Matumizi Mbadala Ya Bilioni 40 za Kampeni CCM!

Mimi nimeshikwa na kigugumizi, mwaka 2005 kagada Agriculture walikwapua sh billioni 40 na uchunguzi usiokuwa rasmi ulibaini zilikwenda kwenye uchaguzi wa CCM. Sio nia yangu kuongelea mambo ya zamani lakini ukwapuaji ule na uchangishaji wa amount inayolingana na ile ya zamani hauna mahusiano? bila shaka yapo.Cha kunishangaza zaidi ni pamoja na sasa kuwa na sheria ya kudhibiti matumizi ya fedha chafu. Endapo mtu atachangia hela chafu watawezaje kuchuja kwamba hizi ni safi na hizi ni safi?Pili matumizi ya bilioni 40 kwenye uchaguzi kwa nchi masikini kama tanzania ambayo wagonjwa wawili huchangia kitanda kimoja na wanafunzi kukaa chini bila madawati inaingia akilini kweli? Kuna haja ya kufikiri upya kwamba tunataka nini na nini kianze
 
Tatizo hapa ni jinsi gani viongozi wetu wanaonyesha umimi zaidi ya kutumukia watu. Kama kweli unaweza kubuni njia ya kupata bilioni 40 kwa ajili ya kukurudisha madarakani lakini matatizo ya msingi ya unawaongaoza huna mbinu ya kutatua mpaka msaada toka nje hii inatupa picha ya tunaongozwa na aina gani ya watu.
 
Sasa sheria ya uchaguzi ya nini wakati wao ndio watu wa kwanza kuvunja?? hii wanaitunga sheria kwa ajili ya Chama gani?? mbona ndio hawa ndio watu wakubwa wa kutoa rushwa
 
Jana usiku CCM wamezindua kampeni ya kuchangia kampeni kwa kutumia simu za mkononi!

Makadirio ni kwamba watakusanya taslimu 40,000,000,000/=(bilioni 40)!

Mimi nilipotazama jinsi washiriki wale walivyochangamka kutoa kwa kutuma ujumbe, nilihamasika kwamba iwapo ungeanzishwa uchangiaji wa namna hiyo kwaajili ya madawati ya shule zote nchini, hakuna mtoto ambae angekaa kwenye vumbi!

Kama jana, ziliweza kupatikana milioni 20 ndani ya dakika 5 tu za uchangiaji, je kwa miaka 5 ya uongozi wa JK, wananchi wangechanga kiasi gani, na tungekuwa wapi?

Kwanini wabongo tunapenda kufanya fund-raising za 'Disposable cash, kama hizi kampeni, tisheti na harusi, unlike kuwekeza kwenye investment za kudumu kama elimu, afya na miundombinu?

Ningekuwa mimi ndo JK, ningesubiri hela yote hiyo ichangwe, kisha natangaza ghafla kwamba hakutakuwa na kampeni, hela zote zinatumika kupeleka maji, au kujenga dispensari vijijini!

NINA HAKIKA 100% KWAMBA CHAMA CHANGU KINGECHAGULIWA BILA KUPINGWA NA RAIA YEYOTE...Unaonaje?



Kwa kusema ukweli sasa Wadanganyika tumefikia hatua mbaya sana ya kuunga mkono ufisadi kwa uwazi.Mimi naona ingekuwa vema kama kungewekwa sheria kuwa mtu mmoja awe na maximum ya kuchangia sivyo Mheshimiwa JK ni zilezile pesa zilizoibiwa EPA,mikataba ya kitapeli,richmond ,buzwagi na mingine mingi zitapitia mlango wa nyuma na kukusaidia kushinda tena.Kama JK unataka tukuelewe basi inatakiwa uweke ukomo wa kuchangia sivyo mafisadi watakuchangia pesa nyingi.Kumbuka JK hutuba yako ya kwanza wewe mwenyewe ulishangaa pesa yote hii CCM wametoa wapi,
Angalia jinsi wafanyakazi wanavyoteseka na mishahara midogo,leo bila aibu ati mnachangishana pesa yote hiyo.
Angalia JK ulivyosema hujui kwa nini tanzania ni nchi maskini je unakumbuka,bilionni 40 kuzikamua toka kwa wananchi wa kawaida huo ni uongo hapo kuna watu watapewa pesa katika simu zao na kuchangia kujifanya ni wao kumbe zimetokana na ufisadi(Kumbuka epa ya kagoda na wote ambao ni wezi pesa hiyo ilitumika kwenye kampeni ya kukuweka madarakani.
Kumbuka marekani wanavyoumia wanapochangia pesa nyingi mpaka wanafikia hatua ya kusema tanzania inaongoza kwa misaada mingi leo pesa ya misaada unachangia uchaguzi kuna maendeleo kweli.
Watanzania tubadilike na tuanzishe harambee kama kenya za kuchangia elimu na sio harusi kama inavyosemekana kuwa watanzania ni mabingwa wa kuchangia harusi duniani.
 
