kuna wananchi wengi ambao wanaamini kuwa wahishimiwa ni miungu wadogo.
 
Je hili neno muheshimiwa mbunge, diwani, raisi na nk. Linachangia kupunguza uwajibikaji? Lilianza lini katika historia ya tanzania? Nawakilisha.
 
Lilianza kiswahili kilipoanza

Hapana lilianza baada ya Nyerere kuondoka madarakani,na hakika sijui maana yake nini.
Ukiachia mbali neno hilo kuna majina tumepewa tunaitwa 'wananchi wao' au 'wananchi wa kawaida'.
Bila kutafakari tumeyapokea maneno hayo hatuoni ubaya tunapoitwa hivyo.Kwamba sisi ni mali zao na ni wa kawaida na wao si wa kawaida.
 
Wanaitwa waheshimiwa kwa sababu wana vyeo vikubwa hivyo wao si wananchi wa kawaida.Kifupi wao pamoja na mawaziri,majaji,mahakimu,madiwani ni wa daraja jingine hivyo wamependa kuitwa hivyo wakimaanisha wao ni WAHESHIMIWA na wanaowaongoza na kuwahukumu au kuwatoa hatiani yaani wananchi wa kawaida mimi na wewe tu WADHARAULIWA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom