Matumizi Mbadala Ya Bilioni 40 za Kampeni CCM!

PakaJimmy

JF-Expert Member
Apr 29, 2009
16,203
8,724
Jana usiku CCM wamezindua kampeni ya kuchangia kampeni kwa kutumia simu za mkononi!

Makadirio ni kwamba watakusanya taslimu 40,000,000,000/=(bilioni 40)!

Mimi nilipotazama jinsi washiriki wale walivyochangamka kutoa kwa kutuma ujumbe, nilihamasika kwamba iwapo ungeanzishwa uchangiaji wa namna hiyo kwaajili ya madawati ya shule zote nchini, hakuna mtoto ambae angekaa kwenye vumbi!

Kama jana, ziliweza kupatikana milioni 20 ndani ya dakika 5 tu za uchangiaji, je kwa miaka 5 ya uongozi wa JK, wananchi wangechanga kiasi gani, na tungekuwa wapi?

Kwanini wabongo tunapenda kufanya fund-raising za 'Disposable cash, kama hizi kampeni, tisheti na harusi, unlike kuwekeza kwenye investment za kudumu kama elimu, afya na miundombinu?

Ningekuwa mimi ndo JK, ningesubiri hela yote hiyo ichangwe, kisha natangaza ghafla kwamba hakutakuwa na kampeni, hela zote zinatumika kupeleka maji, au kujenga dispensari vijijini!

NINA HAKIKA 100% KWAMBA CHAMA CHANGU KINGECHAGULIWA BILA KUPINGWA NA RAIA YEYOTE...Unaonaje?
 
Naamini unamuongelea JK mwingine mwenye akili timamu huyo wetu hapana wanataka cash iwe rahisi kuziiba mara moja sasa kamati ya uenyekiti wa Zakia Meghji aliyeshindwa kabisa kabisa kazi ya kulinda fedha zenye uangalizi kama wa central bank unampa funguo tena? ni mpaka watanzania tutakapofia mitaani kwa risasi za moto ndio kama ya juzi huko wapi sijui ndio solution ya huo upumbavu tunaoulea.
 
Waheshimiwa, jana CCM ilizindua kampeni ya uchangiaji kwa wanaachama na wakereketwa kama wanavyojiita niliangalia lakini kuna kitu hapa tuchangieni:

Mwenyekiti wa taifa CCM kwa kusisitiza uchangiaji alisema

Jamani tuichangieni CCM, tukukumbuke chama hiki kilivyoifanyia nchi hii. Je? Wanajamvi bila CCM nchi hii haingekua hapa? Au ingekua mbali zaidi? Na je ni CCM imeifanyia Nchi mambo mazuri au Inchi ndio imeifanyia CCM kua hapo?

Karibuni.
 
Jana usiku CCM wamezindua kampeni ya kuchangia kampeni kwa kutumia simu za mkononi!

Makadirio ni kwamba watakusanya taslimu 40,000,000,000/=(bilioni 40)!

Mimi nilipotazama jinsi washiriki wale walivyochangamka kutoa kwa kutuma ujumbe, nilihamasika kwamba iwapo ungeanzishwa uchangiaji wa namna hiyo kwaajili ya madawati ya shule zote nchini, hakuna mtoto ambae angekaa kwenye vumbi!

Kama jana, ziliweza kupatikana milioni 20 ndani ya dakika 5 tu za uchangiaji, je kwa miaka 5 ya uongozi wa JK, wananchi wangechanga kiasi gani, na tungekuwa wapi?

Kwanini wabongo tunapenda kufanya fund-raising za 'Disposable cash, kama hizi kampeni, tisheti na harusi, unlike kuwekeza kwenye investment za kudumu kama elimu, afya na miundombinu?

Ningekuwa mimi ndo JK, ningesubiri hela yote hiyo ichangwe, kisha natangaza ghafla kwamba hakutakuwa na kampeni, hela zote zinatumika kupeleka maji, au kujenga dispensari vijijini!