Kama wewe ni Mpiganaji wa kweli kama kwenye jina lako, basi utawaonea huruma kubwa walalahoi wanaoishi vijijini, mpaka leo baada ya miaka 49 ya Uhuru, wanaishi kwenye nyumba za udongo! Unabisha? Tembelea sehemu yoyote hapa nchini, ukiwa njiani kwenye barabara kuu utaziona nyumba lukuki za udongo, wanazoishi ndugu zetu hawa, wakulima (?), maskini wa kutupwa, kwao hata mlo wa siku moja hawana uhakika nao. Haya ndiyo MAISHA BORA?

Unasema tuichangie CCM, kwa lipi bora walilolifanya? Waulize hao wenzetu. Hivi weye huna SONI? Unatazama yale uliyoyapata wewe, lakini wale ambao hawana hata kidogo huna habari nao. Kisha wasema tuichangie CCM? Ahadi hewa walizopewa wenzetu hawa, nadhani wewe ulikuwa mmojawapo wa kwenda kufanya kampeni ili kupata kura zao, kisha unasema CCM ichaguliwe tena?

Fainali Oktoba 2010!

Najua kwamba alichokisema JK na Makamba, kwamba ushindi kwa CCM ni lazima kitakuwa kweli, kwa kuwa mfumo wetu we kisiasa ni wa SIMPLE MAJORITY. Hata kama kuna mgombea pekee, wa CCM, akipigiwa KURA MOJA TU, ilhali yuko peke yake, basi ameshinda. Lakini iko siku Wadanganyika watakataa kudanganyika.

CCM ibeni kura. CCM wekeni sheria za kuwabana wananchi wasiwe na uhuru wa kuchagua viongozi wawatakao. CCM toeni pesa lukuki kununua kura za walalahoi, mtakuwa mmewapa nafuu ya muda mfupi, si ya muda mrefu.

Mbwa wako mwenyewe, ukimtesa kwa muda mrefu, iko siku ATAKUNG'ATA!

./Mwana wa Haki

Waheshimiwa, jana CCM ilizindua kampeni ya uchangiaji kwa wanaachama na wakereketwa kama wanavyojiita niliangalia lakini kuna kitu hapa tuchangieni:

Mwenyekiti wa taifa CCM kwa kusisitiza uchangiaji alisema

Jamani tuichangieni CCM, tukukumbuke chama hiki kilivyoifanyia nchi hii. Je? Wanajamvi bila CCM nchi hii haingekua hapa? Au ingekua mbali zaidi? Na je ni CCM imeifanyia Nchi mambo mazuri au Inchi ndio imeifanyia CCM kua hapo?

Karibuni.
 
quote_icon.png
Originally Posted by Geoff
Ccm hoyeeeeee!....




quote_icon.png
Originally Posted by Fidel80
Zidumu fikra za mwenyekiti wa chama.
CCM oyeeeeee.

PJ our president 2025 oyeeeeeeeeeee!!!
 
akili ni nywere kila mtu ana zake..hizo ndiyo akili zetu watanzania..eee mungu shusha mkono wako..utuokoe waja wako..
 
Mara nyingi nasoma post zenu wala sizijibu.....kazi yangu kusoma naju yepi hoja za msingi na yepi pumba! Katika hili sikubaliani nanyi. Suala la kukusanya fedha za kampeni kwaajili ya CCM ni jambo jema wala sioni tatizo. Leo hii CHADEMA wakichangisha fedha kwaajili ya kampeni yao na uhakika you dont comments at all badala yake mtasema chama kinajizatiti kupata ushindi! Tatizo la wana JF ni kwamba karibia WOTE ni wapinzani wa chama Tawala CCM! Sijaona hoja yoyote ya msingi katika hili na katika mengine yote yalopita isipokua ni porojo mingi za Waswahili ! Badala ya kujadili issues kama East African Federation na impacts zake mnamjadili JK akikusanya fedha kwa wapiga kura wake ili kuwezesha chama kushinda. Ninyi mngetaka achangishe wapi, kwa nani kama siyo kwa wapenzi wa chama chake? Angeanza tu kampeni bila fund-raising si mtasema kaiba? Acheni TAARAB, Maneno maneno, chokochoko na Uswahili wenye nia ya kuchafuana. Kama mnaweza nanyi changisheni hamnyimwi..lakini yote tisa CCM kitashika tena hatam na mtaongozwa na serikali yake kama kawaida. Nilishasema mimi SIYO mwanachama wa chama chochote cha siasa bali an "OBSERVER". Tafakari!!!!
 
