abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
ZITTO KABWE:
Matumaini mapya yameanza kuchomoza
Zitto Kabwe
Toleo la 240
23 May 2012
JUMATATU hii ya Mei 21, nimeanza ziara yangu ya mafunzo hapa Uholanzi pamoja na wabunge wenzangu pamoja na Katibu wa Kamati ya Bunge. Wabunge wenzangu Nasir wa Korogwe, Kafulila wa Kigoma Kusini na Sarah Msafiri kutoka Morogoro wameungana nami katika ziara hii.
Malengo ya ziara yetu ya mafunzo ni kuhusu masuala ya mafuta na gesi. Wizara ya Mambo ya Nje ya Uholanzi kupitia ofisi ya Mambo ya Nje ya Tanzania wameongeza idadi ya wabunge katika ziara hii kutoka wabunge wawili walioonekana kudhamiria kujua sekta ya mafuta na gesi (ambao ni mimi na Januari Makamba). Lakini Januari ameteuliwa kuwa naibu waziri, hayupo kwenye ziara hii.
Jopo letu hili limepata muhtasari kuhusu sekta ya mafuta na gesi hapa Uholanzi, tumeelezwa kwa jinsi gani leseni za uchimbaji mafuta zinatolewa na mapato yanavyokusanywa kwa uadilifu. Tumeelezwa kwamba Serikali ya Uholanzi hukusanya jumla ya Euro bilioni 11 (zaidi ya trilioni 22 za Tanzania, zaidi ya bajeti ya Tanzania ya trilioni 14) kama mapato kutokana na sekta hii ya mafuta na gesi.
Wanakusanya takriban asilimia 85 ya mapato ya jumla kutoka katika mafuta na gesi, katika eneo la Groningen (ambalo ni kubwa zaidi barani Ulaya).
Kutoka katika pato hilo, asilimia 45 ni kodi inayokusanywa kutoka katika kampuni za gesi na mafuta (kati ya kampuni kubwa zaidi ni Shell na ExxonMobil) na asilimia 40 kutoka katika ile ya asilimia 85 ni kodi na gawiwo kutoka katika kampuni ya Serikali ya gesi na mafuta ya EBN.
Kutoka katika maeneo mengine ukiachilia mbali Groningen, Uholanzi hukusanya asilimia kati ya 40 na 65 ya mapato. Katika leseni zote isipokuwa zile za zamani tu, nchi hii imekuwa na hisa katika kampuni mbalimbali za mafuta na gesi.
Hapa Uholanzi hakuna mikataba kama ile tuliyozoea Tanzania (yaani Production Sharing System - PSA) kwamba kampuni husika katika uwekezaji ndizo wakandarasi wakubwa. Faida kubwa ya mfumo wa PSA ni kwamba nchi inabaki kuendelea kuwa mmiliki wa rasilimali.
Hata hivyo, katika mifumo hii iwe huu wa PSA wa Tanzania au huu wa hapa Uholanzi mambo muhimu zaidi ni uwazi na uwajibikaji katika sekta nzima.
Tulikutana na Naibu Waziri Mkuu, MaximeVerhagen. Nimewasilisha salamu zetu za dhati kwake kwamba tungependa ushirikiano huu kati ya nchi zetu uendelee kudumu. Ni ushirikiano wenye tija kubwa sana kwa nchi hizi mbili.
Nilimkumbusha kuhusu hazina yetu kubwa ya gesi iliyovumbuliwa ikiwa ni pamoja na uvumbuzi wa visima vitano vilivyoko chini ya kampuni za Kiingereza ya British Gas, kisima kimoja cha kampuni ya StatOil na visima vingine vidogo vya Songosongo, MnaziBay, Mkuranga na Nyuni, wilayani Kilwa.
Nilimweleza Naibu Waziri Mkuu kuhusu dhamira yetu ya kuiona Tanzania kuwa moja ya nchi za Afrika ambayo utajiri wake unanufaisha wananchi wake. Nimemweleza katika utambulisho wangu kuwa; Baadhi ya viongozi vijana Tanzania tumedhamiria kupandikiza matumaini mapya katikati ya dimbwi la msongo wa mawazo miongoni mwa vijana wenzetu.