NINA HAKIKA 100% KWAMBA CHAMA CHANGU KINGECHAGULIWA BILA KUPINGWA NA RAIA YEYOTE...Unaonaje?

Wazo limekwenda shule hili lakini la kujiuliza ni je, JK huyu na CCM yake wana akili kma hizo?
 
Jana usiku CCM wamezindua kampeni ya kuchangia kampeni kwa kutumia simu za mkononi!

Makadirio ni kwamba watakusanya taslimu 40,000,000,000/=(bilioni 40)!

Mimi nilipotazama jinsi washiriki wale walivyochangamka kutoa kwa kutuma ujumbe, nilihamasika kwamba iwapo ungeanzishwa uchangiaji wa namna hiyo kwaajili ya madawati ya shule zote nchini, hakuna mtoto ambae angekaa kwenye vumbi!

Kama jana, ziliweza kupatikana milioni 20 ndani ya dakika 5 tu za uchangiaji, je kwa miaka 5 ya uongozi wa JK, wananchi wangechanga kiasi gani, na tungekuwa wapi?

Kwanini wabongo tunapenda kufanya fund-raising za 'Disposable cash, kama hizi kampeni, tisheti na harusi, unlike kuwekeza kwenye investment za kudumu kama elimu, afya na miundombinu?

Ningekuwa mimi ndo JK, ningesubiri hela yote hiyo ichangwe, kisha natangaza ghafla kwamba hakutakuwa na kampeni, hela zote zinatumika kupeleka maji, au kujenga dispensari vijijini!

NINA HAKIKA 100% KWAMBA CHAMA CHANGU KINGECHAGULIWA BILA KUPINGWA NA RAIA YEYOTE...Unaonaje?


Mkuu PakaJimmy nakubaliana kabisa na wewe kwamba kampeni kama hii ya kuichangia CCM ingeanzishwa ili kukusanya pesa za madawati na hata majengo ya madarasa basi shule zetu nyingi nchini za msingi na sekondari zingekuwa katika hali ya kuridhisha sana na hakuna mtoto ambaye angekaa chini au hata kukosa vitabu vya shule. Tatizo lilikuwepo ni kwamba Viongozi wetu hawana hamasa kabisa ya kupambana na tatizo hili sugu miaka nenda miaka rudi na hivyo hawalipi kipaumbele kama wanavyotoa kipaumbele kwa kuchaguliwa kwao na Wabunge toka chama chao. Hali hii inasikitisha sana lakini ndiyo ukweli halisi wa mambo.

Ikija kwenye michango ya Vipaimara, Harusi n.k. huko ndiyo wala sitaki kuangalia kabisa maana ni kama watu wanachangia kwa sifa huyu akitoa laki basi mimi nitoe laki moja na nusu na yule mwingine atataka kutoa laki mbili. Ukiwaambia watu hawa tuchangie katika mambo ya maendeleo kama kusafisha labda hata katika eneo tunaloishi ili kulisafisha na kupanda maua au kuna shule ya jirani ambayo ina hali mbaya inahitaji matengenezo basi wote huingia mitini, bado Watanzania tuna mentality za ajabu sana katika kujiletea maendeleo wenyewe mpaka hapo tutakapbadilisha mentality hizi zilizokaa kinyumenyume nchi yetu itabaki nyuma sana kimaendeleo.
 
mwerevu huangaria sana atokako

yuko wapi

anakwenda wapi, bali mjinga huangalia sana alipo

vipi mawazo kama ya PakaJimmy yangekuwa yamo vichwani mwa

viongozi wetu? kweli taifa lingesonga mbele, Eeee Mungu Baba tusaidie

asante PakaJimmy kwa mawazo mazuri, nakubariana nawe kwa 100%
 
Wanaochangiwa pesa hiyo kwani ni sisi M? au ni wahuni wachache wanaojiita sisi M?

Kwa kadri ninavyojua mimi sisi M ilishakufa na Nyerere na sasa kuna kikundi cha wahuni fulani wameamua kutumia dola kwa kujiita sisi M.

