GIBA KB
JF-Expert Member
- Jul 3, 2012
- 367
- 110
Za asubuhi wanajamvi,
Nianze kwa kusema mimi ni daktari nimemaliza degree yangu ya udaktari mwaka 2008 pale Muhimbili na sasa nachukua masters ya pediatrics (Magonjwa ya watoto) Mandela University Arusha.
Serikali imetoa sera mpya ya elimu ambayo imeazimia kiswahili kutumika kama lugha ya kufundishia kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu. Matumizi ya kiswahili kwa chuo kikuu hasa kwa fani za Afya itakuwa ngumu kwa sababu:
1)Hatuna wataalamu waa kutosha wa kuweza kutafsiri vitabu vinavyotumika kwa kiswahili.
2)Fani za udaktari zina maneno mengi magumu ambayo hata kwa kiingereza unaweza ukashindwa kuyaelewa.
3)Kutumia kiswahili kufundishia kutamnyima daktari nafasi ya kupata ajira nzuri tu nje ya nchi.Mfano UN,Unicef,South Africa n.k
4)Hatuna teknolojia tunayoweza kutumia hata km tutajifunza kwa kiswahili.
Hizo ni baadhi tu ila zipo nyingi.Hili suala ni muhimu sana liangaliwe vizuri.Sio kwamba napinga kiswahili kisitumike la hasha!! Napenda ty lakini maandalizi yawepo ya kutosha.
Nianze kwa kusema mimi ni daktari nimemaliza degree yangu ya udaktari mwaka 2008 pale Muhimbili na sasa nachukua masters ya pediatrics (Magonjwa ya watoto) Mandela University Arusha.
Serikali imetoa sera mpya ya elimu ambayo imeazimia kiswahili kutumika kama lugha ya kufundishia kuanzia shule ya msingi hadi chuo kikuu. Matumizi ya kiswahili kwa chuo kikuu hasa kwa fani za Afya itakuwa ngumu kwa sababu:
1)Hatuna wataalamu waa kutosha wa kuweza kutafsiri vitabu vinavyotumika kwa kiswahili.
2)Fani za udaktari zina maneno mengi magumu ambayo hata kwa kiingereza unaweza ukashindwa kuyaelewa.
3)Kutumia kiswahili kufundishia kutamnyima daktari nafasi ya kupata ajira nzuri tu nje ya nchi.Mfano UN,Unicef,South Africa n.k
4)Hatuna teknolojia tunayoweza kutumia hata km tutajifunza kwa kiswahili.
Hizo ni baadhi tu ila zipo nyingi.Hili suala ni muhimu sana liangaliwe vizuri.Sio kwamba napinga kiswahili kisitumike la hasha!! Napenda ty lakini maandalizi yawepo ya kutosha.