Kwamba inawezekana kwa nchi za Afrika kuwa tajiri kutokana na gesi na mafuta, sambamba na kuwapo kwa ustawi bora wa utawala na demokrasia. Hiyo inawezekana kwa kutumia vizuri rasilimali za nchi.
Kwamba hatutaki kurudia makosa yaw engine (kama nchi za Nigeria inayopoteza mabilioni ya fedha katika uvunaji mafuta) na hata makosa yetu wenyewe katika sekta ya madini. Na kama makosa yakifanyika, basi yawe makosa mapya si kurudia ya zamani.
Waziri Mkuu alituahidi kuwa tayari kusaidia maendeleo ya sekta ndogo ya gesi nchini Tanzania na hasa kwa upande wa maendeleo ya rasilimali watu. Ajenda hiyo ilijadiliwa zaidi katika Wizara ya Mambo ya Nje na ikakubaliwa kuwapo kwa ufadhili kwa wanafunzi kutoka Tanzania kwa ajili ya kusomea masuala ya mafuta na gesi ili nchi iweze kuwa na watalaamu wa kutosha katika sekta hiyo.
Alipendekeza kwamba Tanzania itumie mapato ya gesi kutengeneza miundombinu, sambamba na deni la taifa kwa maslahi ya vizazi vijavyo. Alielezea nia ya Uholanzi kuwa kitovu cha uzalishaji gesi barani Ulaya.
Ziara yetu inaendelea kwa mujibu wa ratiba. Tumedhamiria kujifunza na kile tulichojifunza na tutakachojifunza tutakipenyeza katika sera yetu mpya ya gesi nchini na katika mpango mkuu kuhusu gesi (Gas Master Plan).
Nina matumaini makubwa tutafanikiwa kama taifa licha ya msongo mkubwa wa mawazo unaowazonga wananchi wetu. Lazima tujenge nchi tunayoitaka.
Matumaini mapya yameanza kuchomoza
Zitto Kabwe
Toleo la 240
23 May 2012
JUMATATU hii ya Mei 21, nimeanza ziara yangu ya mafunzo hapa Uholanzi pamoja na wabunge wenzangu pamoja na Katibu wa Kamati ya Bunge. Wabunge wenzangu Nasir wa Korogwe, Kafulila wa Kigoma Kusini na Sarah Msafiri kutoka Morogoro wameungana nami katika ziara hii.
Malengo ya ziara yetu ya mafunzo ni kuhusu masuala ya mafuta na gesi. Wizara ya Mambo ya Nje ya Uholanzi kupitia ofisi ya Mambo ya Nje ya Tanzania wameongeza idadi ya wabunge katika ziara hii kutoka wabunge wawili walioonekana kudhamiria kujua sekta ya mafuta na gesi (ambao ni mimi na Januari Makamba). Lakini Januari ameteuliwa kuwa naibu waziri, hayupo kwenye ziara hii.
Jopo letu hili limepata muhtasari kuhusu sekta ya mafuta na gesi hapa Uholanzi, tumeelezwa kwa jinsi gani leseni za uchimbaji mafuta zinatolewa na mapato yanavyokusanywa kwa uadilifu. Tumeelezwa kwamba Serikali ya Uholanzi hukusanya jumla ya Euro bilioni 11 (zaidi ya trilioni 22 za Tanzania, zaidi ya bajeti ya Tanzania ya trilioni 14) kama mapato kutokana na sekta hii ya mafuta na gesi.
Wanakusanya takriban asilimia 85 ya mapato ya jumla kutoka katika mafuta na gesi, katika eneo la Groningen (ambalo ni kubwa zaidi barani Ulaya).
Kutoka katika pato hilo, asilimia 45 ni kodi inayokusanywa kutoka katika kampuni za gesi na mafuta (kati ya kampuni kubwa zaidi ni Shell na ExxonMobil) na asilimia 40 kutoka katika ile ya asilimia 85 ni kodi na gawiwo kutoka katika kampuni ya Serikali ya gesi na mafuta ya EBN.