Mara nyingi nasoma post zenu wala sizijibu.....kazi yangu kusoma naju yepi hoja za msingi na yepi pumba! Katika hili sikubaliani nanyi. Suala la kukusanya fedha za kampeni kwaajili ya CCM ni jambo jema wala sioni tatizo. Leo hii CHADEMA wakichangisha fedha kwaajili ya kampeni yao na uhakika you dont comments at all badala yake mtasema chama kinajizatiti kupata ushindi! Tatizo la wana JF ni kwamba karibia WOTE ni wapinzani wa chama Tawala CCM! Sijaona hoja yoyote ya msingi katika hili na katika mengine yote yalopita isipokua ni porojo mingi za Waswahili ! Badala ya kujadili issues kama East African Federation na impacts zake mnamjadili JK akikusanya fedha kwa wapiga kura wake ili kuwezesha chama kushinda. Ninyi mngetaka achangishe wapi, kwa nani kama siyo kwa wapenzi wa chama chake? Angeanza tu kampeni bila fund-raising si mtasema kaiba? Acheni TAARAB, Maneno maneno, chokochoko na Uswahili wenye nia ya kuchafuana. Kama mnaweza nanyi changisheni hamnyimwi..lakini yote tisa CCM kitashika tena hatam na mtaongozwa na serikali yake kama kawaida. Nilishasema mimi SIYO mwanachama wa chama chochote cha siasa bali an "OBSERVER". Tafakari!!!!
 
Utaratibu huu wa kuwataka wana CCM kuchangia angalau sh. 1,000/= kwa mwezi kama ilivyotangazwa siku ya uzinduzi unatia huzuni moyoni. Naamini kwamba wanaCCM wa kuchangia hiyo shilingi elfu moja kwa mwezi ni wale Watanzania maskini ambao wengi wao wanabangaiza ili waweze kupata hela ya kula na watoto wao. Kwa kijijini na hata mjini, elfu moja ni hela nyingi. Mimi nilidhani viongozi wa juu wa CCM watawahamasisha 'mabepari na mapapa' walio ndani ya chama hicho ndio wachangie Chama chao na kuwaacha wanachama maskini waendelee kuhangaikia maisha yao, kumbe wanadhamiria kuwakamua hata walalahoi! Ama kweli Ubepari ni Unyama na mwenye shibe hamjui mwenye njaa!
 
kiukweli nashindwa kuelewa yaani ndani ya dk5 wamepata 20m sasa hadi uchaguzi ufike hiyo octoba zitakuwa zimefika kiasi gani??
kama kweli wanauchungu na nchi yao hao wana ccm hizo pesa wanazo changisha zitumike kununua madawa hospitalini, vitanda hospitalini waboreshe hospitali zote zime na vifaa vyote muhimu,amshine za mionzi nk, wajenga zahati kwa wingi, madawati ya watoto zetu hii itatusaidia sie kina tomaso kuamini ni chama chenye uchungu na nchi yao lakini kuchangisha pesa kwa ajili ya kujinufaisha wachache hiyo haijakaa sawa kabisa.
kuna mambo mengi ya kusaidia jamii bila kutegemea wafadhili nje watusaidie, kukodisha ule ukumbi pale mlimanicity ni bei gani, garama ya vyakula na vinywaji vya sikuile ni bei gani, malipo ya posho za wajumbe waliohudhuria nia bei gani bado hujalipia wapambaji na washehereshaji wa shughuli yenyewe nadhani kwa usiku ule tu garama walizo zitumia nia zaidi ya 20m! swali langu ni JE NANI ALIFADHILI ULE UZINDUZI AMA PESA ZA SHUGHULI ILE ZILITOKA WAPI ??
 
Mara nyingi nasoma post zenu wala sizijibu.....kazi yangu kusoma naju yepi hoja za msingi na yepi pumba! Katika hili sikubaliani nanyi. Suala la kukusanya fedha za kampeni kwaajili ya CCM ni jambo jema wala sioni tatizo. Leo hii CHADEMA wakichangisha fedha kwaajili ya kampeni yao na uhakika you dont comments at all badala yake mtasema chama kinajizatiti kupata ushindi! Tatizo la wana JF ni kwamba karibia WOTE ni wapinzani wa chama Tawala CCM! Sijaona hoja yoyote ya msingi katika hili na katika mengine yote yalopita isipokua ni porojo mingi za Waswahili ! Badala ya kujadili issues kama East African Federation na impacts zake mnamjadili JK akikusanya fedha kwa wapiga kura wake ili kuwezesha chama kushinda. Ninyi mngetaka achangishe wapi, kwa nani kama siyo kwa wapenzi wa chama chake? Angeanza tu kampeni bila fund-raising si mtasema kaiba? Acheni TAARAB, Maneno maneno, chokochoko na Uswahili wenye nia ya kuchafuana. Kama mnaweza nanyi changisheni hamnyimwi..lakini yote tisa CCM kitashika tena hatam na mtaongozwa na serikali yake kama kawaida. Nilishasema mimi SIYO mwanachama wa chama chochote cha siasa bali an "OBSERVER". Tafakari!!!!