Lakini ndugu zangu huyo sisi M mwenyewe alishakufa zamaaaaaani.

Ukimtaka anayejiita sisi M leo wewe nenda kwa wanaojiita makada ambao ni Usalama wa wezi a.k.a.usalama wa taifa, Polisi, katibu kata/tarafa, tume ya uchaguzi, wakuu wa mikoa na wilaya, wakurugenzi wa wilaya... unaweza ongeza orodha utakavyo, hao ndio sisi M wenyewe lakini chama kama chama kilishakufa mwe!
 
Naomba sehemu ya pesa zinazochangwa zitumike kumpeleka mwenyekiti wa CCM kupimwa akili na ikiwezekana asigombee tena maana hana la manufaa kwa nji yetu!
 
Good strategy!
Wanajua wasipochangisha hela za kampeni,mtasema wamewaibia tena kutoka benki kuu yenu.
 
Hata ungechanga $40 billion kwa madawati, bado asilimia kubwa ya wanafunzi wataendelea kukaa kwenye vumbi tuu hadi kiama...think about that!
 
Lets be critical for a minute..tuache kuchonga kaa wanasiasa.

Hivi unaezaje kupinga kuchangishana hela ya kampeni wakati unakubaliana na mfumo wa siasa uliopo.

This is open contradiction to me.
 
cripple minded............leaders,the main motive here, is self-advancement and these methods are unscrupulous!!!!!!
 
They just want to justify dirty monies from somewhere.... mie naona watz tunapigwa changa la macho lakini CAG yupo atatuarifu baadaye
 
They just want to justify dirty monies from somewhere.... mie naona watz tunapigwa changa la macho lakini CAG yupo atatuarifu baadaye

Ha ha ha..nilikuwa na mawazo kama yako.

Nadhani suala hili lipo wazi, and guess what, pesa zitachotwa mahali, halafu watapewa Voda ya King Maker au any other collaborator halafu mtaambiwa zimechangwa na waTz kupitia sms..lol

..Mazingaombwe njoo utamu kolea! LMFAO
 
Shule nyingi za serikali hata vyoo hazina na kuna shule nyingi ukipita unakuta choo cha watoto kimeandikwa "choo hiki kimejengwa kwa msaada wa walipa kodi wa Japan". Unafikiri fedha za kufanya hayo hazipo? Fedha zipo; wanagawana hawa watu na vizazi vyao na marafiki zao. Fundraising kama hizo wakizifanya kwa ajili ya kujenga madarasa, kuweka madawati, kujenga vyoo vya shule, n.k. tutawauliza; na fedha za kodi mmeweka wapi?

Hapa wana kisingizio cha kusema hawaruhusiwi kuchota kwenye mifuko ya kodi. Ingawa fedha itakuwa hiyo hiyo ila itazunguka tu kwa kutumia mlango wa nyuma. Hakuna watanzania walioko tayari kuichangia CCM bilioni arobaini isipokuwa wale walio sehemu ya uozo unaofanywa na CCM. Hawa watachota huko kwa posho za mara mbili mbili, safari na semina uchwara, malipo kwa kazi hewa, n.k. halafu watazihamishia kwenye mfuko wa kampeni kwa madai kuwa wamechangia.

Halafu nani ata audit nani amechangia nini? Kuna wale ambao wakichangia wanataka wajulikane ili mkuuu wa nchi awaone kuwa wamechangia. Hawa hawawezi kutumia utaratibu huu ambao hauwapi fulsa ya kuonekana wametoa ngapi! Kwa hiyo njia pekee ya kuzipata fedha hizo ni kwa kundi lile linalokula Maposho parallel kutunga vikao na kulipana hayo maposho na hizo fedha kuzunguka na kuingia kwenye mfuko huo wa kampeni.
 
Shule nyingi za serikali hata vyoo hazina na kuna shule nyingi ukipita unakuta choo cha watoto kimeandikwa "choo hiki kimejengwa kwa msaada wa walipa kodi wa Japan". Unafikiri fedha za kufanya hayo hazipo? Fedha zipo; wanagawana hawa watu na vizazi vyao na marafiki zao. Fundraising kama hizo wakizifanya kwa ajili ya kujenga madarasa, kuweka madawati, kujenga vyoo vya shule, n.k. tutawauliza; na fedha za kodi mmeweka wapi?