Kutoka katika maeneo mengine ukiachilia mbali Groningen, Uholanzi hukusanya asilimia kati ya 40 na 65 ya mapato. Katika leseni zote isipokuwa zile za zamani tu, nchi hii imekuwa na hisa katika kampuni mbalimbali za mafuta na gesi.
Hapa Uholanzi hakuna mikataba kama ile tuliyozoea Tanzania (yaani Production Sharing System - PSA) kwamba kampuni husika katika uwekezaji ndizo wakandarasi wakubwa. Faida kubwa ya mfumo wa PSA ni kwamba nchi inabaki kuendelea kuwa mmiliki wa rasilimali.
Hata hivyo, katika mifumo hii iwe huu wa PSA wa Tanzania au huu wa hapa Uholanzi mambo muhimu zaidi ni uwazi na uwajibikaji katika sekta nzima.
Tulikutana na Naibu Waziri Mkuu, MaximeVerhagen. Nimewasilisha salamu zetu za dhati kwake kwamba tungependa ushirikiano huu kati ya nchi zetu uendelee kudumu. Ni ushirikiano wenye tija kubwa sana kwa nchi hizi mbili.
Nilimkumbusha kuhusu hazina yetu kubwa ya gesi iliyovumbuliwa ikiwa ni pamoja na uvumbuzi wa visima vitano vilivyoko chini ya kampuni za Kiingereza ya British Gas, kisima kimoja cha kampuni ya StatOil na visima vingine vidogo vya Songosongo, MnaziBay, Mkuranga na Nyuni, wilayani Kilwa.
Nilimweleza Naibu Waziri Mkuu kuhusu dhamira yetu ya kuiona Tanzania kuwa moja ya nchi za Afrika ambayo utajiri wake unanufaisha wananchi wake. Nimemweleza katika utambulisho wangu kuwa; Baadhi ya viongozi vijana Tanzania tumedhamiria kupandikiza matumaini mapya katikati ya dimbwi la msongo wa mawazo miongoni mwa vijana wenzetu.
Kwamba inawezekana kwa nchi za Afrika kuwa tajiri kutokana na gesi na mafuta, sambamba na kuwapo kwa ustawi bora wa utawala na demokrasia. Hiyo inawezekana kwa kutumia vizuri rasilimali za nchi.
Kwamba hatutaki kurudia makosa yaw engine (kama nchi za Nigeria inayopoteza mabilioni ya fedha katika uvunaji mafuta) na hata makosa yetu wenyewe katika sekta ya madini. Na kama makosa yakifanyika, basi yawe makosa mapya si kurudia ya zamani.
Waziri Mkuu alituahidi kuwa tayari kusaidia maendeleo ya sekta ndogo ya gesi nchini Tanzania na hasa kwa upande wa maendeleo ya rasilimali watu. Ajenda hiyo ilijadiliwa zaidi katika Wizara ya Mambo ya Nje na ikakubaliwa kuwapo kwa ufadhili kwa wanafunzi kutoka Tanzania kwa ajili ya kusomea masuala ya mafuta na gesi ili nchi iweze kuwa na watalaamu wa kutosha katika sekta hiyo.
Alipendekeza kwamba Tanzania itumie mapato ya gesi kutengeneza miundombinu, sambamba na deni la taifa kwa maslahi ya vizazi vijavyo. Alielezea nia ya Uholanzi kuwa kitovu cha uzalishaji gesi barani Ulaya.
Ziara yetu inaendelea kwa mujibu wa ratiba. Tumedhamiria kujifunza na kile tulichojifunza na tutakachojifunza tutakipenyeza katika sera yetu mpya ya gesi nchini na katika mpango mkuu kuhusu gesi (Gas Master Plan).
Nina matumaini makubwa tutafanikiwa kama taifa licha ya msongo mkubwa wa mawazo unaowazonga wananchi wetu. Lazima tujenge nchi tunayoitaka.