By the way, who are you hata tujali kama unajibu ama hujibu posts za hapa JF? Kumbuka we are in a free democratic country where freedom of expression is one's constitutional right. Sasa kama michango ya watu humu inakukera just go for a walk! CCM waibe mara ngapi, mbona walishaiba jamani? Au mara hii umeshasahau sakata la EPA?
 
Mara nyingi nasoma post zenu wala sizijibu.....kazi yangu kusoma naju yepi hoja za msingi na yepi pumba! Katika hili sikubaliani nanyi. Suala la kukusanya fedha za kampeni kwaajili ya CCM ni jambo jema wala sioni tatizo. Leo hii CHADEMA wakichangisha fedha kwaajili ya kampeni yao na uhakika you dont comments at all badala yake mtasema chama kinajizatiti kupata ushindi! Tatizo la wana JF ni kwamba karibia WOTE ni wapinzani wa chama Tawala CCM! Sijaona hoja yoyote ya msingi katika hili na katika mengine yote yalopita isipokua ni porojo mingi za Waswahili ! Badala ya kujadili issues kama East African Federation na impacts zake mnamjadili JK akikusanya fedha kwa wapiga kura wake ili kuwezesha chama kushinda. Ninyi mngetaka achangishe wapi, kwa nani kama siyo kwa wapenzi wa chama chake? Angeanza tu kampeni bila fund-raising si mtasema kaiba? Acheni TAARAB, Maneno maneno, chokochoko na Uswahili wenye nia ya kuchafuana. Kama mnaweza nanyi changisheni hamnyimwi..lakini yote tisa CCM kitashika tena hatam na mtaongozwa na serikali yake kama kawaida. Nilishasema mimi SIYO mwanachama wa chama chochote cha siasa bali an "OBSERVER". Tafakari!!!!

Hakuna anayeumizwa na kuchangisha fedha kwaajili ya chama, ISHU INAYOSHANGAZA WANAJAMVI WENGI, NI...KWANINI kutafuta hela kwa walipa kodi (40billion or more) kwaajili ya kuzifanyia kampeni, kununua tisheti na mabango, wakati zingefanya kitu chochote cha maana na cha kudumu ingekuwa credible zaidi!
Ni kitu gani ambacho wananchi watamkumbuka nacho huyu jamaa basi?...au vita ya Comoro?..inatuhusu?

Kwanini asilihusishe taifa zima kuchangisha pesa za kufanya kumbukumbu japo ya kituo cha afya kwa kila kijiji?...au ni-tuponde maisha, kufakwaja?
Wanachi wenyewe, hali ngumu hivyo, unataka hadi 300/=waliyonayo wakupe wewe, ufanye kampeni...this is too acidic!

Sijaelewa unachotetea bwana NALI!
 
Ikiwa tunaweza kujichangisha 20m ndani ya dk5 kwanini tunaomba misaada nje?? hii ni sawa na kujivua nguo hadharani tena TV ya Taifa inaonyehsa live mambo yanavyo kwenda halafu kesho na kesho kuta tunapiga hodi kwa wafadhili kuomba misaada, mbali ya TBC pia walikuwapo Star TV na ITV hizi TV station zote ni zinaonekana ktk mataifa mangapi hapa ulimwenguni???
Nakumbuka ule msemo wa Makamba "nitume mimi bwana"
 
Kwa kweli haya ni mawazo mazuri sana, unfortunately ubinafsi unatutawala sana hadi tunadharau masuala nyeti kama haya. Ila katika serikali kuna wenye mawazo kama haya, shida ni moja tu kwamba hawana mamlaka za maamuzi.
 
Hii injulikana kabisa!...Fundraising hizi zinatumika kama smoke-screen kuwazuga watu, ili waelewe kwamba nccm walichangisha, kumbe vyanzo vyao ni vilevile vya mwaka 2005!Lakini wajanja tushawastukia!Na huyu jamaa wa Push-Mobile ni mdau nini wa filthness inayoendelea kwenye system ya sisiem nini?

Rafiki,
Ishu sio kujua where the catch is,it's what you do with the information.
Now,you have a plan in mind?
 
Back
Top Bottom