Hapa wana kisingizio cha kusema hawaruhusiwi kuchota kwenye mifuko ya kodi. Ingawa fedha itakuwa hiyo hiyo ila itazunguka tu kwa kutumia mlango wa nyuma. Hakuna watanzania walioko tayari kuichangia CCM bilioni arobaini isipokuwa wale walio sehemu ya uozo unaofanywa na CCM. Hawa watachota huko kwa posho za mara mbili mbili, safari na semina uchwara, malipo kwa kazi hewa, n.k. halafu watazihamishia kwenye mfuko wa kampeni kwa madai kuwa wamechangia.

Halafu nani ata audit nani amechangia nini? Kuna wale ambao wakichangia wanataka wajulikane ili mkuuu wa nchi awaone kuwa wamechangia. Hawa hawawezi kutumia utaratibu huu ambao hauwapi fulsa ya kuonekana wametoa ngapi! Kwa hiyo njia pekee ya kuzipata fedha hizo ni kwa kundi lile linalokula Maposho parallel kutunga vikao na kulipana hayo maposho na hizo fedha kuzunguka na kuingia kwenye mfuko huo wa kampeni.


This time hawapendi akina Manji, Somaia, RA, Karamagi, Vallambhia, Jeetu...plus other rubbish wajulikane kuwa ndio waliochanga kwani itawaweka wazi kuwa wana ndoa na mafisadi lakini kwa vile tena wanahitaji msaada wao ili washinde uchaguzi basi wamebuni njia muafaka ya kupokea pesa zao toka mlango wa nyuma na hao jamaa piga ua , garagaza, biduabidua lazima watatoa pesa kulinda ufisadi wao, unafikiri hawajui hasira za watanzania?
 
Lets be critical for a minute..tuache kuchonga kaa wanasiasa.

Hivi unaezaje kupinga kuchangishana hela ya kampeni wakati unakubaliana na mfumo wa siasa uliopo.

This is open contradiction to me.

Nani anaekubaliana nao?...Ni kwamba ndo uliopo...labda kwasasa tuseme kwa kifupi kabisa kuwa ni "'whether we like or not"...Of course kuna mawazo mbadala bana...kuna CCJ!
 
Nani anaekubaliana nao?...Ni kwamba ndo uliopo...labda kwasasa tuseme kwa kifupi kabisa kuwa ni "'whether we like or not"...Of course kuna mawazo mbadala bana...kuna CCJ!

Siongelei kukubaliana na CCM naongelea kukubaliana na mfumo wa kisiasa wa sasa, uliopo in practice. Mojawapo ya requirement ya mfumo wa sasa ni kufanya uchaguzi ili kueka 'masultan' kisheria mahali pao palipoinuka. Sasa huezi ukakubali mfumo wa uchaguzi na ukadhani uchaguzi utafanyika bila pesa kukusanywa.
 
Good strategy!
Wanajua wasipochangisha hela za kampeni,mtasema wamewaibia tena kutoka benki kuu yenu.

Hii injulikana kabisa!...Fundraising hizi zinatumika kama smoke-screen kuwazuga watu, ili waelewe kwamba nccm walichangisha, kumbe vyanzo vyao ni vilevile vya mwaka 2005!Lakini wajanja tushawastukia!Na huyu jamaa wa Push-Mobile ni mdau nini wa filthness inayoendelea kwenye system ya sisiem nini?
 
Wanasiasa hawawezi kuwakumbuka Wanafunzi, Manesi au Madaktari.
Fedha nyingi ya kodi inaelekezwa katika ununuzi wa magari ya kifahari na samani za
maofisi sisizo na viwango hawajali kuhusu madawati kwani watoto wao wengi wanasomea
katika shule za binafsi.
 
Back
Top Bottom