Bakari Maligwa
Member
- Aug 18, 2010
- 65
- 22
...Nadhani ipo haja sasa kwa wapanga-sera na au wataalamu wa kada ya elimu na taaluma kuketi na kufanya uamuzi mgumu juu ya sera ya elimu Tanzania. Elimu ya Tanzania inakwenda segemnege na shelabela huku waliyesoma zamani wakibaki wakiduwaa! Matokeo ya kidato cha nne 2010 ni kielelezo tosha kwa jinsi sera na au mipango mibovu ilivyozaa asilmia 49.6 ya wanafunzi waliyofeli..na hata kufanya asilmia 80 ya watahiniwa wa 2010 kupata daraja la IV na SIFURI (0). Uchunguzi wangu wa haraka unaonesha kwamba sababu kubwa za kufeli kwa watahainiwa wengi ni:
USHAURI:
TAHADHARI: TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA!
- Ukosefu wa umadhubuti wa sera na mipango mikakati ya elimu ya Tanzania;
- Ukosefu wa wataalamu (walimu) wa kutosha kufundisha masomo maalumu na ya ziada;
- Ukosefu wa weledi kwa baadhi ya walimu wanaoajiriwa sasa (hususan wa vodafasta);
- Kukosekana kwa ari na moya wa kujitolea kwa walimu na wafanyakazi wengine katika sekta ya elimu nchini;
- Ukosefu wa dhana za kufundishia na au vifaa vya kujifunzia;
- Ukosefu na au upungufu wa vitabu vya kiada na au ziada kwa shule nyingi za serikali;
- Ukosefu wa maabara na vifaa vya sayansi (kemia, elimu ya viumbe na fizikia) kwa shule nyingi za serikali;
- Shule za kata kuendeshwa kisiasa badala ya utaalam na ualimu;
- Wanafunzi kukosa juhudi, nmaarifa na nidhamu ya kujifunza na kufundishika;
- Mahusiano mabovu baina ya ushirikiano pande-tatu (waalimu + wazazi + wanafunzi); na
- Serikali kushindwa kuwekeza kwenye rasilimali watu wa kutosha wenye tija na maslahi mazuri ya mishahara na mazingira mazuri ya kufundishia.
USHAURI:
- serikali iache siasa kwenye taaluma
- serikali ichukue hatua za makusudi kurekebisha hali hii kinyume chake miaka ijayo, yaani, 2011 hadi 2015 tutashuhudia wimbi kubwa la wahitimu kufeli mitihani ya kidato cha nne na hata cha sita na vyuo kadhalika
- serikali ichukue hatua za makusudi kuanzisha mfumo mpya wa kuchuja wanafunzi wanaotakiwa kuingia sekondari na kuachana na mfumo wa sasa wa kila mwanafunzi lazima asome sekondari
- serikali iboreshe maslahi ya waalim na ijenge mazingira mazuri ya kufundishia
- wanafunzi wajengewe misingi ya maarifa, ari na nidhamu juu ya mchakato wa elimu
TAHADHARI: TUSIPOZIBA UFA TUTAJENGA UKUTA!