Mwanajamii
JF-Expert Member
- Mar 5, 2008
- 7,063
- 68
CCM ni chama kinachopoteza umaarufu wake kwa kashifa nyingi zikiwemo za ufisadi wa baadhi ya makada wake. Makada hao wenye nguvu kubwa ya fedha na mtandao mkubwa ndani ya chama na serikali wamekataa kukubali kuwa wao ni magamba na kwa maana hiyo wamesababisha utekelezaji wa dhana ya kujivua gamba kuwa ngumu ndani ya chama hicho.
Viongozi, Wanachama na wapenzi wa CCM wanatakiwa kuelewa kuwa mafisadi ni mwiba mkubwa ndani ya chama hico na wasipoangalia watakipeleka kubaya.
Yaliyotokea Arumeru ni moja ya mambo machafu yanayofanywa na mafisadi hao kwa nguvu ya pesa na hivyo kuendelea kukipa chama taswira mbaya katika jamii. Kwa matokeo yoyote yatakayopatikana Arumeru CCM lazima wayakubali na iwe mwanzo wa wao kutambua kuwa wananchi wamechoka vitendo vyao vya matumizi ya fedha katika chaguzi na kwamba wananchi ndiyo wenye nguvu za kuchagua viongozi wanaowataka na si watu wachache wenye fedha kuwachagulia watu wanaowataka wao kwa maslahi yao ya kisiasa.
Nawasilisha.
Viongozi, Wanachama na wapenzi wa CCM wanatakiwa kuelewa kuwa mafisadi ni mwiba mkubwa ndani ya chama hico na wasipoangalia watakipeleka kubaya.
Yaliyotokea Arumeru ni moja ya mambo machafu yanayofanywa na mafisadi hao kwa nguvu ya pesa na hivyo kuendelea kukipa chama taswira mbaya katika jamii. Kwa matokeo yoyote yatakayopatikana Arumeru CCM lazima wayakubali na iwe mwanzo wa wao kutambua kuwa wananchi wamechoka vitendo vyao vya matumizi ya fedha katika chaguzi na kwamba wananchi ndiyo wenye nguvu za kuchagua viongozi wanaowataka na si watu wachache wenye fedha kuwachagulia watu wanaowataka wao kwa maslahi yao ya kisiasa.
Nawasilisha.