Matukio ya kukumbukwa katika mwaka 2008

Balantanda

JF-Expert Member
Jul 13, 2008
12,476
4,752
Heshima mbele wakuu,mwaka 2008 ndo huoooo unakaribia kuisha,ni vema tukatumia nafasi hii kujikumbusha baadhi ya matukio ya kusisimua(ndani na nje ya Tanzania) ambayo yalitokea kwa mwaka 2008 na daima yatakuwa yakukumbukwa...

Mimi kwa kuanzia nina matukio takribani matano(05) kama ifuatavyo:-1.Mchakato wa uchaguzi wa Rais wa Marekani(hasa ndani ya chama cha Democrats) ambao ulimalizika kwa Barack Hussein Obama kuweka historia kwa kuwa Mmarekani mweusi wa kwanza kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani....2.Kitendo cha baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi wa fedha za EPA kufikishwa mahakamani na kuachiwa kwa dhamana baada ya muda mfupi....3.Kitendo cha mawaziri wastaafu waandamizi BASIL PESAMBILI MRAMBA,DANIEL YONA na aliyekuwa katibu mkuu GRAY MGONJA kufikishwa mahakamani kwa kosa la kutumia vibaya madaraka yao na kuliingizia taifa hasara na kuachiwa kwa dhamana....4.Timu yetu ya Taifa ya mpira wa miguu(Taifa Stars) kupata tiketi kushiriki mashindano ya CHAN huko Ivory Coast mwezi February,2009....na tukio la mwisho kwangu kulikumbuka ni kitendo cha EDWARD NGOYAI LOWASSA kujiuzulu kuwa PM baada ya kutuhumiwa kujihusisha na mambo ya Ze Richmond...Ni hayo tu wakuu,tukumbushane mengine basi
 
Last edited by a moderator:
Heshima mbele wakuu,mwaka 2008 ndo huoooo unakaribia kuisha,ni vema tukatumia nafasi hii kujikumbusha baadhi ya matukio ya kusisimua(ndani na nje ya Tanzania) ambayo yalitokea kwa mwaka 2008 na daima yatakuwa yakukumbukwa.

Mods naomba hii iunganishwe na hiyo nyingine hapo juu yenye heading sawa na hii
 
Mimi yangu kali kuliko zote ni ya Rais kumfukuza aliyekuwa Gavana wa Benki kuu ambaye alikuwa ameandika barua ya kujiuzulu. Sijawahi kusikia katika dunia hii mtu aliyeandika barua ya kujiuzulu akifukuzwa kazi. Nadhani hiyo itaingia kwenye guiness book.
 
Tukio kubwa la kukumbukwa ni kiini macho tunachofanyiwa watanzania katika hiki kinachoitwa vita dhidi ya ufisadi
 
Heshima mbele wakuu,mwaka 2008 ndo huoooo unakaribia kuisha,ni vema tukatumia nafasi hii kujikumbusha baadhi ya matukio ya kusisimua(ndani na nje ya Tanzania) ambayo yalitokea kwa mwaka 2008 na daima yatakuwa yakukumbukwa...

Mimi kwa kuanzia nina matukio takribani matano(05) kama ifuatavyo:-
1.Mchakato wa uchaguzi wa Rais wa Marekani(hasa ndani ya chama cha Democrats) ambao ulimalizika kwa Barack Hussein Obama kuchaguliwa kuwa Rais wa Marekani....
2.Kitendo cha baadhi ya watuhumiwa wa ufisadi wa fedha za EPA kufikishwa mahakamani na kuachiwa kwa dhamana baada ya muda mfupi....
3.Kitendo cha mawaziri wastaafu waandamizi BASIL PESAMBILI MRAMBA,DANIEL YONA na aliyekuwa katibu mkuu GRAY MGONJA kufikishwa mahakamani kwa kosa la kutumia vibaya madaraka yao na kuliingizia taifa hasara na kuachiwa kwa dhamana....
4.Timu yetu ya Taifa ya mpira wa miguu(Taifa Stars) kupata tiketi kushiriki mashindano ya CHAN huko Ivory Coast mwezi February,2009....
na tukio la mwisho kwangu kulikumbuka ni kitendo cha EDWARD NGOYAI LOWASSA kujiuzulu kuwa PM baada ya kutuhumiwa kujihusisha na mambo ya Ze Richmond...Ni hayo tu wakuu,tukumbushane mengine basi

Bwana Balantanda, asante sana kwa kumbusho la mwaka 2008.
Mimi ningeweka
-la mzee Ngoyai Lowassa na Richmond la kwanza
-la mzee wa nyasi Basil Mramba , Yona na Mgonja la pili
-la Jeetu Patel,"the untouchable" na wadau wa EPA, la tatu

Lakini twasubiri kufungua mwaka 2009 kwa Kagoda issues.
 
Kubwa ninalolikumbuka mwaka 2008 ni watu wanaotaka kutajirika kupitia viungo vya maalbino. Kuanzia hao waganga, watafutao utajiri mpaka wale wanaoenda kuua ama kukata viungo vya Albino. Kwa akili ndogo tu, hivi hawa jamaa wote wanaoshiriki katika matendo haya wakijaaliwa kupata mtoto Albino watakimbilia kumkata viungo ama watafanya nini?. Jaribu kufikiri mfanya biashara atafutae kiungo cha albino, ama mganga, akarudi nyumbani akaambiwa "Hongera umepata mtoto", kuangalia ni Albino atafanyaje?.
 
Jamani mie sijui vipi? iliyo niacha hooi ni Raisi wa nchi kusema ukitaka kula lazima uliwe!! na kuirudia rudia hadi kila mtu akaelewa kuwa ni tusi! ilhali watanzania nchi nzima wanampata live! na bila soni akamalizia,..... "ehe,ehe tehe...shekhe sina maana hiyo"
 
Pia nakumbuka tukio la Yanga kugomea mchezo na Simba katika mashindano ya klabu bingwa ya CECAFA
 
Mimi yangu kali kuliko zote ni ya Rais kumfukuza aliyekuwa Gavana wa Benki kuu ambaye alikuwa ameandika barua ya kujiuzulu. Sijawahi kusikia katika dunia hii mtu aliyeandika barua ya kujiuzulu akifukuzwa kazi. Nadhani hiyo itaingia kwenye guiness book.

Huenda ikawa inahusiana na mambo ya mafao Sijui sheria au taratibu za kujiuzuru ( sp) na kuachishwa kazi zikoje, lakini mara nyingi ukiachishwa kazi hupati marupurupu yote.
 
Kitendo cha serikali kumuachia Gavana Balali muda wote aliokuwa nchini hata alipokuwa U.S.A bila kumhoji kuhusu kashfa ya EPA.

Kitendo cha serikali/mahakama kumuachia fisadi wa RADAR Vithlani kuweza kutoroka nchini na baadae kutoa international arrest warrant through interpol.
 
Jamani mie sijui vipi? iliyo niacha hooi ni Raisi wa nchi kusema ukitaka kula lazima uliwe!! na kuirudia rudia hadi kila mtu akaelewa kuwa ni tusi! ilhali watanzania nchi nzima wanampata live! na bila soni akamalizia,..... "ehe,ehe tehe...shekhe sina maana hiyo"

Duu?? aliimwaga wapi hiyo mkuu? sikuipata hiyo..
 
Sitasahau rais alivyopopolewa na mawe kule mbeya. Naomba 2009 tuwe ngangari zaidi ili wajue hapendi matendo yao.
 
....Richmond,EPA,Kagodas,Wangwe's death, Uchaguzi Tarime, ATCL's saga

-Wizi/Kuvuja kwa mitihani ya Kidato cha nne ndani na nje ya NECTA
-Kufungwa kwa baadhi ya shule za sekondari (Form 6) siku chache kabla ya mitihani ya mwisho kwa sababu ya ukosefu wa chakula. Wamefunga likizo ndefu badala ya fupi kwa ajili ya sikukuu hadi 6/2/2009 siku mbili kabla ya mitihani kuanza.
 
Anaejiuzulu huondoka na hadhi ya uwajibikaji. Anaefukuzwa hupoteza hadhi hiyo na huwa amedhalilishwa kiasifulani. Ongezea viatu alivyovurumishiwa George W Bush.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom