boma2000
JF-Expert Member
- Oct 18, 2009
- 3,280
- 310
JF,
Kama ulifuatilia kulikuwa na habari kwenye magaze wiki iliyopita, yakidai kuwa "wafanyakazi wa Air Tanzania" hawaitaki Menejimenti na wameishauri Serikali iondoe menejimenti haraka!
Wasijue kuwa hawana wadhifa wa kuiamuru Serikali wala hawajui mipango ya Serikali juhudi zao ziligonga mwamba baada ya Waziri kujibu bayana kuwa "Too early to phase out ATC's Management"
Wazushi hao walifadhaika sana na sasa wameibukia kwenye JF kumwaga uzushi wao na sumu> Hawa ni watu hatari sana, na anayetaka ukweli akaulize kama mke wa Mattaka anania ya kuanzisha Bureau De Change.
Ushauri wangu wa bure kwao inaonyesha dhahiri walivyo na chuki binafsi! Wana mufilis wa mawazo mapya na wengi wao ni wazembe walio changia kulifikisha shirika hapa lilipo! na kwamba hata ikija Menejimenti gani vigogo vizee hivyo vitaendelea kuwa kikwazo cha maendeleo ya Kampuni, wengi wao ni wazee waliokwisha kata tamaa ya kimaisha na hawana muelekeo.
Ni vyema wakaeleza ukweli watu wajue, kuliko kupotosha umma eti na Breaking News Feki" Nawashauri wajitahidi kuboresha maisha yao na kuacha kupika majungu kila kukicha! Tuleteeni habari zenye kina na mizania hapa ni JF bwana sio kijiwe cha wazushi wazee!!!
Wewe ni Mattaka, pia tunakujua kuwa wewe ni