Matumizi ya Mitandao Jamii Kwenye Chaguzi

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Wakati ambapo Uchaguzi mkuu unakaribia Wanateknohama wanashauku ya
kujua mambo mbalimbali kwa njia ya mtandao kuanzia kupashana habari ,
majadiliano motomoto na masuala mengine mengi sana yanayohusiana na
Uchaguzi mijadala hiyo itakuwa kuanzia Kwenye majukwaa ya wazi ambapo
watu hudumia majina halisi kama www.wanabidii.net mpaka kwenye blogu
mbalimbali nchini tembelea www.afrigator.com chagua nchi ya Tanzania
huo ni mtandao unaoweza kutumia kufuatilia blogu mbalimbali za afrika
lakini zilizosajiliwa kwenye mtandao huo tu .
Unaweza kujiuliza jinsi teknohama haswa mitandao jamii inavyoleta
mabadiliko kwenye jamii nyingi duniani haswa wakati wa uchaguzi mkuu
kuanzia kukusanya taarifa za wanachama kwa njia ya mtandao mpaka pale
wanachama hao wanapo changa hela kwa ajili ya wagombea wao kwa njia ya
mtandao na hata pale watu wanapotuma matokeo ya uchaguzi kwa njia ya
mtandao hizi zote ni hatua kubwa katika maendeleo .

Nchi mbalimbali duniani zimeweza kutumia teknohama kwenye shuguli zao
mbalimbali zinazohusisha uchaguzi kwa mafanikio makubwa sana hata kama
chaguzi hizo zilileta vurugu na manunguniko kwa wale walioshindwa ,
kuanzia kuanzisha tovuti za vyama mbalimbali vya siasa au hata blogu
za mwanachama mmoja mmoja na kurasa zingine nyingi sana za mitandao .

Fikiria chama kinavyotaka kupanga kampeni Fulani kwa sasa si lazima
wote kukutana sehemu moja ambapo wanatumia gharama na muda mwingi
kuandaa mkutano wanaweza kutumia huduma za sms kuwasiliana kwa kutumia
namba walizozihifadhi za mwanachama wao kuwasiliana na sasa idadi ya
wamiliki wa simu imeongezeka na watu wengi wamesajili namba zao za
simu ni rahisi zaidi .

Hata pale ambapo kumetokea tishio la wizi wa kura na kero zingine
zozote watu wanaweza kutumia simu zao wa mikononi kwa ajili ya
kupashana habari taarifa na huduma zingine haswa kwa vijana mfano
wanaosimamia vituo vya kupiga kura .

Na pale ambapo watu wako vijijini kabisa ambapo ni ngumu kufika kwa
sababu kadhaa jamii hizo zinaweza kutumia simu zao za mikono kwa ajili
ya kupashana habari na taarifa zingine moto moto .

Tanzania ni moja ya nchi ambayo imewahi kuonja utamu wa matumizi ya
teknohama kwenye shuguli za uchaguzi zaidi kuanzia mwaka 2005 ambapo
vyama vya siasa viliwasiliana na wanachama wao kutumia mtandao na hata
baadhi ya wagombea kuanzisha blogu na huduma zingine kwenye mtandao .

Mwaka huu tunaingia kwenye uchaguzi tena baada ya miaka zaidi ya 4
ambapo kumetokea maendeleo makubwa kwenye sekta ya teknohama kwa
ujumla kuanzia matumizi ya simu za mkono zenye uwezo mkubwa mpaka
kuanzishwa kwa mitandao jamii ambapo watu wanaweza kuwasiliana na
wananchi wao moja kwa moja .

Mitandao jamii ndio haswa imechukuwa nafasi kubwa kwenye chaguzi
mbalimbali kwa siku za karibuni kuanzia pale raisi wa marekani
alivyokuwa anatumia mtandao wa youtube kuwasiliana na mashabiki wake
mpaka serikali ya iran ilivyojaribu kufunga baadhi ya mitandao jamii
isiweze kutembelewa na raia wananchi hiyo waliokuwa ndani ya nchi .

Kilichotokea nchini iran sio harakati mpya tu kwa njia ya mtandao pia
ni funzo kwa jamii zingine duniani sasa kuwekeza zaidi kwenye masuala
ya ulinzi kwenye teknohama pamoja kuwa na wafanyakazi bora kwenye
ulingo huu wa teknohama .

Muda unazidi kwenda sana watu wanazidi kupata maendeleo sasa hivi
inakadiriwa zaidi ya nusu ya watu wote duniani wanamiliki simu za
mikononi na mitandao ya jamii inazidi kuchipukia kila kukicha pamoja
na program mbalimbali za kutumia kwenye mitandao hiyo huku watu zaidi
wakiunganishwa kwenye mtandao au huduma zingine za mawasiliano .

Kwa mwendo huu wa kasi katika ukuaji wa teknohama ina maanisha huko
mbeleni ujumbe unaweza kusambaa dunia nzima kwa sekunde tu au unaweza
kusambazwa ujumbe kwenda kwa kundi Fulani la watu kwa sekunde tu
serikali za sehemu hizo lazima zijue wajibu wake endapo chochote
kitatokea .

Utumiaji wa Teknohama haswa mitandao jamii inatofautiana haswa
kutegemeana na vifaa vinavyotumika kwenye tovuti au anuani za mitandao
mbalimbali mfano kwenye uchaguzi wa marekani mgombea uraisi wa
marekani aliweka matangazo kwenye mtandao wa michezo ya kompyuta kwa
ajili ya wachezaji wa michezo hiyo ,akaanzisha chaneli kwenye mtandao
wa youtube .

Hapa kwetu chama kinaweza kuanzisha channel yake kwenye mtandao wa
youtube , inaweza kuanzisha blogu za wagombea wake kupitia tovuti ya
chama husika na wagombea hao wanaweza kuanzisha kurasa zingine kupitia
mitandao mingine kama facebook kwa ajili ya kuwasiliana na watu au
twitter na mashabiki au wapenzi wao wanaweza kuwafuatilia moja kwa
moja kutumia barua pepe au simu zao za mikono .

Matumizi haya pia yanaweza kuleta changamoto kwa kampuni zinazozalisha
magazeti au vyombo vingine vya habari vinavyotumia karatasi kwa ajili
ya kuwasilisha taarifa zao kwa sababu wengi watakuwa wanafuatilia
habari na matukio kutumia mitandao jamii ni vizuri kampuni za habari
haswa magazeti kufungua kurasa zao za mitandao jamii ili kuweza kwenda
sambamba na mabadiliko ya sasa .

Kwa kumalizia naona kizazi kipya cha viongozi ambao hawashindi chaguzi
kwa Wizi wa Kura au kutumia njia chafu bali kwa matumizi bora ya
Teknohama haswa mitandao ya jamii ambayo wanaitumia kuwaunganisha na
wapenzi na mashabiki wao wengine mifano iko wazi kuanzia kwenye
uchaguzi wa marekani mpaka huu wa uingereza mwaka huu na hata raisi wa
Venezuela anavyohangaika kwenye mtandao wa Twitter mpaka kuajiri
wafanyakazi maalumu wa kuwasiliana na wananchi .

Hata kama viongozi wengi hawapendi au hawana muda wa kujiunganisha
kwenye mitandao jamii lakini wanaweza kuajiri watu kama Kiongozi wa
Venezuela alivyofanya kuandika na kutoa huduma zingine kwenye blogu
zao au kurasa zao za mitandao

Kama unapenda kuingia kwenye Ulimwengu wa Mitandao jamii hizi ndio
faida zake .

1 - Watu wa Teknohama wanatumia muda mwingi kwenye Mtandao kuliko
Televisheni na Radio kwahiyo una uhakika wa kunyanyuka .

2- Huduma zake nyingi ni bure au zina unafuu na haziharibu kama
mazingira kama mtu akiamua kubandika matangazo njiani na kutupa
karatasi hovyo .

3 – Huduma za Mawasiliano kwa sasa zimeshuka kutokana na sababu kadhaa
na huduma hizo pia sasa zimekuwa na kasi kubwa pamoja na huduma hizo
kupanuka maeneo mengi sana nchini .
4 – Picha zinaongea zinaongea kuliko chochote unachoweza kufikiria
wewe haswa ukipata mpiga picha mzuri na ziwekwe vizuri kwenye mtandao
wako

Unaweza kutembelea Anuani zifuatazo kwa uone jinsi unavyoweza
kuzitumia kwenye shuguli zako za uchaguzi mwaka huu wa 2010

www.youtube.com
www.orkut.com
www.ning.com
www.twitter.com
www.facebook.com
www.blogger.com
www.mozes.com
www.ourmedia.com
www.mybloglog.com
www.othersonline.com
www.presidentialquest.com
www.NewsAssignment.net
www.groups.yahoo.com
www.groups.google.com
www.Linkedin.com
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom